Wataalamu wa lugha nisaidieni

Wataalamu wa lugha nisaidieni

ragin

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2015
Posts
7,391
Reaction score
9,378
habari za majukumu wapendwa! kama nitakuwa nimekosea jukwaa basi niwatake radhi kwanza.
ila kama ni sahihi basi niendelee na swala langu hili hapa chini.

neno "TOKA NJE au TOKA NDANI" huwa linatajwa mda upi?

pale mhusika akiwa ndani basi huna budi kumwambia atoke ndani au atoke nje ili akuone wewe ulieko nje ukimsubiria?

neno TOKA sehemu zingine linaeleweka pindi likitumika na watu
mfano mtu amekaa chini alafu mwenzie akaona mdudu awe nyoka au ng'e ili mdudu huyo asimuume utamwambia yule alie kaa chini kuwa TOKA HAPO " (yaani alipokaa chini).

lakini hapa TOKA NJE AU TOKA NDANI ndio huwa sielewi linatumikaje na linadefine veepi ukilitamka.

nipo ndani ya nyumba ila mgeni akija utasikia TOKA NJE nawakati mda huo nipo ndani si inabidi niambiwe TOKA NDANI kuna mgeni huku!!
ila wengi wanatumia neno TOKA NJE wakati mhusika yupo ndani.

naomba wataalamu wa lugha mnisaidie ha maneno utofauti wake.
 
Toka nje (wewe ukiwa ndani unamwambia aliyeko nje atoke huko nje labda aje ndani)

Toka nje(wote mkiwa ndani unamuamrisha mwenzako aende nje)

Toka ndani(ukimwamrisha mwenzako mliyeko naye ndani atoke ndani na kwenda nje)

Toka ndani(wewe ukiwa nje unamuamuru mwenzako aliyeko ndani atoke huko/humo ndani na kuungana na wewe nje)

Kwa ujumla maana ya kauli hizi NADHANI hutumika kulingana na muktadha wa wakati huo.
 
toka nje (wewe ukiwa ndani unamwambia aliyeko nje atoke huko nje labda aje ndani)

toka nje(wote mkiwa ndani unamuamrisha mwenzako aende nje)



toka ndani(ukimwamrisha mwenzako mliyeko naye ndani atoke ndani na kwenda nje)

toka ndani(wewe ukiwa nje unamuamuru mwenzako aliyeko ndani atoke huko/humo ndani na kuungana na wewe nje)

kwa ujumla maana ya kauli hizi NADHANI hutumika kulingana na muktadha wa wakati huo.
ok
walau nepata mwelekeo.
 
habari za majukumu wapendwa! kama nitakuwa nimekosea jukwaa basi niwatake radhi kwanza.
ila kama ni sahihi basi niendelee na swala langu hili hapa chini.

neno "TOKA NJE au TOKA NDANI" huwa linatajwa mda upi?

pale mhusika akiwa ndani basi huna budi kumwambia atoke ndani au atoke nje ili akuone wewe ulieko nje ukimsubiria?

neno TOKA sehemu zingine linaeleweka pindi likitumika na watu
mfano mtu amekaa chini alafu mwenzie akaona mdudu awe nyoka au ng'e ili mdudu huyo asimuume utamwambia yule alie kaa chini kuwa TOKA HAPO " (yaani alipokaa chini).

lakini hapa TOKA NJE AU TOKA NDANI ndio huwa sielewi linatumikaje na linadefine veepi ukilitamka.

nipo ndani ya nyumba ila mgeni akija utasikia TOKA NJE nawakati mda huo nipo ndani si inabidi niambiwe TOKA NDANI kuna mgeni huku!!
ila wengi wanatumia neno TOKA NJE wakati mhusika yupo ndani.

naomba wataalamu wa lugha mnisaidie ha maneno utofauti wake.
Toka Nje unamwambia mtu uliyoko naye ndani
Toka ndani unamwambia mtu aliyeko
Ndani wakati huo wewe upo nje

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom