brigedia mafia
JF-Expert Member
- Jul 21, 2016
- 2,264
- 2,275
Wafuatao ni wanamuziki wanaolazimisha fani hali ya kuwa uwezo wao mdogo/umepungua kwa kiasi kikubwa
1: Juma Kasimu kiroboto a.k.a Nature
Huyu jamaa nyimbo zake anazozitoa siku hizi zinaboa sana kuliko kufurahisha , Nature bhana alikuwa kipindi hicho cha Sonia au mtoto Idd ila siku hizi anazingua tu analazimisha kitu ambacho hakiwezi
Hata ukae usikilize nyimbo zake za zamani na za sasa hivi ni ukweli usiopingika kwamba nyimbo zake za zamani zilikuwa na amsha amsha sana tofauti na za siku hizi
Ushauri: Napenda kumshauri Nature aendelee tu na kilimo kama cha vitunguu ,nyanya ,mpunga nk ndio kitu anachokiweza mziki aachane nao kabisa maana kila wimbo anaoutoa ni mbaya kuliko uliopita=full]419787[/ATTACH]
2: Kr Mullah
Binafsi huyu jamaa huwa sielewi watu wanampendea nini kwanza mchafu ,hajielewi yaan yupo yupo tu kwa kifupi na hata leo ukiniuliza wimbo alioimba Kr si ujui hata mmoja sina uhakika kama ana wimbo wowote huyu jamaa zaidi ya kuimba vipande vichache alivyoimba alipokuwa TMK wanaume family
Nashangaa sana mvutano baina ya TID mnyama na Nature kuhusu huyu jamaa
Ushauri: namshauri kr aende sober house kwanza arudi katika hali ya kawaida kisha aachane na mziki akawe konda wa daladala atapendeza sana tena na hivi unadhifu kwake ni zero atafaa sana maana asilimia kubwa ya makonda ni watu wasiojipenda (wachafu wachafu)
View attachment 419710
3: Snura Mushi
Huyu dada naye mziki haujui kabisa zaidi ya uswahili swahili tu na kuchezesha chezesha makalio kila kukicha
Mashabiki wake wengi wanampendea anavyomwaga radhi hovyo kwenye show zake na kwenye video zake lakini si uwezo wake wa uimbaji
Ushahidi wa huu upo kwenye video ya chura, chura iliyofungiwa ilimpa kiki sana na ilipendwa sana ila tazama chura ya sasa hivi ambayo imefuata maadili ,watu wengi hawaikubali wala nini na ndio maana huyu dada kila kukicha anagombana na Basata kwa kosa la kuvunja maadili kwa kuwa anajua fika asipovunja maadili na kuyaanika maungo ya kike show zake zitamdodea ndio maana anafanya juu chini kutafuta watu wa kumwaga radhi kwenye show zake
Ushauri: namshauri aache kuimba mziki ajiunge na hawa wanaocheza na kanga moja jukwaani au ajiunge na hawa wanaopiga vigoma asilia au watu wa baikoko ndio kitu an
achokiweza
4:Lina Sanga
Huyu naye tangu atoe wimbo wa olethemba hamna cha maana alichokibakisha kwenye mziki bora aachane nao kabisa aangalie kingine cha kufanya.Inaonesha huyu mwanadada kuna mtu alisimama nyuma yake kumsukuma kwenye mambo yake ya mziki sasa inaonekana jamaa kashaonja tunda akaona amtose mazima na kusababisha binti ayumbe sana
Ushauriamoja na kuyumba sana kimziki huyu binti kipaji bado anacho sema kinaachotakiwa inabidi abadili aina ya mziki anaoimba ,inabidi akaimba nyimbo zinazomtukuza Mungu atapendeza sana ,huyu binti anajua sana kuimba nyimbo za kuleta faraja mfano mzuri wimbo wake wa malkia wa nguvu
5: Enock Bella
Huyu dogo naye kuimba hajui ila anafichwa na uwepo wa kwenye kundi
Sidhani kama anaweza kusimama peke yake kama msanii wa kujitegemea pasi na kumshirikisha yeyote kwenye wimbo wake
Ushauri: namshauri kijana aendeleze kipaji chake cha ku dance atafika mbali kama mwenzake Mose Iyobo
6: Aika
Huyu demu kwa kiasi kikubwa anamtegemea sana Nahreel ila yeye binafsi kutoa wimbo wa peke yake na ku hit si rahisi ,ukitaka kuamini hivyo msikilize kwenye interview mbalimbali akiambiwa aimbe uone vichekesho
Ushauri: namshauri huyu msichana atafute pesa za haraka haraka aboreshe gym fitness center yake na vibiashara vyake vidogo vidogo maana atakapopigwa chini tu na Nahreel huo ndio utakuwa mwisho wake wa mziki ,sasa ni bora aboreshe zaidi huku na kuwekeza nguvu ya kutosha kuliko kujichosha na mziki maana kuimba hajui
7:Temba
Huyu jamaa naye mziki umemkalia kushoto sana siku hizi ingawaje analazimisha tu ,tofauti na zamani enzi za nampenda yeye, side mnyamwezi, mkono mmoja ,nyimbo nyingi anazotoa siku hizi anakuwa anaongea ongea tu mwanzo mwisho badala ya kuimba
Ushauri: huyu jamaa naona inabidi apewe msasa wa kutosha na Mrisho Mpoto awe naye ana ghani mashairi maana huko ni kuongea ongea tu mwanzo mwisho kama anavyofanya mpoto au kama vipi arudi kwenye fani yake ya kucheza kikapu atapendeza sana na urefu wake.
