Watangaza nia; wako kimya na hili.

Watangaza nia; wako kimya na hili.

Sinamboga

Member
Joined
Dec 6, 2012
Posts
86
Reaction score
38
Mpaka sasa hakuna mtangaza nia aliyeongea ni kwa namna gani atakabiliana na mabadiliko ya tabia Nchi, uchafu unaondelea kukithiri katika miji yetu,kwenye mito, maziwa na kupotea kwa maeneo kijani katika miji mingi kutokana na ujenzi holela.
Ama hili halipo katika Ilani????/
 
hayo yote hayana mana la msingi tunaangalia atawafanyaje mafisadi basi, maana kero namba moja nchini ni ufisadi
 
Bado sijaona kichwa cha mtu wa kuwa raisi.. Sio upinzani wala chama tawala. Watazame usoni tuu utajua
 
Watanzania wanajua kufua nguo na ubishoo, ukisema mambo ya mazingira, wala hakuna anayejali. Ngoja siku moja yaje magonjwa ya uchafu sugu, tutakufa kama wapumbavu.
 
Back
Top Bottom