Waraka wa wazi kwa Dkt. Kitima

Waraka wa wazi kwa Dkt. Kitima

Kumbe kufa ni kawaida sana. Kwanini hao mapadri na masista ashtuke?
 
Nadhani ktk kundi lao huyu amewazidi wenzake kidogo.
Yes, nimesoma bandiko lote la muandishi, ingawa nayo ilikuwa ni changamoto kutokana na style ya muandishi.

Kwa maoni yangu, angeweza kuandika sentensi moja tu, "tusiogope kufa," kuliko kutuchosha kwa bandiko lake refu.
 
Naona ngonjera ndeefu,mbona mtumish hakutaja corona? Kasema wamekufa kwa matatizo ya magonjwa ya kutopumua vizuri.Ya corona mnatafsiri nyie
 
Nani alikwambika tawala zote zimetokana na Mungu, wana wa Israel walimkataa Mungu baada ya waamuzi wakapata mfalme Saul, Ahabu Mfalme, Pharao wa Misri, Herode hawa ni baadhi ya watawala ambao hawakutokana na Mungu. Manabii ambao waiitwa waonaji ndiyo waikuwa wanangoza tawala za kifalme mfano Nathaniel kipindi cha Mfalme Daudi, Eliya Mtisbi kipindi cha Mfalme Ahabu na mkewe Yezebeli, ni mifano wa manabii waliongoza tawala za kifalme chini yamwngozo wa Mungu

Leo hii watawala wakisiasa ndiyo wanataka kuwaongoza viongozi wa kidini au kiroho hawataki waambiwe ukweli kama Yohana Mbatizaji kwa Herode. Tunawahitaji viongozi wetu wa kiroho waseme kweli hata kama kina Herode watachukia.
 
Hao mapadri na masista walikuwa hawavai barakoa? Waliipata wapi hiyo korona? Wanapumuliana hukohuko kanisani? Waliambukizana wakiwa wapi? Kama tatizo ni waumini si wafunge ibada zote ili kujikinga?

Kwanini matamko yao wasiyatolee kwenye ibada zao wakati wa matangazo? Kama wanaamini katika Mungu kwa nini hatusikii wakihamasisha watu kuingia katika maombi na kuchukua tahadhari kama raisi alivyotamka? Mbona hatukuwahi kuwasikia wakitutamgazia mapadri na masista waliokufa kwa UKIMWI? Au hivyo sio vifo?

Vifo vingi vinatokea Tanzania wanakaa kimya. Hivi hawa watu hawajui kwamba jamii ikiingia katika hofu kubwa, madaktari na manesi nao wataingiwa na hofu na kuwaogopa hata wagonjwa wa malaria na hivyo watu watakufa hovyo kwa magonjwa mengine? Hivi wanajua kwamba uhai wa mtanzania unategemea sana uhusiano mzuri na daktari?

Wamwache raisi afikiri namna sahihi ya kukabiliana na hilo tatizo endapo akijiridhisha kwamba lipo. Hata raisi akitangaza lockdown hao masista na mapadri wana uwezo wa kuishi ndani ya majumba yao bila shida. Maisha yao sio yetu. Ebu muacheni raisi wetu, yeye anaijua nchi yake, anayajua maisha watanzania, anatujua tulivyo. Kelele zenu zisije zikamtumbukuza shimoni alafu nyinyi wenyewe mukaaza kumzomea.
 
Maandishi meengi kumbe lengo lako kutuvuruga tu, mara walei sijui kuhani. Ulipojichanganya uliposema kipindi huyo padri akiwa kiongozi walifariki watu 160 anaowaongoza bili kufafanua ni kipindi cha muda gani ila unasahau padri kasema ndani ya miezi miwili vifo 85, nafikiri nawewe ulipaswa kusema hivyo vifo 160 ni ndani ya muda gani? Mzee ule ugonjwa wenu wa changamoto ya kupumua upo?
 
