BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,011
Warioba, kafara EPA kushitakiwa
Mwandishi Wetu Oktoba 15, 2008
Raia Mwema~Muungwana ni Vitendo
Jeetu Patel na matajiri wenzake kupeta
Ni funika kombe mwanaharamu apite
KUNA uwezekano mkubwa kwamba Waziri Mkuu mstaafu, Jaji Joseph Warioba akaingizwa matatani kutokana na uchunguzi unaofanyika ndani ya kampuni ya uchimbaji dhahabu ya Mwananchi Gold, Raia Mwema imeambiwa.
Hayo yakiendelea, kuna habari pia kwamba karibuni Serikali itapeleka mahakamani kesi ya kuwashitaki wahusika ‘dhaifu' wa tuhuma za wizi wa Fedha katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania hatua zote hizo zikilenga kufunika kombe mwanaharamu apite.
Vyanzo kadha vya habari vimeiambia Raia Mwema kwamba kesi hizo zimekuwa zikiandaliwa ili pamoja na mambo mengine, zikianza ziweze kushusha joto la kisiasa lililopanda kutokana na kuonekana kana kwamba watawala hawachukui hatua thabiti juu ya tuhuma za ufisadi zinazowakabili wanasiasa na matajiri kadhaa walio karibu na chama tawala wakati huu wa kuelekea katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.
Kwa mujibu wa habari hizo, kesi hizo, zinatakiwa ziendelee hadi hata baada ya 2010 ili kutoa picha kwamba utawala umedhamiria kupambana na ufisadi hata kama kesi hizo zitakuwa zikitajwa tu na watuhumiwa, hasa wale wa EPA wakiwa ndani chini ya tuhuma kama za hujuma ya uchumi, kughushi na kula njama kuiba.
Kama hatimaye zitafunguliwa katika kiasi cha wiki chache sasa kabla ya Oktoba 31 siku ambayo imetangazwa kuwa ya mwisho ya watuhumiwa kurejesha fedha za EPA, kesi hizo zitakuwa zikiendelea tu mahakamani kama ambavyo imekuwa ikiendelea nyingine ya aina hiyo ya aliyekuwa Balozi wa Tanzania Italia, Profesa Costa Mahalu.
Kwa upande wake Jaji Warioba, mmoja wa wakosoaji wakubwa wa jinsi vitendo vya kifisadi vinavyoshaniri nchini, anahusishwa na kampuni ya uchimbaji wa dhahabu ya Mwananchi Gold ambamo yeye ni Mwenyekiti wa Bodi na ambako chama tawala, Chama cha Mapinduzi (CCM) kinahusishwa.
Taarifa za wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) zinaonyesha kuwa, Mwananchi Gold Company Limited ni kampuni binafsi ambayo wamiliki wake ni Benki Kuu ya Tanzania (hisa 500), Shirika la Maendeleo la Taifa ( NDC hisa 375), Mwananchi Trust Company Ltd (hisa 1,123) na Chimera Company Limited (hisa 500).
Alipoulizwa wiki hii juu ya habari hizo za kushitakiwa, Jaji Warioba alisema kwamba hakuwa amesikia juu ya habari hizo lakini akasema pia kwamba alisoma tu magazetini siku kadhaa zilizopita kwamba maandalizi ya kesi hiyo yalikuwa mbioni.
" Kweli sijasikia kuhusu kuwapo kwa kesi hiyo. Nilisoma tu wiki chache zilizopita katika gazeti moja kuwa kesi hiyo ipo," alisema Jaji Warioba.
Mmoja wa maofisa waandamizi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) yenye dhamana na uchunguzi wa kesi za aina hiyo ameiambia Raia Mwema kwamba kati ya kesi kadhaa inazoandaa TAKUKURU kesi ya Mwananchi Gold imo.
Habari zaidi zimesema kwamba baadhi ya wakurugenzi wa Mwananchi Gold kama Yusuf Mushi wamepata kutafutwa wahojiwe lakini ikashindikana kwa ugonjwa na kwamba Mkurugenzi mwingine, Vulfrida Mahalu katika siku za karibuni amehojiwa mara mbili na TAKUKURU. Raia Mwema haikufanikiwa kuwapata kueleza undani wa mahojiano hayo.
Kwa upande wa EPA wanaotajwa kufikishwa mahakamani ni wamiliki wa kampuni za Changanyikeni Residential Complex Limited, Malegesi Law Chambers, G&T International Limited na Karnel Meals Holdings Ltd.
Nyaraka zinaonyesha kwamba Changanyikeni Residential Complex inamilikiwa na Jose Van de Merwe, Samson Mapunda na Charles Mabina wakati Maregesi Law Chambers inamilikiwa na Beredy Maregesi, ambaye pia anatajwa kumiliki kampuni ya G&T International Limited akiwa na mwenzake Octavio Timoth.
Kampuni Karnel Meals Holdings Ltd inamilikiwa na Johnson Lukaza na Mwesigwa Rutakyamilwa Lukaza ikiwa imepata usajili Agosti 4, 1998.
Habari zinasema ni Maregesi, Mapunda na Lukaza tu ambao ndio watakaofikishwa mahakani katika hatua inayozua minong'ono ya kuwa watuhumiwa wakubwa wa fedha za EPA wanakingiwa kifua kwa kuwa wana uhusiano wa karibu na chama tawala.
" Ni kama sasa wanataka kutolewa kafara. Hata muda uliotolewa wa Oktoba 31 ni kama uliwalenga wao. Wamekuwa wakikataa kurudisha fedha wakidai kwamba wao walifanya kazi, walioiba ni hao ambao sasa wanaelezwa kwamba wamerudisha. Kwamba wao sasa wanataka kushitakiwa huku wakubwa wakiachwa maana yake kubwa ni kwamba watawala wanafunika kombe," alisema mmoja wa watu walio karibu na watuhumiwa hao.
Kampuni zilizokwiba fedha nyingi zaidi kutoka akaunti ya EPA na ambazo sasa kwa utaratibu huu wamiliki wake hawataguswa ni pamoja na ya Kagoda Agricultural Limited na nyingi za mfanyabiashara mwenye asili ya kiasia, Jeetu Patel.
Kwa mujibu wa wakaguzi Kagoda ilighushi nyaraka zilizotumika kuchota zaidi ya shilingi bilioni 40 wakati Jeetu Patel, naye amechota zaidi ya nusu ya fedha zilizoibwa akitumia kampuni nane.
Maofisa wa Serikali hususan wale wa vyombo vya dola wakiwamo wajumbe wa kikosi kazi (task force) kilichokabidhiwa kazi ya kuchunguza na kuchukua hatua dhidi ya wahusika waliochota fedha hizo, walipoulizwa kuhusu kushitakiwa kwa wachache tu katika wizi wa EPA wote walidai kwamba muda aliotoa Rais Jakaya Kikwete kukamilika kwa suala hilo haujakwisha.
Mkurugenzi wa Upelelezi wa Jinai (DCI), Robert Manumba, ambaye alitajwa na vyanzo vya habari kwamba ofisi yake ndiyo inakamilisha taratibu za kuwashitaki wahusika aliiambia Raia Mwema jana Jumanne kwamba hawezi kuzungumzia suala hilo kwa kuwa msemaji wa kikosi kazi (task force) ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika.
Kauli kama hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk. Edward Hosea naye hakuwa tayari kuzungumzia hatua ambayo wamefikia katika kuwashitaki wahusika, huku Ofisa Mwandamizi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu, akisema kwamba kila kitu kitajulikana siku chache zijazo.
Mapema Jumatatu wiki hii, Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Jinai, Peter Kivuyo, aliliambia Raia Mwema kwamba mtu anayeweza kuzungumzia masuala ya EPA ni ofisa mwenzake aliyemtaja kwa jina la Kasara, ambaye hata hivyo alipotafutwa kwa simu alisema hakuwa tayari kuzungumzia suala hilo.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), Elieza Feleshi naye hakuwa tayari kuzungumzia kuhusu mashitaka dhidi ya watuhumiwa wa EPA, kwa maelezo kwamba jana Jumanne ilikuwa ni siku ya mapumziko na alikuwa katika shughuli za kifamilia.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika, ambaye ndiye anayeelezwa na wenzake kuwa anapaswa kuzungumzia suala hilo hakuweza kupatikana jana Jumanne huku msemaji wake, Omega Ngole akisema kwa sasa hawako katika nafasi ya kuzungumzia suala hilo.
Hata hivyo, Raia Mwema limethibitishiwa kwamba Maregesi, Mapunda na Lukaza, wanatajwa kuwa watu watakaotolewa kafara kutokana na kile kilichoelezwa kwamba wamekuwa na "jeuri ya Kiafrika" kwa kukataa kulipa fedha wanazotuhumiwa kuzichota.
