Watanzania hatuna budi kujivunia watu hawa

Watanzania hatuna budi kujivunia watu hawa

daah...mleta uzi uko poa kweli?? sijakusoma yaani
 
Kwanza hongera kwa kuwa umeonyesha unamkubali Dr Magufuri, ndani ya CCM kwenyewe kuna viongozi wanajua kabisa jamaa akishika madaraka hatawavumilia wakileta upuuz.

Ndio namkubali. Lakini kura yangu hapati akiwa ccm labda ahamie ukawa kuongeza nguvu kampeni za Lowasa ili tuizike ccm kwa pamoja.
 
Mara nyingi imezoeleka kwamba kitu ukiwa nacho huwezi ona umuhimu wake mpaka pale kitakapotoweka...

Nchi yetu imejaaliwa kuwa na baadhi ya watu ambao ni hazina kwa taifa letu, wale wanaowaponda watu hawa basi kwa namna moja ama nyingine either wana maslahi yao binafsi, chuki, wivu au wanawakubali kiaina Sema unafiki tu unawasumbua mioyoni mwao.

1,Dr Magufuli
Hakuna mtu asiyetambua michango wake kwa taifa hili, katika wizara zote alizowahi kuziongoza ameziendesha kwa ufanisi mkubwa sana, ni mtu makini, asiyeyumbishwa hovyo hovyo, anayesimamia kile anachokiamini, mchapakazi, mwenye kuzingatia na kusimamia ipasavyo maadili na sheria za kazi.

Yeye naye ni binadamu hawezi kuwa perfect 100% ana mapungufu yake kama binadamu wengine lakin ni mmoja kati ya viongozi bora kuwahi kutokea kwenye nchi hii ukilingnisha na wale tulionao na ambao tumeshawahi kuwa nao.

Kwa bahati nzuri kuna watu wameona bidii yake ktk kulitumikia taifa hili na wakamchagua kugombea urais nawapongeza sana maana waliona mbali na Inshallah! kwa uwezo wa Mungu Mwenyezi ndiye Rais wetu mtarajiwa.

2,Diamond Platinum,
Tanzania kiukweli kwa kipindi kirefu tumekuwa hatuna kitu tunachoweza kujivunia linapokuja suala la michezo na burudani,kuanzia mpira wa miguu, netball, ridhaa, muziki nk... Diamond ameweza kuitanganza nchi yetu vyema ktk tasnia ya burudani, sasa hiv Afrika nzima anajulikana kutokana na mafanikio yake kimuziki, sasa hiv hata ukiwa Ulaya ukaulizwa unatoka nchi gani kama lugha haipandi vyema ukisema tu Diamond Plutnum Nana! najulikana tu umetoka Tanzania, hatuna budi kumpongeza na kujivunia kijana huyu kwani ni hazina kwa taifa letu.

Pia amekua mfano kwa vijana wengi kuwaonyesha kwamba muziki unaweza kuwa kazi inayoheshimika na yenye kipato kikubwa endapo tu utaifanya kwa weledi na heshima zote.... Tuwaenzi Watu Hawa Pasipo Kusubiri Mpaka Waondoke Ndio Tuanze Kutoa Sifa Na Pongezi Za Kinafiki.

PLEASE LET US KEEP ON BEING PROUD OF THESE INFLUENTIAL PEOPLE.

nilifikiri unaandika kitu cha maana,hivi unajua maana ya MTU influencial?
 
Sisi vijana wa Tanzania kura zetu zote tutampa Lowasa... Lowasa atatuletea ajira kwa vijana na elimu bure mpaka chuo kikuu... Lowasa ndio tumaini pekee la vijana
Rudi ufute post yako, Lowasa chali
 
Huyu kibarua wa mr. Washroom Liquor padlocks atutilee ushuzi hapa. Ahhh najuta kupeleka macho yangu kwenye hii article na kupotexa muda wangu. Next time use ur brains not ur masa......
 
Hakuna umasikini mbaya kama umasikini WA mawazo
 
Hakuna umasikini mbaya kama umasikini WA mawazo

Subir baada ya Oct 29 ndo utanielewa vizur maana kwa sasa nahis ubongo wako umezungukwa na masizi & ukungu.
 
Ndio namkubali. Lakini kura yangu hapati akiwa ccm labda ahamie ukawa kuongeza nguvu kampeni za Lowasa ili tuizike ccm kwa pamoja.

Tayari mafisadi wametinga ukawa kumechafuka watu mahiri kisiasa wanakimbia ukawa makufuli hawezi kujivunjia heshima yake kujiunga na kambi ya fisadi
 
Atajuta maana kapoteza mengi sana ikiwemo fedha nying tu


1390616702918272.jpg
 
Tuendelee Kujivunia Watu Hawa,Maana Ni Zawadi Tuliyopewa.
 
Back
Top Bottom