ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,131
- 931
Mjiulize mbona hayatokei katika nchi za wenzenu?? wananchi wanapofikia hapa ujue wamepoteza imani!! watu wanatafuta kwa jasho na wengine wanatumia jasho kidogo tu kuchukua kile kilichopatikana kwa jasho jingi..ukiomba dola ifanye kazi yake unakuta dola nayo inakutaka utoe tena jasho vinginevyo hakuna msaada..hapo ndipo inafikia watu kutumia njia ya mkato kama hizi za kurahishisha maamuzi tu (kuiba si kosa lenye kustahili adhabu ya kifo) lakini wananchi hawajui haya kutokana na mfumo wa maisha uliowekwa na wenye mamlaka..turekebishe haya kwa kuangalia yale yajayo mbele, hali itazidi kutisha..