Ghibuu, acha uongo, sisi Zanzibar tunaijua kuliko unavyodhani wewe, usije ukashangaa tunaonana kila siku, Walio chomewa wana nyumba imara na maduka imara, na wengine wemewaajiri Wazanzibari, na maduka yenyewe ni ya Kitalii, Tourism Souvernir na wengi wa Wazanzibari isipokuwa wahindi ndio wenye maduka ya namna hii, wengi ni Wakenya, Wabara na Wahindi, sawa inawezekana yalikuwepo pia mabanda madogo, lakini eneo la Mnarani kulikuwa na makaazi.
Unajua history ya Kijiji cha wabara cha KIBANDA UGALI Kiwengwa? alivunja Rais Karume mwaka 2005 na Kujenga Hoteli 2 moja yake, Sultan Sands Hotel, na hekalu la mkewe Mama Shadya, eti alishauriwa na ZATI shirikisho la wawekezaji wa Kitalii ambayo mwenyekiti wake ni Simai Said Mohamed, mdogo wake Hassan Kichwa, wamiliki ya Mercury Restaurant hapo Bandarini, cha ajabu huyo Simai amepewa Uwakilishi, na usiniambie kuwa hii familia ni safi ya Kina Simai, ila nasemaje, kulikuwepo wawekezaji wengi wa bara hapo Kibanda ugali, walitumia pesa nyingi sana kujenga nyumba za maana na biashara kubwa kubwa za Kitalii, siku moja bila taarifa, saa kumi usiku, Greda au makatapila yalifika na kuanza kubinua kila nyumba bila hata kuamsha watu, walitoka wanawake na watoto uchi wakijiuliza ni mwisho wa dunia? lakini badala ya Jeshi tiifu kwa Rais wa Zanzibar la JKU liliwacheka tu na kuwaamuru wasionekane popote maeneo ya karibu. pia miezi 3 iliopita unakumbuka Kendwa? maduka yote na minisupermarket nyingi za wabara zilizostawi, ilitoka amri kwa viongozi wa Juu zivunjwe mara moja, mbona za wanzibari hazivunjwi?