Tuwajue Waswahili na Uswahili wao

Tuwajue Waswahili na Uswahili wao

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
22,492
Reaction score
33,051
TUWAJUE WASWAHILI NA USWAHILI WAO

Sifa kuu ya Waswahili ni uungwana.
Hebu tuwajue Waswahili na Uswahili wao.

Picha ya kwanza inawaonyesha Waswahili katika Baraza la Wazee wa TANU mwaka wa 1957.

Picha ya chini yake inamuonyesha Mswahili Mzee Mshume Kiyate akimvisha kitambi kumfariji Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere baada ya kurejea madarakani kufuatia maasi ya Tanganyika Rifles mwaka wa 1964.

Picha inayofuatia inamuonyesha tena kulia Mswahili Mzee Mshume Kiyate kamshika mkono Julius Nyerere, pembeni ya Nyerere ni Waswahili Wazaramo Makisi Mbwana na Mzee Mwinjuma Mwinyikambi.

Hii ilikuwa mwaka wa 1962 siku ya kupiga kura ya Rais nafasi iliyokuwa ikigombewa na Julius Nyerere (TANU) na Mswahili Mluguru Zuberi Mtemvu (Congress).

Picha inayofuatia ni safari ya kwanza ya Mwalimu Nyerere UNO mwaka wa 1955 kulia ni Mswahili Msukuma Bi. Chiku bint Said Kisusa, Mswahili Mndengereko Bibi Titi Mohamed, Bi. Mwamvita Mwinyamani, Julius Nyerere, Mswahili Mchagga Lucy Lameck na Bi. Tatu bint Mzee.

Picha ya mwisho nimeipa jina ''Wamanyema Wanne na Mzanaki Mmoja.''

Ningeweza kuipa jina: ''Waswahili Wamanyema Wanne na Mzanaki Mmoja'' lakini itakuwa sijamtendea haki Mwalimu Nyerere kwa sababu yeye akijinasibu sana na Uswahili kufikia hadi kutunga mashairi na kuvaa kofia ya mkono.

Picha hii ilipigwa 1956 Dodoma Train Station: Kulia ni Haruna Iddi Taratibu, Saadan Abdu Kandoro, Julius Nyerere, Sheikh Mohamed Ramia na Iddi Faiz Mafungo.

Hawa Waswahili kuwaeleza historia zao inahitaji kitabu kizima.

Katika picha hizi kuna Mswahili Mdigo Dossa Aziz, Mswahili Mrufiji, Said Chamwenyewe, Sheikh Issa Nasir, Mshume Kiyate, Mswahili Mmashomvi Jumbe Tambaza, Mswahili Mzanzibari Sheikh Suleiman Takadir, Mswahili Mmanyema Mweka Hazina wa kwanza wa TANU na Mweka Hazina wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika Iddi Faiz Mafungo mkusanya fedha na mratibu wa safari ya Nyerere UNO 1955, Mswahili Msukuma Bi. Chiku mke wa Mswahili Mwarabu Shariff Abdallah Omar Attas aliyewaleta wanawake katika TANU, kwa kuwataja wachache na machache yao.

Waswahili hawa watu waungwana kwa tabia na hulka kwa kila hali.

Walifanya makubwa katika kupigania uhuru wa Tanganyika wakiwa bega kwa bega na Julius Nyerere lakini walizizuia ndimi zao kueleza waliyofanya.

Hawakupata kueleza michango yao hadi wanaingia kaburini.
Leo hawathaminiwi na si wengi wanaowajua wazalendo hawa.

Hawa ndiyo Waswahili wa Tanganyika na Uswahili wao.
Lipi baya walilofanya?

1769434580450.png
1769434605431.png
1769434622856.png
1769434639385.png
1769434658485.png
 
TUWAJUE WASWAHILI NA USWAHILI WAO

Sifa kuu ya Waswahili ni uungwana.
Hebu tuwajue Waswahili na Uswahili wao.

Picha ya kwanza inawaonyesha Waswahili katika Baraza la Wazee wa TANU mwaka wa 1957.

