Waraka wangu kwa Madaktari!!

Dark City

JF-Expert Member
Oct 18, 2008
16,253
11,599
Ndugu Madaktari wote na wale wenye mapenzi mema,


Nimepata habari za kusikitisha kwamba PM amekwanda kukutana nanyi bila mawasiliano ya karibu na viongozi wenu na kukuta hamko ukumbini. Kama kawaida ya watawala wetu (ambao kiukweli walitakiwa kuwa viongozi), ametoa maagizo yake. Kwamba lazima mrudi kazini kesho Jumatatu na ambaye hatarudi kazini amejifukuziisha. Pia inasemekana amepiga marufuku mikutano yote ya madaktari.

Huu ni uthibitisho mwingine wa matumizi ya nguvu kupita kiasi kama ambavyo serikali imezoea kufanya huko nyuma. Nawaomba mpime uzito wa maagizo ya PM kwa kulinganisha na madai yenu. Natambua kuwa katika hali kama hii, ni rahisi watu kuanza kufikiria kitakachowakuta kesho au kesho kutwa baada ya kufukuzwa kazi. Ila naomba mtambue kuwa dokta habanwi kufanya kazi ya serikali. Kwa hiyo mnaweza kutumia ujuzi wenu mahali pengine lakini mkiwa watu wenye hadhi na heshima inayolingana na taaluma yenui

Ila kama mtaona kuwa bila kufanya kazi serikalini hakuna maisha tena, basi nawashauri mrudi kazini kesho asubuhi na mapema. Hata hivyo kama hilo litatokea, basi mjue kuwa huo ndio utakuwa mgomo wenu wa mwisho kabisa labda baada ya kizazi chenu kuisha.

Mungu awabariki madaktari wetu na awape uvumilivu na busara/hekima ili mpiganie hatima yenu wenyewe na generations zote za madaktari wa nchi hii.

God bless you all,

Dark City,
 
nadhani kesho watafuta kada ya udaktari tanzania.mamia ya madaktari wako safarini kwenda dar kwenye kikao endelevu..
 
Ushauri mzuri sana naungana nawe kwa yote isipokuwa kuwashauri kesho asubuhi wawahi kazini, kama ulivyosema hii itakuwa mwisho wa migomo yao na dharau kubwa kwa taaluma yao, nadhani hakuna haja ya kuogopa, endeleeni na mikutano yenu wawatumie FFU. Shime madaktari msijidhalilidhe kwa vitisho vya huyu aliyepinda.
 
nadhani kesho watafuta kada ya udaktari tanzania.mamia ya madaktari wako safarini kwenda dar kwenye kikao endelevu..


Kweli kabisa,

Ndiyo maana nina hamau ya kuiona Thisi time tomrrow!!

DC!!
 
ndugu wapendwa madaktari,poleni sana kwa msukosuko unaoendelea.

nawapongeza kwa kufikisha ujumbe wenu kwa watanzania na watawala.


Nina ushauri kwenu jiono hii,sikiliza.

Nakuombeni mrudi kazini,mimi nauona mgomo wenu kama ni ombi kwa baba na hakika amekusikieni hata kama hamjaonana mkaongea (mmepishana)

Tafakarini madhara/matokeo ya keshokutwa kwa familia zenu.kwa kweli itakuwa ni kiama kwenu.

Acheni kugombana na mzazi wenu,kwa kuwa mlishaonana na mawaziri nina imani madai yenu yameshamfikia waziri mkuu.

Wahudumieni watoto wenu,mama zenu,wajomba zenu na hasa dada zenu ambao ni wajawazito na sasa wameyaweka maisha yao mikononi mwenu kama ndio wakombozi pekee.
 
Nakumbuka wakati wa utawala wa Mwinyi kuna wanafunzi pale UD waliwahi kufanya madudu wakafukuzwa wote.

Upo wakati pia sikumbuki ilikuwa ni awamu ya nani pale mhimbili waliwahi kutimuliwa madaktari wote.sasa madaktari msipambane na dola.RUDINI KAZINI HUKU MKIENDELEA KUTUMIA DIPLOMASIA KUDAI HAKI ZENU.
 
DC, kama kweli serikali inajali wananchi, tutajua kesho

maana wao wakiugua wanaenda india, kwahiyo hata hospitals zetu zikiwa hazina madaktari wao hawaathiriki
 
ndugu wapendwa madaktari,poleni sana kwa msukosuko unaoendelea.

nawapongeza kwa kufikisha ujumbe wenu kwa watanzania na watawala.


Nina ushauri kwenu jiono hii,sikiliza.

Nakuombeni mrudi kazini,mimi nauona mgomo wenu kama ni ombi kwa baba na hakika amekusikieni hata kama hamjaonana mkaongea (mmepishana)

Tafakarini madhara/matokeo ya keshokutwa kwa familia zenu.kwa kweli itakuwa ni kiama kwenu.

Acheni kugombana na mzazi wenu,kwa kuwa mlishaonana na mawaziri nina imani madai yenu yameshamfikia waziri mkuu.

Wahudumieni watoto wenu,mama zenu,wajomba zenu na hasa dada zenu ambao ni wajawazito na sasa wameyaweka maisha yao mikononi mwenu kama ndio wakombozi pekee.

Kumbukeni kitu kimoja kuwa success never comes without sacrifice. Madaktari inabidi mjitoe muhanga ili vizazi vijavyo vya madaktari vije vipate heshima wanayostahili madaktari wote duniani, msipojitoa muhanga mtakuwa wasaliti kwa vizazi vijavyo vya madaktari
 
Ndugu Madaktari wote na wale wenye mapenzi mema,


Nimepata habari za kusikitisha kwamba PM amekwanda kukutana nanyi bila mawasiliano ya karibu na viongozi wenu na kukuta hamko ukumbini. Kama kawaida ya watawala wetu (ambao kiukweli walitakiwa kuwa viongozi), ametoa maagizo yake. Kwamba lazima mrudi kazini kesho Jumatatu na ambaye hatarudi kazini amejifukuziisha. Pia inasemekana amepiga marufuku mikutano yote ya madaktari.

Huu ni uthibitisho mwingine wa matumizi ya nguvu kupita kiasi kama ambavyo serikali imezoea kufanya huko nyuma. Nawaomba mpime uzito wa maagizo ya PM kwa kulinganisha na madai yenu. Natambua kuwa katika hali kama hii, ni rahisi watu kuanza kufikiria kitakachowakuta kesho au kesho kutwa baada ya kufukuzwa kazi. Ila naomba mtambue kuwa dokta habanwi kufanya kazi ya serikali. Kwa hiyo mnaweza kutumia ujuzi wenu mahali pengine lakini mkiwa watu wenye hadhi na heshima inayolingana na taaluma yenui

Ila kama mtaona kuwa bila kufanya kazi serikalini hakuna maisha tena, basi nawashauri mrudi kazini kesho asubuhi na mapema. Hata hivyo kama hilo litatokea, basi mjue kuwa huo ndio utakuwa mgomo wenu wa mwisho kabisa labda baada ya kizazi chenu kuisha.

Mungu awabariki madaktari wetu na awape uvumilivu na busara/hekima ili mpiganie hatima yenu wenyewe na generations zote za madaktari wa nchi hii.

God bless you all,

Dark City,

Huu ni uchochezi sasa... hebu tuwaache madaktari waamue wenyewe jamani... wakifukuzwa utawasaidia kupata hizo nafasi???
 
Kama kweli mgomo huu ni wa madaktari wote hakuna maamuzi ya kuwafukuza kazi yatakayo chukua nafasi kesho, Pamoja na kwamba Serikali imekuwa ikitumia maguvu kwenye maamuzi yao mbalimbali kuna mifano mingi hapo. Ila Tatizo langu kwa Madaktari ni kwanini mmegoma kukutana na PM leo, suala la kwamba leo ni jumapili kama ndio sababu pekee binafsi siiungi mkono kwani hata Kitabu Kitakatifu Biblia kinasema huwezi kumwacha punda shimoni kisa tu ni siku ya sabato mlipaswa kwenda kukutana nae hata kama leo ni jumapili, unless otherwise pana sababu nyingine ya ninyi kutotokea ukumbini, malalamiko yenu ni ya msingi lakini suala la kutotokea ukumbini mimi siliungi mkono.
 
Serikali yenyewe imeshindwa kuziedesha Hospital wataweza kuajiri madokta wapya? kwa pesa gani walionao. Naungamkono Madaktari hakuna kurudi nyuma, mpaka kieleweke
 
Ushauri mzuri sana naungana nawe kwa yote isipokuwa kuwashauri kesho asubuhi wawahi kazini, kama ulivyosema hii itakuwa mwisho wa migomo yao na dharau kubwa kwa taaluma yao, nadhani hakuna haja ya kuogopa, endeleeni na mikutano yenu wawatumie FFU. Shime madaktari msijidhalilidhe kwa vitisho vya huyu aliyepinda.

Mkuu mie nakubaliana nawe. Sasa hivi madaktari wanahitaji kuwa na mshikamano wa hali ya juu ili kupambana na hii Serikali dhalimu. Natumai hiyo kesho wataendelea na mgomo na kutokubali vitisho vya kipumbavu toka Serikali dhalimu.
 