Imeelezwa kwamba tokea awali watuhumiwa hao wamekuwa wakigoma ‘kutoa ushirikiano' jambo ambalo limeelezwa kuwakera baadhi ya wanasiasa na watendaji wa Serikali walioamua sasa kuwaburuza mahakamani.
Raia Mwema imethibitisha kwamba bado akaunti za watuhumiwa hao zinaendelea kushikiliwa hata baada ya muda wa miezi sita kisheria kupita kwa maelekezo ya ofisi ya Mwanasheria Mkuu.
Habari zinaeleza kwamba awali watuhumiwa hao walikuwa wafikishwe mahakamani sambamba na maofisa wa BoT waliohusika katika mchakato wa EPA, lakini uamuzi huo ulibadilishwa baada ya tishio kutoka kwa watumishi hao kwamba ‘wataanika' kila kitu hadharani wakitolewa kafara.
"Baada ya watumishi hao wa BoT kutishia kumwaga kila kitu hadharani, mwelekeo umebadilika na sasa wataitwa kama mashahidi wa upande wa serikali kesi hizo zitakapofikishwa mahakamani, lakini bado wanaweza kuiharibia serikali watakapoamua kutaja watu ambao wamefichwa," anasema mtoa habari wetu aliye karibu na vyombo vya dola.
Raia Mwema imefahamishwa kwamba kesi hizo zinatarajiwa kutumika kama mwavuli wa kuivusha serikali kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, kukwepa wimbi la manung'uniko ya wazi kwamba serikali ya CCM imekuwa ikiwalea watuhumiwa wa ufisadi, wengi wakiwa ni wafadhili wa chama hicho.
Wakaguzi wa ndani na wale wa nje, walibaini kuwapo kwa wizi mkubwa wa fedha katika akaunti ya EPA katika kipindi cha mwaka mmoja pekee wa 2005/2006 ambako zilipotea zaidi ya Shilingi bilioni 133.
Wakaguzi hao walibaini kwamba kati ya fedha hizo shilingi bilioni 90 ni zile ambazo zimethibitika kuchotwa kwa kutumia nyaraka za kughushi, sehemu kubwa zikiwa zimekwenda kwa wafanyabiashara wawili, wamiliki halisi wa Kagoda Agricultural Limited na Jeetu Patel kupitia kampuni zake nane.
Ripoti ya Wakaguzi wa Kampuni ya Ernst and Young waliofanya kazi kwa niaba ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ilionyesha kwamba kiasi cha Shilingi 90,359,078,804.00 zililipwa kwa kampuni 13 ambazo zilitumia kumbukumbu, nyaraka na hati zilizo batili na za kugushi na kwamba kampuni hizo hazikustahili kulipwa chochote.
Wakaguzi hao na Ikulu kupitia taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wake, Philemon Luhanjo, Januari 9, 2008, walipendekeza moja kwa moja bila kuuma maneno kwamba wahusika wa kampuni hizo 13 wachukuliwe hatua za kisheria mara moja, kauli ambayo Rais Kikwete aliirejea katika hotuba yake bungeni, lakini bila ukali tena.
Makampuni ambayo Jeetu Patel anahusika nayo na ambayo yamethibitika kughushi nyaraka na kuchota fedha BoT ni Navycut Tobacco (T) Limited, Ndovu Soaps Limited, Bina Resorts Limited, Bencon International Limited, Maltan Mining Company Limited, Bora Hotels & Apartments Limited, Venus Hotels Limited, and B.V. Holdings Limited.
Pamoja na kampuni hizo za Jeetu Patel, kampuni nyingine zilizohusika na jinai ya kughushi nyaraka ni pamoja na Kagoda Agriculture Limited ambayo wanaoonekana katika nyaraka ni John Kyomuhendo mwenye hisa 40 na Francis William anayemiliki hisa 60 katika kampuni hiyo.
Kampuni nyingine ni V.B & Associeties Company inazomilikiwa na Devendra Patel na Jantkumar Chandubhai Patel na Changanyikeni Residential Complex Limited inayomilikiwa na Jose Van de Merwe, Samson Mapunda na Charles Mabina ikiwa na makao yake, Sinza, Kumekucha, Dar es Salaam.
Pia katika orodha hiyo ya kampuni 13 zilizoghushi nyarakaambazo wahusika wake wamependekezwa kuchukuliwa hatua za kisheria mara moja ni Money Planners & Consultants inayomilikiwa na Paul Nyingo na Fundi Kitungi na kampuni ya Njake Hotel & Tours Limited inayomilikiwa Japhet Lema, Anna Lema, Abel Lema, Derick Lema na Benard Lema wa Arusha.
