Wasira live tbc

Wasira live tbc

Afadhali ya huyu Mzee 'Tyson' Wassira akiacha zake hasira za ajabu ajabu huwa anaweza akapambanua japo jambo.

Je huyu Werema ndio tuseme ni wa nini huko tena kwa HUU MSWADA WENYE UTAPIAMLO badala ya kumchukua Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar mwenye uwezo wa kuacha sheria zenyewe zijieleze kupitia mdomoni mwake badala ya yeye Werema alivyo na kawaida ya kujieleza yeye binafsi badala ya kuzipa nafasi sheria zetu?????

Kama ningalikua na mamlaka huyu Werema ningempeleka kujifunza kazi Mahakama ya Wilaya huko Kifuandui walau kwa kipindi cha miaka miwili na badala yake Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Mhe Makungu kuchukua nafasi yake katika ofisi ya serikali ya Muungano.

Werema ..., bure kabisa!!!

Sijui nitumie lugha gani lakini ni MAKOSA MAKUBWA kwa hali ilivyo sasa (baada ya kuundwa kwa serikali y umoja wa kitaifa) kwa viongozi kutoka Tanzania Bara kuongea mambo yanayogusia Zanzibar bila uwepo wa uwakilishi kutoka Zanzibar. Kwa mfano huu mswada ni wa Jamhuri ya Muungano, sasa kwa nini ni viongozi wawili tu toka Bara (Werema & Wassira) ndio wako TBC? Hao waliowatuma Wasira na Werema kuja TBC kwa nini wasimwalike mwanasheria mkuu wa Zanzibar ajumuike nao kuuza huu mswada?
 
Nimejaribu kuufuatilia mjadala lakini sipati chochote zaidi ya utetezi wa Wasira na Werema juu ya mapungufu ya muswada wa katiba, kimsingi kinachoonekana kuna kampeni ya ccm kujisafisha dhidi ya madudu yao kupitia vyombo vya habari.
 
MHESHIMIWA WASSIRA ALIPATAJE KUTEULIWA KUWA WAZIRI WA UTAWALA BORA KAMA
HATA MAMBO MADOGO MADOGO NDANI YA HII DHANA PANA SANA BADO
YAONEKANA KUMPASHIDA; AU NI MAKUSUDI TU!!!

Eti huyo ndio Waziri wa Utawala Bora asiyejua hata maana ya Katiba na kwamba ni mdau yupi aliye ha jukumu gani mle ndani.

Eti Rais ndiye Mkuu wa Nchi hivyo kuunda Tuma wa Kujitengenezea yeye Mkataba (Katiba) ambayo ndio sisi wananchi tunatarajiwa tuje tuutumie kama msingi wa kumuajiri nayo rais huyo huyo kazi; Subutu Mzee Wasira - hilo kaliondoe kabisaaaaaaaaaaaa akilini mwako mpaka darini!!!

Kama ambavyo unavyomuona Rais Kikwete kuwa ni Mkuu wa Nchi na hivyo vivyo ndivyo alivyo Mkuu wa Chama kimojawapo Mshindani katika vinyang'anyiro mbalimbali vya siasa hapa nchini hivyo kamwe Kikwete hawezi hata siku moja kujitualia jukumu la kutengeneza SHERIA MAMA ambayo ndiyo itakayotumika kuamulia mchezo mzima wa USHINDANI kati ya Chama Chake (CCM) dhidi ya vile ambavyo ambavyo haviongozi yeye.

Nadhani kesho akiamka waziri huenda DHANA YA UTAWALA BORA nao ukawa umeamka ndani yake na akaanza kuifanyia kazi kwa njia nyoofu bila kupindisha pindisha mambo kwa maslahi binafsi ya siku mbili tatu hivi.

Wasira amesema rais ndo ataunda tume sababu yeye ndo mkuu wa nchi
 
yani nimeshindwa kuvumilia na kuendelea kuwatazama hawa majuha wanapotosha wananchi kwa gharama zetu walipa kodi
 
Mi nimeckiliza bt wakiulizwa swali wanajibu utumbo,hata confidence ya kujib maswali hawana,wangemleta lissu pangewaka moto kwan lissu ni kiboko cha werema.
 
