Warusi wengi waunga Mkono mabadiliko ya katiba

Warusi wengi waunga Mkono mabadiliko ya katiba

mkiluvya

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2019
Posts
815
Reaction score
733
1592042570773.png

Rais wa Urusi Vladmir Putin amesema Warusi wengi zaidi wameunga mkono mpango wake wa mabadiliko ya katiba ili kumpa mwanya wa kubakia madarakani, Putin amesema Raia wengi nchini humo wamekubali mpango huo ambao utamwezesha Putin kusalia kwenye kiti cha Urais
 
Huyu Putin ni mswahili pure, ni rangi tu. Hana maana kabisa. Kumbe ndio maana hata yale mapipa yao wameyasifia wee wakati hata hayana kitu. Bure kabisa.
Mapipa yapi hayo yalokua bure naubure wake upi ?!
Kwa ulimwengu wa sasa ulivyo wa kibabe inatakiwa wababe ndo waongoze nchi.
Hakika anatakiwa aongoze jamaa mpaka atakaposhindwa ndio uwe mwisho wake.
 
Russia is Putin & Putin is Russia.
Inawezekana umeijua Russia juzi wakati wa Putin. Uzuri wa historia ni kua waliyosalia madarakani kwa kubadilisha katiba walitoka kwa aibu.

Badala ya kutengeneza taasisi imara na iache ipambane na mbabe USA yeye anataka kubaki ili apambane na USA wakati anajua yeye ni uhai anapita tu.
 
View attachment 1477196
Rais wa Urusi Vladmir Putin amesema Warusi wengi zaidi wameunga mkono mpango wake wa mabadiliko ya katiba ili kumpa mwanya wa kubakia madarakani, Putin amesema Raia wengi nchini humo wamekubali mpango huo ambao utamwezesha Putin kusalia kwenye kiti cha Urais


Ukiona hivyo ujue kuna jambo limemtia "Wazimu" Putin kutoka huko USA, nafikiri ni SPACE X, chini ya Putin hivi sasa Wanasayansi wa Russia hawalali kwa kutafuta space craft yenye ubora kuliko Space X.
 
Alikuwa rais awali alipo maliza mda wake akachaguliwa kuwa waziri mkuu, hawamu iliyofuatia akarudi kuwa rais tena sasa ameongezewa mda tena.
Ongera zake
 
Inawezekana umeijua Russia juzi wakati wa Putin. Uzuri wa historia ni kua waliyosalia madarakani kwa kubadilisha katiba walitoka kwa aibu.

Badala ya kutengeneza taasisi imara na iache ipambane na mbabe USA yeye anataka kubaki ili apambane na USA wakati anajua yeye ni uhai anapita tu.
Ni ukweli Urusi, zamani ikiitwa USSR kabla ya kusambaratika imepita mikononi mwa wababe wengi.

Ila kwa sasa Putin anaonekana hapo Kremlin amepamudu vyema kuanzia misukosuko ya ndani (rejea vita mbili za Chechnya, changmoto ya kiuchumi baada ya vikwazo, misukosuko ya kisiasa na wapinzani wake) mpaka kwenye ulingo wa kimataifa (vita na Georgia, mgogoro Ukraine, Crimea, Syria, Libya, mgogoro na US, EU).

Hivyo bado ataendelea kuwepo hapo ikulu (kama atakuwa hai) wakati wakisubiri kuunda hizo taasisi, kama atatoka kwa aibu hatakuwa wa Kwanza wala wa mwisho ndio siasa zilivyo.
 
Putin kapendekeza mabadiliko yenye faida kwa Warusi, ila ukiangalia unaona ni kama vile anataka kujipendelea yeye tu.

Vipengele muhimu alivyovipendekeza ni

*Rais anaweza kugombea kwa mihula mingine 2 baada ya kumaliza mihula yake 2
*Bunge liwe na uwezo wa kuchagua waziri mkuu na baraza lake

* Bunge liwe na uwezo wa kumfukuza kazi jaji mkuu na mwanasheria mkuu

* Rais anashilikiana na bunge kuteuwa wakuu wote wa vyombo vya usalama

*Kiwango cha mshahara wa chini hakiwezi kuwa chini ya kiwango cha matumizi ya kujikimu

*Kuongeza kiwango cha mafao ya uzeeni
 
Back
Top Bottom