Wasomi Wapinga: Dr. Lweitama adai Hakuna Mapya; Bashir Ally asema CCM haiwezi kufanikiwa kubadilika

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797

Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Azavery Lwaitama, alisema kuwa hakuna safu mpya ndani ya CCM kwani Kinana ni yule yule aliyekuwa akisimamia chaguzi zote zilizowaleta washindi kwa mizengwe.


Alisema hata Migiro licha ya kuwa mwadilifu lakini hana ushawishi mkubwa ndani ya CCM kama alivyo Prof. Anne Tibaijuka, kwani kutokana na utendaji wake angeingia kwenye safu hiyo angeweza kuwasaidia.

“Nguvu ya Migiro wakati huo ilikuwa UWT, kwa sasa si mbunge, hivyo bado ni vigumu kwa CCM kusema imepanga safu mpya ya kuwavusha. Kwa muda mfupi watafanikiwa kuweka ghiriba kwa watu lakini baadaye watarejea kulekule,” alisema.


Dk. Lwaitama aliweka bayana kuwa kilichofanyika ni kwa rais kutaka kuendelea kulifurahisha kundi la rafiki yake wa zamani, Edward Lowassa, baada ya kubaini kuwa ndiye nguvu ya CCM ili kuendeleza utamaduni wa viongozi kulindana.


Alifafanua kuwa Mukama ndiye alikuwa adui mkubwa wa Lowassa na kundi lake, hivyo asingeweza kuachwa aendelee na wadhifa wa ukatibu mkuu wakati hawafurahishi maswahiba wa Kikwete.


Mhadhiri huyo alibainisha kuwa Kikwete amebaini kuwa Lowassa ndiye nguvu ya CCM, hivyo amemua kumjengea mazingira ya kuwasambaratisha wanaompinga ili kuwe na utulivu ndani ya chama.


“Kwa hiki walichokifanya CCM ni dhahiri kuwa walioko ndani ya chama wataendelea kubaki wa walioko nje hawana sababu ya kuwashawishi kuingia huko,” alisema.


Naye mhadhiri mwingine wa UDSM, Bashir Ally, alisema kuwa hana hakika kama CCM wanaweza kufanikiwa kujibadilisha kwani wameacha kuhangaika na masuala ya msingi ili kuvuka hapa walipo.


“Ili uweze kusonga mbele kama taasisi ni lazima uwe na vitu vitatu, kwanza historia ya taasisi husika, pili ni dira au lengo la nini unataka kufanya na tatu ni nguvu ya rasilimali watu na vitu,” alisema.


Kwa mujibu wa mhadhiri huyo, CCM inayo nguvu kazi na vitu, yaani viongozi wengi wazuri na mali kama viwanja, majengo, magari na vinginevyo ila inakosa dira na historia yake.


Alisema kuwa wakati huu ulikuwa wa CCM kuhangaika na dira na historia ya nchi na chama chao, kujitambua kuwa wao ni chama cha wanyonge na si matajiri kama sasa.


“Huu si wakati wa wao kubadili sura za viongozi maana hilo wamefanya mara nyingi lakini hawajafanikiwa, hivyo lazima wajitafakari wametoka Dodoma na ajenda gani ya kuwatumikia wanyonge, watu wana njaa, wanaporwa viwanja, fedha zao zinatoroshewa nje, je, wamekuja na majibu hayo?” alihoji.


Bashir alipingana na kauli ya Rais Kikwete ya kuwalaumu wapinzani kuwa hawaoni mafanikio yaliyofanywa na CCM, akisema ni dhahiri kuwa hayo yanayofanyika si sehemu ya mahitaji yao ya msingi.


“CCM si chama cha matumaini ya watu wanyonge, tena kama zamani, hiki labda kinafaa kutawala Marekani kwa matajiri. Wamekuja na maazimio kwenye mkutano wao ambayo yalisemwa na CHADEMA kwenye ilani yao wakayapinga kuwa hayawezekani,” alisema.
 
Watu ni wale, viongozi ni walewale hakuna jipya , ufisadi ndan ya chama ni palepale nani anaweza kuchukua hatua juu ya mafisadi na walishindwa nini tangu awal. hakuna jipya bali ccm sasa ni chama cha matajiri maskini wataendelea kufa njaa kwa kushabikia ulaji wa wachache wasio na nia ya kuwakomboa. Watanzania wenzangu tubadilike !!!!!!
 
Wametutengenezea chupa mpya but mvinyo mmmh ni ule ule...........kumbe Mukama katoswa ili kumridhisha Loh-hasa??? yangu ni maombi tu sasa
 
Lwaitama kachemka,Lowasa kachezeshewa cheusi chekundu na hata safu ilioingia haiko upande wake nadhani hajui undani wa makundi ya CCM,huyu bashiri hua simuamini coz consistency yake ktk mijadala hua inafuata upepo,hebu mtafute shivji aseme hawa bado sana,angekuwapo chachage au horoub othman tungepanda analysis ya kina sio ushabiki tu wa kipuuzi
 
Lwaitama na Bashir ninyi ni wapinzani wa ccm na ccm ina wanachama wake ndio waliofanya uamuzi nyie mwaitakia nn? ubongo wenu msidhani ni bora kuliko wa wengine,, ccm kuwa chama cha wakulima na wafanyakazi haina maana kuzuia wa2 wengine kugombea nafasi hata kama ni matajiri msitudumaze watanzania maisha ya binadamu ni kusonga mbele acheni ushamba wa siasa , lwaitama nenda ukafundishe kama vp anzisha na wewe chama chako.
 