Hii kweli ni hoja ya msingi kabisaaaa ulivyosema ndugu yangu wala tusikalie ukweli na ukweli mtupu unaposemwa.

Sijui nitumie lugha gani lakini ni MAKOSA MAKUBWA kwa hali ilivyo sasa (baada ya kuundwa kwa serikali y umoja wa kitaifa) kwa viongozi kutoka Tanzania Bara kuongea mambo yanayogusia Zanzibar bila uwepo wa uwakilishi kutoka Zanzibar. Kwa mfano huu mswada ni wa Jamhuri ya Muungano, sasa kwa nini ni viongozi wawili tu toka Bara (Werema & Wassira) ndio wako TBC? Hao waliowatuma Wasira na Werema kuja TBC kwa nini wasimwalike mwanasheria mkuu wa Zanzibar ajumuike nao kuuza huu mswada?
 
wakuu, nyie ambao mnawasikiliza mtuambie kile wanachozungumza, sisi wengine tuko mbali na hilo ni jambo la muhimu, sio thread inaanzishwa halafu mnaponda tu, wengine hatujui hata nini kinaendelea,

Hata kama ni utumbo hebu mtujulishe nini kinazungumzwa huko..

Kaka wewe umenena jamani JF tusiwe tunaponda tuuuuu ila tuelimishe so, Mjadala ulikua kama ifuatavyo:-

-Wasira kasema na leo kweli nimemshagaa sana akua wasira kama ninayemjua katulia na kaongea jambo la msinngi kuwa mswada wa kupata katiba mpya utachapishwa kwa lugha ya kiswahili na pia umma utaelimishwa na kutoa maoni kupitia wabunge wao, vyombo vya habari NK na wabunge watapewa copy ili waende majimboni mwao kuelimisha.
-watu wasiwe na uoga wowote kuwa huu si mchakato wa kujadili katiba laa, huu ni mchakato wa kujadili kwenda kupata katiba mpya.
-mjadala kuhusu muungano kasema utajadiliwa ruksa ila kwa maudhui yake hapo sina utaalamu wanasheria naomba mtusaidie.
-Kasema maudhui ya kupata ktiba mpya ni sawa ila kwa maoni yake kuwa bado yapo mengine ya msingi yatachukuliwa kwenye hii ya sasa mfano; DINI kuna kifungu katika katiba ya sasa kimejitosheleza kuhusu serikali na madhehebu ya kidini sikifahamu vizuri.

Warema;
-ajikanyaga sana kuwa mswada aukua na kasoro yoyote
-jukumu la kuchagua tume huru tusahau kabisa ni jukumu la rais wa tz na znz kutokana na katiba ya sasa inavyosemwa so, nyie wanasheria naomba kabla ya kwenda kwenye mswada halisi embu tengueni hicho kipengele kinachomruhusu rais kuwa na mamlaka ya kuchagua tume ili hayo mamlaka yarudishwe kwa wananchi kwanza kuliko kulaamu tuuu then mwisho wake wanatupiga bao.
-wako kwenye mjadala hata kesho anaenda znz kujadili na mwanasheria wao ili wapate kauli mbiu kuhusu muungano.
-kamati or tume aitahusisha wanasiasa ila itateuliwa na rais kutoka watu mbalimbali kama kina shevji, bomani, etc so, hapa hata kama wanasiasa hawachaguliwi ila watakaochaguliwa nahisi ni mrengwa wa rais or kada wa chama ila kama wananchi watashirikiswa+wanaharakati kwenda kuchagua tume basi itakua huru tuwe makini hapa wajanja hawa.

Maswali:
znz-kunawakati walishawakilisha maoni yao kwenye tume ya mswada wa katiba ya znz moni 14 lakini hata moja alikuchukuliwa kwenye tume?

