Waraka wa wazi kwa Dkt. Kitima

Waraka wa wazi kwa Dkt. Kitima

Mwazo anasema ni mkazi wa Geita huku mwisho anasema address ya Dar es Salaam. Hilo tu linatosha kuonyesha wewe ni mdanganyifu

Pili kanisa Katoliki Msemaji wake ni Katibu wa TEC ambaye ni Padri Kitima, pia na hiki hujui hivyo wewe sio mkatoliki Kama ulivyojitambulisha.

Tatu Dr. Padri Kitima ameongea Kama taasisi kwa kusema wanafamilia yake wamekufa 85 ndani ya kipindi Cha miezi 2 hivyo Kuna shida. Wewe unaifanya hujui. Hivi wakifa wabunge 85 kwa miezi 2 kwa kushindwa kupumua Bunge litaendelea? Je speaker hatoongea?

Umekosa hoja dhidi ya kilichosemwa badala yake umeamua ku attach personality

Ukiona msomi anajua na hoja za ajabu kamahizi jua Kuna maslahi yanapiganiwa.

By the way nimeambiwa wewe ndio muuza majeneza pale Muhimbili hivyo unataka watu waendelee kufa mfanye biashara. Pole sana
 
Huwa hampendi kuambiwa UKWELI enyi pro gvt.
Lkn haya n matokeo ya kanisa kuyafumbia maovu yanayoendelea katika taifa hili,kanisa mmekuwa mstari wa mbele kujipendekeza kwa huyu mtu ambaye hafai kabisa kuwa kiongozi wa taifa.
Nachelea kuamini kama kanisa katoliki lina collective responsibility kwa sa sa kuna mdudu amepenyezwa ili kuwagawa msiwe kitu kimoja.
Naona wale maaskofu kutoka kanda pendwa naona wapo kimya tu hawataki kuzungumza jambo lolote lililo against na huyu Mkuu wa malaika, Naona kuna kitu hakipo sawasawa.
 
Huyu atakuwa MATAGA anayejua kuandika.
Lakini umepata muda wa kusoma andiko lake lote?

Sijui kama linakidhi sifa hiyo ya "kujua kuandika."

Lakini mbali ya hilo.

Nimetambua sasa kwamba huko waliko 'MATAGA' kama ulivyowaita, kuna kitengo/kundi maalum lililopewa kazi za namna hii, kukanusha na kusuta kila panapotokea serikali kusemwa.
Utaona, baada ya bandiko kuwekwa, kuna msululu wa timu nzima umejipanga kutetea bandiko, pamoja na kuwa bovu.

Hii siyo mara ya kwanza kushuhudia mpangilio wa namna hii hapa JF.

Iliyobaki tu sasa, nadhani ni kuwafanyia utafiti wa kutosha wahusika ili dhana hii iimarike bila ya mashaka yoyote.
 
Hivi covid 19 ni issue ya kisiasa? Ifike mahali tuwaache wataalamu wa afya wafanye kazi yao
 
Dogo mleta mada hata kama maisha yako yanategemea kujipendekeza kamwe usiache kusema kweli Padre Dkt.Kitima sio saizi yako kwenye uelewa na kuchanganua mambo.
Tafuta MATAGA wenzio ndio muanze kubishana.
 
lako real na sio fake ID hapa jukwaani,weka email yako! Ndipo hapo uone moto wa Kitima! Sasa unamjibu Kitima kwa jina fake?? Kitima kahudumu Saut zaidi ya miaka 10,wanafunzi 168 kufariki nikawaida sana,tofauti na Mapadiri 20 ndani ya miezi 2!
Ninakubaliana na mengine uliyoandika huko juu, lakini siyo hili hapa.

Kutakuwa na kasoro kubwa sana "wanafunzi 168 kufariki" kwenye chuo hata ndani ya miaka hiyo kumi!

Kutakuwa na hitilafu kubwa sana ndani ya chuo hicho.

