Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu),Stephen Wassira,anadaiwa kutibua mitandao ya makada wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) waliojipanga kuusaka Urais wa mwaka 2015 kupitia chama hicho,Tazama Tanzania limeelezwa.
Habari za uhakika zilizopatikana kutoka mikoa inayounda Kanda ya Ziwa,zimetaja mwanasiasa huyo mkongwe nchini kwamba kwa sehemu kubwa amekuwa kikwazo kwa baadhi ya mitandao kujijenga katika ukanda huo.
Kanda ya Ziwa inatajwa kuwa moja ya kanda muhimu katika mbio za urais,ambayo imekuwa ikifanikisha ushindi wa si tu kwa wagombea urais,bali wote wanaosaka nafasi za juu za uongozi ndani ya CCM, na hasa ujumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) Taifa.
Kwa mujibu wa Habari hizo,Wassira ametajwa kuwa kikwazo kikuu kwa baadhi ya Makada wa CCM wenye nia ya kugombea urais mwaka 2015,baada ya wasimamizi wa mitandao hiyo kutakiwa kuweka msimamo wao wazi kwanza kama nao wako tayari kumuunga mkono mwanasiasa huyo endapo na yeye ataamua kujitosa katika kinyang'anyiro hicho cha urais.
Wassira anatajwa kukubalika kwa kiasi kikubwa katika ukanda huo wa Kanda ya Ziwa, na kwahiyo wengi wa wanamitandao ya urais 2015 wamekuwa wakipigana vikumbo kumtaka awaunge mkono katika mbio zao hizo, ili kupitia kwake waweze pia kuungwa mkono na wajumbe wa vikao vya uteuzi kutoka kanda hiyo.
Hata hivyo, gazeti hili limeambiwa kwamba matokeo ya vikumbo hivyo vya wanamitandao hiyo ya urais katika kanda hiyo ya Ziwa,yamekuwa si ya kuridhisha baada ya kubainika kuwa hata Wassira mwenyewe anayo nia ya kugombea urais mwaka 2015 ingawa yeye binafsi hajaweka wazi nia yake hiyo.
Kutokana na hali hiyo,imeelezwa kwamba makada wote wa CCM wanaokwenda kutafuta uungwaji mkono katika kanda hiyo,wamekuwa wakipewa sharti linalowataka na wao wakubali kufanya kazi ya ziada kuwashawishi wajumbe kutoka katika kanda zao wamuunge mkono Wassira endapo naye ataamua kuweka jina.
Bofya hapa upate uhondo kamili
Habari za uhakika zilizopatikana kutoka mikoa inayounda Kanda ya Ziwa,zimetaja mwanasiasa huyo mkongwe nchini kwamba kwa sehemu kubwa amekuwa kikwazo kwa baadhi ya mitandao kujijenga katika ukanda huo.
Kanda ya Ziwa inatajwa kuwa moja ya kanda muhimu katika mbio za urais,ambayo imekuwa ikifanikisha ushindi wa si tu kwa wagombea urais,bali wote wanaosaka nafasi za juu za uongozi ndani ya CCM, na hasa ujumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) Taifa.
Kwa mujibu wa Habari hizo,Wassira ametajwa kuwa kikwazo kikuu kwa baadhi ya Makada wa CCM wenye nia ya kugombea urais mwaka 2015,baada ya wasimamizi wa mitandao hiyo kutakiwa kuweka msimamo wao wazi kwanza kama nao wako tayari kumuunga mkono mwanasiasa huyo endapo na yeye ataamua kujitosa katika kinyang'anyiro hicho cha urais.
Wassira anatajwa kukubalika kwa kiasi kikubwa katika ukanda huo wa Kanda ya Ziwa, na kwahiyo wengi wa wanamitandao ya urais 2015 wamekuwa wakipigana vikumbo kumtaka awaunge mkono katika mbio zao hizo, ili kupitia kwake waweze pia kuungwa mkono na wajumbe wa vikao vya uteuzi kutoka kanda hiyo.
Hata hivyo, gazeti hili limeambiwa kwamba matokeo ya vikumbo hivyo vya wanamitandao hiyo ya urais katika kanda hiyo ya Ziwa,yamekuwa si ya kuridhisha baada ya kubainika kuwa hata Wassira mwenyewe anayo nia ya kugombea urais mwaka 2015 ingawa yeye binafsi hajaweka wazi nia yake hiyo.
Kutokana na hali hiyo,imeelezwa kwamba makada wote wa CCM wanaokwenda kutafuta uungwaji mkono katika kanda hiyo,wamekuwa wakipewa sharti linalowataka na wao wakubali kufanya kazi ya ziada kuwashawishi wajumbe kutoka katika kanda zao wamuunge mkono Wassira endapo naye ataamua kuweka jina.
Bofya hapa upate uhondo kamili