Watanzania tukosoane kwa nia ya kujenga na sio kubomoa- Clouds 360

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,504
113,618
Wanabodi,

Tanzania ni yetu sote, kwa Watanzania wote kuwa na haki sawa, hadhi sawa, na tunawajibu wa pamoja wa kulijenga taifa letu, individually na collectively kwa kuwa wazalendo wa kweli wa taifa letu, hivyo kunapotokea ukosoaji wowote, ukosoaji huu, ufanyike kwa nia njema ya kujenga na sio kubomoa.

Haya ni miongoni mwa yalizosungumzwa leo kwenye kipindi cha 360 kinachorushwa na Clouds TV, toka kwa watangazaji, Hasan Ngoma na Ceaser, na kiukweli huyu mtangazaji Ceaser, ni mzuri sana kwa kujenga hoja, nimependa kwa jinsi alivyo construct arjument ya uzalendo, na kui drive home kwa mfono mzuri sana, kuashiria pamoja na tofauti zetu za kiitikadi, kisiasa, na kivyama, lakini linapokuja suala la maslahi ya taifa, Watanzania tuwe wamoja.

Wakatumia speeches za Lipumba na John Cheyo za jana pale Ikulu.

Declaration of Interest
Kwanza naomba kukiri, mimi ni miongoni mwa watu ambao nilikuwa siisikilizi Clouds Radio wala kuangalia Clouds TV, kwa sababu niliiona kama ni media ya vijana, hivyo kuwahesabu they are not serious, ila mara moja moja nilikuwa nasikiliza Jahazi nikiwa kwenye gari, nikawaona kama ni wapayukaji na ni watu wa kujipendekeza pendekeza sana hadi kuonekana kama kujikomba kwa CCM, hivyo nikawapotezea, ila nilipokuja kujua kuwa kumbe Magufuli anaangalia 360, ndipo na mimi nikaanza kuwaangalia, nikakuta they are fine, haswa Baby Kabae. Hivyo siku hizi naangalia Clouds.Kama Magufuli Anaangalia Clouds TV na Kuipongeza, Kunatuma ...

Naunga Mkono Hoja ya Uzalendo na Kukosoa Kwa Hoja Kwa Nia Njema ya Kujenga.
Japo hoja hii imetolewa na hawa vijana wadogo, lakini mimi, pamoja na ukongwe wangu, naunga mkono hoja hii ya tutofautiane kiitikadi, tukosoane kwa hoja, kwa lengo la kujenga na sio kubomoa, lakini linapokuja suala la maslahi ya taifa, tutangulize uzalendo kwa kuweka pembeni tofauti zetu, na kuungana kwa pamoja, tuwe wamoja kwa kutanguliza mbele maslahi ya taifa, yaani Tanzania kwanza, mengine yote yatafuatia.

Uzalendo ni Nini, na Mzalendo ni Nani?
Uzalendo ni ile hali ya kuwa na moyo wa upendo wa dhati kwa taifa lako, hadi kuwa tayari kulifia, hivyo mzalendo ni mtu yoyote anayefanya jambo lolote la kizalendo, mfano mzuri ni kwenye hii vita ya kupigania rasmilimali mali upande wa rasilimali madini, watu kama kina Tundu Lissu, Zitto Kabwe, JJ Mnyika, ni watu waliyeonyesha uzalendo mkubwa zaidi kuliko Watanzania wengi, wakati huo Magufuli akiwa ni sehemu ya waliolifikisha taifa hili hapa, akiwa ni waziri, wakati haya madudu yote yakipitishwa ndani ya baraza la mawaziri, lakini leo kwa vile Magufuli ndio amayafumua, kwa sasa sifa na pongezi zote za uzalendo wa kweli, zinakwenda kwa rais Magufuli kwa vile amefanya mambo makubwa ya kuonekanika. Thamani halisi ya uzalendo, sio kufanya mambo ya kizalendo ya kuonekanika, bali kuna wazalendo kibao silent heroes, wanaofanya mambo makubwa kabisa yasionekana, hawataji popote, hawapongezwi, hawapewi vyeti, lakini ni wazalendo kuliko hawa wanaoonekana, na mmoja wa wazalendo hawa ni huu mtandao wa JF.