Labda useme kufa kwa ajali moja inayohusu wanafunzi wengi kwa mpigo. Zikiwa ajali mbili, katika muda huo huo, bado kuna maswali muhimu ya kuwauliza chuo.
 
Sijapenda alichokifanya kitima, lakini huyu alichoandika ni aibu.
IQ ndogo.

Rejea vaccine fake zilizokua seized south africa then unganisha dots na mawazo ya Raisi wetu.

Anyway, very few priests go for science at seminary , most of the seminarians who attain priesthood are those who were incapable of understanding science studies.

Most of seminarians who quit seminary schools are those who take science subjects.

Dini imetumika sana kulikolonize bara la afrika.

Hatuhitaji viongozi wa dini sana, tunahitaji imani.

Personality disorders and corruption in church is another Chaos.
 
Wewe pia hapa hujaandika lolote la maana. Huna tofauti yoyote na huyo aliyeleta mada; tena hata pengine yeye akawa bora kidogo zaidi yako.

What has science to do with Fr Kitima's (no actually it's not Fr Kitima personally) presentation, and even for "most seminarians not taking science subjects?
The rest of your writing merits no response.
 
Kazi unayo mamaangu kazi unayo. Sina hakika kama kuna kitu katikati ya masikio yako sina hakika
 
Hii Serikali ndio bogus kabisa kwenye Science kuliko hao viongozi wa Dini, Serikali inasema maombi ya siku tatu yaliponya Corona? Tena anayetamka Hilo ana PhD ya Kemia..!
Anaenda kanisani na kuwaambia waliovaa masks wamekosa imani kwani Mungu ndio atakayetulinda, IQ ya panzi
 
Shida yako ni teuzi. Sitaki kuamini endapo ndani yakanisa kubwa duniani kuna mambulula hivi. Kwakua mko 12 million basi akipotea mmoja hatakiwi kutaftwa!!! Aise
 
Wewe ni muongo mkubwa kwenye takwimu za vifo vya hao wanafunzi.
Mamlaka zote zinatoka kwa Mungu , sawa lakini unafafanuaje mamlaka ya Idd Amin huko Uganda, Bokassa huko Afrika ya Kati, Hitler Wa ujerumani nk. Pale ambapo utawala unaenda kinyume na mapenzi ya Mungu unapoteza uhalali Wa kumuwakilisha Mugu kwa watawaliwa na hivyo utawala huo unamtumikia yule mwovu shetani.

Maelekezo ya utawala huo hayana haki ya kuendelea tuitii. Ni kama mfano binadamu wote tumeumbwa na Mungu mmoja lakini baadhi wameamua kutumikia shetani. Katika historia ya dini watumishi Wa Mungu walisulubiwa sana na tawala zote, kwa hiyo Kitima hatakuwa Wa kwanza.

Namhurumia tu kakanyaga kaa la moto. Namuunga mkono kiongozi Wa kiroho ametimiza wajibu wake. Angalia makala yako ndefu sana lakini supporter hata moja. Uongo na mawazo ovu hata ungetoa research kubwa na nzito sana huwezi kuita uongo ukawa ukweli. Sisi wakatoliki tuko na msimamo Wa kanisa na Father wetu Kitima ,msemaji Wa TEC bila kusahau maana unamshambulia kama vile anajisemea kama wewe.

Sent from my TECNO-J5 using JamiiForums mobile app
 
Unaposema kipindi chake chote hapo SAUT unaongelea kipindi cha muda gani, maana juzi ameongelea kipindi cha miezi 2, Maaskofu 25 masister na manesi 60 wamefariki, jumla ni uhai wa watu 85, kweli idadi yote hiyo ya vifo kwa kipindi cha miezi miwili hamutaki mtu aongee kwa mashaka?
Tuna shida mahali fulani, tena shida kubwa tu.
Mapadri 25!
 