Jeetu Patel katika baadhi ya kampuni anashirikiana na wafanyabiashara wengine wa Dar es Salaam ambao wanatajwa kushiriana naye katika kuhamisha fedha hizo kwenda nje kwa kuzibadili kutoka shilingi za Kitanzania kwenda Dola za Merakani ama Euro bila kufuata mkondo halali wa fedha kinyume cha Sheria ya Udhibiti wa Fedha Haramu.
Miongoni mwa wanaotajwa kushirikiana na Jeetu Patel ni Sidik Yacoubu kupitia kampuni yao ya Ndovu Soap Limited ambayo kwa mujibu wa nyaraka za Wakala wa Leseni na Usajili wa Kampuni (BRELA), kampuni hiyo yenye namba ya usajili 20536 ya Februari 3, 1992, wamiliki wake ni Jayantulal Chandubhai Patel na Sidik Yacoubu.
Katika kampuni ya Bora Hotels and Apartments iliyosajiliwa Septemba 8, 2005 inaonyeshwa katika orodha ya BRELA kwamba wamiliki wake wamo Jayantkumar Chandubhai Patel na Devandra Patel wakati Bina Resort Limited iliyosajiliwa Machi 31, 2005, wamo Jayantikumar Chandubhai Patel na Devendra Patel.
Kampuni ya Maltan Mining Company iliyosajiliwa Machi 8, 1993 inamilikiwa na Jantkumar Chandubhai Patel na Hariharier Radhakrishna wakati Navy Cut Tobacco iliyosajiliwa Oktoba 12, mwaka 1995 inamilikiwa na Jantkumar Chandubhai Patel na Radakrishna.
Kampuni nyingine ni Bencon Limited, B.V Holdings, Venus Hotels na V.B & Associeties Company zinazomilikiwa na Devendra Patel na Jantkumar Chandubhai Patel, ambazo zote zilisajiliwa Aprili 4, 2005.
Katika orodha ya BRELA imo pia kampuni ya Excellent Service Limited inayomilikiwa na Emil Samanya, Peter Sabas na Elisifa Ngowi ambaye anatajwa kuwa ni Ofisa Mwandamizi wa Idara ya Usalama wa Taifa, ambaye yumo katika task force inayochunguza wizi huo. Kampuni hiyo ilisajiliwa Mei 13, 1992 na kupewa namba 26959.
Ngowi anahusishwa pia katika kampuni nyingine ya Clyton Marketing iliyosajiliwa Juni 6, 2005 akiwa na mwenzake Edwin Mtoi, ambaye haikuweza kufahamika mara moja anafanya shughuli gani zaidi ya kuwa katika kampuni hiyo.
Wamiliki wengine waliofahamika ni Rajabu Maranda na Thabit Katunda ambao wanatajwa kumiliki kampuni ya Liqiud Service Limited ambayo usajili wake ulifanyika Desemba 12, 2004 na kupewa namba 15007. Maranda anatajwa kuwa mmoja wa wana CCM mashuhuri mkoani Kigoma na alidaiwa kutaka kuiingiza familia ya viongozi wa juu serikalini katika biashara zake bila mafanikio hususan baada ya Rais Kikwete kuwa makini zaidi.
Wamiliki wengine waliofahamika ni Johnson Lukaza na Mwesigwa Rutakyamilwa Lukaza ambao wao wanamiliki kampuni ya Karnel Meals Holdings Ltd ambayo usajili wake ulipatikana Agosti 4, 1998, Mibale Farm iliyosajiliwa Septemba 2, 2005 na kupewa namba 154039 ambayo inamilikiwa na Kizza Selemani na Farijala Hussein, Malegesi Law Chambers inayomilikiwa na Beredy Malegesi ambayo ilisajiliwa Septemba 24, 2001.
Wamiliki wengine ni Paul Nyingo na Fundi Kitungi, wanaomiliki Kampuni ya Money Planners & Consultants iliyosajiliwa Machi 22, 2005 na Kiloloma & Bros Enterprises inayomilikiwa na Charies Kissa, ambayo ilisajiliwa Aprili 8, 2005.
Katika ukusanyaji wa fedha hizo, task force ya serikali inaelezwa kukusanya shilingi 53,738,835,392/= fedha ambazo Rais Kikwete ameagiza ziingizwe katika mfuko maalumu kwa ajili ya kusaidia sekta ya kilimo zikichanganywa na nyingine zinazotarajiwa kufikia shilingi 64,844,770,688/=
Mwandishi Wetu Oktoba 15, 2008
Raia Mwema~Muungwana ni Vitendo
Jeetu Patel na matajiri wenzake kupeta
Ni funika kombe mwanaharamu apite
KUNA uwezekano mkubwa kwamba Waziri Mkuu mstaafu, Jaji Joseph Warioba akaingizwa matatani kutokana na uchunguzi unaofanyika ndani ya kampuni ya uchimbaji dhahabu ya Mwananchi Gold, Raia Mwema imeambiwa.
Hayo yakiendelea, kuna habari pia kwamba karibuni Serikali itapeleka mahakamani kesi ya kuwashitaki wahusika ‘dhaifu' wa tuhuma za wizi wa Fedha katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania hatua zote hizo zikilenga kufunika kombe mwanaharamu apite.
Vyanzo kadha vya habari vimeiambia Raia Mwema kwamba kesi hizo zimekuwa zikiandaliwa ili pamoja na mambo mengine, zikianza ziweze kushusha joto la kisiasa lililopanda kutokana na kuonekana kana kwamba watawala hawachukui hatua thabiti juu ya tuhuma za ufisadi zinazowakabili wanasiasa na matajiri kadhaa walio karibu na chama tawala wakati huu wa kuelekea katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.
Kwa mujibu wa habari hizo, kesi hizo, zinatakiwa ziendelee hadi hata baada ya 2010 ili kutoa picha kwamba utawala umedhamiria kupambana na ufisadi hata kama kesi hizo zitakuwa zikitajwa tu na watuhumiwa, hasa wale wa EPA wakiwa ndani chini ya tuhuma kama za hujuma ya uchumi, kughushi na kula njama kuiba.
Kama hatimaye zitafunguliwa katika kiasi cha wiki chache sasa kabla ya Oktoba 31 siku ambayo imetangazwa kuwa ya mwisho ya watuhumiwa kurejesha fedha za EPA, kesi hizo zitakuwa zikiendelea tu mahakamani kama ambavyo imekuwa ikiendelea nyingine ya aina hiyo ya aliyekuwa Balozi wa Tanzania Italia, Profesa Costa Mahalu.
Kwa upande wake Jaji Warioba, mmoja wa wakosoaji wakubwa wa jinsi vitendo vya kifisadi vinavyoshaniri nchini, anahusishwa na kampuni ya uchimbaji wa dhahabu ya Mwananchi Gold ambamo yeye ni Mwenyekiti wa Bodi na ambako chama tawala, Chama cha Mapinduzi (CCM) kinahusishwa.
Taarifa za wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) zinaonyesha kuwa, Mwananchi Gold Company Limited ni kampuni binafsi ambayo wamiliki wake ni Benki Kuu ya Tanzania (hisa 500), Shirika la Maendeleo la Taifa ( NDC hisa 375), Mwananchi Trust Company Ltd (hisa 1,123) na Chimera Company Limited (hisa 500).
Alipoulizwa wiki hii juu ya habari hizo za kushitakiwa, Jaji Warioba alisema kwamba hakuwa amesikia juu ya habari hizo lakini akasema pia kwamba alisoma tu magazetini siku kadhaa zilizopita kwamba maandalizi ya kesi hiyo yalikuwa mbioni.
" Kweli sijasikia kuhusu kuwapo kwa kesi hiyo. Nilisoma tu wiki chache zilizopita katika gazeti moja kuwa kesi hiyo ipo," alisema Jaji Warioba.
Mmoja wa maofisa waandamizi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) yenye dhamana na uchunguzi wa kesi za aina hiyo ameiambia Raia Mwema kwamba kati ya kesi kadhaa inazoandaa TAKUKURU kesi ya Mwananchi Gold imo.
Habari zaidi zimesema kwamba baadhi ya wakurugenzi wa Mwananchi Gold kama Yusuf Mushi wamepata kutafutwa wahojiwe lakini ikashindikana kwa ugonjwa na kwamba Mkurugenzi mwingine, Vulfrida Mahalu katika siku za karibuni amehojiwa mara mbili na TAKUKURU. Raia Mwema haikufanikiwa kuwapata kueleza undani wa mahojiano hayo.
Kwa upande wa EPA wanaotajwa kufikishwa mahakamani ni wamiliki wa kampuni za Changanyikeni Residential Complex Limited, Malegesi Law Chambers, G&T International Limited na Karnel Meals Holdings Ltd.