Jee Kumkosoa Rais Magufuli ni Uzalendo au ni Usaliti, hivyo Uzalendo ni Kumsifia Tuu?.
Katika kusifia uzalendo, pia imejengwa dhana ya usaliti, kuwa wale wote wanaomkosoa rais Magufuli ni wasaliti, au wale wote wanaopingana nae ni wazaliti, hivyo tafsiri ya uzalendo ni wale tuu wanaosifia rais, hata akifanya makosa, wao watasifu tuu na kupiga makofi. Ukweli ni kuwa hakuna ubaya wowote kumkosoa rais Magufuli, kama ukosoaji huo unafanyika kwa nia njema kwa lengo la kujenga kwa kumsaidia, huku ukifanywa kwa lugha ya staha yaani constructive criciticism na sio kumbomoa, kumtukana, kumdhihaki au kumdhalilisha kwa lugha ya machukizo. Kumkosoa rais Magufuli sio kukosa uzalendo, wala sio usaliti, tena unaweza kukuta, wale wanaomkosoa rais ndio wazalendo wa kweli na wanamsaidia kuliko wale wanaomsifia na kumuimbia tuu nyimbo za sifa, sjangwe na mapambio, kwa sababu rais Magufuli naye, is only human, can make mistake.

Jee Wanaokosoa Magufuli, Wanamkosoa Kwa Chuki Kwa Vile Hawampendi, Au Wanampenda Sana Ndio Maana Wanamkosoa?.
Kuna makundi makuu matatu ya Wakosoaji wa Rais Magufuli, kuna kundi la the politicians, kuna kundi la hatters, na kundi la realists, truthful na perfectionists
  1. The Politicians -Hawa ni wale ambao Magufuli hakuwa mtu wao, hawa wana mtu wao aliyeshindwa, hivyo hawa, kila kitu ambacho Magufuli, wao watakosoa tuu sio ili kumsaidia, but for political gain. Wengi wa kundi hili ni wapinzani, hii inapelekea kila anayemkosoa rais Magufuli, kunyooshewa kidole kuwa ni mpinzani, kazi yao ni kupinga tuu. Ndiko huku kuiga marufuku mikutano ya kisiasa kulliko ibukia.
  2. Haters- Hili ni kundi la watu wenye chuki tuu kumhusu Magufuli, au chuki kwa CCM, wao kazi yao ni kukosoa tuu tena kwa kutumia lugha mbaya na hata kutukana, hawa ni hate preachers, ambao wana kwenda hadi personal issues na kuingilia his right to privacy, lengo lao ni Magufuli achukiwe. Hii imepelekea kila anayemkosoa rais Magufuli, kuonekana ana chuki na Magufuli, hii inamfanya rais Magufuli kupokea ukoaji huu kwa chuki na huwajibu kwa maneno makali, na ndiko huku neon fyokofyoko lilikoibukia.
  3. Realists, truthful na perfectionists-Hawa ni wakosoaji ambao ni wa kweli, wanamkosoa kwa makosa ya ukweli, hivyo ukosoaji wao ni wa hoja za kweli, unaofanywa kwa nia njema ili kumsaidia, na nyingi ya ukosoaji huu hufanywa constructively yakiwemo mapendekezo ya a way forward, hawa wanamtaka rais Magufuli awe perfect, wanamkosoa sio kwa sababu wanamchukia, bali wanamkosoa kwa sababu wanampenda, kama baba anavyomrudi mwanaye, au mti wa matunda unavyopopolewa. hivyo anapofanya mazuri, watu hawa humpongeza, kwenye kundi hili, ndimo mtoa mada alimo.
Hitimisho
Maendeleo ya kweli Tanzania, yataletwa na wazalendo wa kweli wa nchi hii, kwa kutumia kanuni ya kusema ukweli daima, hata rais akikosea, akosolewe kwa staha kwa kuambiwa ukweli, na yeye kama rais wetu, auchukue ukosoaji wetu humu very positively, kama mimi nilivyo wahi kushauri humu, kuhusu madini, rais mkapa alidanganywa, akadanganyika, rais Kikwete, amedanganywa, akadanganyika, kwenye hili na makinikia rais Magufuli naye, kaisha danganywa, na kuna kila dalili, ameisha danganyika, na hapa nawaomba sana wale wote wenye mapenzi mema na taifa hili, mpigie mstari maneno yangu haya, kuwa Tukikubali kukipokea hiki kishika uchumba cha Acacia cha dola milioni 300, na tukaruhusu mchanga wa makinikia ya dhahabu kusafirishwa, bila kujua kilichomo, then this will be a done deal, forget about Trilioni 450!.Mkapa na Kikwete Walidanganywa na Wakadanganyika!, Magufuli ...

