Watanzania ni wavivu?

Watanzania ni wavivu?

Mie nathibitisha kwa asilimia 1000% , majority ya watz ni wavivu na wanapenda short cut., kuna minority pia ambao ni wachapakazi haswa!! Uwiii msinishambulie please.
Umesema ukweli!
 
Usishange kuona watu wanahangaika kupanda madaladala kwenda kazini ama wengine wanatembea kuwahi kazini. Suala hapa ni hivi; watu hawa hawa wanaowai kwenda kazini wakifika huko hawafanyi kazi, wao ni domo tu, umbea, kuperuzi wasanii feki (bongo fleva) wamefanya nini jana ili wawaige wakiwa kazini, ukienda ofisini mwao kufuata huduma hakun wa kukusaidia. Cha kushangaza ukifika huko ofisini kufuata hiyo huduma utakuta watu kila mmoja kwenye computer akiperuzi wasanii wa marekani wanafanya nini. Utakaa unasuburi, ukiuwauliza utawasikia subiri niko bize.
Ni kweli mbongo_ halisi baadhi ya watu wa kuajiriwa wanatumia nafasi zao kupiga soga na kufanya mambo mengine yasiyo na tija. Hata, hivyo waliojiajiri hawako hivyo wako makini ila wengi hawasongi mbele labda kwa kukosa ubunifu na mitaji
 
Wauza ngada waliokuwa wakifanikiwa walikuwa wamejenga tabia ya kusema eti wao ndo wanaijua pesa kuitafuta, na walikuwa wakiwasema wengine eti hawajuhi kuitafuta pesa. Leo wamekamatwa kelele kisha, wamebaki kumuhandama Makonda kila kukicha
 
Ni kweli mbongo_ halisi baadhi ya watu wa kuajiriwa wanatumia nafasi zao kupiga soga na kufanya mambo mengine yasiyo na tija. Hata, hivyo waliojiajiri hawako hivyo wako makini ila wengi hawasongi mbele labda kwa kukosa ubunifu na mitaji


Ni kweli kabisa.
 
Hizi general statements zinatokana na kuangalia idadi kubwa ya watu... Wengi wetu tunajishughulisha kupata milo mitatu kwa siku ila hatusugui akili kufanya mambo makubwa kama ya akina Dangote vile.
 
Sio watanzania wote ni wavivu....Generalization yako ni kitu kibaya sana, angalau ungekuja na current data from recognizable institute kama ofisi ya taifa ya takwimu.....
 
Sio watanzania wote ni wavivu....Generalization yako ni kitu kibaya sana, angalau ungekuja na current data from recognizable institute kama ofisi ya taifa ya takwimu.....
Utafiti uliofanyika hivi karibuni na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) umebaini kwamba asilimia 71 ya watanzania wanatumia muda mwingi kufanya shughuli zisizokuwa za uzalishaji mali wala tija binafsi kwao na kwa Taifa kwa ujumla.
Akizundua taarifa ya utafiti huo leo jijini Dar es salaam Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama amesema kuwa idadi hiyo hufanya kazi zisizoleta tija kwao na taifa na muda mwingi huutumia kujihudumia binafsi kwa kulala na starehe nyingine.
Ameeleza kuwa takwimu hizo zinaonesha wazi ni kwa namna gani watanzania wanashindwa kujishughulisha katika kufanya kazi zenye kuwaingizia kipato na badala yake wanatumia muda wao mwingi kufanya shughuli zisizo za uzalishaji hasa kufanya starehe mbalimbali.
“Ndugu zangu watanzania unakuta mtu amekaa baa au anacheza “poll table” kuanzia asubuhi mpaka jioni na hujui anafanya kazi gani ya uzalishaji, ndugu zangu tuone aibu basi tujishugulishe tulijenge taifa letu ili kujiletea maendeleo yetu na nchi yetu.”
Aidha, matokeo hayo yamebainisha kuwa asilimia 18.5 ya wananchi wanafanya kazi za uzalishaji na asilimia 10.6 ni wale wanaofanya shughuli za nyumbani zisizo na malipo huku uchambuzi wa kijinsia ukionesha kuwa wanaume asilimia 23.8, wanatumia muda mwingi kwenye shughuli za kiuchumi ikilinganishwa na asilimia 13.5 ya wanawake.
Source: Ripoti: Asilimia 71 ya Watanzania hupoteza muda kufanya yasiyo na tija kwao wala Taifa - wavuti
 
Back
Top Bottom