Jibu la warema: si lazima maoni yote yakubalike inawezekani yako au yangu yakakubalika lakini si yote yakubalike so, nawasiwasi hata haya maoni yetu si yote yatakubalika ila yakwao ndio yakayokubalika tuwe makini hapa wana JF.

Rais anakuaje na madaraka ya kutuchagulia tume? na ukizingatia yeye ni chama tawala na hatakao wachagua aidha watakua na mrengo wake?

Jibu kwa wasira- Ingawa katiba inasema ivyo na baadhi ya mifano aliyotoa pia alisema na hilo kama mnaliona halifai basi ni jambo la kulijadili.

So wana JF hapa zaidi ukiangalia majibu na katiba ya sasa naomba, naomba nyie kina tundu lissu akikisheni kabla ya kujadili huu mswada tengueni kile kifungu kinachomruhusu raisi kuteua tume au kuwa na madaraka ya kuchagulia katiba hiki ni muhuimu sana kabla ya yote

Nawakilisha
 
Kaka wewe umenena jamani JF tusiwe tunaponda tuuuuu ila tuelimishe so, Mjadala ulikua kama ifuatavyo:-

-Wasira kasema na leo kweli nimemshagaa sana akua wasira kama ninayemjua katulia na kaongea jambo la msinngi kuwa mswada wa kupata katiba mpya utachapishwa kwa lugha ya kiswahili na pia umma utaelimishwa na kutoa maoni kupitia wabunge wao, vyombo vya habari NK na wabunge watapewa copy ili waende majimboni mwao kuelimisha.
-watu wasiwe na uoga wowote kuwa huu si mchakato wa kujadili katiba laa, huu ni mchakato wa kujadili kwenda kupata katiba mpya.
-mjadala kuhusu muungano kasema utajadiliwa ruksa ila kwa maudhui yake hapo sina utaalamu wanasheria naomba mtusaidie.
-Kasema maudhui ya kupata ktiba mpya ni sawa ila kwa maoni yake kuwa bado yapo mengine ya msingi yatachukuliwa kwenye hii ya sasa mfano; DINI kuna kifungu katika katiba ya sasa kimejitosheleza kuhusu serikali na madhehebu ya kidini sikifahamu vizuri.

Warema;
-ajikanyaga sana kuwa mswada aukua na kasoro yoyote
-jukumu la kuchagua tume huru tusahau kabisa ni jukumu la rais wa tz na znz kutokana na katiba ya sasa inavyosemwa so, nyie wanasheria naomba kabla ya kwenda kwenye mswada halisi embu tengueni hicho kipengele kinachomruhusu rais kuwa na mamlaka ya kuchagua tume ili hayo mamlaka yarudishwe kwa wananchi kwanza kuliko kulaamu tuuu then mwisho wake wanatupiga bao.
-wako kwenye mjadala hata kesho anaenda znz kujadili na mwanasheria wao ili wapate kauli mbiu kuhusu muungano.
-kamati or tume aitahusisha wanasiasa ila itateuliwa na rais kutoka watu mbalimbali kama kina shevji, bomani, etc so, hapa hata kama wanasiasa hawachaguliwi ila watakaochaguliwa nahisi ni mrengwa wa rais or kada wa chama ila kama wananchi watashirikiswa+wanaharakati kwenda kuchagua tume basi itakua huru tuwe makini hapa wajanja hawa.

Maswali:
znz-kunawakati walishawakilisha maoni yao kwenye tume ya mswada wa katiba ya znz moni 14 lakini hata moja alikuchukuliwa kwenye tume?

Jibu la warema: si lazima maoni yote yakubalike inawezekani yako au yangu yakakubalika lakini si yote yakubalike so, nawasiwasi hata haya maoni yetu si yote yatakubalika ila yakwao ndio yakayokubalika tuwe makini hapa wana JF.

Rais anakuaje na madaraka ya kutuchagulia tume? na ukizingatia yeye ni chama tawala na hatakao wachagua aidha watakua na mrengo wake?

Jibu kwa wasira- Ingawa katiba inasema ivyo na baadhi ya mifano aliyotoa pia alisema na hilo kama mnaliona halifai basi ni jambo la kulijadili.

So wana JF hapa zaidi ukiangalia majibu na katiba ya sasa naomba, naomba nyie kina tundu lissu akikisheni kabla ya kujadili huu mswada tengueni kile kifungu kinachomruhusu raisi kuteua tume au kuwa na madaraka ya kuchagulia katiba hiki ni muhuimu sana kabla ya yote

Nawakilisha

mkuu, asante kwa summary nzuri. at least nimepata mwanga..maana nilikuwa naona watu wanaponda tu, na sikujua wanachoponda ni nini...Kweli JF ni zaidi ya uijuavyo
 
Werema eti alikua hajui nchi tulikabidhiwa toka kwa Malkia au mfalme wa uingereza??? akadesa kwa Wasira!
 
wasira sijamsoma kabisa mswada ulishaondolewa bado anautetea inavoonekana mswada utachakachuliwa na kurudiswa ureure wapo kutuanda wadanganyika

I wish you would have stopped calling us so Bro!!!! They made some of us believe so and we go on "proudly" calling ourselves so!!!!
All in all it is too late for Wassira and Company to bring back the rubbish (constitution review bill) they had presented, for they have now got to abide by the will of the Tanzanians if not Tanganyikas.
 
mkuu omba radhi, kwanza wassira sio mkurya na huu utumbo wako unatunyima haki wakurya, hao wasio wawakilishi wa wakurwa, na wakurya wana nguvu ya umma na mawazo ya kujenga hacha mambo ya ya ovyo
wakurya hao, kwani huwajui?
 
Werema anaposema wameona kwenye mswada huo waweke sheria itakayo zuia watu wengine kuzomea wenzao wakati wa utoaji maoni! Hii ni tafsiri au kejeli.
Kwanza yeye awali kama kawaida alisema muda muafaka Bado, leo ameagizwa na nani kukubali muda umefika!
Wasira anasema uamuzi wa kubadili unatokana na katiba iliyopo kuwa na miaka 50, hivi hii ni akili kweli?
 
Mswada kuondolewa bungeni umeondolewa ila tatizo ni kwamba haujafutwa ili uandaliwe mwingine, tunaendelea kuujadili uleule na haujadiliki. kilichotakiwa ni wananchi ndio waandae muswada huo kupitia ngos zao,mitaa,wawakilish nk,yaani muswada uandaliwe na wananchi, ujadiliwe na ndio upelekwe bungeni. Nawashangaa na siwaelewi wanaosema kwamba huo ni muswada tu sio katiba hivyo haina haja kuupinga,hivi hawajui kwamba mswada mbovu utaleta katiba mbovu kama ukipitishwa?
 
Huyu Wassira historia yake sio mtu wa maadili kwani alishapatwa na hatia ya kutoa rushwa huko nyuma; ukweli ni kwamba ni mtu ambae ni mganga njaa ambae mtu yeyote mwenye kumlipa dau kubwa anaweza kumtumia!! Hawa ccm Asili lazima wawe macho na Wassira kwani yumo humo kwa maslahi yake binafsi na sio ccm kwani hata alipokuwa NCCR alikuwa hivyo hivyo na njaa ndio iliyomfanya kumfuata marehemu Mzee Kawawa ambae ndio aliyemuombea kwa Mkapa ili arudi kundini baada ya katibu mkuu Mangula kumkatalia katakata kwani aliogopa kuanzisha makundi yanayokitafuna chama hivi sasa.
 
mimi nina hakika wasira wakimvua gamba hatakimbilia chadema kesho asubuhi, huyo bwana siasa kwake ni kama mtaji tu, muulize warioba wanajuana vizuri, hata kurudi kwake ccm ni uvyeo tu ndio tulimrudisha, hana issue
 
Back
Top Bottom