tatanyengo
JF-Expert Member
- Mar 30, 2011
- 1,134
- 280
Serikali ina mpango wa kufuta ufaulu wa Daraja la IV (Division IV) kwa wahitimu wa kidato cha IV kwenda kusoma katika vyuo vya ualimu. Suala hilo limedokezwa leo na Naibu waziri -Phillipo Mulugo alipokuwa akijibu swali lililoulizwa na mbunge wa Longido bungeni Dodoma.
Mulugo amesema wameanza kwa kuondoa point 28 na wataendelea kufanya hivyo lengo likiwa kufuta kabisa waliopata Division IV kusomea ualimu.
My take: Division IV ndiyo ushindi kwa watoto wetu wanaosoma katika shule zetu hasa za Kata sasa wakitupwa nje ya ulingo huu litakuwa ni janga la kitaifa.
Binafsi pia sidhani kama kuwachukua walipata division I, II, na III ndiyo kigezo pekee cha kuboresha elimu nchini -serikali iboreshe mazingira kwa walimu na matokeo watayaona!
Mulugo amesema wameanza kwa kuondoa point 28 na wataendelea kufanya hivyo lengo likiwa kufuta kabisa waliopata Division IV kusomea ualimu.
My take: Division IV ndiyo ushindi kwa watoto wetu wanaosoma katika shule zetu hasa za Kata sasa wakitupwa nje ya ulingo huu litakuwa ni janga la kitaifa.
Binafsi pia sidhani kama kuwachukua walipata division I, II, na III ndiyo kigezo pekee cha kuboresha elimu nchini -serikali iboreshe mazingira kwa walimu na matokeo watayaona!