simplemind
JF-Expert Member
- Apr 10, 2009
- 16,695
- 9,580
Dar es Salaam. Aliyekuwa Mwenyekiti wa
Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph
Warioba amewashauri viongozi wazee na
waliokaa madarakani muda mrefu kuacha
kungangania madaraka.
Amesema kuwa ni vyema kwa viongozi
hao kungatuka ili kutoa nafasi kwa vijana
wenye nguvu na akili kulitumikia taifa
katika uongozi.
Warioba aliyasema hayo juzi jijini Dar es
Salaam katika mahojiano maalumu na
gazeti hili, pamoja na mambo mengine
alizungumzia uongozi wa nchi hii.
Mwalimu Julius Nyerere alingatuka akiwa
na nguvu zake kabisa. Kiasili kungatuka ni
dhana ya kuwapisha vijana kuwa mbele
katika kutekeleza majukumu na ninyi
wazee siyo kuondoka, bali kuendelea
kuwapa ushauri na mwongozo,alisema
Jaji Warioba.
Alieleza kuwa kungatuka kunamfanya
aliyechukua hatua hiyo kuishi maisha ya
raha yenye furaha na amani jambo
ambalo yeye sasa analifurahia.
Aliongeza: Haiwezekani mzee ukakaa
kundi moja na kijana wako aliyetahiriwa
juzi, kwani kwa kawaida, kijana akitahiriwa
hupandishwa daraja na kukaa kundi la
wakubwa, hapo wewe baba yake hata
kama una miaka 40, unahamishwa na
kuingia kundi la wazee.
Alifafanua kuwa hata katika uongozi ni
muhimu kungatuka na kuwapisha vijana
ili waweze kutumia akili na nguvu zao
kuendeleza taifa huku wakipata
maelekezo na mwongozo kutoka kwa
wazee.
Maisha yangu sasa baada ya kuacha
uongozi ni ya furaha na amani bila woga
kuliko wakati wowote, tofauti na
nilipokuwa bado kiongozi katika Serikali,
alisema.
Ukiwa kiongozi unaweza kuishi kwa hofu
na shaka huku ukituhumiwa, alibainisha
Jaji Warioba aliyewahi kuwa Waziri Mkuu
na Makamu wa Kwanza wa Rais mwaka
1985 - 1990.
Kauli ya Warioba imekuja huku kukiwa na
kundi kubwa la viongozi wenye umri
mkubwa katika nafasi mbalimbali
madarakani muda mrefu, huku
wakiendelea kutamani nafasi za juu zaidi.
Miongoni mwa viongozi hao, wapo
wanaotajwa kuunda makundi ya kusaka
urais wa Tanzania katika uchaguzi mkuu
ujao mwaka 2015.
Hii siyo mara ya kwanza viongozi wenye
umri mkubwa kutakiwa kungatuka
madarakani.
Januari 14, 2010, Waziri Mkuu Mizengo
Pinda, aliwashauri wazee watumie busara
kupima uamuzi wa kugombea tena nafasi
za ubunge kwenye uchaguzi mkuu. Pinda
alitoa rai hiyo alipokuwa akijibu maswali
ya wahariri katika mkutano alioitisha
kujibu maswali yao jijini Dar es Salaam.
Source: Mwananchi
Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph
Warioba amewashauri viongozi wazee na
waliokaa madarakani muda mrefu kuacha
kungangania madaraka.
Amesema kuwa ni vyema kwa viongozi
hao kungatuka ili kutoa nafasi kwa vijana
wenye nguvu na akili kulitumikia taifa
katika uongozi.
Warioba aliyasema hayo juzi jijini Dar es
Salaam katika mahojiano maalumu na
gazeti hili, pamoja na mambo mengine
alizungumzia uongozi wa nchi hii.
Mwalimu Julius Nyerere alingatuka akiwa
na nguvu zake kabisa. Kiasili kungatuka ni
dhana ya kuwapisha vijana kuwa mbele
katika kutekeleza majukumu na ninyi
wazee siyo kuondoka, bali kuendelea
kuwapa ushauri na mwongozo,alisema
Jaji Warioba.
Alieleza kuwa kungatuka kunamfanya
aliyechukua hatua hiyo kuishi maisha ya
raha yenye furaha na amani jambo
ambalo yeye sasa analifurahia.
Aliongeza: Haiwezekani mzee ukakaa
kundi moja na kijana wako aliyetahiriwa
juzi, kwani kwa kawaida, kijana akitahiriwa
hupandishwa daraja na kukaa kundi la
wakubwa, hapo wewe baba yake hata
kama una miaka 40, unahamishwa na
kuingia kundi la wazee.
Alifafanua kuwa hata katika uongozi ni
muhimu kungatuka na kuwapisha vijana
ili waweze kutumia akili na nguvu zao
kuendeleza taifa huku wakipata
maelekezo na mwongozo kutoka kwa
wazee.
Maisha yangu sasa baada ya kuacha
uongozi ni ya furaha na amani bila woga
kuliko wakati wowote, tofauti na
nilipokuwa bado kiongozi katika Serikali,
alisema.
Ukiwa kiongozi unaweza kuishi kwa hofu
na shaka huku ukituhumiwa, alibainisha
Jaji Warioba aliyewahi kuwa Waziri Mkuu
na Makamu wa Kwanza wa Rais mwaka
1985 - 1990.
Kauli ya Warioba imekuja huku kukiwa na
kundi kubwa la viongozi wenye umri
mkubwa katika nafasi mbalimbali
madarakani muda mrefu, huku
wakiendelea kutamani nafasi za juu zaidi.
Miongoni mwa viongozi hao, wapo
wanaotajwa kuunda makundi ya kusaka
urais wa Tanzania katika uchaguzi mkuu
ujao mwaka 2015.
Hii siyo mara ya kwanza viongozi wenye
umri mkubwa kutakiwa kungatuka
madarakani.
Januari 14, 2010, Waziri Mkuu Mizengo
Pinda, aliwashauri wazee watumie busara
kupima uamuzi wa kugombea tena nafasi
za ubunge kwenye uchaguzi mkuu. Pinda
alitoa rai hiyo alipokuwa akijibu maswali
ya wahariri katika mkutano alioitisha
kujibu maswali yao jijini Dar es Salaam.
Source: Mwananchi