Was Mkapa Wrong on This? Really?

............ can we really blame Ben on privatization? ni vizuri tukijiangalia kwanza sisi wenyewe then tukaangalia ni vipi tumefika tulipo.

Ni kweli Mkuu ukiangalia nchi zilizoendelea.....kusema ukweli watu wanapiga Mzigo Kinoma..........sisi ni wavivu sana...........porojo nyingi........copy/cut and paste kama kazi.............
 
Ni kweli Mkuu ukiangalia nchi zilizoendelea.....kusema ukweli watu wanapiga Mzigo Kinoma..........sisi ni wavivu sana...........porojo nyingi........copy/cut and paste kama kazi.............

Mkuu Ogah, hi ni sehemu moja inayotakiwa kufanyiwa kazi, lakini hata hakuna anayestuka sisi ni wavivu sana, porojo nyingi utendaji kidogo sana.
 
Ila moral justification inaendana na sheria zilizopo kama zasiadiaa kuwajibishaa..
Leo hii tuna umati wa viongozi (kuanzia kata, wilaya,mkoa hadi taifa kwa maana ya wachaguliwa na wananchi) ambao ni washabikii tuu na kuangalia kula yao.

Bunge letuu limeonyesha mfano wa kuwa genge la washangiliaji wa itikadi na rangi zao (mfano suala la Zitto na buzwagi, dk slaa na list of shame) .

Kama taifa tunahitaji strong institutions na sio strong people kwani wanapita. Ni kwa kiasi gani bunge limepigania kuwa na taasisi huru za kupambana na rushwa, mahakama, taasisi za umma zenye tija kwa ajili ya watu zaidi ya kugombania poshoo za vikaoooo????????????????

Sioni tija ya kuwajadili watu ili hali makosa yao hayajengewi msingi wa kurekebisha zaidi ya kuongezaa zaidiiiii..Tulikuwa na mikataba mibovu ya madini na bado ipo, TRL, ATCL nk...Ni nini kinachotufanya tushindwe kuirekebishaaa LEOOOO????
 
Tofautisha mali ya umma na mali ya Mtu binafsi.Ningekuelewa kama ungetolea mifano ya makampuni yaliyobinafsishwa kwa watanzania yakakwama.Kuna mifano mingi ya private businesses zinafanya vizuri tu huko nyumbani.Kumbuka hata hao wazungu ni private companies.
 
kusema alikua wrong unapunguza ukali wa kitendo alichokifanya, yeye enzi za mwalimu angeitwa mhujumu uchumi, yeye aliuza kila shirika ili liendeshwe na wagni na yeye abaki kukusanya kodi tu, hakuna hata nchi moja duniani iliyoendelea kwa serikali yake kukusanya kodi tu bila kujihusisha na ''production and manufacturing'' hata hao washauri wa kizungu wanalijua ilo na ndio mana mkapa alidharauliwa ( mwerevu anaweza akakwambia kitu cha kijinga wewe mwenye akili timamu, ila ukikikubali atakudharau - nyerere ).
hata marekani pamoja na shirika kubwa la magari la general motors lilipofilisika mbona serikali ya obama ilichukua uendeshaji wake na likaingiza pesa kutoka kwa serikali, je si marekani ndio vinara wa soko huria inayoamini nguvu ya soko, kwa nini hawakukubali general motors life?
mkapa infact alienda mbali zaidi hadi akaanzisha ubinafsishaji wa aina yake wa kuuza hata mashirika yenye faida kama nmb huku waziri wake wa fedha, basil mramba akitoa majibu ya kebehi kwa umma wa watanzania kwa kusema ng'ombe alienenepa ndio anafaa kupelekwa mnadani.
ktk watu waliodhuluma umma wa watanzania kuliko wote mkapa anaongoza pengine zaidi hata ya wakoloni.
 
Viongozi hawalaumiwi tu kwa yale waliyoyafanya. Wanalaumiwa vile vile kwa yale waliyoshindwa kufanya. Nyerere aliweza kuanzisha mashirika na Viwanda vingi. Watanzania tukashindwa kuviendesha kwa faida, je vilikuwa viable wakati vinaanzishwa?

