Wataalamu wa ujenzi: Shimo la choo linajaa maji

Wataalamu wa ujenzi: Shimo la choo linajaa maji

Bakulutu

JF-Expert Member
Joined
Nov 30, 2011
Posts
2,578
Reaction score
1,817
Habari wataalam, mwenye ujuzi na hii issue na shimo la choo limejaa nusu(maji) ndani ya wiki 2.

Inaoneka maji yanapanda chini na pia hayanyonywi chini.

Mwenye kujua cha kufanya tafadhali.
 
jee hapo yalipofikia baada ya kujaa wiki mbili hizo yanaongezeka?
 
weka picha watu waweze ona hali ilivyo... kama kuna msaada wa haraka kutokana na mazingira uweze kusaidiwa
 
Habari wa taalamu, mwenye ujuzi na hii issue, na shimo la choo limejaa nusu(maji) ndani ya wiki 2.
Inaoneka maji yana panda chini na pia haya nyonywi chini.
Mwenye kujua chakufanya tafadhali.
Kwanza mshukuru Mungu kwa kuishi sehemu ambayo ina maji ya kutosha. Chimba kusimahapo pembeni utatumia maji ya bure kizazi na kizazi.
Kuhusu shimo la choo ngoja wataalam waje. Asante
 
Unaweza kuta chuni kulikuwa na maji sana saa yanaanza kujaza soak away pit....
 
Hapo tatzo ni kwamba mjenzi alilazmsha au Cjui mlilazmisha kujenga shmo kwenye chem chem bila kuzuia chem kupenya ndan Ya shmo na hili nafkr ni tatzo la fund kwahyo uktaka kurekebsha hyo hal shart utoe uchafu wote ndan ya shmo tuanze kudhbt chemchem na water proof zaid ya hapo hamna Suluhsho zaid ya kupgw salio tu..
 
Hapo tatzo ni kwamba mjenzi alilazmsha au Cjui mlilazmisha kujenga shmo kwenye chem chem bila kuzuia chem kupenya ndan Ya shmo na hili nafkr ni tatzo la fund kwahyo uktaka kurekebsha hyo hal shart utoe uchafu wote ndan ya shmo tuanze kudhbt chemchem na water proof zaid ya hapo hamna Suluhsho zaid ya kupgw salio tu mkuu
 
weka picha watu waweze ona hali ilivyo... kama kuna msaada wa haraka kutokana na mazingira uweze kusaidiwa
Mkuu picha nitawekaje ya ndani na kuna giza ila nimepima limebaki futi 6.5 kati ya futi 12
 
Hapo tatzo ni kwamba mjenzi alilazmsha au Cjui mlilazmisha kujenga shmo kwenye chem chem bila kuzuia chem kupenya ndan Ya shmo na hili nafkr ni tatzo la fund kwahyo uktaka kurekebsha hyo hal shart utoe uchafu wote ndan ya shmo tuanze kudhbt chemchem na water proof zaid ya hapo hamna Suluhsho zaid ya kupgw salio tu..
Zinadhibitiwa ki vipi mkuu, hebu nipe elimu kidogo
 
Water table iko juu sana... Suluhu ni kuwa na system ya kunyonya malighafi na gari au kuunga na public sewer..
Wazo zuri ila inaweza kuwa gharama sana pia hizi public sewage sidhani kama ziko sehemu zote dsm. Location yangu ni Goba njia 4
 
Mkuu picha nitawekaje ya ndani na kuna giza ila nimepima limebaki futi 6.5 kati ya futi 12
Hayo maji yanayojaza shimo la choo yanatoka wapi? Mfumo wa maji taka ni wa mashimo mawili au shimo moja? Asili ya eneo ulilojenga makazi yako ni chemichemi au likoje? Matumizi ya maji hapo kwako yakoje mkuu
 
picha ya eneo la nje la ya hilo septick tank
36959c86775d25d1f075c87121408aa7.jpg
9c6782c661198899835c6e743dfb922d.jpg
259d5c43031ba292c08981704bbfb68e.jpg
 
Tatizo hili Mimi naliweza na ndiyo Kazi zangu zinazoniweka mjini, weka contacts zako ili tukutane private.
 
Hayo maji yanayojaza shimo la choo yanatoka wapi? Mfumo wa maji taka ni wa mashimo mawili au shimo moja? Asili ya eneo ulilojenga makazi yako ni chemichemi au likoje? Matumizi ya maji hapo kwako yakoje mkuu
Kwa makaridio ya juu nimehamia tarehe 5 mwezi huu, nimetumia maji maximum lita elfu 2 japo kwa yalio ingia chooni kama lita 1500, mfumo ni shimo moja, eneo la hapa kulingana na jirani yangu alipima water table iko mita kama 130, hakuna asili ya chemichemi. Ni Goba njia 4 unaweza jua zaidi tatizo la maji goba.
 
Back
Top Bottom