Watanzania ni ignorants au tumelogwa? Oktoba 25, tutafanya informed decision au tutachagua tuu?

Ujinga MKUBWA SANA tulio nao Watanzania ni kusita kutumia fursa tuliyo nayo ya mfumo wa vyama vingi kuwapa mrejesho stahiki wanasiasa na vyama vyao. Tulitakiwa kutumia mfumo huu kuwaadabisha wanasiasa watende yanayostahili kuhakikisha maendeleo, utawala bora na haki vinashamiri nchini. Kwamba kwa kutumia kura zetu tuwe na uwezo wa kubadili vyama na viongozi mara kwa mara tusiporidhika na utendaji wao. Tuwaonyeshe kwamba sisi ndio wenye kauli ya mwisho katika ajira zao.

Badala yake tumekalia kushabikia vyama na watu kama vile ni suala la soka au hata dini kabisa. Tunaabudu watu na vyama badala ya kuona ni wenzetu tu tunaowapa dhamana ya uongozi wafanye kazi na kupisha wengine tukimua. Tumeishia kujenga utamaduni wa kujikomba (sycophancy) kwa watu na vyama badala ya kuwadhibiti inavyostahili. Tunawapa binadamu "gerentii" ya hatamu za dola milele na milele halafu tunashangaa sana wakitutenda na kutuita wapumbavu!

Ukweli ni kwamba kama hatutachukua hatua kamili ya kuanza kubadili vyama na uongozi wa nchi kikamilifu basi tukae tayari kwa adha zisizomithilika. Kwangu mimi CCM ikirejea madarakani mwaka huu hakuna Mtanzania atakayekuwa na stahili ya kulalamika kuhusu uongozi mbaya na manyanyaso ya dola. Kulalamikia viongozi na familia zao kutajirika kwa mtindo wa nepotism na patronage itakuwa ni wivu tu unawasumbua. Hapo tena ni kila mtu kubeba furushi lake: everyone for himself/herself and God for all of us.
 
Pasco Wa Jf Katika Ubora Wako Asiyekuelewa Jamvini Humu Ubora Wa Maandishi Yako, Ndio Hao Mbumbumbu "ignorants" Tunaowazungumzia Hapa
 
Last edited by a moderator:
Wanabodi,

Mtanisamehe sana kwa kuanza huu mjadala kwa maneno makali, kuwa ina
wezekana kabisa sisi Watanzania tulio wengi ni "ignorants!", vichwa maji kabisa!, vichwani ni weupe na watupu!, uwezo wa kufikiri kwa kina (deep thinking). na kufikiri ka tafakuri, ("logical thinking"), ni mdogo!, wengi ni sifuri kabisa, ndio maana hatuna uwezo wa kufanya maamuzi ya maana, "informed decisions", hali inayopelekea, tunapelekwa pelekwa tuu kama ling'ombe, au tufanywa mazuzu!, kiasi kwamba, wengi wetu tunadanganyika kwa viahadi vidogo vidogo ambavyo ni non issues, na immaterial, ambazo sio chanzo bali ni matokeo tuu, badala ya kudeal na issue zenyewe ambazo ndicho chanzo, kilizopelekea haya yatokanayo, havishungulikiwi, havizungumzwi!, haviguswi!.

Hii ignorance ya Watanzania ina cut across society yetu na ku reflect ndani ya kila sekta ya jamii yetu kuanzia ndani ya familia zetu, mitaa yetu, vitongoji vyetu, vyama vyetu, ndani ya bunge letu, hadi ndani ya cabinet yetu!, tuna wabunge ma ignorants mule!, tuna viongozi wetu ma ignorants ndani ya cabinet yetu!, tuna viongozi wa taasisi za umma zenye dhamana ambao ni ma ignorants hadi, tuna viongozi wetu wa vyombo vya dola ikiemo mihimili ambao pia ni ma ignotants, na wana jf wengi tuu pia ni ignorants tuu, nikiwemo mimi mwana JF, ninayeandika hapa, Pasco wa jf, pia ni ignorant tuu!, ila tofauti yangu na wengi
wa maignorants wenzetu, wao wanajikalia kimya, hivyo kuificha hiyo ignorance yao, lakini sisi wengine ambao kwa bahati mbaya sana, hatukujaliwa aibu, tunaionyesha hiyo ignorance yetu kwa ku speak out and expressing our minds, tatizo, ni, in so doing, tunajikuta tumewaambukiza ignorance, hata wengine ambao hawakuwa ignorants!. Sorry for this.

Ni kufuatia ignorance hii, Chama cha Mapinduzi, (CCM), kinaitumia ignorance hii ipasavyo kwa kuifanya ndio mtaji wake wa kupatia kura za ushindi, mwaka hadi mwaka, na October
25 tutaichagua tena CCM kwa kuipa ushindi wa kishindo!.

Hisia za kujiuliza, kama sisi ni ma ignorants au tumelogwa, ni kufuatia kuwa na mtazamo, ya kuwa haiwezekani, watu wenye akili zao timamu, wakafanyiwa mambo ya ajabu ajabu kama haya, tunayofanyia na CCM lakini bado tunaichagua CCM tena na tena!, na October
25, tutaichagua tena!.

Tulipopata uhuru miaka ya 60, maadui wetu wakuu watatu, walikuwa ni Ujinga, Umasikini na Maradhi, lakini hadi leo miaka zaidi ya 54 baada ya uhuru, sio tuu, wale maadui wakuu watatu bado wapo, bali ujinga umeongezeka mara dufu, umasikini sasa ni uliotopea, kila siku ni afadhali ya jana!, na maradhi hadi mengine ni janga, vimeongezeka afadhali ya zamani na enzi za mkoloni, bali pia, tumeongeza idadi ya maadui wakuu, wakiwemo rushwa na ufisadi, ambapo mazao yake ni pamoja na DCP, Deep Green, Meremeta, TanGold, Alex Stewart, EPA, Richimond, Escrow etc, etc.

Tulijiwekea misingi yetu mikuu minne ya maendeleo kuwa ili tuendelee, tulihitaji vitu vinne: Watu, Ardhi, Siasa Safi na Uongozi Bora!. Kwenye hiyo misingi, tulisema Pesa sio msingi, pesa ni matokeo!, hili ndilol lililokuwa kosa pekee la Mwalimu, kutofautiana na misingi ya ukweli ya uchumi, kama ilivyofundishwa na Adam Smith (land, labor, capital na interpreneureship)!. Kwenye ile misingi minne tulidharau capital kwa kudai "pesa sii msingi bali pe
sa ni matokeo!".

Watu tunao na ardhi ya kutosha, yenye rutuba, vyanzo lukuki vya maji, madini, maliasili etc etc tunazo. Tulikuwa na tatizo kidogo la utekelezaji wa siasa safi ya Ujamaa na Kujitegemea na uongozi bora, ndio maana nchi tulizopata nazo uhuru, ile miaka ya 60, wao wakiwa ni masikini wa kutupwa kuliko sisi, with nothing, kana Tiger nations, leo wako mbali!, sababu pekee iliyowafikisha wenzetu pale walipo, wakati sisi tunaendelea kupiga mark time ni Elimu!. Sisi tulitaja tuu kuwa Ujinga ni adui, lakini we never invested on Elimu because we had no capital!. Nyerere aligombana na maprofesor wa uchumi, Kina Prof. Rweyemamu, wakajitimkia zao, akagombana Edwin Mtei na IMF, WB etc matokeo sote tunayajua!.


Kitu kizuri cha ajabu kuhusu sisi Watanzania ni kujifanya kupiga kelele sana as if tunauchukia umasikini, ujinga, maradhi, rushwa na ufisadi, lakini sisi wale wale, mwaka hadi mwaka, tunawachagua watu wale wale, chama kile kile, sera zile zile, tukitegemea matokeo tofauti!, hii ni nini kama sio ignorance at the highest levels?!. Keshokutwa October
25, 2015, tunamalizia kazi, kwa kuirudisha CCM kwa ushindi wa kishindo!.

