"Watangazaji Bora wa mpira Tanzania...."

Umemuweka wapi Juma Nkamia(kwa sasa mbunge)...ilikuwa raha,baada ya goli unaelezwa mtu kafungaje! Utasikia wanauliza,ebu Juma Nkamia waeleze watazamaji....UYU HAYUMO KWELI,NIWEKE SAWA WAKUU.
 
1993 kama sijakosea
No! 1991 ilikuwa, Sifa nyingine ya Charlz ni namna alivyokuwa akiwa nick name wachezaji, na kuwaelezea kiasi kwamba hata sisi wa nje ya Dar tulihisi kama vile tunawaona na pia hata simulizi zake za hapa na pale, mfano aliposema kuna mchezaji alikwenda kupiga penalt akapiga fyongo na mpira ukatoka ukawa wa kurusha badala ya goal kick. Niliishiwa mbavu kwa kicheko
 
Mimi 10 bora wangu ni hawa:

1.Mshindo Mkeyenge
2.Omary Jongo
3.Dominick Chilambo
4.Charles Martin Hilary
5.Barthlomeo Komba
6.Ahmed Jongo
7.Salim Mbonde
8.Abdallah Idrisa Majura
9.Mikidad Mahmoud 'Brother Mick" na
10.Abdul Ngarawa

Mkuu, huyo namba 10, ni noma. Mwaka 1982 Challenge Cup, Stars ya Jeff Allan Hudson pale Nairobi, mechi na Ethiopia, tuko mbele 1 - 0, mara kona inapigwa na Ethiopia wanasawazisha. Akasema la la la.....aaa, goo..... kum...............mae wamerudisha!
 
aah Huko Kenya Lenard Mambo Mbotela ' kadenge ina mupira ,kadenge inakwenda,kadenge napiga njenga lakini golikipa Tairus Omondi nakamata.
 
Hivi Henrick Michael Libuda (RIP) hakuwahi kutangaza mpira au nimechanganya mambo? Pia kuna huyu Shaaban Kisu!
 
WanaJF,mmetosheka na kuridhika kuwa hawa waliotajwa ni watangazaji bora wa mpira Tanzania?
Kikubwa zaidi walichokuwa nacho hao tunowasifia ni uwezo mkubwa waliokuwa nao wa kutambua matukio hata kabla ya mwamuzi kupuliza filimbi, mfano atakwambia offside kabla hata refa hajapuliza filimbi, faulo zote walikuwa wanazijua na wapi zitaelekezwa, move za magoli wanaziona na nyingine huzaa goli, mfano mechi ya Pamba na Anse Bailou ya ushelisheli, ile ya goli 12-0,Chilambo (RIP), anasema goli la tisa hilo naliona,wakati huo Nico Bambaga yupo katikati ya uwanja na mpira na kweli inakwenda kuwa goli.

Siku hizi kuna wengine kona wanasema goal kick,mpira wa kurusha wanasema kona, wengine wanaacha hata kutangaza wanaleta story tofauti na mpira wanaoutangaza, au mfano Stars inacheza unakuta mtangazaji hamjui mchezaji wa Stars mpaka asome namba ya jezi mgongoni wakati hawa wachezaji anawatangaza kila mara. Wanahitaji kutulia na kuendelea kuboresha ili nao tuwafurahie.
 
mechi ya Simba na Villa mtangazaji alikuwa Charles Hillary na alipoanza kutaja kikosi cha Villa ilikuwa balaa kwani kabla hajafika kwa sentahafu kule mpira ulikuwa umeshaanza na ghafla akakatiza kutaja kikosi cha Villa kisha akapiga yowe la Goooooooooooooooo....halafu akasema ''namna gani pale...ni goal Kick...alikwenda vizuri sana pale Majid Musisi, lakini Frank Kasanga Bwalaya alisimama imara pale...namna gani pale Jamhuri kihwelu Mrema alikuwa kazubaa''....halafu akaendelea kutaja kikosi
e bwana eheee, hao ndo wenyewe, wewe hata sasa silikila bbc ulimwengu wa soka, utapendaaaaa
 
No! 1991 ilikuwa, Sifa nyingine ya Charlz ni namna alivyokuwa akiwa nick name wachezaji, na kuwaelezea kiasi kwamba hata sisi wa nje ya Dar tulihisi kama vile tunawaona na pia hata simulizi zake za hapa na pale, mfano aliposema kuna mchezaji alikwenda kupiga penalt akapiga fyongo na mpira ukatoka ukawa wa kurusha badala ya goal kick. Niliishiwa mbavu kwa kicheko
jamani nimefurahi sana.. tatizo hawa vijana wa siku hizi, wanachakachua sana, ahwan ubunifu.....
 
