Watanzania tumeamua kumshitakia Mungu

Watanzania tumeamua kumshitakia Mungu

nguruka wa kig0ma

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2020
Posts
2,943
Reaction score
2,935
Salaam,

Wakati ule mkuu aliposema nitawafanya muishi Kama shetani, wengi tulijua kuwa hao wanaosemwa no wenye ukwasi na wapigaji.

TAKASHANGILIA KWA MAKOFI NA VIGELEGELE

Ilipoanza tumbua tumbua, TUKAFURAHI, Watanzania wenzetu kudhalilishwa hadharani.

Walipotafutwa wenye magodown ya sukari, tukasema, MKUU HUYU KIBOKO anajua Sana tena kila kitu.

Leo hii ninapoandika post hii, tumetambua kuwa kumbe maneneno huumba, yawezekana msemaji hakujua mwisho wa maneno yake ni utimilifu.

Ndiposa watanzania tumefika mahali tumesema TUNAMSHITAKIA MUNGU, maana hakika tunaishi Kama shetani.

Suala la chai asubuhi tulisha sahau kitambo, familia chache Sana zinapata chai asubuhi, kuwa sukari haikamatiki.

Mlo wa mchana nao ukipatikana no bahati

Mzunguko wa pesa mtaani ni Kama haupo.

Watu wanasema afadhali walipokuwepo hao walioitwa wapigaji.

Walipiga wakaingiza hela mtaaani, maisha yalikuwa pesi.

MUNGU TUSAIDIE
 
Hata Marekani ambao wanatoa misaada dunia nzima kuna "watu wazima omba omba" wanaolala mitaani, hawana bima za afya na wanakufa kwa baridi kali! Hakuna kitu kibaya kama UMASKINI WA FIKRA, tunao maskini wa fikra hapa JF, mtaani, kwenye familia zetu, nk...

Mfano hai mimi ninaye kaka wa tumbo moja na mimi, kasoma kazi hataki, eti anataka kujiajili....nimempa mtaji zaidi ya mara 3 hakuna kitu...juzi kanitumia ujumbe kwenye simu eti : "...MDOGO WANGU UNAJUA KIJANA WA KWA MZEE LUSHINGE SASA HIVI DUKA LAKE LIMESIMAMA BAADA YA KUHARIBU MTAJI ALIYOKUWA ANAPEWA na BABA YAKE ZAIDI YA MARA 10.." nimemjibu hivi...KIPATO CHA MZEE LUSHINGE NA CHANGU NI TOFAUTI SANA, sina uwezo wa kukupa mtaji mwingine!

Watu kama kaka yangu wapo wengi kuanzia hapa JF, familia, mtaani, nk ambao wanadhani kazi yaserikali ni kuwawekea "ugali mezani, mitaji na kuwatafutia PISI KALI weekend"

JPM kaza kamba, soon watu wenye akili tu ndio watabaki mjini...!
 
Hata Marekani ambao wanatoa misaada dunia nzima kuna "watu wazima omba omba" wanaolala mitaani, hawana bima za afya na wanakufa kwa baridi kali! Hakuna kitu kibaya kama UMASKINI WA FIKRA, tunao maskini wa fikra hapa JF, mtaani, kwenye familia zetu, nk..
Ndebile mpaka kwenye ubongo
 
Ndebile mpaka kwenye ubongo
Hadi shemeji yako atakuchoka maana bado mitano na wakipa kura ikitupendeza tunaondoa ukomo wa mihula, dadadeki.! Mkuu umeona Krismass ya mwaka huu ilivyokuwa tulivu!
 
Salaam,

Wakati ule mkuu aliposema nitawafanya muishi Kama shetani, wengi tulijua kuwa hao wanaosemwa no wenye ukwasi na wapigaji.

TAKASHANGILIA KWA MAKOFI NA VIGELEGELE

Ilipoanza tumbua tumbua, TUKAFURAHI, watanzania wenzetu kudhalilishwa hadharani.

Walipotafutwa wenye magodown ya sukari, tukasema, MKUU HUYU KIBOKO anajua Sana tena kila kitu.

Leo hii ninapoandika post hii, tumetambua kuwa kumbe maneneno huumba, yawezekana msemaji hakujua mwisho wa maneno yake ni utimilifu.

Ndiposa watanzania tumefika mahali tumesema TUNAMSHITAKIA MUNGU, maana hakika tunaishi Kama shetani.

Suala la chai asubuhi tulisha sahau kitambo, familia chache Sana zinapata chai asubuhi, kuwa sukari haikamatiki.

Mlo wa mchana nao ukipatikana no bahati

Mzunguko wa pesa mtaani ni Kama haupo.

Watu wanasema afadhari walipokuwepo hao walioitwa wapigaji.

Walipiga wakaingiza hela mtaaani, maisha yalikuwa pesi.

MUNGU TUSAIDIE
Tulisha patiwa jina kuwa ni malofa
 
Hadi shemeji yako atakuchoka maana bado mitano na wakipa kura ikitupendeza tunaondoa ukomo wa mihula, dadadeki.! Mkuu umeona Krismass ya mwaka huu ilivyokuwa tulivu!
Hali hiyo inawahusu wapinzani tu
 
Hii imekuwa kama ndoto ya farao miaka kumi ya njaa miaka kumi ya shibe
 
Hapa Mungu wala Shetani hahusiki. Wewe na akili yako
 
ukweli ni kwamba bei ya vitu imepanda sana pia maisha ni magumu hata ajira nazo ni changamoto kwa wengi, Cha ajabu ni kama serikali imeziba maskio au huu ndo uchumi wa kati?
 
Tulia hii ni mitano tena! Mbaya zaidi ndio tupo mwezi wa kwanza 🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣😂😂😂😂😂
 
First they came for the socialists, and I did not speak out—
Because I was not a socialist.

Then they came for the trade unionists, and I did not speak out—
Because I was not a trade unionist.

Then they came for the Jews, and I did not speak out—
Because I was not a Jew.

Then they came for me—and there was no one left to speak for me.

- Martin Niemöller, German clergyman on Nazi oppression.
 
Ndo tutajua nani mwanaume ichi kipindi mpaka Wote mkimbie miji magu shikilia apo apo baba...I can't breath..
 
Back
Top Bottom