Namalizia k
wa kukumbushia hili swali, are we really this ignorant?!, kwa kuchagua tuu ili mradi ni kuchagua, or this time, around tutaonyesha tumeerevuka angalau kidogo, hivyo tutachagua kwa sababu ya kuchagua, yaani kufanya informed decision?!, na sio kujichagulia tuu alimradi tumechagua!.

Na
watakia Jumamosi Njema.

Pasco




Kukujibu swali lako, ni kwamba sisi WatanZania ni watu tuliobarikiwa sana na Mungu na ndiyo maana Mungu siku zote yuko nasi na anatulinda ktk maamuzi yetu!

Sasa sababu hasa za sisi WatanZania kuendelea kuiamini CCM pamoja na mapungufu yake yote ni kwamba hatuoni mbadala, hakuna Chama cha Siasa ambacho kinaweza kusimama leo hii na kusema mimi ni bora zaidi ya CCM kwa sababu nimefanya ABC!

Kwa mfano ni kwa nini niichague UKAWA na kuitosa CCM? Unaweza kunipa sababu ya kunishawishi?
Je, kama tu chadema yenyewe hata Mwenyekiti wake haijulikani hata anapatikanaje na hakuna jinsi unavyoweza kumtoa ni kwa nini basi nikiamini chama kama hicho kwenye kuongoza nchi?
Kama chadema ambacho miaka yote kimemshutumu Lowasa kwa Ufisadi na wote walifanya hivyo kuanzia Mwenye Chama Mtei mpaka wapiga debe akina Msigwa sasa iweje leo hii waniambie Lowasa siyo fisadi na wamkaribishe kugombea Uraisi? Kwanini niwaamini watu kama hawa kuwakabidhi nchi, unaweza kuniambia?

Hivyo kwa kifupi ni kwamba mimi nasema kinyume chake kama WatanZania tukichagua Upinzani yaani fisadi Lowasa &Co. basi tutakuwa tumelogwa, lkn kwa kuwa Mungu anatupenda, anatulinda na kutupigania hilo haliwezi kutokea mpaka hapo upinzani wa kweli utakapotokea,!

Kumbuka hii ni nchi, na Nchi haifanyiwi majaribio!

 
Ni kweli naliona hilo genge.Ndio maana mimi na watanzania wenzangu tunaona ni bora tukaendelea na hili genge tunalolijua mpaka hapo tukapopata mbadala wake kuliko kuingiza Genge jingine tena hatari zaidi.

Hivi baada ya Newton kufariki, sayansi ilisimama? Ni mawazo unatoa lakini sio sahihi. Unajua ni lini utapata mbadala wake kama wewe? Huu mbadala unaona haufai? Mtu kwenye akili timamu atachagua UKAWA sababu, mgombea wake kama ni fisadi, angekuwa kishaungana na akina Mramba. Mnadanganywa na CCM kisa waendelee kutawala na kunyonya, sayansi yoyote bila majaribio huwezi kufika. Ndo maana tunaona wazungu wanafanya makubwa sababu siku zote wana test theories zilizopo. Badilika kaka
 
Mkuu tunaomba ccm mtusaidie na kwa Kuwa mnakiri mmechoka tusaidieni watanzania mnataka watu wa eneo gani ndio waanzishe chama ndo mkione kinafaa?nakumbuka mlianza na Nccr,mkaja kwa Cuf Leo mpo na chadema na ukawa na vyote hivi mliviita majina ya ajabu ajabu,mnataka nini hasa na nchi hii?au mnatulazimisha tutafute kuwangoa kwa Nguvu?

You are missing the point; moja, si kila asiyemkubali Lowasa ni CCM. Mbili, tatizo si CDM wala NCCR wala CUF, TATIZO NI LOWASA NA GENGE ANALOLIWAKILISHA. Hao ndo CCM iliyochokwa kasoro tu sasa hivi wamekuja kwa mgongo wa CDM.
 
Akiwa amekwishatembea mikoa 13, wilaya zake zote na majimbo yote akizungumza na watanzania kwanini wamchague yeye Dkt. Magufuli amekuwa akionekana mtu anayemaanisha kile anachokizungumza ameaahidi yafuatayo mpaka sasa:-

• Ninao uwezo, ujasiri na maarifa ya kubadilisha mfumo wa uongozi na utendaji ili uwatumikie zaidi wananchi na uwezeshe uwajibikaji wa viongozi ambao si waadilifu. Maagizo haya yapo kwenye ilani yetu ya 2015-2020 na nimejiandaa kuyasimamia kwa dhati kabisa. Najua wapo watu wanasema Magufuli mzuri ila mfumo ni mbaya naomba niwahakikishie ndugu zangu mfumo wowote duniani huwekwa na mtu/watu na mtu/watu wanaweza kuubadilisha. Hivyo msiwe na hofu mimi ndiyo MAGUFULI mnanitambua kwa uadilifu na uchapakazi sitabadilika!

• Nitajenga utamaduni mpya wa viongozi kuwajibika kwa matokeo ya kazi tunazowapa. Nawahakikishia sitachelewa wala kusita kuwaweka pembeni viongozi na watendaji watakaokuwa wanatuchelewesha katika kutimiza ahadi zetu kwa wananchi. Nitahakikisha tunakuwa na mpango kazi madhubuti wa kutekeleza ahadi zetu na tutakuwa tunawajulisha wananchi kila hatua ya utekelezaji.


• Natambua ajira ni tatizo la kidunia lakini serikali yangu lazima ikabiliane nalo tena kwa ufasaha sana. Awamu yangu itakuwa ya viwanda. Ambapo serikali kwa kushirikiana na sekta binafsi Tutajenga viwanda kwa usindikaji wa samaki mwambao wa bahari ya Hindi,Ziwa Victoria na Tanganyika; Tutajenga viwanda vya saruji; nyuzi,nguo na magunia; Nyama na bidhaa za ngozi; pembejeo za kilimo; kufufua viwanda vilivyokufa au kudorora na kuweka mazingira rafiki kwa wawekezaji wa ndani na nje kuwekeza katika ujenzi wa viwanda. Kuna umuhimu pia wakutazama sheria, taratibu na kanuni zetu za ajira serikalini nitalifanya hili.


• Tumekuwa tukipambana sana kuona tunajitegemea kibajeti mfano mwaka 2005 bajeti yetu ilikuwa inategemea misaada kwa 34% na leo bajeti yetu 2015/2016 inategemea misaada kwa 8% tu. Awamu yangu tutahakikisha tunajitegemea kamili. Natambua ili tujitegemee lazima tukusanye kodi kwa ufanisi; leo tunakusanya bilioni 900 kwa mwezi toka bilioni 175 kwa mwezi 2005 awamu yangu itakusanya mara tatu zaidi. Tutapunguza misamaha ya kodi na kupunguza matumizi yasiyo ya lazima ili fedha nyingi zaidi ziende kwenye miradi ya maendeleo. Tutazipitia upya tozo za kodi ili ziwe kwenye kiwango ambacho watu wengi zaidi watalipa kodi na kwa hiari. Ikiwa hivyo na serikali tukaisimamia vyema hakika Taifa hili litapaa kimaendeleo.


• Uhakika zaidi wa mapato ndiyo unaotufanya tuseme watoto wetu watasoma bure kuanzia kidato cha kwanza hadi cha nne bure pamoja na kuimarisha miundombinu ya kitaaluma kama madarasa, madawati, vitabu, vyoo, na nyumba za walim pamoja na kuwalipa vizuri ili wafundishe kwa ari zaidi. Pamoja na kuboresha huduma za afya nchini ili zipatikane kwa haraka, gharama nafuu, karibu zaidi kwa uhakika na kuhakikisha upatikanaji wa madawa na vifaa tiba. Pia tutazingatia umuhimu wa kuwaendeleza watumishi wa kada ya afya na kuboresha maslahi yao na mazingira yao ya kazi.