Pole,hao wataalamu wako ndio wanaoambiwa hawana ruhusa kusema chochote juu ya ugonjwa wa corona. Wanataka hata sisi tuendelee kudanganywa kuwa corona ni fluu.Nasikitika sikutegemea wewe utushauri tumpuuze Dr. hali yeye yupo sawa.Yale aliyoyasema ndiyo sahihi.Hivyo sisi waumini tunakupuuza wewe,tena kwa sauti moja na sauti kubwa pamoja na kuandika mashairi mareeefu hayatusaidii chochote.

Kwanza tulishadanganywa mara phneumonia,mara homa kali ya kupumua.mara homa kali ya mapafu nk. Mwisho sasa Corona ipo na imeua watu wengi.Tiba inahitaji ugonjwa ujulikane.Na sio kuficha kwa sababu uchumi wako utaanguka.Sasa kipi bora,kupoteza watu uchumi wako upande au kuponya watu taifa lisonge mbele.Viongozi wa Dini asanteni kwa kuwa wazi sasa.Mungu awatunze.
 
Na Mimi alichonishangaza Doctor huyu ni kuelekeza lawama kwa serikali na wakati huohuo kuwa kipofu wa wajibu wake na wa kanisa!..
Nadhani tatizo kubwa ni kutoelewa hoja kimantiki. Hoja ya Dk. Kitima iko wazi sana, katika hili la corona serikali imekwepa au imezembea wajibu wake! Hivi wewe ni kipofu au kiziwi? Hujaona serikali inavyowafitinisha mpaka mapadri wenyewe kwa wenyewe kwenye hili la corona? Mnajitoa akili mno mpaka mnageuka kuwa aibu tupu!
 
Umeandika mambo mengi, lakini hoja yako kuu ni moja tu. Hamtaki kusikia mawazo tofauti na yale mnayo yapenda nyinyi. Hii nchi siyo mali yenu. Waacheni watu waongee!! Khaa

Unahoji kama huyo Padre anatii mamlaka!! Mamlaka gani? Mbona hata nyinyi tulio wapa hayo mamlaka hamtutii? Zaidi tu ya kutukejeli na kutusimanga?

Mpe Kaisari yaliyo take Kaisari. Na mpe Mwenyezi Mungu yaliyo yake Mwenyezi Mungu. Viongozi wa kanisa hawana mamlaka ya Kaisari. Wana mamlaka kanisani. Nini kinaendelea kwao sasa?
 
Nadhani tatizo kubwa ni kutoelewa hoja kimantiki. Hoja ya Dk. Kitima iko wazi sana, katika hili la corona serikali imekwepa au imezembea wajibu wake! Hivi wewe ni kipofu au kiziwi? Hujaona serikali inavyowafitinisha mpaka mapadri wenyewe kwa wenyewe kwenye hili la corona? Mnajitoa akili mno mpaka mnageuka kuwa aibu tupu!
Nini ambacho hujaelewa kwenye hoja yangu?

Dr Kitima ni kiongozi wa juu kabisa wa kanisa katoliki. Miongoni mwa mikusanyiko mikubwa (ambayo ni hatarishi kwa ugonjwa huu) tuliyonayo ni mikusanyiko ya kidini kupitia maadhimisho ya misa, mafunndisho, jumuiya nk. Sasa taasisi ambayo inaongoza kukusanya watu wengi (waite waumini) na inaamini katika kuchukua tahadhari za kujikinga na korona lakini haitaki kufanya hivyo! Lakini ana kifua cha kutoka nje na kumlaumu mwingine kwa nini hachukui tahadhari! Hawezi kukwepa lawama.

Hata vifo vya mapadre na masista (Mwenyezi Mungu awalaze mahali pema peponi) kwa kipimio chake hicho hicho wengine wanaweza wakasema yeye na uongozi wa kanisa ndio wamesababisha vifo hivyo kwa kushindwa kutekeleza hatua za tahadhari kwa makusudi katika mazingira wanayofanyia kazi (ya kikanisa) ambayo wanawajibika nayo.
 
Back
Top Bottom