Watanzania na maamuzi magumu

Watanzania na maamuzi magumu

Salamander

JF-Expert Member
Joined
Dec 7, 2012
Posts
28,536
Reaction score
15,751
Huna uhakika wa kula na elfu moja pekee uliyonayo unaamua kuinywa kiroba-Ni maamuzi magumu.

Huna kitanda na unaamua kuoa-Hayo pia ni maamuzi magumu.


Huna uwezo wa kumlisha mkeo na unampa ujauzito-Ni maamuzi magumu.


Shule haina waalimu unampeleka mwanao-Pia ni maamuzi magumu.


Daladala imejaa mpaka mlangoni na unaamua kupanda-Ni maamuzi magumu.

Unalipwa laki mbili unamhonga binti laki moja-Hayo ni maamuzi magumu.

Kama maamuzi magumu ni kigezo cha urais karibu Watanzania wote wanafaa kuwa marais.
 
Una mshahara wa Laki 3 halafu unahonga laki 2. Hayo ni maamuzi magumu
 
Una buku 10 mfukoni unamhonga demu yote halafu unatembea kwa mguu tena mchana kutoka Magomeni (kazini) hadi Kimara Baruti (nyumbani) - Huu pia ni uamuzi mgumu!
 
Unajua kabisa nafasi ya uwaziri ilikushinda leo unataka ya urais nao ni uamuzi mgumu
 
Kutoswa na demu na kakuambia hakutaki tena wewe unaendelea kumlilia @PIA HAYO NI MAAMUZI MAGUMU
 
kamtenga chumba wife wake kwa miez6 kisa kamtuhumu jamaa malaya, na mara wife wake kawa mjamzto, jamaa hakuuliza chochote, mpaka wife kaamua kujitaliki akasepa. HAYO MAAMUZI YA JAMAA NI ZAIDI YA MAGUMU
 
Unajua kabisa huwezi kupata kura hata hamsini lakini unachukua fomu, hayo pia ni maamuzi magumu
 
Huna uhakika wa kula, lakini elfu moja pekee uliyonayo unaamua kuinywea kiroba, hayo ni maamuzi magumu.

Huna hata kitanda unaamua kuoa, hayo pia ni maamuzi magumu.

Huna uwezo wa kumlisha mkeo lakini unampa ujauzito, hayo ni maamuzi magumu.

Shule haina walimu na vifaa vya kufundishia lakini unampeleka mwanao, hayo pia ni maamuzi magumu.

Daladala imejaa mpaka mlangoni lakini unaamua kupanda, hayo ni maamuzi magumu.

Unalipwa mshahara laki mbili lakini unamhonga binti laki moja hayo ni maamuzi magumu.

Kama maamuzi ni kigezo cha URAIS basi Watanzania wote wanafaa kua marais wa nchi hii!!!

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Huna uhakika wa kula lakini elfu moja pekee uliyo nayo unaamua kuinywea kiroba hayo ni maamuzi MAGUM
Huna hata kitanda unaamua kuoa hayo pia ni maamuzi MAGUM
Huna uwezo wakumlisha mkeo lakini unampa ujauzito hayo ni maamuzi MAGUM
Shule haina walim na vifaa vya kufundishia lakini unampeleka mwanao hayo pia ni maamuzi MAGUM
Daladala imejaa mpaka mlangoni lakini unaamua kupanda hayo ni maamuzi MAGUM
Unalipwa mshahara laki mbili lakini unamhonga binti laki moja hayo ni maamuzi MAGUM
Kama maamuzi nikigezo cha URAIS bas watanzania wote wanafaa kua MARAIS wa nchi hii!!!

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Kuandika neno zima "MAGUM", na kuacha herufi moja 'U' bado ni maamuzi magumu!
 
unajua ufisadi wa Epa, Esklow, Rada, Richmond Iptl, Mikataba ya Gesi na Madini.. bado unachagua ccm

ni maamuzi magumu.
 
kufanya maamuzi magumu kunahita tafakari ngumu
 
Huna uhakika wa kula na elfu moja pekee uliyonayo unaamua kuinywa kiroba-Ni maamuzi magumu.
Huna kitanda na unaamua kuoa-Hayo pia ni maamuzi magumu.
Huna uwezo wa kumlisha mkeo na unampa ujauzito-Ni maamuzi magumu.
Shule haina waalimu unampeleka mwanao-Pia ni maamuzi magumu.

Daladala imejaa mpaka mlangoni na unaamua kupanda-Ni maamuzi magumu.

Unalipwa laki mbili unamhonga binti laki moja-Hayo ni maamuzi magumu.

Kama maamuzi magumu ni kigezo cha urais karibu Watanzania wote wanafaa kuwa marais.
 
kusoma huu uzi pia ni maamuzi magumu
 
Back
Top Bottom