10:Ally Kiba
Huyu kijana bado ni mwanamuziki mzuri tu na sauti pia si haba tatizo ni kuwa ni mtu mwenye majivuno,vijembe asiye na muelekeo na mtu mwenye kisirani,lawama naasiye penda maendeleo ya mwingine sana sana hapendi kumuona Daimond anavyofanikiwa ,ushahidi wa haya maelezo ,muangalie interviews nyingi anazofanya utagundua jamaa ana kijiba cha roho na mkaanga sumu hodari,usipate shida kumjua macho yake tu yanadhihirisha hayo ,inaonekana kungekuwa kuna sehemu wanauza uchawi angenunua kitambo sana
Ushauri: kijana nafasi ya kubadillika bado ipo badilika haraka sana kabla mambo hayajakuchachia
La sivyo kaimbe taarabu ndio mziki utakao uweza maana ndio mziki uliojaa majungu,wivu, visirani ,uchawi na kuombeana mabaya kila kukicha si ajabu kuona wasanii wa taarabu kutoka bendi mbili tofauti wakikaushiana pindi wakutanapo pamoja kwenye ishu yeyote ile hata kama msibani wataliana bati na si ajabu vijembe vikaanza hapo hapo msibani
1: Juma Kasimu kiroboto a.k.a Nature
Huyu jamaa nyimbo zake anazozitoa siku hizi zinaboa sana kuliko kufurahisha , Nature bhana alikuwa kipindi hicho cha Sonia au mtoto Idd ila siku hizi anazingua tu analazimisha kitu ambacho hakiwezi
Hata ukae usikilize nyimbo zake za zamani na za sasa hivi ni ukweli usiopingika kwamba nyimbo zake za zamani zilikuwa na amsha amsha sana tofauti na za siku hizi
Ushauri: Napenda kumshauri Nature aendelee tu na kilimo kama cha vitunguu ,nyanya ,mpunga nk ndio kitu anachokiweza mziki aachane nao kabisa maana kila wimbo anaoutoa ni mbaya kuliko uliopita=full]419787[/ATTACH]
2: Kr Mullah
Binafsi huyu jamaa huwa sielewi watu wanampendea nini kwanza mchafu ,hajielewi yaan yupo yupo tu kwa kifupi na hata leo ukiniuliza wimbo alioimba Kr si ujui hata mmoja sina uhakika kama ana wimbo wowote huyu jamaa zaidi ya kuimba vipande vichache alivyoimba alipokuwa TMK wanaume family
Nashangaa sana mvutano baina ya TID mnyama na Nature kuhusu huyu jamaa
Ushauri: namshauri kr aende sober house kwanza arudi katika hali ya kawaida kisha aachane na mziki akawe konda wa daladala atapendeza sana tena na hivi unadhifu kwake ni zero atafaa sana maana asilimia kubwa ya makonda ni watu wasiojipenda (wachafu wachafu)
View attachment 419710
3: Snura Mushi
Huyu dada naye mziki haujui kabisa zaidi ya uswahili swahili tu na kuchezesha chezesha makalio kila kukicha
Mashabiki wake wengi wanampendea anavyomwaga radhi hovyo kwenye show zake na kwenye video zake lakini si uwezo wake wa uimbaji
Ushahidi wa huu upo kwenye video ya chura, chura iliyofungiwa ilimpa kiki sana na ilipendwa sana ila tazama chura ya sasa hivi ambayo imefuata maadili ,watu wengi hawaikubali wala nini na ndio maana huyu dada kila kukicha anagombana na Basata kwa kosa la kuvunja maadili kwa kuwa anajua fika asipovunja maadili na kuyaanika maungo ya kike show zake zitamdodea ndio maana anafanya juu chini kutafuta watu wa kumwaga radhi kwenye show zake