Nyaraka zinaonyesha kwamba Changanyikeni Residential Complex inamilikiwa na Jose Van de Merwe, Samson Mapunda na Charles Mabina wakati Maregesi Law Chambers inamilikiwa na Beredy Maregesi, ambaye pia anatajwa kumiliki kampuni ya G&T International Limited akiwa na mwenzake Octavio Timoth.
Kampuni Karnel Meals Holdings Ltd inamilikiwa na Johnson Lukaza na Mwesigwa Rutakyamilwa Lukaza ikiwa imepata usajili Agosti 4, 1998.
Habari zinasema ni Maregesi, Mapunda na Lukaza tu ambao ndio watakaofikishwa mahakani katika hatua inayozua minong'ono ya kuwa watuhumiwa wakubwa wa fedha za EPA wanakingiwa kifua kwa kuwa wana uhusiano wa karibu na chama tawala.
" Ni kama sasa wanataka kutolewa kafara. Hata muda uliotolewa wa Oktoba 31 ni kama uliwalenga wao. Wamekuwa wakikataa kurudisha fedha wakidai kwamba wao walifanya kazi, walioiba ni hao ambao sasa wanaelezwa kwamba wamerudisha. Kwamba wao sasa wanataka kushitakiwa huku wakubwa wakiachwa maana yake kubwa ni kwamba watawala wanafunika kombe," alisema mmoja wa watu walio karibu na watuhumiwa hao.
Kampuni zilizokwiba fedha nyingi zaidi kutoka akaunti ya EPA na ambazo sasa kwa utaratibu huu wamiliki wake hawataguswa ni pamoja na ya Kagoda Agricultural Limited na nyingi za mfanyabiashara mwenye asili ya kiasia, Jeetu Patel.
Kwa mujibu wa wakaguzi Kagoda ilighushi nyaraka zilizotumika kuchota zaidi ya shilingi bilioni 40 wakati Jeetu Patel, naye amechota zaidi ya nusu ya fedha zilizoibwa akitumia kampuni nane.
Maofisa wa Serikali hususan wale wa vyombo vya dola wakiwamo wajumbe wa kikosi kazi (task force) kilichokabidhiwa kazi ya kuchunguza na kuchukua hatua dhidi ya wahusika waliochota fedha hizo, walipoulizwa kuhusu kushitakiwa kwa wachache tu katika wizi wa EPA wote walidai kwamba muda aliotoa Rais Jakaya Kikwete kukamilika kwa suala hilo haujakwisha.
Mkurugenzi wa Upelelezi wa Jinai (DCI), Robert Manumba, ambaye alitajwa na vyanzo vya habari kwamba ofisi yake ndiyo inakamilisha taratibu za kuwashitaki wahusika aliiambia Raia Mwema jana Jumanne kwamba hawezi kuzungumzia suala hilo kwa kuwa msemaji wa kikosi kazi (task force) ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika.
Kauli kama hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk. Edward Hosea naye hakuwa tayari kuzungumzia hatua ambayo wamefikia katika kuwashitaki wahusika, huku Ofisa Mwandamizi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu, akisema kwamba kila kitu kitajulikana siku chache zijazo.
Mapema Jumatatu wiki hii, Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Jinai, Peter Kivuyo, aliliambia Raia Mwema kwamba mtu anayeweza kuzungumzia masuala ya EPA ni ofisa mwenzake aliyemtaja kwa jina la Kasara, ambaye hata hivyo alipotafutwa kwa simu alisema hakuwa tayari kuzungumzia suala hilo.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), Elieza Feleshi naye hakuwa tayari kuzungumzia kuhusu mashitaka dhidi ya watuhumiwa wa EPA, kwa maelezo kwamba jana Jumanne ilikuwa ni siku ya mapumziko na alikuwa katika shughuli za kifamilia.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika, ambaye ndiye anayeelezwa na wenzake kuwa anapaswa kuzungumzia suala hilo hakuweza kupatikana jana Jumanne huku msemaji wake, Omega Ngole akisema kwa sasa hawako katika nafasi ya kuzungumzia suala hilo.
Hata hivyo, Raia Mwema limethibitishiwa kwamba Maregesi, Mapunda na Lukaza, wanatajwa kuwa watu watakaotolewa kafara kutokana na kile kilichoelezwa kwamba wamekuwa na "jeuri ya Kiafrika" kwa kukataa kulipa fedha wanazotuhumiwa kuzichota.
