Makini
Senior Member
- Dec 23, 2014
- 154
- 59
Utaratibu wa kuwazawadia wananchi wanaotoa taarifa za ukwepaji wa kodi umeokoa Sh. 11, 084,166,416 baada ya wasamaria wema 62 kutoa taarifa za vitendo vya ukwepaji kodi.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Idara ya Elimu na Huduma kwa Mlipa kodi TRA, Richard Kayombo, alisema utaratibu huo ni moja ya mipango iliyobuniwa na mamlaka hiyo kudhibiti ukwapaji kodi na kuongeza ukusanyaji wa mapato ya serikali.
"Shabaha kubwa ya mkakati huu ni kuwafanya wasamaria wema kufichua wakwepa kodi na kuhakikisha serikali inakusanya mapato zaidi yatayosaidia kuharakisha maendeleo ya Watanzania," alisema.
Alisema chini ya mpango huo wasamaria wema 62 wamefaidika kwa kuzawadiwa Sh. 193,857,720 kwa kutoa taarifa ambazo zimesaidia kuokoa mabilioni ya fedha zilizotolewa na TRA katika kipindi cha mwaka 2014/2015.
"TRA inawashukuru wote waliofanikisha kuokoa kiasi hiki kikubwa cha kodi kutoka kwa wafanyabiashara wasio waaminifu ambao kwa makusudi hukwepa kodi na kulipotezea taifa mapato," alisema.
Kayombo alisema TRA ilianzisha utaratibu wa kuwazawadia wananchi wanaotoa taarifa za ukwepaji wa kodi kwa kuwazawadia asilimia tatu ya kodi iliyookolewa na kiasi cha zawadi kinatakiwa kisizidi Sh. milioni 20.
"Katika mpango huu taarifa za ukwepaji kodi zinazotolewa huchukuliwa kwa uzito wa hali ya juu na kufanyiwa uchunguzi wa kina ili kuhakikisha kwamba ni za ukweli na mtoa taarifa hubaki kuwa siri ya TRA," alisema.
Alitoa wito kwa wananchi kuendelea kutoa taarifa kuhusu vitendo vyovyote ambavyo vinasababisha mapato ya serikali kupotea ili kuweka uwiano sawa wa kila anayestahili kulipa kodi alipe kwa mujibu wa sheria.
"Mwananchi yeyote mwenye taarifa za ukwepaji wa kodi anashauriwa kupiga simu namba 2137638 au 0784 210208 au anaweza kufika TRA Idara ya Uchunguzi wa Kodi, baada ya hapo hatua stahiki zitachuliwa na mamlaka," aliongeza kusema Kayombo.
Chanzo: Nipashe
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Idara ya Elimu na Huduma kwa Mlipa kodi TRA, Richard Kayombo, alisema utaratibu huo ni moja ya mipango iliyobuniwa na mamlaka hiyo kudhibiti ukwapaji kodi na kuongeza ukusanyaji wa mapato ya serikali.
"Shabaha kubwa ya mkakati huu ni kuwafanya wasamaria wema kufichua wakwepa kodi na kuhakikisha serikali inakusanya mapato zaidi yatayosaidia kuharakisha maendeleo ya Watanzania," alisema.
Alisema chini ya mpango huo wasamaria wema 62 wamefaidika kwa kuzawadiwa Sh. 193,857,720 kwa kutoa taarifa ambazo zimesaidia kuokoa mabilioni ya fedha zilizotolewa na TRA katika kipindi cha mwaka 2014/2015.
"TRA inawashukuru wote waliofanikisha kuokoa kiasi hiki kikubwa cha kodi kutoka kwa wafanyabiashara wasio waaminifu ambao kwa makusudi hukwepa kodi na kulipotezea taifa mapato," alisema.
Kayombo alisema TRA ilianzisha utaratibu wa kuwazawadia wananchi wanaotoa taarifa za ukwepaji wa kodi kwa kuwazawadia asilimia tatu ya kodi iliyookolewa na kiasi cha zawadi kinatakiwa kisizidi Sh. milioni 20.
"Katika mpango huu taarifa za ukwepaji kodi zinazotolewa huchukuliwa kwa uzito wa hali ya juu na kufanyiwa uchunguzi wa kina ili kuhakikisha kwamba ni za ukweli na mtoa taarifa hubaki kuwa siri ya TRA," alisema.
Alitoa wito kwa wananchi kuendelea kutoa taarifa kuhusu vitendo vyovyote ambavyo vinasababisha mapato ya serikali kupotea ili kuweka uwiano sawa wa kila anayestahili kulipa kodi alipe kwa mujibu wa sheria.
"Mwananchi yeyote mwenye taarifa za ukwepaji wa kodi anashauriwa kupiga simu namba 2137638 au 0784 210208 au anaweza kufika TRA Idara ya Uchunguzi wa Kodi, baada ya hapo hatua stahiki zitachuliwa na mamlaka," aliongeza kusema Kayombo.
Chanzo: Nipashe