• Utawala wa Rais Kikwete umejenga vyuo vikuu vikubwa viwili UDOM na Nelson Mandela Arusha. Awamu yangu ilani inaelekeza serikali kujenga viwili pia mbavyo ni Chuo Kikuu Cha Kilimo na Sayansi Shirikishi cha Mwalimu J.K.Nyerere Butiama mkoani Mara na Chuo Kikuu Cha Sayansi za Madini mkoani Shinyanga. Pamoja na kukamilisha ujenzi wa chuo kikuu cha Afyana Sayansi tumizi cha Muhimbili eneo la Mloganzila nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam. Tutakamilisha kwani elimu ya juu ina umuhimu mkubwa sana katika maendeleo ya taifa letu. Serikali yangu pia itaendelea kuongeza bajeti ya mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu na kujenga hosteli za kutosha kwa wanafaunzi waliopo katika vyuo vya umma ili wasome kwa utulivu.

• Natambua nchi yetu ya Tanzania ina utajiri mkubwa wa rasilimali. Lakini nchi kuwa tajiri kwa rasilimali sio sifa. Sifa ni kwa wananchi kuwa matajiri kutokana na rasilimali hizo kupitia mazingira mazuri yaliyowekwa na serikali ili jitihada zao za kujiendeleza ziwanufaishe zaidi. Ninawahakikishia nitaangalia upya utaratibu wa uvunaji rasilimali zetu ikibidi kupitia upya sharia zetu ili wananchi wanufaike zaidi. Pia nitahakikisha watanzania wanashiriki katika uvunaji na sio kuwa vibarua bali kama wamiliki na wawekezaji na kuona mikataba inalinufaisha taifa. Kwa kutambua rasilimali asili hizi huisha na bei zake hubadilika kila wakati tutazitumia vizuri kwa maendeleo ya wananchi hususani kujenga rasilimali watu imara katika sekta muhimu kwa ajili ya kukuza uchumi wa taifa letu kama Afya,Sayansi na Teknolojia, Gesi, mafuta, madini na Uchumi pamoja na Masuala ya ulinzi.

• Nimetumika serikalini kwa miaka 20 bila kupewa onyo, kusimamishwa wala kufukuzwa nawahakikishia sitakuwa na mzaha wa uvumilivu na watendaji wazembe ,wabadhirifu na wanaoendekeza urasimu. Nawahakikishia nitajenga utamaduni mpya wa uwajibikaji. Kutakuwa hakuna kubebana wala kujuana. Nitaimarisha mfumo mzima wa utumishi wa umma ili kuiwezesha serikali kuwatumikia vizuri zaidi wananchi.

• Nawaahidi utumishi uliotukuka, uadilifu na uchapakazi. Mtarajie serikali itakayokuwa inafanya maamuzi sahihi, kwa wakati sahihi na utekelezaji sahihi lakini kwa haraka. Mtarajie uongozi wa kidemokrasia lakini uwepo wa nidhamu serikalini na jamii nzima. Nitasimamia utawala wa sharia hakuna mtu atakayekuwa juu ya sharia na hakutakuwa na mzaha wala majadilano katika kufuata na kutii sharia za nchi. Nitapenda kuona serikali inachapa kazi na wananchi wanachapa kazitu basi! Nitalinda umoja, amani na usalama wan chi yetu kwa nguvu zote.

• Nitatumia maarifa yangu, uwezo wangu na vipaji vyangu vyote na kumtanguliza Mungu wakati wote kutetea maslahi ya Tanzania katika dunia ya leo kwa kuyaenzi mema yaliyofanywa na watangulizi wangu. Nitahakikisha seikali yangu wakati wote inasimamia uadilifu ili kuendelea kuijengea heshima nchi yetu kimataifa. Nitaimarisha uhusiano na nchi zingine lakini nitatumia muda wangu mwingi ndani ya nchi ili kuharakisha maendeleo ya watanzania.

MAGUFULI: MCHAPAKAZI, MUADILIFU NA MFUATILIAJI
HapaKaziTu!!!!!
 
