Watanzania sasa mnaweza kuingia Congo bila Visa

Watanzania sasa mnaweza kuingia Congo bila Visa

Engneeer

Member
Joined
Dec 30, 2021
Posts
86
Reaction score
116
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inapenda kuufahamisha Umma kwamba, Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) imeondoa hitajio la visa kwa Raia wa Tanzania wanaoingia DRC kuanzia March 20, 2025.

Taarifa iliyotolewa na Wizara imesema baada ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) mwezi July 2022 baadaye September 02, 2023, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliondoa utaratibu wa malipo ya visa kwa raia wa DRC kwa matarajio ya nchi ya DRC pia kufuta utaratibu wa kutoza malipo ya visa kwa msingi wa kuungana mkono (reciprocity).

congo visa.png

Serikali ya Jamhuri wa Tanzania inaamini kuwa uamuzi huu wa Serikali ya DRC ni hatua nzuri katika kuimarisha mtangamano na utakuwa na manufaa, ikizingatiwa kuna mwingiliano mkubwa wa Wananchi wa nchi hizi mbili katika masuala mbalimbali ya kijamii na kibiashara, vilevile kuondolewa kwa hitajio la visa kutachochea ukuaji wa uwekezaji, biashara na kupunguza gharama.

“Hatua hii ni moja ya mafanikio ya Serikali ya awamu ya sita, inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, katika kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia na ujirani mwema kwa vitendo, na ni ishara ya Tanzania kuzingatia miongozi ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, pamoja na Mkataba wa Eneo Huru la Biashara la Bara la Afrika (AfCFTA)
 

Attachments

  • 1000075749.jpg
    1000075749.jpg
    111.3 KB · Views: 28
Fursa wakati hawaishi kupigana huko .
Inshort. Sisi Ndio fursa wanataka na sisi tuwe VISA free kwa watu wao.
Mapigano yapo East Congo, West ni sokous kwa kwenda Mbele... yaani unataka kuniambia hawa kina Awilo, Papaa Wemba, Koffie Olomide, ni masajent au!!!.. viuno havikatiki vitani ndugu, shtuka...

Hata Bongo kuna Tanzanite, mbuga wa wanyama, Kilimanjaro mt., ziwa Victoria, tanganyika, manyara, nyasa full mafish, pamba, korosho, mahindi, ngano, alizeti, na bado watu wanalala njaa.... kambi popote mangi.
 
Mapigano yapo East Congo, West ni sokous kwa kwenda Mbele... yaani unataka kuniambia hawa kina Awilo, Papaa Wemba, Koffie Olomide, ni masajent au!!!.. viuno havikatiki vitani ndugu, shtuka...

Hata Bongo kuna Tanzanite, mbuga wa wanyama, Kilimanjaro mt., ziwa Victoria, tanganyika, manyara, nyasa full mafish, pamba, korosho, mahindi, ngano, alizeti, na bado watu wanalala njaa.... kambi popote mangi.

Haya mkuu,kuna lile swali tunajiulizaga why now?
 
Angekuwepo marehemu Ruge mutahaba angekuambia, "changamkia fursa hiyo".

Nchi yenye madini nje nje unapewa Visa free, nini zaidi unataka... we jichange nauli tu na hema lako, kambi popote , nchi yako imetanuka mipaka.
Hawa akina kasongo wanaoenda kwao congo wanarudi na mabangili ya shaba wanashinda wanayatembeza hapa makumbusho afu 5 wao madini hawataki?
 
Hawa akina kasongo wanaoenda kwao congo wanarudi na mabangili ya shaba wanashinda wanayatembeza hapa makumbusho afu 5 wao madini hawataki?
Kwani wamasai wote wapo shimoni mererani? Si ndio hao wapo na biashara za shanga, sandals n.k... maapolo wengi ni kutoka sehemu mbalimbali za nchi...

Kwenye miti Mungu haweki wajenzi, upewe vyote we nani?
 
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inapenda kuufahamisha Umma kwamba, Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) imeondoa hitajio la visa kwa Raia wa Tanzania wanaoingia DRC kuanzia March 20, 2025.

Taarifa iliyotolewa na Wizara imesema baada ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) mwezi July 2022 baadaye September 02, 2023, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliondoa utaratibu wa malipo ya visa kwa raia wa DRC kwa matarajio ya nchi ya DRC pia kufuta utaratibu wa kutoza malipo ya visa kwa msingi wa kuungana mkono (reciprocity).


Serikali ya Jamhuri wa Tanzania inaamini kuwa uamuzi huu wa Serikali ya DRC ni hatua nzuri katika kuimarisha mtangamano na utakuwa na manufaa, ikizingatiwa kuna mwingiliano mkubwa wa Wananchi wa nchi hizi mbili katika masuala mbalimbali ya kijamii na kibiashara, vilevile kuondolewa kwa hitajio la visa kutachochea ukuaji wa uwekezaji, biashara na kupunguza gharama.

“Hatua hii ni moja ya mafanikio ya Serikali ya awamu ya sita, inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, katika kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia na ujirani mwema kwa vitendo, na ni ishara ya Tanzania kuzingatia miongozi ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, pamoja na Mkataba wa Eneo Huru la Biashara la Bara la Afrika (AfCFTA)
Congo nitakie nini kwenda, hiyo tiketi si ni kheri niwachangie ndugu zetu wana Gaza na Palestinian kwa ujumla!
 
Na bado watanganyika watalala TU.eti vita kwani vita inapiganwa nchi nzima?
KAZI ni kipimo cha utu
 
Sawa mdogo wangu
Mi nina duka mbili lubumbashi kaka. Unaruhusiwa kuja fursa kibao hawa jamaa ni watu wa bata sana. Na wapo wengi ni wewe tu ujiongeze. Waliochangamka kule ni wakasai tu
 
Back
Top Bottom