Picha ya chini yake inamuonyesha Mswahili Mzee Mshume Kiyate akimvisha kitambi kumfariji Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere baada ya kurejea madarakani kufuatia maasi ya Tanganyika Rifles mwaka wa 1964.

Picha inayofuatia inamuonyesha tena kulia Mswahili Mzee Mshume Kiyate kamshika mkono Julius Nyerere, pembeni ya Nyerere ni Waswahili Wazaramo Makisi Mbwana na Mzee Mwinjuma Mwinyikambi.

Hii ilikuwa mwaka wa 1962 siku ya kupiga kura ya Rais nafasi iliyokuwa ikigombewa na Julius Nyerere (TANU) na Mswahili Mluguru Zuberi Mtemvu (Congress).

Picha inayofuatia ni safari ya kwanza ya Mwalimu Nyerere UNO mwaka wa 1955 kulia ni Mswahili Msukuma Bi. Chiku bint Said Kisusa, Mswahili Mndengereko Bibi Titi Mohamed, Bi. Mwamvita Mwinyamani, Julius Nyerere, Mswahili Mchagga Lucy Lameck na Bi. Tatu bint Mzee.

Picha ya mwisho nimeipa jina ''Wamanyema Wanne na Mzanaki Mmoja.''

Ningeweza kuipa jina: ''Waswahili Wamanyema Wanne na Mzanaki Mmoja'' lakini itakuwa sijamtendea haki Mwalimu Nyerere kwa sababu yeye akijinasibu sana na Uswahili kufikia hadi kutunga mashairi na kuvaa kofia ya mkono.

Picha hii ilipigwa 1956 Dodoma Train Station: Kulia ni Haruna Iddi Taratibu, Saadan Abdu Kandoro, Julius Nyerere, Sheikh Mohamed Ramia na Iddi Faiz Mafungo.

Hawa Waswahili kuwaeleza historia zao inahitaji kitabu kizima.

Katika picha hizi kuna Mswahili Mdigo Dossa Aziz, Mswahili Mrufiji, Said Chamwenyewe, Sheikh Issa Nasir, Mshume Kiyate, Mswahili Mmashomvi Jumbe Tambaza, Mswahili Mzanzibari Sheikh Suleiman Takadir, Mswahili Mmanyema Mweka Hazina wa kwanza wa TANU na Mweka Hazina wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika Iddi Faiz Mafungo mkusanya fedha na mratibu wa safari ya Nyerere UNO 1955, Mswahili Msukuma Bi. Chiku mke wa Mswahili Mwarabu Shariff Abdallah Omar Attas aliyewaleta wanawake katika TANU, kwa kuwataja wachache na machache yao.

Waswahili hawa watu waungwana kwa tabia na hulka kwa kila hali.

Walifanya makubwa katika kupigania uhuru wa Tanganyika wakiwa bega kwa bega na Julius Nyerere lakini walizizuia ndimi zao kueleza waliyofanya.

Hawakupata kueleza michango yao hadi wanaingia kaburini.
Leo hawathaminiwi na si wengi wanaowajua wazalendo hawa.

Hawa ndiyo Waswahili wa Tanganyika na Uswahili wao.
Lipi baya walilofanya?

View attachment 3534741View attachment 3534742View attachment 3534743View attachment 3534745View attachment 3534746
Baya walilofanya ni kuithamini sana ilimu ahera kuliko elimu dunia. Kukosa kwao elimu dunia, naamini, huenda ndiyo sababu iliyowafanya wakae nyumba ya kijana msomi, mwerevu, na mahiri wa elimu dunia Mwl J.K. Nyerere
 
Mzee Said hebu leta tafakuri ya uchaguzi wa 2025 na pilika zake kulinganisha na enzi tulizopelekewa moto na Mkapa mpaka kutokea Mwembai massacre
 
Baya walilofanya ni kuithamini sana ilimu ahera kuliko elimu dunia. Kukosa kwao elimu dunia, naamini, huenda ndiyo sababu iliyowafanya wakae nyumba ya kijana msomi, mwerevu, na mahiri wa elimu dunia Mwl J.K. Nyerere
Wazazi wetu walikuwa sahihi kutopeleka watoto wao shule za wagalatia, kwa kuogopa watoto wa kufanywa haya mambo kwenye shule za misheni

1769467234955.png
 
Vita yako ya kidini kuhusu historia ya uhuru wa Tanganyika
Gwapole,
Sijafanya vita nilichofanya nimeandika historia ya wazee wangu katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Wengi wamependezewa na historia hii.
 