Vipi maoni yako, uzalendo ni kusifu tuu na kukosoa ni usaliti, au uzalendo wa kweli ni kuusema ukweli daima, no matter unauma kiasi gani?

Paskali
Rejea kuhusu ukosoaji
Mwito Kwa Wana JamiiForums Kuhusu Ukosoaji wa Rais Magufuli ...
Rais Magufuli na serikali yake wakosolewe kwa hoja sio kwa viroja ...
Tusilalamike Tuu, Kulaumu na Kulaani Kila Kitu, Kwenye Mazuri ...
Rais Magufuli Akifanya Mazuri, Apongezwe: Hotuba Yake Kuzima ...
Wana JF, Jee Tuisaidie Serikali Yetu Inaposhindwa Au Tusubiri ...
2017 JF Tubadilike, Tupunguze Kuwa "Barking Dogs, Seldom Bite ...
Wasaidizi wa Rais, Please Msaidieni Rais Wetu Kwenye ...
Jee Aachwe Aseme Tuu, By "Taking The Bitter With The Sweet ...
Naamini Rais Magufuli ana washauri wazuri na anashauriwa ...
 
Wanabodi,

Tanzania ni yetu sote, kwa Watanzania wote kuwa na haki sawa, hadhi sawa, na tunawajibu wa pamoja wa kulijenga taifa letu, individually na collectively kwa kuwa wazalendo wa kweli wa taifa letu, hivyo kunapotokea ukosoaji wowote, ukosoaji huu, ufanyike kwa nia njema ya kujenga na sio kubomoa.

Haya ni miongoni mwa yalizosungumzwa leo kwenye kipindi cha 360 kinachorushwa na Clouds TV, toka kwa watangazaji, Hasan Ngoma na Ceaser, na kiukweli huyu mtangazaji Ceaser, ni mzuri sana kwa kujenga hoja, nimependa kwa jinsi alivyo construct arjument ya uzalendo, na kui drive home kwa mfono mzuri sana, kuashiria pamoja na tofauti zetu za kiitikadi, kisiasa, na kivyama, lakini linapokuja suala la maslahi ya taifa, Watanzania tuwe wamoja.

Wakatumia speeches za Lipumba na John Cheyo za jana pale Ikulu.

Mimi naunga mkono hoja hii ya tutofautiane kiitikadi, tukosoane kwa hoja, kwa lengo la kujenga na sio kubomoa, lakini linapokuja suala la maslahi ya taifa, tuweke mbele maslahi ya taifa kwa kuwa wamoja.

Vipi wewe?.

Paskali
Paskali, please ,acha posts za watu ambao hawakwenda shule. Nilitegemea uandike makala fupi fikirishi, ku define UZALENDO, from there then ndiyo uandike habari kama hii. Wewe ni nguzo ya uandishi wa habari. Unajua walakini uko wapi, kumekuwa na mabishano ya what is uzalendo and from there you can determine who and who is not mzalendo!
Ebu tutafakarishe na definition ya mzalendo kwanza.
(kwa sasa Paskali siwezi kusikiliza waandishi hasa wa vyombo vya habari , hawawezi kusema ukweli ulio rohoni mwao at a risk of closure of their media!), hawwezi kwenda kinyume na matakwa ya "mkuu".
 
