Wasiotaka kuoa/kuolewa wakamatwe

mlinzi mlalafofofo

JF-Expert Member
Apr 20, 2008
277
548
Inafahamika kuwa ndoa ni kitovu cha malezi na makuzi bora katika jamii yoyote duniani. Nje ya ndoa mtu wa aina yoyote anaweza kuzalishwa, mzuri au mbaya, japo mara nyingi uwezekano mkubwa ni kuzaliwa kwa machokoraa, wala ngada n.k.

Imesikika mara nyingi kuwa moja ya sababu kubwa ya watu kushindwa kuoana ni hali ngumu ya kiuchumi.

Kwaiyo basi mimi mlinzi mlalafofofo kama mlipa kodi halali naishauri serikali yangu kugharamia harusi ya kwanza ya mja awaye yoyote ndani ya jamhuri ili kama taifa tuwawezeshe wale wote wenye nia ya kuishi katika muungano wa ndoa.

Kwa wale wote wanaoendelea kuishi kama mke na mume wakipika na kupakua miaka na miaka bila kuwa na mpango wowote wa kuingia makubaliano ya ndoa, watu wa aina hii wamulikwe na sheria na ikiwezekana wakamatwe na kuhojiwa sababu ya wao kufanya hivyo.

Au nasema urongo wajameni?
 
Shida sio kuoa, shida ni gharama baada ya kuoa,
Gharama ya chakula, malazi, burudani, matibabu,


In short, Vijana hatutaki kuoa tumeona wazee mlivyoteseka na ndoa zenu
Wanatupiga vizinga kila siku, hadi unaona kabisa mwamba anateswa na familia. Sasa ya nini kuingia kwenye mateso, eti wenyewe wanasema ndio uanaume, uanaume ni kujitafuta hadi ujipate hata ukiwa una 40+ utalea familia yako kwa amani.

Big up kwa roll model wangu, Kris Lukos, kajisakaaa hadi akaona mwanga, ndio akaanzisha familia. Mwamba ana 56 mtoto wa kwanza ana 14, dadeq analea bila stress.
 
Inafahamika kuwa ndoa ni kitovu cha malezi na makuzi bora katika jamii yoyote duniani. Nje ya ndoa mtu wa aina yoyote anaweza kuzalishwa, mzuri au mbaya, japo mara nyingi uwezekano mkubwa ni kuzaliwa kwa machokoraa, wala ngada n.k.

Imesikika mara nyingi kuwa moja ya sababu kubwa ya watu kushindwa kuoana ni hali ngumu ya kiuchumi.

Kwaiyo basi mimi mlinzi mlalafofofo kama mlipa kodi halali naishauri serikali yangu kugharamia harusi ya kwanza ya mja awaye yoyote ndani ya jamhuri ili kama taifa tuwawezeshe wale wote wenye nia ya kuishi katika muungano wa ndoa.

Kwa wale wote wanaoendelea kuishi kama mke na mume wakipika na kupakua miaka na miaka bila kuwa na mpango wowote wa kuingia makubaliano ya ndoa, watu wa aina hii wamulikwe na sheria na ikiwezekana wakamatwe na kuhojiwa sababu ya wao kufanya hivyo.

Au nasema urongo wajameni?
Bill gets hana mke hivi sasa, je hali yake ya uchumi ikoje
 
mbona unavuka uhuru wa watu mkuu. Ndoa ni hiari. Labda tuseme wazinifu wakamate wapewe kesi ya uhaini na uhujumu uchumi
 
Back
Top Bottom