Wakati viwanda na mashirika hayo yanaanzishwa yalikuwa viable na matatizo yalijitokeza kwenye uendeshaji. Serikali ilivika jukumu la kuyaendesha mashirika na viwanda hivyo lakini ikaviendesha kisiasa na hatimaye vikafikia hali mbaya iliyolazimisha viuzwe au vibinafsishwe. Suala la kuviuza viwanda na mashirika ya umma au kuvibinafsisha lilikuja tu pale ilipokuwa dhahiri kuwa SERIKALI YETU KAMWE HAINA UWEZO WA KUVIENDESHA/KUYAENDESHA mashirika hayo. Ni kama kukiri kuwa serikali ilikuwa incompetent to the core. Suala ni je tulikuwa na uwezo wa kuibadilisha na kuweka serikali nyingine yenye uwezo?

Wataalam wa ushauri wa Benki ya Dunia waliona hilo halipo. Waliona waafrika wote wana mtindio wa ubongo na taahira ya akili. Hivyo wakashauri kuwa ili viwanda hivyo viweze kuendeshwa kwa faida ni lazima viuzwe kwa makampuni ya Wazungu wenye uwezo wa kuyaendesha mashirika na viwanda hivyo. Wakati benki ya Dunia ikishauri hivyo question ya viability ya mashirika na viwanda hivyo haikuwa issue. Ni kwamba with requisite skills na proper financing mashirika na viwanda vyetu vilikuwa na uwezo kabisa wa kujiendesha kwa faida.

Benki ya Dunia walikuwa tayari kutoa financing lakini walikuwa na matatizo makubwa na uendeshaji wa mashirika na viwanda hivyo chini ya Serikali kwani serikali ilishathibitika kuwa a failure. Kwa hiyo tulichotakiwa sisi ni kuyafanyia haki mashirika na viwanda hivyo ya kuyauza au kuviuza kwa wenye uwezo wa kuviendesha na Benki ya Dunia wangetoa hata mikopo. LAKINI .... NARUDIA ... LAKINI TENA MDUDU WETU AKAWA NI YULE YULE.

Hata kuuza kwa wenye uwezo wa kuviongoza au kuyaongoza mashirika hayo tukashindwa. Uuzwaji ukafanyika kivioja kwa sababu wauzaji walikukwa wanafikiria kwanza watanufaikaje binafsi! Matokeo yake uuzaji wote ukageuka kama zoezi la wendawazimu. Ndo maana Mkapa analaumiwa kwa sababu alikuwa rais kipindi hicho. Alishindwa kuonyesha njia na hatimaye na yeye akaingia katika bonanza ya kujigawia. kwa nini asilaumiwe?

Wengine tunalaumu mfumo! Mfumo ni nini jamani? Mifumo si tunaweka sisi. Madaraka makubwa ya rais tumempa sisi. Hakuna atakayeweza kubadilisha madaraka na mfumo huo tunaompa rais wetu isipokuwa rais mwenyewe. Kusema ukweli ni uwongo kusema kuwa watanzania ndo waliompa madaraka makubwa rais. Madaraka makubwa marais wa nchi hii walijipa wenyewe kupitia katiba wanayoibariki wao. Marais ndo wanaamua nani abadililishe katiba na ni wakati gani katiba ibadilishwe. Sasa rais atakayeona katiba au mfumo ni tatizo kwake anashindwa nini kubadilisha? Kushindwa kuweka mfumo efficient ni makosa ya kutofanya na yote hayo inatakiwa lawama ziende kwa viongozi tu. Ikiwa hawawezi kuleta mabadiliko yanayotakiwa kwa nini wasiwe wanatangaza kuwa wameshindwa? Nchi za wenzetu ni viongozi wangapi wameshashindwa na kuachia madaraka? Kwa nini viongozi wa Afrika hawaoni kuwa hawaleti kile kilichotarajiwa badala yake wakishaingia madarakani huanza kujichimbia huko ili wasije toka?

Failure ya sera ya ubinafsishaji kwa kiwango kikubwa lawama inatakiwa zielekezwe kwa viongozi waliotuongoza kipindi hicho. Mkapa was the president then na hana la kujitetea kutokana na failure yetu katika kufanya ubinafishaji prudently!
 
RIP BWM.
P
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…