Wasomi: Kitanda hakizai haramu. ..be civilized(l.w..)

Mkuki mchungu

New Member
Apr 9, 2011
3
0
Jamani mi nimeshindwa kuvumilia. kuna tetesi nilizipata toka kwa mwanazuoni mwenzangu kuwa dada mmoja(kitivo kapuni) wa hapa UD, amezalishwa na mnene mmoja (jina kapuni)hv mwenye madigrii kibao na vyeo kibao na heshima kibao. Cha kushangaza eti alimtosa mdada na mtoto. Kinachoniumiza zaidi ni jinsi mi binafsi NNAVYOMZIMIKIA jamaa kwa msaada wake anaoutoa full time hasa kwa wanazuoni. Jamaa anaonekana poa tena verry civilized inakuwaje hapa?? LAWSCHOOL.
Nliamua kuzifatilia na nkaambiwa huyo mdada alipigwa stop home kwao pale aliposhibishwa na jamaa na akahifadhiwa kwa muda na jamaa. Nlijifanya researcher nkaenda hadi home kwa mdada na mwanae na nkakuta hali ni ovyo sana tena inasikitisha. mara mtoto akalia, ile kumleta du!!! ni jamaa mtupu.
Mi nlidhani wanaume maskini, mafukara, wasioelimika ndo wanaotosa watoto, kumbe hata wanazuoni??? Tena wenye zao?? sasa hii ni roho mbaya au???
Wababa hakuna mwanamke anayejipa ujauzito. Hebu kuweni na huruma kwa hawa viumbe wa mola. Hv tutalimalizaje swala la utoaji mimba, uuaji wa watoto na watoto wa mitaani kama wote tutafanya hv?? Maisha magumu sana jamani, hebu tutumie walau elimu yetu ya madigrii kwa vitendo. Binafsi mama yangu alitendwa hv na dingi, yani wanajamii, mi na mama yangu tuliishi vibaya mno, nakumbuka kuna vipindi tulikuwa hatuli, wakati baba yangu mzazi alikuwa anabadilisha magari hadi leo yupo (kapuni) ingawa alitujali badaye, ilikuwa too late. Inauma sana. Wanajamii inakuwaje hapa hebu nisaidieni. Ntafatilia zaidi hadi nijue ukweli. Ila da kama ni kweli mi ntasikitika sana, Jamaa nnakuaminia kinoma na mi shabiki wako sana. wacha nfatilie.
 
Ni kweli kitanda hakizai haramu lakini vema kuwa mwaminifu na zaidi kuwa mwazi kwa mwezi kama huna mipango ya muda mrefu.
 
tusihukumu wababa kuna wadada wanatabia za kujitegeshea na kunganganizia mimba sasa unategemea nini,huo ndo ujira wao...
 
Jamani eee.. msipende kuingilia mapenzi ya watu. Hivi wewe ulikuwepo walivyokutana, wakapendana, wakachukuana, waka......... hadi wakazaa; wewe ulikuwa wapi?? Nani anashangaa ugomvi wa wapendanao?? wagombanao ndio wapatanao mbona hata kwenye ndoa ugomvi upo??? Waacheni wenyewe watapatana wenyewe msiwahukumu.
Katika kila mgogoro wa mahusiano ukichunguza utaona "THIRD PARTIES" wanahusika.
Kwani kibaya nini??? Tatizo waswahili washamba sana.. katika mapenzi hakuna digrii wala cheo, wala umri ( hii ni maalum kwa wale wanaoamini na kuyajua mapenzi halisi). Kwanini kumhukumu mtu???? We unajua wanapeana nini?? Na nyie wakaka mliozoea kuwaona wadada wote wanafata mali au pesa ni washamba, hiyo "NI WEAKNESS YENU NA YAONYESHA JINSI GANI MLIVYO INSECURED ABOUT BEING LOVED THE WAY U ARE" Ndo mana mnaishia kubwabwaja mali msizonazo na wengine kuiba ili tu eti ampate dada flani, kuhonga vijicent mnahonga na kupendwa hampendwi, kwa taarifa yenu wenzenu hawaongi na wanapendwa kama kawa. I think everyone is free and has the right to love anyone as long as one is happy and has peace with the loved ones. Sikatai wapo wadada wanaofata wanaume wenye nazo kwa maslahi yao wenyewe. Pia wapo wanaowapenda jinsi walivyo. Wanaume msiibe wala msisubiri mtajirike ndo mpendwe, kumbuka mdada anaweza akadondokea tabasamu lako tu au ucheshi wako tu au hata unavyoongea na akawa crazy na kugawa kilaaaa kitu mradi asikupoteze. Mdada mwizi utamjua tu........ kwanza hawezi kabisa kukaa miezi sita bila kumpa kitu ukategemea atadumu kwako. Akiona hamna dalili anaondoka mwenyewe hivyo waweza mpima wako.
Nanyi wanaume mliojaliwa acheni ushamba wa kuwaona wadada wa watu ni wezi. Mkiwa na mawazo hayo, mtaishia kutumiwa tu, mkishalea wanachomoka, kwa nini hamjiamini?????? Pesa si kila kitu, ndo mana wengi wana pesa na hawana amani. Kitu ukimpata yule unayeamini anakupenda na roho yako wewe ikapata amani. Haijalishi ni kidumu au wife.
Third parties acheni ushamba jamani, msiingilie mapenzi ya watu. Hujui na hutajua wanarudiana lini wapi na vipi. Mtaishia kupata aibu watu wazima. Waacheni hao tayari wana kitu kinachowaunganisha hivyo fanyeni yenu. ok!!!!!!!!!!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom