Watangazaji wa E-Fm na mada zisizo na tija

Sep 4, 2016
44
28
Jamani wandishi wa habari, leo hii ni mara ya pili nasikia mkiweka mada zisizo na maana kwenye chombo cha habari e-fm.

Mfano leo nimesikia mnajadili habari kuhusu wanawake weusi na wanawake weupe kanda ya ziwa, kwanini mwanamke mweupe anatolewa mahari kubwa kuliko mweusi. Waendesha mada ni Gerald Hando, Adera, na wengine.

Maoni yangu hii mada iondoeni haraka iwezekanavyo kwa sababu zifuatazo:

1. Haina maana wala haijengi jamii ila inatengeneza matabaka kati ya weusi na weupe, jambo hili mnaliona kama ni dogo lakini linasababisha psychological tortures kwa wasiofahamu na kujifahamu. Unapo weka mada yoyote kwenye chombo cha habari jiulize swali naweka mada hii so what? Ninavyoona swali hili halikuzingatiwa na waanzisha mada hivyo nashauri itolewe na isisikike tena. Tukiendekeza mambo haya mtaleta mada za mwanamke mnene na mwanamke mwembamba, msukuma na mmakonde haya mambo hayafai

2. Nashauri kina mama wanawake wakemee mada za namna hii hazina maana ila ni kuwadhalilisha tu.

3. Michael Jackson alifikia sehemu akajibadilisha akawa na pua ndefu na nyembamba kwa sababu ya mambo kama haya ya kijinga. Walikuwa wanamwambia anapua nene naye akaona bora atafute pua nyembamba.

Mwisho naomba hawa walioanzisha mada hii wahakikiwe vyeti vyao.
 
Siyo kanda ya ziwa tu hata wamasai wana hiyo kasumba.lengo lao ni kuondoa hiyo tabaka ili mweusi na mweupe wawe sawa
 
Siyo kanda ya ziwa tu hata wamasai wana hiyo kasumba.lengo lao ni kuondoa hiyo tabaka ili mweusi na mweupe wawe sawa
Hilo sio lengo kama wana lengo hilo approach yao ni hovyo ndio maana wanatakiwa kukaguliwa vyeti. Huwezi ukawa na lengo la kuondoa jambo harafu ukawa unalijadili kwa namna hiyo. Wamekosea sana approach. Kama wanataka kukomesha tabia hiyo wange mleta mtalaamu akaelimisha jamii na kukemea tabia hiyo.
 
Siyo kanda ya ziwa tu hata wamasai wana hiyo kasumba.lengo lao ni kuondoa hiyo tabaka ili mweusi na mweupe wawe sawa
Umewasikiliza lakini wanavyo jadlli hilo jambo, wanatafuta na advantages za watu weupe na disadvantages za weusi. Huo ni ujinga bora waweke mambo ya maana tusikilize mfano waweke hata habari za mbuga za wanyama, faru jonh au faru ndugai kuliko kutuwekea ujinga huu redioni
 
Jamani wandishi wa habari, leo hii ni mara ya pili nasikia mkiweka maada zisizo na maana kwenye chombo cha habari e-fm. Mfano leo nimesikia mnajadili habari kuhusu wanawake weupe na wanawake weupe kanda ya ziwa, kwanini mwanamke mweupe anatolewa mahali kubwa kuliko mweusi. Waendesha maada ni gerald hando, Adera, na wengine
Maoni yangu hii maada iondoeni haraka iwezekanavyo kwa sababu zifuatazo:
1. Haina maana wala haijengi jamii ila inatengeneza matabaka kati ya weusi na weupe, jambo hili mnaliona kama ni dogo lakini lina sababisha psychological tortures kwa wasio fahamu na kujifahamu. Unapo weka maada yoyote kwenye chombo cha habari jiulize swali naweka maada hii so what???. Ninavyo ona swali hili halikuzingatiwa na waanzisha maada hivyo nashauli itolewe na isisikike tena. Tukiendekeza mambo haya mtaleta maada za mwanamke mnene na mwanamke mwembamba, msukuma na mmakonde haya mambo hayafai
2. Nashauri kina mama wanawake wakemee maada za namna hii hazina maana ila ni kuwa zalilisha tu.
3. Michael Jackson alifikia sehemu akajibadilisha akawa na pua ndefu na nyembamba kwa sababu ya mambo kama haya ya kijinga. Walikuwa wanamwambia anapua nene naye akaona bora atafute pua nyembamba.

Mwisho naomba hawa walio anzisha maada hii wahakikiwe vyeti vyao.