Baya walilofanya ni kuithamini sana ilimu ahera kuliko elimu dunia. Kukosa kwao elimu dunia, naamini, huenda ndiyo sababu iliyowafanya wakae nyumba ya kijana msomi, mwerevu, na mahiri wa elimu dunia Mwl J.K. Nyerere
Nore...
Nadhani huijui historia hii.

Chukua muda ujifunze historia ya Waislam Pwani ya Afrika ya Mashariki na suala la elimu.

Krapf alipofika Vuga kwa Chief Kimweri alimkuta anajua kusoma na kuandika.

Wajerumani waliwakuta wakazi wote wa Pwani ya Afrika ya mashariki wameelimika na zile 3Rs yaani Reading, Writing na Arithmetic na wakisoma katika madrasa kwa miaka mingi wakitumia Arabic Script.

Matokeo yake waliona wivu na wakapiga marufuku matumizi ya herufi za Kiarabu wakalazimisha matumizi ya Roman Script.

Nyerere hakuchagulikuwa kuwa President wa TANU kwa ajili ya elimu yake peke yake.

Kubwa ilikuwa Waislam walitaka kiongozi atoke nje yao ili kuepusha dhana kuwa TAA ni chama cha Waislam.

Nyerere akipewa uongozi wa TAA na TANU kuundwa yeye ndiyo atakaeongoza harakati za kudai uhuru na ile fikra kuwa TANU ni chama cha Waislam itaondoka.

Waasisi wa African Association mwaka wa 1929 wengi wao walikuwa Waislam kwa kuwa Wakristo walikuwa wanakatazwa na viongozi wao kujihusisha na siasa.

Soma kitabu cha Abdul Sykes itaijua vizuri historia ya Julius Nyerere:

1769543470804.png


Angalia picha hiyo hapo chini:

1769543018760.png
 
Watafute Jenerali Ulimwengu na Edwin Mtei uwaambie hizi porojo zako.
 
Watafute Jenerali Ulimwengu na Edwin Mtei uwaambie hizi porojo zako.