Imeelezwa kwamba tokea awali watuhumiwa hao wamekuwa wakigoma ‘kutoa ushirikiano' jambo ambalo limeelezwa kuwakera baadhi ya wanasiasa na watendaji wa Serikali walioamua sasa kuwaburuza mahakamani.
Raia Mwema imethibitisha kwamba bado akaunti za watuhumiwa hao zinaendelea kushikiliwa hata baada ya muda wa miezi sita kisheria kupita kwa maelekezo ya ofisi ya Mwanasheria Mkuu.
Habari zinaeleza kwamba awali watuhumiwa hao walikuwa wafikishwe mahakamani sambamba na maofisa wa BoT waliohusika katika mchakato wa EPA, lakini uamuzi huo ulibadilishwa baada ya tishio kutoka kwa watumishi hao kwamba ‘wataanika' kila kitu hadharani wakitolewa kafara.
"Baada ya watumishi hao wa BoT kutishia kumwaga kila kitu hadharani, mwelekeo umebadilika na sasa wataitwa kama mashahidi wa upande wa serikali kesi hizo zitakapofikishwa mahakamani, lakini bado wanaweza kuiharibia serikali watakapoamua kutaja watu ambao wamefichwa," anasema mtoa habari wetu aliye karibu na vyombo vya dola.
Raia Mwema imefahamishwa kwamba kesi hizo zinatarajiwa kutumika kama mwavuli wa kuivusha serikali kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, kukwepa wimbi la manung'uniko ya wazi kwamba serikali ya CCM imekuwa ikiwalea watuhumiwa wa ufisadi, wengi wakiwa ni wafadhili wa chama hicho.
Wakaguzi wa ndani na wale wa nje, walibaini kuwapo kwa wizi mkubwa wa fedha katika akaunti ya EPA katika kipindi cha mwaka mmoja pekee wa 2005/2006 ambako zilipotea zaidi ya Shilingi bilioni 133.
Wakaguzi hao walibaini kwamba kati ya fedha hizo shilingi bilioni 90 ni zile ambazo zimethibitika kuchotwa kwa kutumia nyaraka za kughushi, sehemu kubwa zikiwa zimekwenda kwa wafanyabiashara wawili, wamiliki halisi wa Kagoda Agricultural Limited na Jeetu Patel kupitia kampuni zake nane.
Ripoti ya Wakaguzi wa Kampuni ya Ernst and Young waliofanya kazi kwa niaba ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ilionyesha kwamba kiasi cha Shilingi 90,359,078,804.00 zililipwa kwa kampuni 13 ambazo zilitumia kumbukumbu, nyaraka na hati zilizo batili na za kugushi na kwamba kampuni hizo hazikustahili kulipwa chochote.
Wakaguzi hao na Ikulu kupitia taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wake, Philemon Luhanjo, Januari 9, 2008, walipendekeza moja kwa moja bila kuuma maneno kwamba wahusika wa kampuni hizo 13 wachukuliwe hatua za kisheria mara moja, kauli ambayo Rais Kikwete aliirejea katika hotuba yake bungeni, lakini bila ukali tena.
Makampuni ambayo Jeetu Patel anahusika nayo na ambayo yamethibitika kughushi nyaraka na kuchota fedha BoT ni Navycut Tobacco (T) Limited, Ndovu Soaps Limited, Bina Resorts Limited, Bencon International Limited, Maltan Mining Company Limited, Bora Hotels & Apartments Limited, Venus Hotels Limited, and B.V. Holdings Limited.
Pamoja na kampuni hizo za Jeetu Patel, kampuni nyingine zilizohusika na jinai ya kughushi nyaraka ni pamoja na Kagoda Agriculture Limited ambayo wanaoonekana katika nyaraka ni John Kyomuhendo mwenye hisa 40 na Francis William anayemiliki hisa 60 katika kampuni hiyo.
Kampuni nyingine ni V.B & Associeties Company inazomilikiwa na Devendra Patel na Jantkumar Chandubhai Patel na Changanyikeni Residential Complex Limited inayomilikiwa na Jose Van de Merwe, Samson Mapunda na Charles Mabina ikiwa na makao yake, Sinza, Kumekucha, Dar es Salaam.
Pia katika orodha hiyo ya kampuni 13 zilizoghushi nyarakaambazo wahusika wake wamependekezwa kuchukuliwa hatua za kisheria mara moja ni Money Planners & Consultants inayomilikiwa na Paul Nyingo na Fundi Kitungi na kampuni ya Njake Hotel & Tours Limited inayomilikiwa Japhet Lema, Anna Lema, Abel Lema, Derick Lema na Benard Lema wa Arusha.