Sio kwamba wanapromote urangi.Huoni kwamba hiki ni kitu ambacho lazima kizue mjadala mkuu ?,iwapo kama kweli kipo huko kwa kina ngosha?.
Hata sisi wengine tulipenda kujua why weupeweupe ni lulu.
Ila to be honest weupe weupe unavutia.In reality unakubaliana nami kwamba kuna rangi ni nzuri zaidi ya nyingine?,namaanisha rangi za kawaida blue,green,red nk
 
Sio kwamba wanapromote urangi.Huoni kwamba hiki ni kitu ambacho lazima kizue mjadala mkuu ?,iwapo kama kweli kipo huko kwa kina ngosha?.
Hata sisi wengine tulipenda kujua why weupeweupe ni lulu.
Ila to be honest weupe weupe unavutia.In reality unakubaliana nami kwamba kuna rangi ni nzuri zaidi ya nyingine?,namaanisha rangi za kawaida blue,green,red nk
Hujitambui hilo ndio tatizo lako kubwa sana. Jambo hilo kama lipo tunaomba mtu aende field akafanye research ya namna hiyo harafu aje na data. Na akija na data kutoka kwenye tafiti aje na kukemea tabia hiyo, kwasababu haijengi.
Siku zote Mh Raisi anasema wekeni mambo ya maana. Sasa ukisha jua mwanamke mweupe anafaa harafu??. Jamani wekeni vitu vinavyojenga.

Watu tunahangaika kutafuta namna ya kupata mlo sio kusikilia ujinga huo, je tutakula rangi???????.
 
Wizara ya habari iingilie kati watu wasio waandishi wa habari kutangaza vipindi redioni..ni Tanzania tu ambapo mtu anatoka kwenye uigizaji na kuwa mwandishi wa habari...mifano ipo mingi, kuanzia clouds xxl ni promotion ya bangi na ukiukwaji mkubwa wa maadili...akina kicheko hakuna jipya ni matusi yasio na ishu...

save our future generation...radio zirudi kwenye maadili.
 
content monitoring must put in place...shilawadu wolper anasema yupo tayari kitembea na mume wa mtu ili ajue kama k yake inanuka?? really tv zinefikia huko??? watangazaji vihiyo watoke kwenye medias
 
Hujitambui hilo ndio tatizo lako kubwa sana. Jambo hilo kama lipo tunaomba mtu aende field akafanye research ya namna hiyo harafu aje na data. Na akija na data kutoka kwenye tafiti aje na kukemea tabia hiyo, kwasababu haijengi.
Siku zote Mh Raisi anasema wekeni mambo ya maana. Sasa ukisha jua mwanamke mweupe anafaa harafu??. Jamani wekeni vitu vinavyojenga.

Watu tunahangaika kutafuta namna ya kupata mlo sio kusikilia ujinga huo, je tutakula rangi???????.

Yaani we ndio kobe wa baharini hayo ni mambo ya kijamii yapo katika jamii zetu hivo kujadiliwa ni kawaida saa nyingine akili lazima irelax ina maana wewe 24/7 unawaza kutafuta mlo tu nothing else? Na kutafuta kote mlo bado umekonda hivo huo ulioandikia hii thread ni mkono au mninga?
 
hiyo station hivi inasikika dar tuu eeh?
Pwani, Dar,Naanza.Na pia mwaka huu wa naenda mikoa mwingine 10.Ni radio inayomkosesha usingizi Ruge..Wamejipanga wana jua Sio kama yule Hassan Ngoma wa 360 kuvamia mazungumzo ya wenzake Na kujifanya anajua kila kitu.E- FM Ni Kwi kwi!!!
 
Umewasikiliza lakini wanavyo jadlli hilo jambo, wanatafuta na advantages za watu weupe na disadvantages za weusi. Huo ni ujinga bora waweke mambo ya maana tusikilize mfano waweke hata habari za mbuga za wanyama, faru jonh au faru ndugai kuliko kutuwekea ujinga huu redioni

Hata nami nimesikia ni ujinga mtupu hadi kuna mwanamke mmoja anadai kwamba wanawake weusi hawapendezi wanapovaa nguo ila weupe wanapendeza hapo ndio nilipochoka na kuchoka.
 
Yaani we ndio kobe wa baharini hayo ni mambo ya kijamii yapo katika jamii zetu hivo kujadiliwa ni kawaida saa nyingine akili lazima irelax ina maana wewe 24/7 unawaza kutafuta mlo tu nothing else? Na kutafuta kote mlo bado umekonda hivo huo ulioandikia hii thread ni mkono au mninga?
Kwa akili yako kila jambo lililoko kwenye jamii linatakiwa kuwekwa redioni???. Nahofia uelewa wako mzee. Si kila habari ni habari
 
Yaani mada za kipuuzi na kishenxi kabisa.., hazina tija na wala hazijengi, huku tunaita ni 'kukosa kazi'.
 
Kuna stesheni gani ya radio ina mada zenye Tija..?
Na hata ikitokea mada inaonyesha uelekeo wa kuwa na tija, Je hao waongoza mada wana weledi..?
 
Hilo sio lengo kama wana lengo hilo approach yao ni hovyo ndio maana wanatakiwa kukaguliwa vyeti. Huwezi ukawa na lengo la kuondoa jambo harafu ukawa unalijadili kwa namna hiyo. Wamekosea sana approach. Kama wanataka kukomesha tabia hiyo wange mleta mtalaamu akaelimisha jamii na kukemea tabia hiyo.
Wamejadilije ili tuweze kushirikiana na wewe kukemea?
 
Back
Top Bottom