Mimi ni mtanzania na nimemuelewa.Ni kweli tunapenda kujadili sana viungo vyetu vya uzazi na maeneo yaliyo jirani yake.
Umaarufu wa mwanaume umekuwa ni katika uwezo wake wa kufanya ngono na siyo ubunifu wa kisayansi nateknolojia!Angalia tu majukwaa husika uone ushiriki wetu.
Tunapenda sana pesa kwa ajili ya starehe lakini hatupendi kazi!
Tuache kutukana kwani maoni ya mleta uzi yanaweza kuwa yana maana kwetu iwapo tutajitazama wenyewe kuona kama taswira hiyo ni ya kweli basi tuichukue kama changamoto kwetu,tuifanyie kazi bila kelele,siku moja utawaona wakitoa maoni tofauti na hayo.