Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,445
- 3,403
ULAJI wa nyama hapa nchini uko kwa kiwango cha chini ambapo sasa ulaji umefikia kilo 15 huku Shirika la Afya Duniani (WHO) likitaja mtu wa kawaida anatakiwa kula angalau kilo 50 kwa mwaka.
Akizungumza jana kwenye paredi ya mifugo kwenye maonesho ya mifugo na wakulima maarufu Nanenane yanayofanyika katika Viwanja vya Nzuguni Jijini Dodoma, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo, Profesa Elisante ole Gabriel alisema kwa mujibu wa WHO kwa Tanzania bado ulaji si mzuri ambapo takwimu zinaonesha mwaka 2017/ 18 ulaji wa nyama ulikuwa kilo 10 kwa mwaka.
"Angalau sasa tumefikisha kilo 15 kwa mwaka, bado tuko chini sana. Watanzania wajitahidi kula nyama ambayo ni sahihi," alisema.
Pia alisema sasa unywaji wa maziwa umefikia lita 200 kwa mwaka, lakini mwaka 2018/19 unywaji wa maziwa ulikuwa lita 54 kwa mwaka.
"Wakati Rais John Magufuli akiingia madarakani wizara ilikuwa ikichangia Sh bilioni 14 lakini imeongezeka hadi kufikia Sh bilioni 44.5, sawa na ongezeko la asilimia zaidi ya 200,”alisema.
Pia mifugo imeongezeka sasa kuna ng'ombe milioni 33, mbuzi milioni 23, kondoo zaidi ya milioni sita, kuku milioni 83 na kuku mayai yamefika bilioni nne.
"Mayai peke yake ni bilioni 800 hii ni jambo kubwa sana, lazima juhudi ziongezwe," alisema
Kwa upande wake, mgeni rasmi katika maonesho hayo ambaye ni Kaimu Mkuu wa mkoa ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda alisema sekta ya mifugo ikisimamiwa vizuri itachangia fedha za kutosha katika pato la taifa.
Alisema kwa wilaya ya Bahi asilimia 80 ya makusanyo ya ndani yanatokana na mifugo.
Angelina Lutambi Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida alisema maonesho hayo yamekuwa ni elimu kwa wananchi na watendaji wa ngazi mbalimbali za serikali na yamekuwa njia nzuri ya kujifunza.
Mkoa wa Singida uchumi wake unategemea kilimo na sekta ya mifuko ikiwa na idadi ya mifugo zaidi ya milioni 1.3.
Mkuu wa Wilaya ya Chemba, Simon Odunga alisema wataendelea kuhamasisha ufugaji wenye tija.
Akizungumza jana kwenye paredi ya mifugo kwenye maonesho ya mifugo na wakulima maarufu Nanenane yanayofanyika katika Viwanja vya Nzuguni Jijini Dodoma, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo, Profesa Elisante ole Gabriel alisema kwa mujibu wa WHO kwa Tanzania bado ulaji si mzuri ambapo takwimu zinaonesha mwaka 2017/ 18 ulaji wa nyama ulikuwa kilo 10 kwa mwaka.
"Angalau sasa tumefikisha kilo 15 kwa mwaka, bado tuko chini sana. Watanzania wajitahidi kula nyama ambayo ni sahihi," alisema.
Pia alisema sasa unywaji wa maziwa umefikia lita 200 kwa mwaka, lakini mwaka 2018/19 unywaji wa maziwa ulikuwa lita 54 kwa mwaka.
"Wakati Rais John Magufuli akiingia madarakani wizara ilikuwa ikichangia Sh bilioni 14 lakini imeongezeka hadi kufikia Sh bilioni 44.5, sawa na ongezeko la asilimia zaidi ya 200,”alisema.
Pia mifugo imeongezeka sasa kuna ng'ombe milioni 33, mbuzi milioni 23, kondoo zaidi ya milioni sita, kuku milioni 83 na kuku mayai yamefika bilioni nne.
"Mayai peke yake ni bilioni 800 hii ni jambo kubwa sana, lazima juhudi ziongezwe," alisema
Kwa upande wake, mgeni rasmi katika maonesho hayo ambaye ni Kaimu Mkuu wa mkoa ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda alisema sekta ya mifugo ikisimamiwa vizuri itachangia fedha za kutosha katika pato la taifa.
Alisema kwa wilaya ya Bahi asilimia 80 ya makusanyo ya ndani yanatokana na mifugo.
Angelina Lutambi Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida alisema maonesho hayo yamekuwa ni elimu kwa wananchi na watendaji wa ngazi mbalimbali za serikali na yamekuwa njia nzuri ya kujifunza.
Mkoa wa Singida uchumi wake unategemea kilimo na sekta ya mifuko ikiwa na idadi ya mifugo zaidi ya milioni 1.3.
Mkuu wa Wilaya ya Chemba, Simon Odunga alisema wataendelea kuhamasisha ufugaji wenye tija.