kimatire
JF-Expert Member
- Nov 27, 2008
- 371
- 93
Hilo nalo linaniacha hoi hasa nikisafiri na mabasi yetu yaendayo Mikoani!!Kwamba , imezoeleka kuwa basi lisimame porini abiria washuke kwenda kuchuma dawa.
Kwa wale ambao hawafahamu msemo huo ni kwenda kujisaidia haja ndogo na kubwa porini!!Karne hii ya uharibifu wa mazingira,maradhi lukuki ya kuambukiza, kipindu pindu, kichocho na wenzake bado watanzania tunajisaidia porini kuwaachia wengine maradhi ilimradi wasafiri tumefika salama???
Jamani hakuna uwezekano wa kuwa na vituo vyenye vyoo katikati ya mapori yetu hata kama ni vya kulipia wasafiri wakavitumia kuliko neno hilo linalotumika kwenda kuchuma dawa?Bado karne hii tuko kwenye maisha ya ujima kiasi hicho??
JF hebu tuwe mawakili katika kupinga uchafuzi huu wa mazingira yetu.
Kwa wale ambao hawafahamu msemo huo ni kwenda kujisaidia haja ndogo na kubwa porini!!Karne hii ya uharibifu wa mazingira,maradhi lukuki ya kuambukiza, kipindu pindu, kichocho na wenzake bado watanzania tunajisaidia porini kuwaachia wengine maradhi ilimradi wasafiri tumefika salama???
Jamani hakuna uwezekano wa kuwa na vituo vyenye vyoo katikati ya mapori yetu hata kama ni vya kulipia wasafiri wakavitumia kuliko neno hilo linalotumika kwenda kuchuma dawa?Bado karne hii tuko kwenye maisha ya ujima kiasi hicho??
JF hebu tuwe mawakili katika kupinga uchafuzi huu wa mazingira yetu.