Huwa najiuliza kwamba nani anayefanya au kushawishi maamuzi kwenye CCM. Mwenyekiti, M/Mwenyekiti, Katibu, Sekretariati, Wanachama, NEC, Kamati Kuu? Kwani karibia vyote nilivyovitaja hapo vimefanyiwa mabadiliko isipokuwa Mwenyekiti na hakuna la maana lililotokea zaidi. Kwa hiyo naamini kabisa CCM inaendeshwa kwa matakwa na ushawishi mkubwa wa Mwenyekiti. Hizi zingine ni blah blah tu. CCM ipo mikononi mwa Mwenyekiti.
 
uKWELI MAANA YAKE NINI?NDEGE WA AINA MOJA HUTEMBEA PAMOJA WALIOCHGULIWA NI WANA CCM KWA MANUFAA YA CCM. KAMA LENGO LA CCM NI KULINDA MAFISADI NA UTAWALA WA KINDUGU BASI WALIOCHAGULIWA WANAJUKUMU HILO KAMA NI KUSAIDIA WANYONGE BASI SAFU YOTE ILIYOTEULIWA NI SAFI NI JUKUMLAO LA MSINGI NDO HILO. TUNASUBIRI TUONE LENGO LAO
 

Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Azavery Lwaitama, alisema kuwa hakuna safu mpya ndani ya CCM kwani Kinana ni yule yule aliyekuwa akisimamia chaguzi zote zilizowaleta washindi kwa mizengwe.

Alisema hata Migiro licha ya kuwa mwadilifu lakini hana ushawishi mkubwa ndani ya CCM kama alivyo Prof. Anne Tibaijuka, kwani kutokana na utendaji wake angeingia kwenye safu hiyo angeweza kuwasaidia.
hapo kwenye red vipi? hao akina mama wawili prof tibaijuka na dr migiro ni kina mama wa shoka sasa kudai mmoja ni zaidi ya mwengine simwelewi mzee rwaitama, au mzee rwaitama anataka kuleta kauhaya?
 
To me Lwaitama sounds like a "biggest loser" in his life. Sio analyst wa kutumainiwa kwa sasa kama alivyokuwa Seth Chachage, maoni yake yanaweza kuzua hisia za kikabila to some extent.

Tibaijuka ni Waziri na anatekeleza sera za chama ndani ya serikali ambalo ni jukumu kubwa sana kwake, leo hii unapokuja na agenda ya kusema kuwa ni bora zaidi ya Migiro na angepaswa kuwa ndani ya Sekretarieti! to me sounds like another hyper confusion in the political arena.

Na wasi wasi kuwa hajui majukumu ya sekretarieti ya Chama. Hii si kazi ya kuandaa vikao na kutawanyika baada ya vikao kwisha, hii ni kazi ya uratibu wa kila siku ndani ya chama katika ngazi ya utendaji na si sehemu ya kupumzika na kula shavu. Tibaijuka hapa atajigawaje kama mjumbe wa Sekretarieti (mtendaji ndani ya chama) na kama Waziri (mtendaji ndani ya Serikali)?.
 
halaf anapomtetea Mukama, mimi sio CCm lakini huyu Mukama kachemsha balaa na maamuzi ya msingi kabisa kumpiga chini kama kweli wanataka shinda 2015...huyu bwana nadhani ndio wale waliosemwa waache kutumia nguvu ya polisi katika siasa......
 
Lweitama anazeeka vibaya.

Kwani ameshafika umri wa kustaafu? naona grafu yake ya kufikiri ilishafika kwenye peak sasa ina decline.
 
Lwaitama na Bashir ninyi ni wapinzani wa ccm na ccm ina wanachama wake ndio waliofanya uamuzi nyie mwaitakia nn? ubongo wenu msidhani ni bora kuliko wa wengine,, ccm kuwa chama cha wakulima na wafanyakazi haina maana kuzuia wa2 wengine kugombea nafasi hata kama ni matajiri msitudumaze watanzania maisha ya binadamu ni kusonga mbele acheni ushamba wa siasa , lwaitama nenda ukafundishe kama vp anzisha na wewe chama chako.

Ha ha ha.. Tajiri agombee uongozi ili iweje..? Ana historia ya uongozi toka akiwa mdogo..? Tunachoona matajiri wote wanaingia kwenye uongozi kwenye chama chenu wanakuwa na sababu maalumu.. Nazo ni au kulinda au kuongeza wigo kwenye biashara zao na kupata unafuu au kutolipa kabisa kodi zao.. Na ndo maana kinazidi kuandamwa na kusakamwa.. No genuine efforts to cleanse it & there'll never be..!
 
Una maana Mukama ni Mhaya? Besides, nadhani ni vibaya kuhama kwenye hoja na kuanza kujadili makabilia. Inadidimiza uwezo wetu wa kufikiri nje ya boksi.
Uhaya unammshumbua eti Mukama aliweza,Tibaijuka angefaa.Wahaya kwa ukabila hawajambo
 
Lwaitama kachemka,Lowasa kachezeshewa cheusi chekundu na hata safu ilioingia haiko upande wake nadhani hajui undani wa makundi ya CCM,huyu bashiri hua simuamini coz consistency yake ktk mijadala hua inafuata upepo,hebu mtafute shivji aseme hawa bado sana,angekuwapo chachage au horoub othman tungepanda analysis ya kina sio ushabiki tu wa kipuuzi

Hujui huyo Lwaitama ni CDM?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom