Watanzania na maamuzi magumu

Watanzania na maamuzi magumu

unaona demu ana mtu au unajua huyu ni mke wa mtu UNAMFUATA NA KUMTONGOZA hayo ni maamuzi magumu
uNAAMBIWA NA MANGI JUMLA YA BEI YA VITU NI 65000 wewe unataka upunguziwe hadi 1000 hayo ni maamuzi magumu
 
Kuendelea kuishi tz nayo ni maamuzi magumu sana.tupongezane tu.
 
Hatujaxoea maamuzi mengine na mbaya zaidi hata tukiambiwa bado tunangangania yale2 km vile ambavyo wagumu wote watakavyofanya maamuzi magumu ya kuwachagua wagumu wao waso na haya km paka mwizi wale2 mafisi wadi ambao wote wanatangaza nia. Sioni tofauti yao mateja w pale togo street anamuona njagu anaficha uso kwa kipande cha gaxeti eti njagu asimuone!!! Walah waTZtwaliw
 
WATANZANIA NA MAAMUZI MAGUMU.

1. Huna uhakika wa kula na elfu moja pekee uliyonayo unaamua kuinywa Kiroba - Ni maamuzi magumu.

2. Huna kitanda na unaamua kuoa - Hayo pia ni maamuzi magumu.

3. Huna uwezo wa kumlisha mkeo na unampa ujauzito - Ni maamuzi magumu.

4. Shule haina waalimu unampeleka mwanao - Pia ni maamuzi magumu.

5. Daladala imejaa mpaka mlangoni na unaamua kupanda - Ni maamuzi magumu.

6. Unalipwa laki mbili unamhonga binti laki moja - Hayo ni maamuzi magumu.

7. Kama utasoma hapa na kushindwa kuweka maamuzi magumu unayoyajua - Utakuwa unamaamuzi magumu mnoo...!

8. ***
 
Back
Top Bottom