Kuna jamaa (Msukuma) alibahatika kusafiri kutoka Kijijini kwake kwenda sehemu ya mbali kidogo. Wakati wa kurudi ilimbidi apige lapa (atembee kwa mguu) sababu usafiri aliotumia wakati wa kwenda ulikuwa ni msaada tu a.k.a lift. Baada ya kurudi kijijini kwake akawa anawahadithia ndugu na jamaa jinsi alivyosafiri. Alipoulizwa ulipanda gari gani wakati wa kwenda....jamaa akawa mkali, "Nakwambia mimi sikupanda GARI nilipanda SCANIA".........Tehe teeheeeeeee, kwa hiyo jamaa akaendelea kukana kabisa hakupanda gari bali alipanda SCANIA. Hadi naondoka eneo la tukio jamaa alibaki na msimamo wake kuwa hajapanda GARI ila alipanda SCANIA!!! Wasukuma bwanaaaaa!!!