Warioba Anataka Nini Hasa?


!
!
mata core
 
Umeona salim akienda kwenye tv kuongea?anayoyaongea warioba kwenye tv ni maoni yake au ya tume?
Warioba kaenda kama mwananchi wa kawaida na kama waendavyo kina Sabato na wasomi uchwara wengine so kila mtu anajua mnamgwaya kwakuwa anatibua vitumbua vyenu vya kifalme
 
Kwa maneno mengine William anasema hapa Tanzania kuna watu wako huru kuongea na wapo ambao hawana ruhusa ya kuongea!

Hivi kwa nini hii CCM ya "sasa" hawataki Jaji Warioba aongee? Au wanahofia atawaumbua "vinyonga?". Tayari tunajua Asha Bakari "kaufyata" baada ya kufika Dodoma, nyie wengine zamu yenu ya kufumuliwa itawadia.
 

Nilitarajia kuwa ungekuja hapa kutueleza anachokitaka Warioba.
Kwa kukusaidia ni hivi; Nenda kwa aliyewafundisheni kumshambulia na kumtukana Warioba halafu akawaacheni solemba na kwenda kumpa Nishani katika siku ya Muungano. Muulize hivi yeye na Warioba wana Agenda gani ambayo iliyojificha wasiyotaka watanzania wengine wajue?
Tena umuulize Je, Mafundisho aliyowapa ya kumshambulia Warioba ilikuwa ni kipimo cha akili kwa wana CCM kama walilielewa somo la kuwa za kuambiwa changanya na zako?
Tena usisahau kumuuliza kuwa je, aliposema mjiandae kisaokolojia, alimaanisha nini? Maoni ya wananchi au chenga za mwili na namna atakavyowalisheni matango pori na kuwaacha solemba? Na umuulize yeye yupo wapi hasa, Upande wa Warioba/wananchi au wa wahafidhina wa Chama.

Please do so na utujie na majiu utakuwa umetusaidia sna Mkubwa.Yangu ni hayo tu.
Wasalaam.
 
Warioba hajichokonoi mwenyewe. Angalia Wabunge walio wengi Bungeni walivyokuwa wanasema, badala ya kujadili Rasimu ya Katiba walikuwa wanamjadili Warioba. Ukawa wameondoka Bungeni lakini bado mling'ang'ana na Warioba, makalabrasha ya Rasimu yamefunikwa. Funueni makalabrasha ya Rasimu ya Katiba ya CCM muipitishe haraka. Maamuzi ya mwisho yako kwa Wananchi kusema ndio au hapana. Vyombo vya Habari hususani magazeti nayo yakapata habari za kuuza magazeti yao haraka. Andika Warioba ukurasa wa kwanza utauza haraka.
 

Umeuliza WARIOBA ANATAKA NINI, lakini nafikiri kuna haja ya kukuuliza wewe ndio unataka nini kwenye hii therad yako, au kipi hujaelewa kuhusu Warioba.

Hivi unaweza kusema ni yeye ndio alijipeleka mwenyewe labda pale ITV kwenye kile kpindi cha Dk 45 akaomba ahojiwe kuhusu maoni ya tume yake against upinzani anaoupata kutoka CCM? au aliitwa na hao ITV wenyewe?

Kwenye red unazungumzia report ya Rushwa kwamba mbona Warioba haishikii bango. Napata wasiwasi na uelewa wako kuhusu report ya Rushwa Biggie, maana yeye akishakabidhi report mwenye kazi ya kuendelea nayo ni alemtuma. Hata ile report ya Rushwa mfano Serikali ingeamua kuivalia njuga na kukamata wahusika, kama kuna ambae angeipinga basi Warioba angewajibika kuijibu kama anavyofanya now. But waliomtuma waliamua kuikalia baada ya kuona inawahusu watu wanaohusiana nao.

Kwenye blue sekta nyingi za serikali zimejaa watu serikali, ambao kwa wasiojua kutenganisha basi zimejaa makada wa CCM. Ubaya tu ni kua CCM ilishawa-corrupt wajumbe wa kada mbalimbali serikalini kushinikiza serikali 2. Na hata wajumbe wa serikali za mitaa ambao wengi wao ni wa CCm waliamriwa kuhakikisha wanawapitisha watu wa CCM kwenye mabaraza ya katiba ili iwe rahisi kuwarubuni. Kana kwamba haitoshi, Nape Nauye akatumia muda mwingi tu kuandaa mikutano mbalimbali na makada wenu wa CCM kuwashawishi kutokubali serikali 3. Kwa kujua hili ndio maana Warioba na Tume yake waliwapiga chenga haya makundi.

Warioba katika mahojiano yale ya jana amesisitiza kitu kimoja, kuwa iwe sample ilikua ndogo au haikutosha, iwe amechakachua au lah, wanaompinga hawasikilizi au hawajibu "contents za hoja" zilizotolewa na wananchi, bali wanatumia sababu zao binafsi zisizo na mashiko. Nawe umeenda kulekule kwamba ktika paragraph zako zote hapo juu, hakuna hata moja uliyojibu hoja za wananchi wa Zanzibar au wa Bara.
 
Kama yeye siy msemaji wa wananchi iweje mumshambulie Warioba binafsi na siyo wananchi au wajumbe wenzuye wa Tume?
Onyo Kingunge kaisha waonya haswa ninyi vijana mnaomshambulia Warioba.

- Tatizo hata Warioba hawezi kujibu hoja za Serikali 2, uamuzi wa wananchi Warioba sio msemaji wao ndipo ninapopata shida kumuelewa ninaamini ana washauri siajui wanamshauri vipi maana this is more than maoni now!!

Le Mutuz System
 
Wewe umaarufu wako ni mdogo hata huko katika chama chenu wanachama wa Wilaya tu hawakufahamu, uulishindwa kuutumia umaarufu wa baba yako kujijenga kisiasa kama wenziyo wanavyofanya, Si unawaona walivyochangamkia fursa wewe utakesha na hautokuwa kama Baba yako na hata kufuata nyayo zake umeshindwa kabisa.

 
Tatizo wewe hujawekeza kwenye siasa halafu unataka uongozi so lazima ujiondoe akili ili ufanikiwe.
 
amejichokea anaona alisahaulika kwa hiyo anataka kurudi kwenye siasa labda
 
Malecela upo Sahihi Warioba sio Mungu ni wapotofu wanaosema Huwezi kumkosoa Asokoselewa ni MUNGU PEKEE , Wengine wote wanakosolewa tu JAPO ni KWA HOJA NA SI MATUSI.
Misingi wa Hoja ya Serikali 3 ni Kuwa eti ni Maoni ya Watanzania Wengi,TAKWIMU ZAO WENYEWE ZINAWAUMBUA KUWA HILI SI SAHIHI.
HITIMISHO linalotokana na TAKWIMU ZA "KUPIKA" haliwezi Kuwa HITIMISHO SAHIHI ni BATILI TOKEA AWALI Lugha ya Kisheria "VOID AB INITIO"
CCM walipita,CDM ,CUF nk nk Lakini akachagua CCM tu why???? kaons CCM tu.....????
Ukweli alijua JK Mbaya wao(MWALIMU NYERERE FOUNDATION) atabaki ktk Historia Kama Kiongozi aliyewezesha KATIBA ya Wananchi WENYEWE.
Wao wakaona ni sehemu ya KU SETTLE SCORES kwa Kuanzisha Mchakato wa UASI SERIKALI 3 ili JK aonekane amevunja LULU YA MUUNGANO kupitia NIA Njema ya Mchakato wa KATIBA.
WARIOBA na Baadhi ya Watu Ndani ya Timu Yake SI wote Hawakuwa na NIA Njema na JK binafsi kwa a Wachambuzi Makini Wanajua Hilo!!
Taasisi Yao ikimshambulia Mfululizo Miaka ya mwanzo wa Kipindi Cha Pili wa Miaka 5 ya mwisho, Airport akirejea toka USA alipohojiwa kuhusu Mashambulizi ya Taasisi ya Nyerere Foundation ikiongozwa na BUTIKU,SALIM,WARIOBA wote Wajumbe WAANDAMIZI WA TUME YA KATIBA ALIMJIBU MUANDISHI Yule aliyeuliza Swali Nanukuu "wewe hujui kwa NINI wananishambulia mimi na Serikali Yangu???, Hakika Ningeshangaa Saana Kama Wangenisifia, katika Dunia Hii Huwezi Kusifiwa/kupendwa na watu wote Hatua Ungekuwa Mwema kiasi Gani ,Asilimia 15 watakupenda,15%watakuchukia,60% watafuata upepo" mwisho wa kumnukuu JK.
JK Alitumia Busara ya Wazee "Mchawi Mpe Mwanao Akulelee" Ila Mchawi Huyu AKAMPA SUMU MTOTO WA JK Hakumlea Vema.
Ukweli utajulikana tu
William upo Sahihi Kabisa
 