Jeetu Patel katika baadhi ya kampuni anashirikiana na wafanyabiashara wengine wa Dar es Salaam ambao wanatajwa kushiriana naye katika kuhamisha fedha hizo kwenda nje kwa kuzibadili kutoka shilingi za Kitanzania kwenda Dola za Merakani ama Euro bila kufuata mkondo halali wa fedha kinyume cha Sheria ya Udhibiti wa Fedha Haramu.
Miongoni mwa wanaotajwa kushirikiana na Jeetu Patel ni Sidik Yacoubu kupitia kampuni yao ya Ndovu Soap Limited ambayo kwa mujibu wa nyaraka za Wakala wa Leseni na Usajili wa Kampuni (BRELA), kampuni hiyo yenye namba ya usajili 20536 ya Februari 3, 1992, wamiliki wake ni Jayantulal Chandubhai Patel na Sidik Yacoubu.
Katika kampuni ya Bora Hotels and Apartments iliyosajiliwa Septemba 8, 2005 inaonyeshwa katika orodha ya BRELA kwamba wamiliki wake wamo Jayantkumar Chandubhai Patel na Devandra Patel wakati Bina Resort Limited iliyosajiliwa Machi 31, 2005, wamo Jayantikumar Chandubhai Patel na Devendra Patel.
Kampuni ya Maltan Mining Company iliyosajiliwa Machi 8, 1993 inamilikiwa na Jantkumar Chandubhai Patel na Hariharier Radhakrishna wakati Navy Cut Tobacco iliyosajiliwa Oktoba 12, mwaka 1995 inamilikiwa na Jantkumar Chandubhai Patel na Radakrishna.
Kampuni nyingine ni Bencon Limited, B.V Holdings, Venus Hotels na V.B & Associeties Company zinazomilikiwa na Devendra Patel na Jantkumar Chandubhai Patel, ambazo zote zilisajiliwa Aprili 4, 2005.
Katika orodha ya BRELA imo pia kampuni ya Excellent Service Limited inayomilikiwa na Emil Samanya, Peter Sabas na Elisifa Ngowi ambaye anatajwa kuwa ni Ofisa Mwandamizi wa Idara ya Usalama wa Taifa, ambaye yumo katika task force inayochunguza wizi huo. Kampuni hiyo ilisajiliwa Mei 13, 1992 na kupewa namba 26959.
Ngowi anahusishwa pia katika kampuni nyingine ya Clyton Marketing iliyosajiliwa Juni 6, 2005 akiwa na mwenzake Edwin Mtoi, ambaye haikuweza kufahamika mara moja anafanya shughuli gani zaidi ya kuwa katika kampuni hiyo.
Wamiliki wengine waliofahamika ni Rajabu Maranda na Thabit Katunda ambao wanatajwa kumiliki kampuni ya Liqiud Service Limited ambayo usajili wake ulifanyika Desemba 12, 2004 na kupewa namba 15007. Maranda anatajwa kuwa mmoja wa wana CCM mashuhuri mkoani Kigoma na alidaiwa kutaka kuiingiza familia ya viongozi wa juu serikalini katika biashara zake bila mafanikio hususan baada ya Rais Kikwete kuwa makini zaidi.
Wamiliki wengine waliofahamika ni Johnson Lukaza na Mwesigwa Rutakyamilwa Lukaza ambao wao wanamiliki kampuni ya Karnel Meals Holdings Ltd ambayo usajili wake ulipatikana Agosti 4, 1998, Mibale Farm iliyosajiliwa Septemba 2, 2005 na kupewa namba 154039 ambayo inamilikiwa na Kizza Selemani na Farijala Hussein, Malegesi Law Chambers inayomilikiwa na Beredy Malegesi ambayo ilisajiliwa Septemba 24, 2001.
Wamiliki wengine ni Paul Nyingo na Fundi Kitungi, wanaomiliki Kampuni ya Money Planners & Consultants iliyosajiliwa Machi 22, 2005 na Kiloloma & Bros Enterprises inayomilikiwa na Charies Kissa, ambayo ilisajiliwa Aprili 8, 2005.
Katika ukusanyaji wa fedha hizo, task force ya serikali inaelezwa kukusanya shilingi 53,738,835,392/= fedha ambazo Rais Kikwete ameagiza ziingizwe katika mfuko maalumu kwa ajili ya kusaidia sekta ya kilimo zikichanganywa na nyingine zinazotarajiwa kufikia shilingi 64,844,770,688/=