Watanzania na CCM: Vipi, Dr.Regnald Mengi Urais 2015?

Watanzania na CCM: Vipi, Dr.Regnald Mengi Urais 2015?

mshumbue-soi

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2013
Posts
1,842
Reaction score
1,148
Heshima kwenu.

Tanzania kwa awamu ijayo ili kusababisha ukuaji wa Uchumi kuwafikia Wananchi wa kawaida au wakipato cha chini.

Na ili kuweza kutoa ajira kwa vijana ambao ndo wengi kwa mujibu wa sensa

Na ili kuweza kusababisha Uvunaji wa Rasilimali hasa Gesi kuwanufaisha wananchi wa kawaida

Na vilevile kuleta ustawi wa Jamii

Nitoe hoja kuna umuhimu wa Dr. Reginald Mengi akatuongoza ktk kuzitatua Changamoto zinalokabili Taifa letu.

1,Anauwezo wa kuitoa jamii from zero to hero.
2.Ana busara ya hali ya juu hana utani kwa maamuzi ya maslahi ya wengi.
3.Anawapenda watanzania kile anachopata kimevuka mipaka ya ndugu, jamaa na kuwafikia watanzania bila ubaguzi wowote.
4.Amethibitisha ni problem solver wa jamii.
5.Amewatoa watanzania mbali wakawa na matumaini

Itoshe kusema waliokaribu wamsihi kwa niaba yangu yetu tunaoamini uongozi ni kuonyesha njia sio kuchekacheka, utani na kujilimbikizia mali WAMSIHI ajiandae na CCM waache utani tulitazame taifa letu tumwombe atuongoze kupambana na umaskini, ujinga na maradhi
 
Mh: msemaji naunga mkono kwa 100% Dr Mengi anaweza kama si kuzuga ila kupitia vyama viwili vya siasa CHADEMA na NCCR - REFORMS
 
gongo mbaya sana unamjua kweli mengi wewe au unamsikia kwenye redio tu.
 
umekaa kisiasa zaidi...
ungesema tanzania inatakiwa iconcentrate kwenye elimu, walimu wawepo mashuleni, wanasayansi wapewe kipaumbele, tubase kwenye science and technology kuliko siasa, serikali isomeshe wanafunzi bora nje ya nchi, tujaribu kutumia raw materials wenyewe kumanufacture products na kufanya exports kuliko tunavoimport sasa hivi ningekuelewa..
Hizi za nani anafaa ni siasa tu... swala ni nini kinafaa ili kuinyanyua tanzania.. binadamu yeyote yule anaweza kubadilika ndani ya dakika, we are all greedy, hiyo ni natural... We unayetaka apewe urais unamjua vizuri?? hakuna amjuaye mtu kuliko mtu mwenyewe
 
siku mengi akiwa rais vitaru vya mafuta na gesi vyato vitakuwa vyake.
 
kila mtu tunamuona hafai kuwa rais ,inabidi tuache ushabiki wa kichama,tuungane kwa pamoja kuchagua mtu ambaye anaweza kutuunganisha watanzania wote na kuimarisha taasisi zote muhimu.tupo kwenye kipindi kibaya mno cha ombwe la uongozi,
 
mshumbue-soi tunaemjua walau kidogo Mengi wala hatupati tabu kabisa, fuatilia historia yake vizuri utangundua ni hivi karibuni ndio ameanza kutafuta umaarufu ili aje afanye hicho alichokutuma wewe uje ufanye, Mengi hana busara sena muonekano na sura yake ndio vinawaficha wengi. All in all aje agombee alafu ataona matokeo yake
 
Last edited by a moderator:
2010 was 70!, 2015 will be 75!, this is the age of the beginning of "mind incapacitation!"
Do we real need a president this old?, nadhani age ya EL is the last we can accommodate!.
Pasco
 
Nchi hii kwa sasa mtu yoyote anaweza kuwa raisi hata mimi mwenyewe naweza hivyo naunga mkono hata Mengi anaweza pia.
 
Heshima kwenu.

Tanzania kwa awamu ijayo ili kusababisha ukuaji wa Uchumi kuwafikia Wananchi wa kawaida au wakipato cha chini.

Na ili kuweza kutoa ajira kwa vijana ambao ndo wengi kwa mujibu wa sensa

Na ili kuweza kusababisha Uvunaji wa Rasilimali hasa Gesi kuwanufaisha wananchi wa kawaida

Na vilevile kuleta ustawi wa Jamii

Nitoe hoja kuna umuhimu wa Dr. Reginald Mengi akatuongoza ktk kuzitatua Changamoto zinalokabili Taifa letu.

1,Anauwezo wa kuitoa jamii from zero to hero.
2.Ana busara ya hali ya juu hana utani kwa maamuzi ya maslahi ya wengi.
3.Anawapenda watanzania kile anachopata kimevuka mipaka ya ndugu, jamaa na kuwafikia watanzania bila ubaguzi wowote.
4.Amethibitisha ni problem solver wa jamii.
5.Amewatoa watanzania mbali wakawa na matumaini

Itoshe kusema waliokaribu wamsihi kwa niaba yangu yetu tunaoamini uongozi ni kuonyesha njia sio kuchekacheka, utani na kujilimbikizia mali WAMSIHI ajiandae na CCM waache utani tulitazame taifa letu tumwombe atuongoze kupambana na umaskini, ujinga na maradhi
Reginald Mengi ni Nduma kuwili!!
1. Anampinga Waziri Mhongo lakini anampenda Kikwete Kuliko Watanbzania.
2.Amepiga marufuku magazeti yote kuandika habari za upungufu wa Kikwete huku yeye akiwa wa Kwanza kutetea uhuru wa vyombo vya habari
3. Anataka wazawa wamiliki mali wakati yeye mwenyewe viwanja vyake amemuuzia Shubashi Patel alipatwa kutajwa kuwa fisadi papa na Mengi huyo huyo.
4 Mengi alikuwa mzee wa kanisa la KKT Azania Front lakini wakati huo huo anaingia misikini na kuswali kama muislamu kutafuta uaris unaosema wewe.
5.Anajifanya yupo CHADEMA lakini kapewa kibali na CCM kiasi cha kuaminika kuongea na mabalozi wa nchi mbalimbali kama raisi.
6.Hapo utagundua kuwa Mengi ana kaserikali kake!!
7.Ulisha wahi kuona wapi mpinzani ana aminika na CCM???
 
2010 was 70!, 2015 will be 75!, this is the age of the beginning of "mind incapacitation!"
Do we real need a president this old?, nadhani age ya EL is the last we can accommodate!.
Pasco

Pasco,

Hebu kuwa mkweli, hivi mbona ni kuwadhihaki na kuwatukana watanzania, huyu mtu wa mipasho na kutafuta totoza umri wa mjuu wake awe rais wa Tanzania?

Wapeni heshima watanzania, mgesema apendekezwe awe raisi wa heshima wa MISS TANZANIA, hapo mbarikiwe
 
Naona mnatafuta mbadala wa Lowassa!
Mshaona maji yamezidi unga eeh!

This time hata muazime shetani kutoka kuzimu kama mgombea wa CCM mtajuta mbele ya Dr W.P.Slaa!

Mtafuteni Salary Slip atawasimulia!
 
Back
Top Bottom