Nani anataka lockdown nyie? Kwani tahadhari walizozitoa serikali mwaka jana wakizutumia mwaka huu kuna tatizo? Dr Mpango alitoa machozi mbele ya kamera
 
"Vifo vya watu 25 na masista 60"!....
Yaleyale ya ......"ajali imeuwa watu 15 na wamasai 7......"
 
Yani basi tu kwakuwa taarifa imetolewa na kiongozi wa kiroho serikali inashindwa chakumfanya ila kama ingalikuwa watu kama sisi tayari tumeshabambiwa kesi za uhujumu uchumi siku nyingi sana.
 
Bandiko refu,
Watawala ni mamlaka iliyoamriwa na Mungu, he mamlaka za kiaskofu, kipadri na kichunfaji zimeamliwa na Nani?

Ulimpigia kura magufuli, je ukishawashahi mchagua hata muinjilist, katekista licha padri askofu na mchngaji?

Ogopa kugombana na Mungu kijana atakupiga pigo baya

Sent from my TECNO KC6 using JamiiForums mobile app
 
Umeandika mambo mengi sana mpaka unaweza mchosha msomaji

Comment za watu wengi zimeku shambulia sanaa, mtoa mada lazima kuna kitu hakipo sawa. ASIVAE MIWANI YA MBAO

Rai yangu tusitumie nguvu nyingi sana kuuficha ukwel Dr. kitima kwa miaka mingi amekua rolel model kwa mengi.

Kwa watu wanao elewa POLITICAL SCIENCE, kuna mambo mengi sana kwenye hilo somo. Kuna ku uhadaa Umma, kuna kupindisha ukwel kwa manufaa ya Umma, n.k

Anachotaka kukifanya huyu mwandishi ni kuuzima moto kwa petrol
 
Kujikomba kwa aina hii unatutia aibu.
Hujui kuwa mapadre licha ya kuendesha ibada kila siku, hasa jumapili , wako exposed?
Na haiingii akilini mwako kuwa wamezika watu wengi sana waliokufa kwa corona?
Muwage na akili basi hata kama mnajikomba!
 
Kujikomba kwa aina hii unatutia aibu.
Hujui kuwa mapadre licha ya kuendesha ibada kila siku, hasa jumapili , wako exposed?
Na haiingii akilini mwako kuwa wamezika watu wengi sana waliokufa kwa corona?
Muwage na akili basi hata kama mnajikomba!
Mimi nitajikomba na kumuombea raisi wangu kuliko hao wengine, raisi ana mzigo mkubwa sana juu ya taifa hilo kuliko hao wanaotawala watu wa imani moja.
 
Context ya arguments zako na muelekeo ni ule tunaona wazi kusupport washirikina.
Usichojua ni kwamba nchi hii sio ya kidini lazima utambue kuwa hata washirikina ni sehemu ya taifa. Kwa hiyo raisi hawezi kutawala nchi kivatican au kizungu.
 
Huo ni uamuzi wako mkuu.
Ila sote tunamuombea Rais wa madaraka makubwa nchini, ayatende mema daima na kuutukuza Ukuu wa Mungu, Ukweli daima.
Na tunafanya hivyo kila jumapili.

Tukiona maandishi " mene mene tekel upharsin " ukutani, kama mapadre wanavyoonyesha ukweli, tujirudi nyuma na kutafakari.
Tatizo mheshimiwa Mimi sijaliona hilo kanisa kubeba sura ya Yesu wanayemuhubiri. Inawezekana hata hayo maneno mene mene yanalihusu hata hilo kanisa. Hivi hujatambua kwamba hivi sasa duniani hata fasheni ya vijana kujiunga na usista na upadri inaondoka kwa sababu ya matendo ya hao watu? Kwa tabia zao watu wanaanza kusita kuwafanya watoto zao kuwa mapadri au masista.
 
Na Mimi alichonishangaza Doctor huyu ni kuelekeza lawama kwa serikali na wakati huohuo kuwa kipofu wa wajibu wake na wa kanisa!

Kanisa lilishatoa waraka wa maelekezo kwa wakleri na walei juu ya umuhimu na namna ya kujikinga na korona! Mimi ni mkatoliki ninayehudhuria misa kila jumapili lakini makanisa tofauti kulingana na ratiba yangu, hivyo tangazo hilo nililisikia makanisa tofauti niliyohudhuria.

Kinacho nisikitisha ni kwamba makanisa mengi ya RC hayana mpango kabisa wa kutkeleza waraka huo. Waumini wanarundikana kanisani na kwenye shughuli nyingine za kanisa bila tahadhari yeyote. Hakuna cha barakoa (labda upende mwenyewe), hakuna cha kunawa mikono na waumini wanajazana kwenye bench bila kuacha nafasi.

Viongozi wapo, Dr Kitima yupo, tena Katibu wa TEC, mwenyekiti wa Baraza la maaskofu yupo, maaskofu wapo, mapadre wapo! Kinachonishangaza Dr ana guts gani za kunyoshea vidole wengine( japo kiujanja) wakati mwenyewe ameshindwa kuchukua hatua kwenye himaya yake ambayo ana mamlaka nayo?

Kwa kweli hana moral authority ya kukosoa. Asidondokee kwenye siasa za Jamaa zetu ambao wana kosoa wakati wenyewe hawachukui hatua za kujikinga. Hao iko wazi wanatafuta political mileage.
Na wewe umechukua hatua gani? Umewahi siku za ibada kuomba walau dakika 5 utoe tahadhari na kukumbusha kujikinga kwa waumini wenzako? Unamnyooshea kidolek
Kimoja mwenzako lakini vidole 3 vinakunyooshea wewe mwenyewe.
 
Kama nimewahi kuona barua ndefu halafu mbovu hii imevunja rekodi.yaani mamlaka za Mungu zitii mamlaka za binadamu kwani Padri Kutima yuko chini ya nani kama unavyodhani.Baba Mtakatifu akitaka kuongea aombe ruhusa Italia wewe ni RC gani.Sauti ya Kitima ni sauti ya kanisa ambayo ni ya Mungu.mamlaka zinzosemwa katika biblia na ambazo lazima ziheshimiwe ni za kikanisa hizo za uchaguzi mkuu hazina uhusiano.heshimu mamlaka za kikanisa maana zimetokana na Mungu siyo kutuandikia upotofu wako.kusema tu kuwa hakuna adui wakati yupo kunakusaidiaje.ugonjwa huu una unabii hebu uchunguze si kuandika vitu vya ajabu.
 
Tatizo mheshimiwa Mimi sijaliona hilo kanisa kubeba sura ya Yesu wanayemuhubiri. Inawezekana hata hayo maneno mene mene yanalihusu hata hilo kanisa. Hivi hujatambua kwamba hivi sasa duniani hata fasheni ya vijana kujiunga na usista na upadri inaondoka kwa sababu ya matendo ya hao watu? Kwa tabia zao watu wanaanza kusita kuwafanya watoto zao kuwa mapadri au masista.
Usihamishe magoli, swala hapa ni ukweli.
Hata JPM anasema msema kweli ni mpenzi wa Mungu.
Kinacho tutia shaka ni serikali yake kutotii ukweli huu.
Watu wanakufa kw corona halafu tunupuuza ukweli huo na kutafuta visingizio vingine vya uongo.
Uongo ni tabia kuu ya yule mwovu.
Mene mene tekeli inamhusu kila mtu aupindishaye ukweli na kushabikia uongo, na haijalishi wewe ni padre, raisi au mtu baki.
Mwalimu aliwahi kusema , Ukweli una tabia moja, utajitokeza na kumuaibisha yule anayejaribu kuuficha.
 
Back
Top Bottom