Hakuna hata siku moja hicho chama chenye ubora unaotaka wewe utakiona hapa TZ, hata nyerere wakati anakabidhiwa nchi wazungu walikuwa na wasiwasi lakini walifika mahala wakatuamini wakatukabidhi nchi sasa tunasonga.

Tofauti ya kipindi hicho na sasa ni kwamba Nyerere alikuwa anawakilisha wenye nchi katika kudai uhuru kutoka kwa wageni. Suppose mtawala wa kizungu angekuja TANU na kutaka wampe uongozi wa kudai uhuru kutoka kwa wazungu wenzake, unaouna hiyo inge-make sense? Ndo scenario ya Lowasa ilivyo, tunampa fisadi na kundi lake mamlaka ya kutukomboa kutoka ufisadi, unategemea nini hapo?
 
Mimi ni Mtanzania.Siwezi kushiriki kuiuza nchi yangu kwenye hilo "Genge la wafanyabiashara lililoingia ubia na Mtei"!!Sahauni...

Genge la wafanya Biashara upo nao huko wauza ngada na wauza pembe za ndovu wanaoingiza mizigo bandarini bila kulipia kodi
 
Kwahiyo ujanja na werevu na kutokuwa ignorant na zuzu ni kuikabidhi nchi kwa hilo genge la wapiga DEAL likiongozwa na MTEI na UKOO wake???!!CCM imechoka,YES!Lakini Tanzania bado hakuna chama mbadala wa CCM.Tatizo la afya ya akili Tanzania ni kubwa kuliko inavyodhaniwa.Kama mtu anaorodhesha matatizo yake then anaona hilo genge la wapiga deal na watu wenye tuhuma lukuki Lowassa,Rostam Aziz ,Ndessapesa,mtei ndio watatuzi wa matatizo yenu.UZENI NCHI YENU KWA KARATASI.
Ndio hiyo jamaa pasco anazunguzia hapo juu hata wewe bado upo kwenye kundi hilo ili mradi umechagua mtu au chama ambacho matokeo yake hayaonekanekani kwa miaka 54. CCm ina hati mmiliki ya akili zetu?Amua leo kukombolewa mpe kura yako Lowasaa
 
Kaka Pasco. Hapa nilipo nayahuburi haya maneno yako usiku na mchana. Ujinga uliotujaa Watanzania ndio msingi wa wanasiasa wetu. Ujuha huu ndio huwapa watawala wetu kiburi cha kufanya wanayotaka. Na wanafanya kila njia tubaki wajinga ili watatutawale milele. Ila kwakua dunia haitaacha watu wake nyuma milele, basi nasi tunasukumwa kidogo kidogo na maazimio ya kimataifa kama MDG, n.k. Wacha shule za kata zifanye angalau 60% iwe imepita shule japo kuondoa uoga (maana elimu na ujuzi haipo katika misingi ya shule zetu kabisa) utakua mwanzo wa mwisho wa watawala uchwara.
Mwisho nikuondoe woga; usiogope kabisa kusema we are ignorants...hilo ni kweli kabisa iwe kwa uchunguzi au kwa maneno ya vijiweni. 80% ya Watanzania katika kila sekta ni ignorants wa kutupwa kabisa.
 
Last edited by a moderator:
You are missing the point; moja, si kila asiyemkubali Lowasa ni CCM. Mbili, tatizo si CDM wala NCCR wala CUF, TATIZO NI LOWASA NA GENGE ANALOLIWAKILISHA. Hao ndo CCM iliyochokwa kasoro tu sasa hivi wamekuja kwa mgongo wa CDM.
Wala sijui umeandika nini?
 
Kuna jamaa kila akiniona lazima apige kizinga... nimemchunia baada ya kugundua kuwa anaishabikia CCM iliyomfanya kuwa masikini wa fikra hadi mali ... Inatia kinyaa kuishabikia CCM iliyoshindwa katika kila Nyanja za kimaendeleo ..
 
Back
Top Bottom