Wazo zuri sana. Laknini swali langu ni hili, Je ni kweli kwamba nikikosoa kwa nia njema ya kujenga nitabaki salama kwenye nchi hii? Hapa ndipo penye tatizo. Ninaweza kukosoa kwa nia nzuri tu ya kujenga na wala si kubomoa, lakini hilo linaweza kutafsiriwa kuwa ni uchochezi na nikaishia pabaya. Kwa hiyo hapa kwetu ili uwe salama ni aidha upongeze au weka zip mdomoni.
 
kukosoa kwa kujenga.. swali kujenga wapi? au kujenga nini? inawezekana kabisa mimi katika kukosoa kwangu ukaona nakosoa ili nibomoe kwako then nijenge kwangu na hapo ndipo ugomvi unapokuja.kukosoa lengo kubwa liwe kujenga.lakini ,kujenga wapi?kujenga kwa nani? na je anayekosolewa anajua lengo ni kujenga?au yeye anaamini kila anayekosoa anabomoa kwake?
 
Tafsiri ya uzalendo awamu hii ni kupiga mapambio tu kwa watawala na miungu watu wao,uukisema ukweli na kutoa mawazo mbadala yanaonyesha uovu na udhaifu wa miungu watu hawa inakuwa benduki,uumehongwa na kila matusi!!!

Swali-MSwali-Magufuli aliingia madarakani na kukua sukari 1kg she ngapi? Aliyesema alikuta she 5000 kwa kg nae atashitakiwa kwa kupika data ama atapigiwa makofi tu?!
 
..tatizo hakuna HAKI na USAWA miongoni mwa VYAMA VYA SIASA.

..Wapo watu hawana lugha za staha hata kidogo kwa wenzao, lakini wakati huohuo wanataka wao waheshimiwe.

..Pia iwe ni mwiko kutumia MABAVU kujibu hoja za kisiasa/wanasiasa.
 
Ni dhana nzuri kabisa, ambayo inaenda samba mba na kumpa mtu sifa yake pale anapokuwa amefanya vizuri ili iwe rahisi kumkosoa pale anapokuwa amefanya vibaya. Ni ukweli usiopingika kuwa ukimsifu mtu kwa jambo zuri, siku akikosea utakuwa katika nafasi nzuri ya kumkosoa. Lakini, kama mtu amefanya jambo zuri ambalo kila mtu anaona kuwa ni zuri, halafu wewe unapinga kwa nguvu zote, hapo hata siku akifanya baya, ukajitokeza kukosoa, hutaaminika.

Lakini Mkuu Pascal, wewe ni miongoni mwa Waandishi Nguli, tena mimi ni miongoni mwa wateja wako wakati wa msimu fulani hivi kupitia vipindi vya PPR na 7,7 au 8,8. Sasa imekuwaje katika Andiko lako hapo juu, umeandika kama mtu wa kawaida hivyo kwa kuchanganya lugha ya Malkia na hii ya Taifa letu, mbona ungeandika katika lugha moja miongoni mwa hizo kuliko hayo mabaka mabaka.
 
Mkuu watakwambia Cheyo na Lipumba ni CCM B wao wanataka kauli za kina Msigwa ''
Peter Msigwa: Kazi ya kiongozi wa upinzani ni kuwachochea wananchi waione Serikali haifai
 
Wanabodi,

Tanzania ni yetu sote, kwa Watanzania wote kuwa na haki sawa, hadhi sawa, na tunawajibu wa pamoja wa kulijenga taifa letu, individually na collectively kwa kuwa wazalendo wa kweli wa taifa letu, hivyo kunapotokea ukosoaji wowote, ukosoaji huu, ufanyike kwa nia njema ya kujenga na sio kubomoa.

Haya ni miongoni mwa yalizosungumzwa leo kwenye kipindi cha 360 kinachorushwa na Clouds TV, toka kwa watangazaji, Hasan Ngoma na Ceaser, na kiukweli huyu mtangazaji Ceaser, ni mzuri sana kwa kujenga hoja, nimependa kwa jinsi alivyo construct arjument ya uzalendo, na kui drive home kwa mfono mzuri sana, kuashiria pamoja na tofauti zetu za kiitikadi, kisiasa, na kivyama, lakini linapokuja suala la maslahi ya taifa, Watanzania tuwe wamoja.