Ushauri: namshauri aache kuimba mziki ajiunge na hawa wanaocheza na kanga moja jukwaani au ajiunge na hawa wanaopiga vigoma asilia au watu wa baikoko ndio kitu an
4:Lina Sanga
Huyu naye tangu atoe wimbo wa olethemba hamna cha maana alichokibakisha kwenye mziki bora aachane nao kabisa aangalie kingine cha kufanya.Inaonesha huyu mwanadada kuna mtu alisimama nyuma yake kumsukuma kwenye mambo yake ya mziki sasa inaonekana jamaa kashaonja tunda akaona amtose mazima na kusababisha binti ayumbe sana
Ushauriamoja na kuyumba sana kimziki huyu binti kipaji bado anacho sema kinaachotakiwa inabidi abadili aina ya mziki anaoimba ,inabidi akaimba nyimbo zinazomtukuza Mungu atapendeza sana ,huyu binti anajua sana kuimba nyimbo za kuleta faraja mfano mzuri wimbo wake wa malkia wa nguvu
5: Enock Bella
Huyu dogo naye kuimba hajui ila anafichwa na uwepo wa kwenye kundi
Sidhani kama anaweza kusimama peke yake kama msanii wa kujitegemea pasi na kumshirikisha yeyote kwenye wimbo wake
Ushauri: namshauri kijana aendeleze kipaji chake cha ku dance atafika mbali kama mwenzake Mose Iyobo
6: Aika
Huyu demu kwa kiasi kikubwa anamtegemea sana Nahreel ila yeye binafsi kutoa wimbo wa peke yake na ku hit si rahisi ,ukitaka kuamini hivyo msikilize kwenye interview mbalimbali akiambiwa aimbe uone vichekesho
Ushauri: namshauri huyu msichana atafute pesa za haraka haraka aboreshe gym fitness center yake na vibiashara vyake vidogo vidogo maana atakapopigwa chini tu na Nahreel huo ndio utakuwa mwisho wake wa mziki ,sasa ni bora aboreshe zaidi huku na kuwekeza nguvu ya kutosha kuliko kujichosha na mziki maana kuimba hajui
7:Temba
Huyu jamaa naye mziki umemkalia kushoto sana siku hizi ingawaje analazimisha tu ,tofauti na zamani enzi za nampenda yeye, side mnyamwezi, mkono mmoja ,nyimbo nyingi anazotoa siku hizi anakuwa anaongea ongea tu mwanzo mwisho badala ya kuimba
Ushauri: huyu jamaa naona inabidi apewe msasa wa kutosha na Mrisho Mpoto awe naye ana ghani mashairi maana huko ni kuongea ongea tu mwanzo mwisho kama anavyofanya mpoto au kama vipi arudi kwenye fani yake ya kucheza kikapu atapendeza sana na urefu wake.
10:Ally Kiba
Huyu kijana bado ni mwanamuziki mzuri tu na sauti pia si haba tatizo ni kuwa ni mtu mwenye majivuno,vijembe asiye na muelekeo na mtu mwenye kisirani,lawama naasiye penda maendeleo ya mwingine sana sana hapendi kumuona Daimond anavyofanikiwa ,ushahidi wa haya maelezo ,muangalie interviews nyingi anazofanya utagundua jamaa ana kijiba cha roho na mkaanga sumu hodari,usipate shida kumjua macho yake tu yanadhihirisha hayo ,inaonekana kungekuwa kuna sehemu wanauza uchawi angenunua kitambo sana
Ushauri: kijana nafasi ya kubadillika bado ipo badilika haraka sana kabla mambo hayajakuchachia
La sivyo kaimbe taarabu ndio mziki utakao uweza maana ndio mziki uliojaa majungu,wivu, visirani ,uchawi na kuombeana mabaya kila kukicha si ajabu kuona wasanii wa taarabu kutoka bendi mbili tofauti wakikaushiana pindi wakutanapo pamoja kwenye ishu yeyote ile hata kama msibani wataliana bati na si ajabu vijembe vikaanza hapo hapo msibani