  1. The Life and Times of Abdulwahid Sykes 1924 –1968 The Untold Story of the Muslim Struggle against British Colonialism in Tanganyika, Minerva Press London, 1998 translated into Kiswahili as Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes 1924-1968 Historia Iliyofichwa Kuhusu Harakati za Waislam Dhidi ya Ukoloni wa Waingereza, Phoenix Publishers, Nairobi, 2002.
  2. The Torch on Kilimanjaro, Oxford University Press, Nairobi, 2006
  3. Contributing author for an African anthology: The Mermaid of Msambweni and Other Stories, Oxford University Press 2007, Nairobi.
  4. Contributing author Dictionary of African Biography (DAB), Oxford University Press 2011, New York.
  5. Uamuzi wa Busara, Abantu Publications 2008, Dar es Salaam.
  6. Watu Mashuhuri Katika Uhuru wa Tanganyika No. 1, Ibn Hazm Media Centre, 2018, Dar es Salaam.
  7. Watu Mashuhuri Katika Uhuru wa Tanganyika No.2, Ibn Hazm Media Centre 2018, Dar es Salaam
  8. Dar es Salaam na Wazalendo Wake Mashujaa Katika Kupigani Uhuru wa Tanganyika Ibn Hazm Media Centre 2018, Dar es Salaaam
  9. Watu Mashuhuri Katika Kuulingania Uislam Tanzania, Sheikh Ilunga, Ibn Hazm Media Centre 2018, Dar es Salaam
  10. Dola, Kanisa na Tatizo la Udini Tanzania, Ibn Hazm Media Centre, 2018, Dar es Salaam
  11. The School Trip to Zanzibar, Africa Proper Education Network 2020, Dar es Salaam
  12. Rajabu Ibrahim Kirama, Jemadari wa Vita Kuwa Jemadari wa Uislam, Readit, 2020, Dar es Salaam
  13. Sal Davis, An Autobiography, Readit/Amazon, 2023, Dar es Salaam
  14. In Praise of Ancestors (1987) Africa Events (London).
  15. Abdulwahid Sykes: Founder of Political Movement (1988) Africa Events (London).
  16. Islam and Politics in Tanzania (1989) Al Haq International (Karachi)
  17. The Plight of Tanzanian Muslim (1993) Change (Dar es Salaam).
  18. Tanzania - The "Secular" Unsecular State (1995) Change (Dar es Salaam).
  19. The Question of Muslim Stagnation in Education in Tanzania - A Muslim Riddle (Paper presented at the Conference of the Global World of the Swahili Intercultural Dialogue on the Indian Ocean Zanzibar, February 20 - 23, 2003).
  20. Islamic Education and Intellectualism in Eastern Africa ‘Themes from the Pulpit in Tanganyika (Tanzania Mainland) 1800 – 2000’ (Paper presented at International Symposium on Islamic Civilisation in Eastern Africa Kampala, Uganda organised by the Islamic Conference Research Centre for Islamic History, Art and Culture (IRCICA), Istanbul and the Islamic University in Uganda, Mbale December 15th – 17th 2003).
  21. Sheikh Hassan bin Ameir - The Moving Spirit of Muslim Emancipation in Tanganyika (1950 – 1968) (Paper presented at Youth Camp Organised by Zanzibar University, World Assembly of Muslim Youth (WAMY) and Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) 27th February – 4th March 2004).
  22. Islamic Movement and the Christian Lobby in Tanzania - the Experience of the late Prof. Kighoma Ali Malima (1938 – 1995) (Paper Presented to Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) Sokoine University of Agriculture (SUA) Morogoro 11th April 2004).
  23. Terrorism in East Africa the Tanzanian Experience (Paper Presented at the Conference on Islam, Terrorism and African Development University of Ibadan, Nigeria 8th - 10th February 2006).
  24. Al Marhum Sheikh Kassim bin Juma bin Khamis (1940 – 1994) and the Pork Riots of 1993. (Paper Presented at the Regional Conference on Islam in Eastern Africa: Islam Encounter with the Challenges of the 21st Century 1st - 3rd August 2006, Kenyatta University, Nairobi.
  25. Muslim Bible Scholars of Tanzania – The Legacy of Sheikh Ahmed Deedat (1918 – 2005) Paper Presented at the International Symposium on Islamic Civilisation in Southern Africa Organised by The Organisation of Islamic Conference Research Centre for Islamic History, Art and Culture (IRCICA) The National AWQAF Foundation of South Africa (AWQAF SA 1 – 3 September 2006 University of Johannesburg.
  26. Tanzania: A Nation Without Heroes Seminar Organised by IFRA French Institute for Research in Africa and BIEA British Institute in East Africa 23rd and 24th September 2013 at IFRA Nairobi.
  27. Awards: Several Awards
  28. Visiting Scholar: (2011)
  29. University of Iowa, Iowa City, USA
  30. Northwestern University, Chicago, Illinois, USA
  31. Zentrum Moderner Orient (ZMO), Berlin.
  32. OTHER COUNTRIES VISITED
  33. Zambia, Ethiopia, Great Britain, Swaziland, Msumbiji, Zimbabwe, Zambia, Sudan, Egypt, Saudi Arabia, United Arab Emirates, Oman, Yemen, Uganda, Switzerland, Iran, France, Netherlands, Turkey and Abu Dhabi.
1769547515962.png
1769547650166.png
1769547204377.png
1769547445363.png
1769547383347.png
 
Nore...
Nadhani huijui historia hii.

Chukua muda ujifunze historia ya Waislam Pwani ya Afrika ya Mashariki na suala la elimu.
Krapf alipofika Vuga kwa Chief Kimweri alimkuta anajua kusoma na kuandika.

Wajerumani waliwakuta wakazi wote wa Pwani ya Afrika ya mashariki wameelimika na zile 3Rs yaani Reading, Writing na Arithmetic na wakisoma katika madrasa kwa miaka mingi wakitumia Arabic Script.

