Watanzania hatuna budi kujivunia watu hawa

Watanzania hatuna budi kujivunia watu hawa

Marco Polo

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2014
Posts
13,345
Reaction score
21,243
Mara nyingi imezoeleka kwamba kitu ukiwa nacho huwezi ona umuhimu wake mpaka pale kitakapotoweka...

Nchi yetu imejaaliwa kuwa na baadhi ya watu ambao ni hazina kwa taifa letu, wale wanaowaponda watu hawa basi kwa namna moja ama nyingine either wana maslahi yao binafsi, chuki, wivu au wanawakubali kiaina Sema unafiki tu unawasumbua mioyoni mwao.

1,Dr Magufuli
Hakuna mtu asiyetambua michango wake kwa taifa hili, katika wizara zote alizowahi kuziongoza ameziendesha kwa ufanisi mkubwa sana, ni mtu makini, asiyeyumbishwa hovyo hovyo, anayesimamia kile anachokiamini, mchapakazi, mwenye kuzingatia na kusimamia ipasavyo maadili na sheria za kazi.

Yeye naye ni binadamu hawezi kuwa perfect 100% ana mapungufu yake kama binadamu wengine lakin ni mmoja kati ya viongozi bora kuwahi kutokea kwenye nchi hii ukilingnisha na wale tulionao na ambao tumeshawahi kuwa nao.

Kwa bahati nzuri kuna watu wameona bidii yake ktk kulitumikia taifa hili na wakamchagua kugombea urais nawapongeza sana maana waliona mbali na Inshallah! kwa uwezo wa Mungu Mwenyezi ndiye Rais wetu mtarajiwa.

2,Diamond Platinum,
Tanzania kiukweli kwa kipindi kirefu tumekuwa hatuna kitu tunachoweza kujivunia linapokuja suala la michezo na burudani,kuanzia mpira wa miguu, netball, ridhaa, muziki nk... Diamond ameweza kuitanganza nchi yetu vyema ktk tasnia ya burudani, sasa hiv Afrika nzima anajulikana kutokana na mafanikio yake kimuziki, sasa hiv hata ukiwa Ulaya ukaulizwa unatoka nchi gani kama lugha haipandi vyema ukisema tu Diamond Plutnum Nana! najulikana tu umetoka Tanzania, hatuna budi kumpongeza na kujivunia kijana huyu kwani ni hazina kwa taifa letu.

Pia amekua mfano kwa vijana wengi kuwaonyesha kwamba muziki unaweza kuwa kazi inayoheshimika na yenye kipato kikubwa endapo tu utaifanya kwa weledi na heshima zote.... Tuwaenzi Watu Hawa Pasipo Kusubiri Mpaka Waondoke Ndio Tuanze Kutoa Sifa Na Pongezi Za Kinafiki.

PLEASE LET US KEEP ON BEING PROUD OF THESE INFLUENTIAL PEOPLE.
 
Tunajivunia magufuli kwa kuuza nyumba za serikali kwa hawara zake na kununua meli mbovu na ya zamani ya Bagamoyo
 
Kawaambie hao watu wako,hasa LI_DIAMOND kuwa kuna maisha nje ya siasa.
Kura tutampa LOWASSA na DIAMOND tuzo za kimataifa na hata za ndani ATAZISIKIA kwa wengine!.
WASISITIZIE wawakumbuke MARLOW na Mr Nice maana wana hali mbaya mno!.
 
Sisi vijana wa Tanzania kura zetu zote tutampa Lowasa... Lowasa atatuletea ajira kwa vijana na elimu bure mpaka chuo kikuu... Lowasa ndio tumaini pekee la vijana

Tatizo sio elimu bure mpaka chuo ndugu bali njia atakazotumia Ili hiyo elimu bure mpaka chuo kikuu ipatikane... Lowasa anazo shule zake anaziendesha wanafunz ktk hizo shule mbona hawasomi bure? Na Ada wanayolipa kwa mwaka ww, wadogo zako ama wanao mnasoma shule ya kata na diploma juu.... Shtuka ww sio kila unachoambiwa unakubali tu uwe unachanganya na zako japo kidogo tu.
 
ah ah ah ab kweli nouma sana, Tz inajulikana africa nzima sababu ya diamond, jeh xplastaz walioimba cypher BET ambayo inajulikana ulimwengu mzima utasemaje!! mihemko ni hatari sana
 
Ni Lowassa tu, labda ulilenga kulinganisha magufuli na diamond kwenye jukwaa la fiesta
 
Kawaambie hao watu wako,hasa LI_DIAMOND kuwa kuna maisha nje ya siasa.
Kura tutampa LOWASSA na DIAMOND tuzo za kimataifa na hata za ndani ATAZISIKIA kwa wengine!.
WASISITIZIE wawakumbuke MARLOW na Mr Nice maana wana hali mbaya mno!.

Sio kosa lako unahitaji kuelimishwa tu... Katiba ya nchi haimzuii mtu kuonyesha hisia zake kwa chama akipendacho.. Mbona mmeanza kumchukia kitambo tu na bado nyota yake inazidi kung'aa?... Alafu hao wasanii uliowataja kamwe usiwalinganishe na Diamond hata kidogo, Platinum Ni habar nyingine leo akisema aache muziki anauwezo wa kulisha na kusomesha familia yenu yote.
 
elimu ndio maisha.
bila elimu hata mziki itakua mgumu.
chagua elimu
chagua UKAWA ,
chagua LOWASA.
 
Tatizo ni kuwa ukimkubali Magufuli ni kuikubali ccm, ccm haitakiwa chini ya jua, ni kichefu chefu.
 
Tatizo ni kuwa ukimkubali Magufuli ni kuikubali ccm, ccm haitakiwa chini ya jua, ni kichefu chefu.

Kwanza hongera kwa kuwa umeonyesha unamkubali Dr Magufuri, ndani ya CCM kwenyewe kuna viongozi wanajua kabisa jamaa akishika madaraka hatawavumilia wakileta upuuz.
 
Back
Top Bottom