Basi mshauri JK aunde tume nyingine na mwenyekiti awe Nape!, ivi Marekani mlikuwa mnafanya nini uko kama hoja zenu ndo izi aisee!. sasa unalalamika ya kuwa mzee kazi yake imeisha so hasiongee? mungetaka hasiongee msingefungia tovuti ya tume ili sisi wananchi wa kawaida tupate kilichofanywa na tume, sasa tovuti mmefunga na kuongea mnataka hasiongee? kuna nini sasa hapo. hakitoa hoja zinazoitaji majibu nyie mnakurupuka kama gesi ya CHIBUKU ati huyu mzee anavuruga nchi, jibu kwanza hoja afu tuoneshe anavuruga vipi nchi, as a matter of fact nyie ma-CCM ndo mnavuruga nchi uku mmetufunga kitambaa cheusi cha utulivu ila nyie mnakiita amani. baba Riz mpaka leo hajaweza kujibu kwanini akienda zanzibar anaufyata na mwenzie ndo anapigiwa mizinga...
 
Mkuu, siku hizi inakera kusikiliza taarifa za habari. Hakuna kituo/radio ambayo haitakuwa na habari za CCM za kunadi serikali mbili, huko ZBC ndio balaa tupu.
 
Kama yeye siy msemaji wa wananchi iweje mumshambulie Warioba binafsi na siyo wananchi au wajumbe wenzuye wa Tume?
Onyo Kingunge kaisha waonya haswa ninyi vijana mnaomshambulia Warioba.
Sijui ni malezi au nini!!!!! Mpaka mzee Kingunge kaongea na kuwaasa waache upuuzi wa kumshambulia mzee Warioba bado pana vijukuu vinatutumka tu, aibu sana.
 
Ndiyo maana hata serikali ilimshinda wakati akiwa waziri mkuu mpaka akajiudhuru wadhifa wake ni miongoni mwa watu wa hovyo kabisa wanaopenda kulazimisha mambo hata kama hayana maana yapite.
wewe ndo hovyo kama makalio yako.
 
Mwanzisha mada huna credibility ya kumkosoa Warioba. We ni mchanga sana kitaaluma, kiitikadi, kimaono, kifikra, kiuzoefu, kiumri, kiuzalendo na kila kitu humfikii katu, jana tu alikuwa live dak 45 mbona TANESCO walizima umeme?
Mnaweweseka sana maCCM na aluta continua tunasongesha.
 
Kama na sura zingine wataendelea kumshambulia Warioba basi nitaamini kwamba ana matatizo lakini kama sura zingine watapunguza jazba basi tatizo litakuwa WALITAKA MAMBO WANAYOYATAKA WAO kwenye muundo wa serikali. Unajua walijipanga kwenye mabaraza ya kata ambao wajumbe wengi ni wao na mzee akashituka majibu yanafanana akayapotezea (hapa ndio shida na ndio maana wanang'aka maana wanajua nini kilichomo kwenye mabaraza ya kata, hata NECTA wakikuta majibu yanafanana wanafuta matokeo). Kwa kuwa rasimu ya katiba imepokelewa na serikali maana yake ipo sawa maana amekusanya kile ambacho kilikuwemo kwenye term of reference / adidu za rejea vinginevyo angerudishwa field kukusanya more info.
 

- Swali langu ni dogo sana naona umeenda mbali na mapovu mengi pole sana, nimeuliza Warioba anataka nini hasa? Anachokifanya sasa hivi sio kawaida why?

Le Mutuz System
 

- Soma tena mada kaka hapa sijauliza credibility ya Warioba ninauliza anataka nini maana anayoyafanya sio madogo anatafuta nini hasa?

Le Mutuz System
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…