Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,842
- 31,073
Miongoni mwa kauli za hovyo kabisa ambazo amewahi kutoa Wassira, basi ya leo inaweza kushika chati.Ameyasema hayo bungeni hivi punde kwamba Ukawa wasiporudi CCM wataendelea na vikao kwa kutafuta akidi itakyokidhi kanuni.
View attachment 158428
Ukawa wanazo hoja za msingi kabisa za kutoka kwenye bunge la katiba nazo ni pamoja na CCM kutaka kuitia kapuni Rasimu ya katiba ya Tume ya Mário iliyotokana na maoni ya wananchi na badala yake kutaka `kuchomeka` katiba yao yenye maoni ya vigogo wa CCM waliopo madarakani pekee!
Sasa kwa mazingira hayo yeye Wassira anataka ukawa warrudi kwenye bunge la katiba ili wawasaliti wananchi waliotoa maoni yao yaliyomo kwenye Rasimu ya katiba ambayo maccm wanataka kuitia kapuni?!
Kwa kuwa yeye Wassira ameshautangazia umma wa watanzania kuwa wapo tayari kuchakachua kanuni zinazohisu quoram kwa lengo moja tu la kupitisha Rasimu yao mbadala ya CCM, basi ni bora waendelee na nia yao hiyo ovu, badala ya kutaka kutishia nyau, wakidhani kuwa ukawa watatishika na huyo nyau wake Wassira, anayewatishia naye.