Watanzania tumezidi kulalamika - Zambia zaidi ya Magufuli

bulabo

JF-Expert Member
Aug 20, 2015
620
759
Watanzania tupunguze kulalamika. Serikali iliyopita watu walikuwa wakilalamika leo Magufuli anataka kuipanga Serikali upya nao wanalalamika. Mtaisha lini kulalamika. Kila miaka ni kulalamika tu.

Nani atatufanya tusilalamike??? Huwa najiuliza maswali kama wafanyabiashara kodi wanazolipa kwenye EFD wanatuwekea sisi walaji inakuwaje walalamike? Pili kama ulikuwa na hotel sasa haina wateja jiulize wateja wameenda wapi?? Kama ulizoea safari kila siku leo hazipo badili mfumo wa maisha.

Zambia wamebana kila kitu ni zaidi ya Tanzania. Nenda zambia ukajionee maisha yalivyo magumu. Tubadili mfumo wetu wa maisha wa kuetegemea mteremko.

Mimi naomba Rais aendelee hivi hivi ili Tanzania iwe kwenye mstari
 
Ulitaka kutuambia kwamba umewahi kwenda zambia! Hatuwezi kujifananisha na nchi mbovu kama zambia! Otherwise tunashukuru kwa taarifa ila shida sio za kujisifia ukiona umefikia stage hiyo ujue huyo mtu ni masikini na hana matarajio so inabidi ajisifie ionekane umasikini ni jambo zuri sana na la kujisifia!
 
hivi lengo ni kubana au kuwafanya wenye nchi waishi maisha mezuri? nadhani tunatakiwa tuishi kama malaika tofauti na tulivyokuwa tunaishi kama mashetani. big up baba j.
 
Watanzania tupunguze kulalamika. Serikali iliyopita watu walikuwa wakilalamika leo Magufuli anataka kuipanga Serikali upya nao wanalalamika. Mtaisha lini kulalamika. Kila miaka ni kulalamika tu.

Nani atatufanya tusilalamike??? Huwa najiuliza maswali kama wafanyabiashara kodi wanazolipa kwenye EFD wanatuwekea sisi walaji inakuwaje walalamike? Pili kama ulikuwa na hotel sasa haina wateja jiulize wateja wameenda wapi?? Kama ulizoea safari kila siku leo hazipo badili mfumo wa maisha.

Zambia wamebana kila kitu ni zaidi ya Tanzania. Nenda zambia ukajionee maisha yalivyo magumu. Tubadili mfumo wetu wa maisha wa kuetegemea mteremko.

Mimi naomba Rais aendelee hivi hivi ili Tanzania iwe kwenye mstari
Mkuu kwa hiyo unasifia ugumu wa maisha ya wazambia, kukua kwa uchumi wa nchi yeyote duniani kunapimwa kwa unafuu wa maisha ya wananchi wake kama vile mfumuko wa bei, huduma bora n.k.
 
Back
Top Bottom