Wataalamu wa kutengeneza mashine

Wataalamu wa kutengeneza mashine

nkobhe255

JF-Expert Member
Joined
Sep 26, 2017
Posts
234
Reaction score
292
Jamani, mimi nimemaliza chuo mwaka huu mwezi july, nilikuwa na project fulani ambayo nilitaka mnisaidie ili niweze kui accomplish vizuri.

Mimi naishi kijijini ambapo watu huvuna mahindi hadi gunia 100 kwa kila mmoja. Sasa huwa wanahangaika jinsi ya kubungua mahindi na hivyo kutumia gharama kubwa kuwalipa wabunguaji ambao hata hivyo hutumia mda mwingi.

Sasa nilikuja na wazo la kutaka kutengeneza mashine ya kubungua mahindi(Maize Sheller), sasa nimefuatilia baadhi ya tutorials za youtube jinsi ya kuzitengeneza, lakini sikufanikiwa kuzipata, bali nilizozipata ni tutorials za jinsi inavyo fanya kazi.

MASWALI YANGU

1)Je, nikiweka roller inayozunguka yenye vyuma itasaga hayo mahindi badala ya kuyabungua.

2) Ni vifaa gani na mtaji gani niweze kuinvest ili nifanikiwe?
 
wazo zuri, nakupongeza kwanza kwa hatua ya kutaka kutatua tatizo katika jamii yako hiyo ndiyo maana ya kuitwa msomi
 
Nenda SIDO mkoa uliopo ungekuwa iringa kuna sehemu vijana wanatengeneza ningekuelekeza
 
Yaaa nielekeza kwa sasa niko Iringa mjini, I can go to learn bro
Okay the factory or firm is found near or beside barabara mbili u will found men who manufacturing different machines kusaga kukoboa na kupukuchua fuata hiyo barabara mpaka jirani na uwanja wa mwembetogwa
 
samahani unavyosema kubungua unamaanisha kupukuchua yani kutenganisha mahind na mabuzi
 
Okay the factory or firm is found near or beside barabara mbili u will found men who manufacturing different machines kusaga kukoboa na kupukuchua fuata hiyo barabara mpaka jirani na uwanja wa mwembetogwa
Tumia kiswahili, au nenda Youtube uanze kusoma english grammar.
Kusema "factory or firm" duh! alafu unakuja na "near or beside" duh! "u will found men" duh! "who manufacturing" duh!
Hahaha ila ahsante sana kwa kunichekesha leo.
 
Okay the factory or firm is found near or beside barabara mbili u will found men who manufacturing different machines kusaga kukoboa na kupukuchua fuata hiyo barabara mpaka jirani na uwanja wa mwembetogwa
Kwenye kiinglish wewe ni Mtu mdogo. Lakin usijali. Utajua tu. usipochafuka utajifunzaje?
 
Mkuu vijiji gan ivo vinafursa hadhwim km hii na ni mkoa gan
 
Back
Top Bottom