Ndallo
JF-Expert Member
- Oct 1, 2010
- 7,619
- 4,292
Tukiwa tunaelekea kwenye uchaguzi wa wabunge jimbo la Arumeru Mashariki baada ya kutokea kifo cha muheshimiwa Sumari, lilijitokeza dosari moja kutoka kwa wanaojiita wazee wakimila wanaojulikana kama Washili kua hawatakubaliana na musheshimiwa Godbless Lema kufanya kampeni kwa mgombea wa Chadema kwakua alitoa maneno ya kashfa kwenye mazishi ya muheshimiwa Sumari ambayo kwao Washili hao wameona kitendo hicho kimewazalilisha.
Basi habari zinazoendelea hapa maeneo ya Usa River na vitongoji vilivyojirani na jimbo hili la Arumeru Mashariki ni kua Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimepata habari kua vizee hivyo vinavyojiita Washili ni usanii fulani kukwamisha juhudi za chama cha chadema kukosa nguvu kumbe vizee hivi vinatumia kinga hii ya kikwako kwakujiita wazee wa jadi huku wakipeleka nguvu kwa watoto wao wanaogombea kinyanganyiro hiki cha ubunge Arumeru Mashariki.
Mtakumbuka pia vizee hivi ndivyo vilivyotoa kauli na kuweka matangazo mji mzima wa Arusha kua watavunja chungu kwa wale woote waliohusika na sakata lile lililopelekea kwa kijana wao ambae ni mfanyabiashara maarufu aliyetumikia kifungo cha miaka mitano jela kwakile walichosema alihusika na mauaji yakutumia silaha na kupora madini ya wafanyabiashara wenye asili ya Kiasia. Washili hawa walitaka waliohusika wajitokeze ili waombe msamaha ama sivyo watavunja chungu, lakini tukio hili likaishia hewani.
Chadema imeshashtukia njama hizi zinazoendelea kupitia kwa vizee hivi vinavyojiita Washili ili kukwamisha juhudi za Chama Cha Demokrasia na Maendeleo lakini shime Chadema tusonge mbele! ALUTA CONTINUE!
Basi habari zinazoendelea hapa maeneo ya Usa River na vitongoji vilivyojirani na jimbo hili la Arumeru Mashariki ni kua Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimepata habari kua vizee hivyo vinavyojiita Washili ni usanii fulani kukwamisha juhudi za chama cha chadema kukosa nguvu kumbe vizee hivi vinatumia kinga hii ya kikwako kwakujiita wazee wa jadi huku wakipeleka nguvu kwa watoto wao wanaogombea kinyanganyiro hiki cha ubunge Arumeru Mashariki.
Mtakumbuka pia vizee hivi ndivyo vilivyotoa kauli na kuweka matangazo mji mzima wa Arusha kua watavunja chungu kwa wale woote waliohusika na sakata lile lililopelekea kwa kijana wao ambae ni mfanyabiashara maarufu aliyetumikia kifungo cha miaka mitano jela kwakile walichosema alihusika na mauaji yakutumia silaha na kupora madini ya wafanyabiashara wenye asili ya Kiasia. Washili hawa walitaka waliohusika wajitokeze ili waombe msamaha ama sivyo watavunja chungu, lakini tukio hili likaishia hewani.
Chadema imeshashtukia njama hizi zinazoendelea kupitia kwa vizee hivi vinavyojiita Washili ili kukwamisha juhudi za Chama Cha Demokrasia na Maendeleo lakini shime Chadema tusonge mbele! ALUTA CONTINUE!