Wakatumia speeches za Lipumba na John Cheyo za jana pale Ikulu.

Mimi naunga mkono hoja hii ya tutofautiane kiitikadi, tukosoane kwa hoja, kwa lengo la kujenga na sio kubomoa, lakini linapokuja suala la maslahi ya taifa, tuweke mbele maslahi ya taifa kwa kuwa wamoja.

Vipi wewe?.

Paskali
Pascal Mayalla ukosoaji haupangwi na mkosolewa.

Wanakiri kukosea! Wanaleta na kebehi, tambo, majigambo, dharau na ubabe.

Ni sawa unapigwa makonzi halafu unatishwa kuwa ukilia kwa sauti itakuletea matatizo!!!!

HUU SASA UJINGA ULIOPEA.
 
Huyu Hassan ngoma alitishiwa kufukuzwa kazi na kusimamishwa kazi last week name boss wake bwana Ruge mutahaba?
 
Ni nani wa kujenga UZALENDO au umoja huo unaouzungumzia?

Wapi sehemu sahihi ya Mtanzania kuuliza maswali yake na kupata majibu ambayo nayo yanaweza kuzalisha swali?

Uzalendo ni kukaa kimya, uzalendo ni kushauri kile ambacho watawala watapenda kukisikia?

Au Uzalendo ni kuihoji serikali yako pale unapoona kuna ukakakasi ili upate jibu na uridhike ikiwezekana utoe ushauri ambao kama ni mzuri upokelewe na kufanyiwa kazi na mrejesho upewe.

MF; Mh Rais alimsifia Mh Kitila Mkumbo kwenye moja ya michango yake juu ya wanafunzi wa UDOM

MH RAIS alikiri hadharani hapa neno UZALENDO lilitendewa haki.

Vilevile nikitoa mawazo potofu nisichukuliwe kuwa sio MZALENDO yawapasa watawala WANIJIBU kwa ufasaha .

Ikiwezekana waniite na kunionesha uhalisia nijisifu kukanyaga Ikulu,nijisifu kukanyaga hazina nijisifu kutembelea majengo ya kodi yangu na kupewa fafanuzi nikijivunia Uzalendo.

Lkn ninapokosea nikijibiwa kwa dharau au ninapohoji kwa mantiki na mtawala akaona ni mantiki na kuigeuza kuwa yake na kujifanya ni ubunifu wake. Na kunishambulia kwa kejeli UZALENDO

Unakuwa mgumu.
 
Wanabodi,

Tanzania ni yetu sote, kwa Watanzania wote kuwa na haki sawa, hadhi sawa, na tunawajibu wa pamoja wa kulijenga taifa letu, individually na collectively kwa kuwa wazalendo wa kweli wa taifa letu, hivyo kunapotokea ukosoaji wowote, ukosoaji huu, ufanyike kwa nia njema ya kujenga na sio kubomoa.

Haya ni miongoni mwa yalizosungumzwa leo kwenye kipindi cha 360 kinachorushwa na Clouds TV, toka kwa watangazaji, Hasan Ngoma na Ceaser, na kiukweli huyu mtangazaji Ceaser, ni mzuri sana kwa kujenga hoja, nimependa kwa jinsi alivyo construct arjument ya uzalendo, na kui drive home kwa mfono mzuri sana, kuashiria pamoja na tofauti zetu za kiitikadi, kisiasa, na kivyama, lakini linapokuja suala la maslahi ya taifa, Watanzania tuwe wamoja.

Wakatumia speeches za Lipumba na John Cheyo za jana pale Ikulu.

Mimi naunga mkono hoja hii ya tutofautiane kiitikadi, tukosoane kwa hoja, kwa lengo la kujenga na sio kubomoa, lakini linapokuja suala la maslahi ya taifa, tuweke mbele maslahi ya taifa kwa kuwa wamoja.

Vipi wewe?.