Ndugu Madaktari wote na wale wenye mapenzi mema,


Nimepata habari za kusikitisha kwamba PM amekwanda kukutana nanyi bila mawasiliano ya karibu na viongozi wenu na kukuta hamko ukumbini. Kama kawaida ya watawala wetu (ambao kiukweli walitakiwa kuwa viongozi), ametoa maagizo yake. Kwamba lazima mrudi kazini kesho Jumatatu na ambaye hatarudi kazini amejifukuziisha. Pia inasemekana amepiga marufuku mikutano yote ya madaktari.

Huu ni uthibitisho mwingine wa matumizi ya nguvu kupita kiasi kama ambavyo serikali imezoea kufanya huko nyuma. Nawaomba mpime uzito wa maagizo ya PM kwa kulinganisha na madai yenu. Natambua kuwa katika hali kama hii, ni rahisi watu kuanza kufikiria kitakachowakuta kesho au kesho kutwa baada ya kufukuzwa kazi. Ila naomba mtambue kuwa dokta habanwi kufanya kazi ya serikali. Kwa hiyo mnaweza kutumia ujuzi wenu mahali pengine lakini mkiwa watu wenye hadhi na heshima inayolingana na taaluma yenui

Ila kama mtaona kuwa bila kufanya kazi serikalini hakuna maisha tena, basi nawashauri mrudi kazini kesho asubuhi na mapema. Hata hivyo kama hilo litatokea, basi mjue kuwa huo ndio utakuwa mgomo wenu wa mwisho kabisa labda baada ya kizazi chenu kuisha.

Mungu awabariki madaktari wetu na awape uvumilivu na busara/hekima ili mpiganie hatima yenu wenyewe na generations zote za madaktari wa nchi hii.

God bless you all,

Dark City,

Wananchi wengi wako nyuma ya madaktari,tunajua wanachopigania!inatakiwa wawe na msimamo wa dhati!
 
Nakumbuka wakati wa utawala wa Mwinyi kuna wanafunzi pale UD waliwahi kufanya madudu wakafukuzwa wote.

Upo wakati pia sikumbuki ilikuwa ni awamu ya nani pale mhimbili waliwahi kutimuliwa madaktari wote.sasa madaktari msipambane na dola.RUDINI KAZINI HUKU MKIENDELEA KUTUMIA DIPLOMASIA KUDAI HAKI ZENU.

Usilete vitu vya kusadikika na ambavyo hauna uhakika navyo!
 
Huu ni uchochezi sasa... hebu tuwaache madaktari waamue wenyewe jamani... wakifukuzwa utawasaidia kupata hizo nafasi???


Watanzania wengi tuko kama wewe...tunataka watoto wazaliwe ila mama asitoke damu hata tone moja!!
 
Mkuu mie nakubaliana nawe. Sasa hivi madaktari wanahitaji kuwa na mshikamano wa hali ya juu ili kupambana na hii Serikali dhalimu. Natumai hiyo kesho wataendelea na mgomo na kutokubali vitisho vya kipumbavu toka Serikali dhalimu.


Kweli mkuu,

Kama wakiweza kuvuka masaa 24 ya kuanzia leo saa 6 usiku...watakuwa wamepiga hatua muhimu katika kuifanya taaluma ya udaktari urejeshewe heshima yake!!

Babu DC
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Usilete vitu vya kusadikika na ambavyo hauna uhakika navyo!
Nimewahi kushiriki katika migomo mingi tangia nipo A level hadi chuo. kuna migomo ambayo nilishiriki kikamilifu na kuna migomo ambayo nilishiriki kama sehemu ya jumuiya. Sasa huwa unafika wakati kama huu ambao linatolewa tamko kwamba kufikia kesho ingieni madarasani na kama mtu hataingia darasani basi amejifukuza. Hatua hii huwa ni kimbembe manake hapa ndipo wana mgomo hufarakana baada ya kufikiria wametoka wapi wanategemewa na nani na mipango yao ni ipi! Wengi hurudi nyuma.
 
Nimewahi kushiriki katika migomo mingi tangia nipo A level hadi chuo. kuna migomo ambayo nilishiriki kikamilifu na kuna migomo ambayo nilishiriki kama sehemu ya jumuiya. Sasa huwa unafika wakati kama huu ambao linatolewa tamko kwamba kufikia kesho ingieni madarasani na kama mtu hataingia darasani basi amejifukuza. Hatua hii huwa ni kimbembe manake hapa ndipo wana mgomo hufarakana baada ya kufikiria wametoka wapi wanategemewa na nani na mipango yao ni ipi! Wengi hurudi nyuma.

Ni kweli kabisa Mkuu wengine wana wake zao na watoto na hawana income nyingine hivyo hapa wanakuwa njia panda huku wakiwa hawajui wataendelea vipi kujikimu wao na familia zao katika kipindi hiki kigumu kwao. Kama wataamua kuendelea na mgomo basi tuanzishe michango kupitia hapa jamvini ili kuwasaidia hawa wenzetu katika hali ngumu zitakazowakabili siku za usoni.
 
Back
Top Bottom