Matokeo yake waliona wivu na wakapiga marufuku matumizi ya herufi za Kiarabu wakalazimisha matumizi ya Roman Script.

Nyerere hakuchagulikuwa kuwa President wa TANU kwa ajili ya elimu yake peke yake.
Kubwa ilikuwa Waislam walitaka kiongozi atoke nje yao ili kuepusha dhana kuwa TAA ni chama cha Waislam.

Nyerere akipewa uongozi wa TAA na TANU kuundwa yeye ndiyo atakaeongoza harakati za kudai uhuru na ile fikra kuwa TANU ni chama cha Waislam itaondoka.

Waasisi wa African Association mwaka wa 1929 wengi wao walikuwa Waislam kwa kuwa Wakristo walikuwa wanakatazwa na viongozi wao kujihusisha na siasa.

Soma kitabu cha Abdul Sykes itaijua vizuri historia ya Julius Nyerere:

View attachment 3535288

Angalia picha hiyo hapo chini:

View attachment 3535282
Asante sana mzee MS kwa kunifumbua macho ya kwa nini waisilamu hawakujiweka mbele kudai uhuru wa Tanganyika.
 
Asante sana mzee MS kwa kunifumbua macho ya kwa nini waisilamu hawakujiweka mbele kudai uhuru wa Tanganyika.
Nore...
Siku zote Waislam walikuwa mstari wa mbele katika harakati za siasa na kudai uhuru wa Tanganyika.

Waasisi wa African Association mwaka wa 1929 ni hawa wafuatao: Kleist Abdallah Sykes, Mzee bin Sudi, Ibrahim Hamisi, Ali Said Mpima, Zibe Kidasi, Suleiman Majisu, Cecil Matola, Raikes Kusi na Rawson Watts.

Kleist Sykes anaeleza haya katika mswada wa kitabu alichoandika kabla ya kufariki mwaka wa 1949 kuwa Wakristo walikuwa wachache katika African Association kwa kuwa Kanisa liliwaonya na kujihusisha na siasa.

(Unaweza kusoma historia hii: Daisy Sykes Buruku, ''The Townsman: Kleist Sykes,'' katika Iliffe (ed) Modern Tanzanians, Nairobi, 1973, uk. 95-114. Angalia vilevile A.D. Sykes ''The Life of Kleist Sykes,'' University of Dar es Salaam Ref. No. JAN/HIST/143/15).

Baada ya kuunda African Association hao Waislam sita wakaunda Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika) mwaka wa 1933 kuepusha kupitisha madai yao kwa serikali kupitia African Association kwani walitaka chama hicho kisiguswe na harakati za Waislam dhidi ya serikali.

Juu ya tahadhari hii uongozi wa African Association na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika ukawa katika mikono ya Mzee bin Sudi (President) na Kleist Sykes (Secretary).

Ikawa mambo yote ya Waislam kwenda serikalini yanapitia Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika.

Mwaka wa 1950 baada ya mapinduzi ya uongozi TAA ikawa chini ya uongozi wa Mufti Sheikh Hassan bin Ameir Abdulwahid Sykes, Hamza Mwapachu, Sheikh Said Chaurembo, Steven Abdallah Mhando, Dr. Kyaruzi na John Rupia.

Hawa walikuwa wajumbe katika TAA Political Subcommittee na ndiyo iliyoweka mikakati ya kuunda TANU na kumuingiza Nyerere katika uongozi wa TAA mwaka wa 1953.

Ikiwa bado hujaelewa nifahamishe.

Historia yote ya kudai uhuru wa Tanganyika ni historia ya Waislam.

Ukitaka taarifa zaidi soma historia ya Dr. Kwegyr Aggrey na historia ya Kleist Sykes zote zimo ndani ya Dictionary of African Biography (DAB) 2011.

Ukisoma rejea hizo nilizokuwekea hapa macho yako sasa yatafunguka.

Mimi ni kati ya waandishi 500 kutoka kona zote za dunia walioandika hilo kamusi.

1769723630768.png
 
Back
Top Bottom