Paskali

Kamarada wangu siku hizi unakuwaje tena? Una uhakika kwamba hao unaowasifia wanafanya vile inavyostahili kufanyika hasa kwa Vyombo vya Habari? Labda nianze tu kwa kuweka wazi Kwako kwamba Mimi ni CCM tena ' Kindakindaki ' na hili sitolificha humu ila kwa muda mrefu sasa Clouds Media Group imekuwa ni 100% ' Kibaraka ' wa Serikali na hasa Chama Tawala chetu cha CCM huku mara nyingi wakiwa ' wanadhihaki ' mno juhudi za ' Wapinzani ' na kuna wakati mwingine pia hawa Watangazaji hudiriki hata ' Kuwasanifu ' Viongozi wa Upinzani mfano wa CHADEMA na CUF kitu ambacho nina uhakika kabisa Wewe ( Kamarada ) wangu unajua kwamba katika ' tasnia ' yetu ya Uandishi wa Habari hakitakiwi kufanyika and its unprofessional kabisa.

Ukiwa ni mfuatiliaji mzuri na Media za Tanzania hasa hizi za ' Electronics ' hutopata shida / taabu kujua kwamba CMG ni pure ' Pro CCM ' na nadhani kwa jicho kubwa la ' Marketing ' hawa Watu wanaweza wakajikuta wanajiua wenyewe na huko baadae wakaanguka vibaya hasa ukizingatia kwamba siyo ni wana CCM tu ndiyo wanapeleka pale ' matangazo ' bali kuna hata Wadau wengine pia ambo ni non CCM.

Nadhani Clouds Media Group ili kuzidi kukijengea ' Heshima ' yake kwa audience wake ilipashwa ijihalalishe kwamba yenyewe ni ' Neutral ' medi house kisha wajikite sana mno katika kufanya chambuzi ' mjumuisho ' za Kisiasa ambazo zitawafanya wazidi kuwa very objective tofauti na walivyo very subjective Kimaudhui kwa sasa.

Kamarada leo umeniangusha sana na bahati mbaya Mimi sijazoea na sipendi ' Unafiki ' hivyo nimekukosoa hivyo hivyo japo Wewe na Mimi ni ' Wadau ' wakubwa sana Kitaaluma na Kiuweledi. Hizi Media za Tanzania zikiachwa hivi ipo siku yale ya Redio ile ya RTLM yataikumba Tanzania na tutatafutana hapa mjini Mkuu.

Kazi njema / Majukumu mema ' Kamarada '.
 
Wanabodi,

Tanzania ni yetu sote, kwa Watanzania wote kuwa na haki sawa, hadhi sawa, na tunawajibu wa pamoja wa kulijenga taifa letu, individually na collectively kwa kuwa wazalendo wa kweli wa taifa letu, hivyo kunapotokea ukosoaji wowote, ukosoaji huu, ufanyike kwa nia njema ya kujenga na sio kubomoa.

Haya ni miongoni mwa yalizosungumzwa leo kwenye kipindi cha 360 kinachorushwa na Clouds TV, toka kwa watangazaji, Hasan Ngoma na Ceaser, na kiukweli huyu mtangazaji Ceaser, ni mzuri sana kwa kujenga hoja, nimependa kwa jinsi alivyo construct arjument ya uzalendo, na kui drive home kwa mfono mzuri sana, kuashiria pamoja na tofauti zetu za kiitikadi, kisiasa, na kivyama, lakini linapokuja suala la maslahi ya taifa, Watanzania tuwe wamoja.

Wakatumia speeches za Lipumba na John Cheyo za jana pale Ikulu.

Mimi naunga mkono hoja hii ya tutofautiane kiitikadi, tukosoane kwa hoja, kwa lengo la kujenga na sio kubomoa, lakini linapokuja suala la maslahi ya taifa, tuweke mbele maslahi ya taifa kwa kuwa wamoja.

Vipi wewe?.

Paskali
Mkuu paskali kwanza nikusifu kwa thread zako ambazo umekuwa unazitoa humu wewe huwa unakuwa mkweli ckuzote na huegemei upande wowote....binafsi mimi siwezi ku act uzalendo wakati viongozi wenyewe wakuu wamekua na dharau na maneno ya kejeli kwa sisi maskini kila siku alafu maana ya uzalendo ckuhz ni kumsifia magufuli kwa kila kitu???
 
Mimi naunga mkono hoja hii ya tutofautiane kiitikadi, tukosoane kwa hoja, kwa lengo la kujenga na sio kubomoa, lakini linapokuja suala la maslahi ya taifa, tuweke mbele maslahi ya taifa kwa kuwa wamoja.
P. mimi nikiona au kusikia neno uzalendo hapa Tz nasubiri tu kujua kuna atakae itwa msaliti au si mzalendo. Linatumika kubomoa watu na kujenga wale wapendwao na upande fulani. Ukipishana nao kauli basi wewe msaliti.

Hapo penye nyekundu pia pamejaa utata mtupu. Maslahi ya taifa ni yepi na nani ana amua haya ndo maslahi ya taifa. Kuwa wamoja ina maana gani? Wewe (sio wewe PM) unapotaka unasema tuwe wamoja hapo hapo unawazodoa wenzako kwa lugha ya ajabu ajabu. Hutaki wenzako wasikike kitaifa-hati kila mtu isipokuwa wewe apige local politics (hati jimboni kwake na yeye Tz ndo iwe jimboni kwake). Wakizungumza bungeni watasikika kitaifa basi fungia bunge live (labda PM na wenzake wenye nyenzo watajua yaendeleayo bungeni) wengi wetu tuko gizani tunasubiri magazeti kama yanafika kwetu. Kila event yako basi TV na Maradio yote yanarusha. Upinzani hauna platform kabisa wamebakia twitter au press conference (very limited audience). Wenye ujasiri wa kuzungumza tunaona yanayowakuta: TL ni mfano, ZZK professa kesha ambiwaamshughulikie mbona wao watoapo takwimu au matamko zisizo/yasiyo sawa wako poa tu.

Watawala wasipo kuwa na strategy ya kuwaleta waTz pamoja sidhani kama kutakuwa na mshikamano wanao utaka wao.
 
Wanabodi,

Tanzania ni yetu sote, kwa Watanzania wote kuwa na haki sawa, hadhi sawa, na tunawajibu wa pamoja wa kulijenga taifa letu, individually na collectively kwa kuwa wazalendo wa kweli wa taifa letu, hivyo kunapotokea ukosoaji wowote, ukosoaji huu, ufanyike kwa nia njema ya kujenga na sio kubomoa.

Haya ni miongoni mwa yalizosungumzwa leo kwenye kipindi cha 360 kinachorushwa na Clouds TV, toka kwa watangazaji, Hasan Ngoma na Ceaser, na kiukweli huyu mtangazaji Ceaser, ni mzuri sana kwa kujenga hoja, nimependa kwa jinsi alivyo construct arjument ya uzalendo, na kui drive home kwa mfono mzuri sana, kuashiria pamoja na tofauti zetu za kiitikadi, kisiasa, na kivyama, lakini linapokuja suala la maslahi ya taifa, Watanzania tuwe wamoja.

Wakatumia speeches za Lipumba na John Cheyo za jana pale Ikulu.

Mimi naunga mkono hoja hii ya tutofautiane kiitikadi, tukosoane kwa hoja, kwa lengo la kujenga na sio kubomoa, lakini linapokuja suala la maslahi ya taifa, tuweke mbele maslahi ya taifa kwa kuwa wamoja.

Vipi wewe?.

Paskali
Mimi nakubaliana na maoni yako Pascal. Lakini kuna mambo ambayo ingefaa yafanyiwe ufafanuzi zaidi au yatofautishwe. Kukosoa na kutukana. Kukosoa in jambo jema sana na hasa ukikosoa na kutoa maoni yako mbadala. Kutukana ni kutumia lugha ya kuudhi bila kutoa hoja. Na kwa sasa watu wengi wameegemea kutukana. Haijengi lolote.
 
Back
Top Bottom