Dark City
JF-Expert Member
- Oct 18, 2008
- 16,253
- 11,599
Ndugu Madaktari wote na wale wenye mapenzi mema,
Nimepata habari za kusikitisha kwamba PM amekwanda kukutana nanyi bila mawasiliano ya karibu na viongozi wenu na kukuta hamko ukumbini. Kama kawaida ya watawala wetu (ambao kiukweli walitakiwa kuwa viongozi), ametoa maagizo yake. Kwamba lazima mrudi kazini kesho Jumatatu na ambaye hatarudi kazini amejifukuziisha. Pia inasemekana amepiga marufuku mikutano yote ya madaktari.
Huu ni uthibitisho mwingine wa matumizi ya nguvu kupita kiasi kama ambavyo serikali imezoea kufanya huko nyuma. Nawaomba mpime uzito wa maagizo ya PM kwa kulinganisha na madai yenu. Natambua kuwa katika hali kama hii, ni rahisi watu kuanza kufikiria kitakachowakuta kesho au kesho kutwa baada ya kufukuzwa kazi. Ila naomba mtambue kuwa dokta habanwi kufanya kazi ya serikali. Kwa hiyo mnaweza kutumia ujuzi wenu mahali pengine lakini mkiwa watu wenye hadhi na heshima inayolingana na taaluma yenui
Ila kama mtaona kuwa bila kufanya kazi serikalini hakuna maisha tena, basi nawashauri mrudi kazini kesho asubuhi na mapema. Hata hivyo kama hilo litatokea, basi mjue kuwa huo ndio utakuwa mgomo wenu wa mwisho kabisa labda baada ya kizazi chenu kuisha.
Mungu awabariki madaktari wetu na awape uvumilivu na busara/hekima ili mpiganie hatima yenu wenyewe na generations zote za madaktari wa nchi hii.
God bless you all,
Dark City,
Nimepata habari za kusikitisha kwamba PM amekwanda kukutana nanyi bila mawasiliano ya karibu na viongozi wenu na kukuta hamko ukumbini. Kama kawaida ya watawala wetu (ambao kiukweli walitakiwa kuwa viongozi), ametoa maagizo yake. Kwamba lazima mrudi kazini kesho Jumatatu na ambaye hatarudi kazini amejifukuziisha. Pia inasemekana amepiga marufuku mikutano yote ya madaktari.
Huu ni uthibitisho mwingine wa matumizi ya nguvu kupita kiasi kama ambavyo serikali imezoea kufanya huko nyuma. Nawaomba mpime uzito wa maagizo ya PM kwa kulinganisha na madai yenu. Natambua kuwa katika hali kama hii, ni rahisi watu kuanza kufikiria kitakachowakuta kesho au kesho kutwa baada ya kufukuzwa kazi. Ila naomba mtambue kuwa dokta habanwi kufanya kazi ya serikali. Kwa hiyo mnaweza kutumia ujuzi wenu mahali pengine lakini mkiwa watu wenye hadhi na heshima inayolingana na taaluma yenui
Ila kama mtaona kuwa bila kufanya kazi serikalini hakuna maisha tena, basi nawashauri mrudi kazini kesho asubuhi na mapema. Hata hivyo kama hilo litatokea, basi mjue kuwa huo ndio utakuwa mgomo wenu wa mwisho kabisa labda baada ya kizazi chenu kuisha.
Mungu awabariki madaktari wetu na awape uvumilivu na busara/hekima ili mpiganie hatima yenu wenyewe na generations zote za madaktari wa nchi hii.
God bless you all,
Dark City,