n00b
JF-Expert Member
- Apr 10, 2008
- 1,006
- 2,667
KIKOSI maalumu cha vyombo vya usalama chini ya Jeshi la Polisi, kimewatia mbaroni jijini Dar es Salaam watuhumiwa watano muhimu wa mauaji ya Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza, Liberatus Barlow.
Habari za uhakika kutoka vyanzo vyetu vya ndani zimethibitisha kukamatwa kwa watuhumiwa hao muhimu ambao wanatarajiwa kuhojiwa na kusafirishwa kwenda Mwanza kushitakiwa.
Gari aina ya HILUX (T 777 BFY) linalodaiwa hayati RPC Liberatus Lyimo Barlow wa Mwanza, alikuwa akiendesha siku mauti yake yalipomkuta kwa kuuawa papo hapo kwa kupigwa risasi na watu wanaosadikiwa kuwa ni MAJAMBAZI Kitangiri Jijini Mwanza Tar 13/Oktoba/2012.
Hii ni developing story kutoka - Watano mbaroni Dar wakihusishwa na mauaji ya RPC Barlow | Fikra Pevu
Habari za uhakika kutoka vyanzo vyetu vya ndani zimethibitisha kukamatwa kwa watuhumiwa hao muhimu ambao wanatarajiwa kuhojiwa na kusafirishwa kwenda Mwanza kushitakiwa.
Gari aina ya HILUX (T 777 BFY) linalodaiwa hayati RPC Liberatus Lyimo Barlow wa Mwanza, alikuwa akiendesha siku mauti yake yalipomkuta kwa kuuawa papo hapo kwa kupigwa risasi na watu wanaosadikiwa kuwa ni MAJAMBAZI Kitangiri Jijini Mwanza Tar 13/Oktoba/2012.
Hii ni developing story kutoka - Watano mbaroni Dar wakihusishwa na mauaji ya RPC Barlow | Fikra Pevu
IJUMAA, OCTOBA 26, 2012 | NA JOHN MADUHU, MWANZA
*Yumo mwanamke mmoja, wanaume wanne
JESHI la Polisi nchini, limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa watano wanaodaiwa kuhusika na kifo cha aliyekuwa Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Mwanza, marehemu Liberatus Barlow. Pia jeshi hilo limefanikiwa kukamata bunduki iliyotumika kumuua kamanda huyo.
Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba, aliwambia waandishi wa habari jijini Mwanza jana kuwa, watuhumiwa hao walikamatwa jijini Dar es Salaam ambako walikimbilia baada ya mauaji.
Katika mkutano huo, Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Said Mwema, naye alikuwapo.
Aliwataja waliohusika na mauaji hayo ambao bado wako jijini Dar es Salaam kabla ya kusafirishwa kwenda Mwanza, kuwa ni Muganyizi Peter (36) ambaye alitajwa na wenzake kuwa ndiye aliyefyatua risasi iliyomuua Kamanda Barlow.
Watuhumiwa wengine ni Chacha Mwita (50), Majige Marwa (48), Edward Kasutwa ambaye umri wake bado haujafahamika na mwanamke mmoja, Bhoke Mwita (42).
Pamoja na idadi hiyo, alisema Jeshi la Polisi bado linawasaka watuhumiwa wengine wawili waliokuwa katika tukio hilo.
Kwa mujibu wa DCI Manumba, kabla ya tukio hilo la mauaji, watuhumiwa hao ambao ni majambazi walikuwa wamefanya matukio matatu ya ujambazi katika maeneo tofauti jijini Mwanza kwa kupora vitu mballimbali kabla ya kukutana na Kamanda Barlow.
Alisema kwamba, watuhumiwa hao walifanya ujambazi kwa kuvamia Baa ya New Tuliza iliyopo eneo la Rumala majira ya saa nne usiku kwa kupora pombe na simu za wateja na kuondoka.
"Baadaye walivamia super market na kupora vitu mbalimbali na baadaye kumvamia mama mmoja na kumpora simu.
"Baada ya tukio hilo, ndipo walikutana na Kamanda Barlow na kumuua kwa kumpiga risasi shingoni kwa kutumia bunduki aina ya short gun na kufariki papo hapo.
"Walipokutana na Kamanda Barlow, watu hao walikuwa wakielekea Kitangiri kupumzika na walipomulikwa na taa za gari la kamanda, walimvamia wakati kamanda akigeuza gari na kuanza majibishano.
"Tukio hilo lilimfanya Kamanda achukue redio yake kwa ajili ya kutoa taarifa kwa wasaidizi na hapo ndipo walipomuua na haya ni kutokana na maelezo yao baada ya kuwahoji," alisema.
Akizungumzia namna polisi walivyofanikiwa kuwatia nguvuni watuhumiwa hao, alisema Jeshi la Polisi liliamua kujipanga kikamilifu kwa kuunda vikosi mbalimbali vya ukamataji na kuhoji pamoja na kikosi cha kufuatilia matukio yote muhimu ya simu ndani na nje ya nchi.
Alisema kuwa, polisi walifanikiwa kupitia kikosi cha mawasiliano, kukamata simu iliyokuwa ikitumiwa na mwanamke aliyekuwa na Kamanda Barlow ambayo iliporwa na majambazi hayo wakati wa tukio na baadaye kuanza kutumiwa na mwanamke mmoja jijini Dar es Salaam.
"Baada ya polisi kumfuatilia mwanamke huyo, alitoa ushirikiano ambao ulifanikisha kuwakamata watuhumiwa hao wakiwa jijini Dar es Salaam na walikutwa na silaha hiyo.
"Inasemekana pia watu hao walikuwa wamehusika na tukio la uporaji wa fedha katika kiwanda kimoja jijini Dar es Salaam.
"Baada ya kuwakamata watuhumiwa hao, walikiri kuhusika na tukio hilo la mauaji ya Kamanda Barlow pamoja na kukiri kuhusika na matukio mbalimbali ya mauaji na uhalifu katika maeneo mbalimbali hapa nchini," alisema DCI Manumba.
Naye IGP alisema Jeshi la Polisi bado liko imara na limeimarika zaidi baada ya tukio hilo na kuonya kuwa halitawaonea huruma wahalifu.