Mkuu, huyo namba 10, ni noma. Mwaka 1982 Challenge Cup, Stars ya Jeff Allan Hudson pale Nairobi, mechi na Ethiopia, tuko mbele 1 - 0, mara kona inapigwa na Ethiopia wanasawazisha. Akasema la la la.....aaa, goo..... kum...............mae wamerudisha!


ah aha ha ha ha aaaa duuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu
 
Jamani na mimi namkumbuka ezekiel malongo.,nae alikua fundi sana wakupachika majina haya ni machache...joseph kaniki kumbakumba...,athumani magoli machupa.., cristopher alex masawe meku.,amri saidi jamp stam..,anakwenda sekilojo chambua..,chambua na mpira...chambua anawachambua lalalaaaa goooo...!!
 
Si mnamkumbuka Dada Halima Mchuka...Yule mtangazaji wa mpira wa kwanza wa kike hapa Tanzania!, siku hizi hasikiki katika kituo chake cha kazi, Zamani Redio Tanzania na sasa TBC Taifa kwa sababu alipata maradhi ya kupooza upande wa kulia miaka minne iliyopita. Katika mahojiano yake na mtangazaji kutoka Mlimani TV, Halima amesema alisaidiwa sana na Mr. Mchata(RIP) katika kufanikisha ndoto zake za kuwa mtangazaji wa kike wa mpira wa miguu. Ameongeza kuwa mechi yake ya kwanza ilikuwa kati ya SIMBA na YANGA...Dada Halima anaendelea kuuguza maradhi yake ya kupooza akikaa na Ndugu yake huko Mikocheni...na bado ana imani kuwa atarudi katika hali yake ya kawaida ili andelee na kazi yake ya utangazaji.....WanaJF naomba tumkumbuke katika sara dada yetu Halima Mchuka apone haraka ili afanikishe lengo lake kuu la kuwa mtangazaji bora wa kike Duniani kama alivyotamka mwenyewe.

Source: Mlimani TV/Jarida la habari/22-05-2011...
 
KWa Kweli Ilikuwa KAzi na Burudani
Unakutana na Vichwa Viwili hapa Dar
Yaani Charles Hillary na Mpinzani wake Ahmed Jongo....kwani Mmoja alikuwa Simba na Mwingine Yanga. Ilikuwa Raha sana Simba na Yanga halafu Refarii ni Juma Ali David
 
Si mnamkumbuka Dada Halima Mchuka...Yule mtangazaji wa mpira wa kwanza wa kike hapa Tanzania!, siku hizi hasikiki katika kituo chake cha kazi, Zamani Redio Tanzania na sasa TBC Taifa kwa sababu alipata maradhi ya kupooza upande wa kulia miaka minne iliyopita. Katika mahojiano yake na mtangazaji kutoka Mlimani TV, Halima amesema alisaidiwa sana na Mr. Mchata(RIP) katika kufanikisha ndoto zake za kuwa mtangazaji wa kike wa mpira wa miguu. Ameongeza kuwa mechi yake ya kwanza ilikuwa kati ya SIMBA na YANGA...Dada Halima anaendelea kuuguza maradhi yake ya kupooza akikaa na Ndugu yake huko Mikocheni...na bado ana imani kuwa atarudi katika hali yake ya kawaida ili andelee na kazi yake ya utangazaji.....WanaJF naomba tumkumbuke katika sara dada yetu Halima Mchuka apone haraka ili afanikishe lengo lake kuu la kuwa mtangazaji bora wa kike Duniani kama alivyotamka mwenyewe.

Source: Mlimani TV/Jarida la habari/22-05-2011...

Tayari hatunae tena
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom