Waraka kwa Mstahiki Meya Boniface Jacob

Waraka kwa Mstahiki Meya Boniface Jacob

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2015
Posts
14,242
Reaction score
34,917
Mstahiki meya,

Pole sana kwa Hujuma zinazoendelea juu yako na Mameya wenzako ambao wako chini ya mwamvuli wa UKAWA.

Binafsi nimeshuhudia namna ambavyo umekua ukijitoa (kucompromise na serikali),hata kama ni kwa kujiumiza nafsi yako, au maamuzi na Itikadi za chama chako, kwako maendeleo ya wananchi wa kinondoni bila kujali vyama vyao ndio imekua kipaumbele chako.

Nakumbuka ulivyoamua kushiriki mbio za Mwenge, naujua vizuri msimamo wako juu ya hili, lakini ulifunika kombe mwanaharamu apite.

Najua ambavyo uzinduzi wa Program ya Jeshi la Polisi pale Biafra, mgeni rasmi akiwa Rais ulivyohujumiwa na bado ukapigwa madongo huku hata wewe haupo, haikukufanya urudi nyuma kuwatumikia watu wako. Spidi ndio kwanza naona imeongezeka

Mstahiki Meya,
Nimesoma maelezo yako mara baada ya ziara ya Rais Kinondoni, nimepatwa na simanzi sana. Hasa hasa hujuma ya mradi wa kuzoa takataka na kuanzisha kiwanda cha mbolea, ambao ni msaada kutoka Ujerumani.Hili si la kufumbia macho kabisa.

Nimekutana na wadau kadhaa, wa vyama na Itikadi tofauti, kama wakazi wa kinondoni, tumedhamiria kuuokoa mradi huo, ilimradi utuhakikishie kwamba kodi wanayoitaka serikali ya TZS 900m ikipatikana, waliotuahidi msaada, wako tayari kurudi.

Tumepiga hesabu ya wakazi 90,000 pekee wa Kinondoni watakaokuwa tayari kuchangia TZS 10,000 tutakua tayari tumepata TZS 900m. Lakini tunadhamiria kupokea hata kiasi kidogo kama 500 au hata mwenye kikubwa zaidi ya 100,000.

Tunaomba uanzishe account maalum za Tigopesa, Mpesa, Aitelmoney, Halotel money kwa Jina la Meya na tulete kampeni ya kukusanya pesa hizo ngazi ya Kata, Mtaa, Nyumba kwa nyumba na mtu kwa mtu.

Kama Serikali haitaki kutupa maendeleo acha tupambane kwa nguvu zetu tuwaonyeshe udhaifu walio nao.

Nitakuwa mstari wa mbele, kama utaridhia wazo hili kuhakikisha tukafanikiwa na mradi uanze mara moja.

NAKUTAKIA UTUMISHI ULIOTUKUKA KWA WANANCHI WAKO, MUNGU YUKO NAWE SIKU ZOTE NA DAIMA HAKI HUSIMAMA KWENYE UKWELI

Sam Ntakamulenga

Mkazi wa Kinondoni,
Mtumishi wa watu wa Urambo Mashariki
 
WARAKA WANGU KWA MSTAHIKI MEYA WA MANISPAA YA KINONDONI MH Boniface Jacob

Samwel Ntakamulenga

Mstahiki meya,
Pole sana kwa Hujuma zinazoendelea juu yako na mameya wenzako ambao wako chini ya mwamvuli wa UKAWA

Binafsi nimeshuhudia namna Ambavyo umekua ukijitoa (kucompromise na serikali),hata kama ni kwa kujiumiza nafsi yako,au maamuzi na Itikadi za chama chako,Kwako maendeleo ya wananchi wa kinondoni bila kujali vyama vyao ndio imekua kipaumbele chako

Nakumbuka ulivyoamua kushiriki mbio za Mwenge, Naujua vizuri msimamo wako juu ya hili,lakini ulifunika kombe mwanaharamu apite

Najua Ambavyo uzinduzi wa program ya jeshi la polisi pale biafra,mgeni rasmi akiwa Rais ulivyohujumiwa,na bado ukapigwa madongo huku hata wewe haupo,Haikukufanya urudi nyuma kuwatumikia watu wako.Spidi ndio kwanza naona imeongezeka

Mstahiki Meya,
Nimesoma Maelezo yako mara baada ya ziara ya Rais Kinondoni,Nimepatwa na Simanzi sana.Hasa hasa Hujuma ya mradi wa kuzoa takataka na kuanzisha kiwanda cha mbolea,ambao ni msaada kutoka ujerumani.....Hili si la kufumbia macho kabisa

Nimekutana na wadau kadhaa,wa vyama na Itikadi tofauti,kama wakazi wa kinondoni,tumedhamiria kuuokoa mradi huo,Ilimradi utuhakikishie kwamba kodi wanayoitaka serikali ya TZS 900m ikipatikana, waliotuahidi msaada,wako tayari kurudi

Tumepiga hesabu ya wakazi 90,000 pekee wa kinondoni watakaokuwa tayari kuchangia TZS 10,000 tutakua tayari tumepata TZS 900m.Lakini tunadhamiria kupokea hata kiasi kidogo kama 500 au hata mwenye kikubwa zaidi ya 100,000.

Tunaomba uanzishe account maalum za Tigopesa,Mpesa,Aitelmoney,Halotel money kwa Jina la Meya na tulete kampeni ya kukusanya pesa hizo ngazi ya kata,Mtaa,Nyumba kwa nyumba na mtu kwa mtu

Kama Serikali haitaki kutupa maendeleo acha tupambane kwa nguvu zetu tuwaonyeshe udhaifu walio nao.

Nitakuwa mstari wa Mbele,Kama utaridhia Wazo hili kuhakikisha tukafanikiwa na Mradi uanze mara moja.

NAKUTAKIA UTUMISHI ULIOTUKUKA KWA WANANCHI WAKO, MUNGU YUKO NAWE SIKU ZOTE NA DAIMA HAKI HUSIMAMA KWENYE UKWELI

Sam Ntakamulenga

Mkazi wa Kinondoni,
Mtumishi wa watu wa Urambo Mashariki
 
Wazo zuri, ndugu yangu uliyeleta post hii. Mimi siyo mkazi wa Dar/ Kinondoni lakini nipo tayari kuchangia. Tukiukosa mradi huu, wazungu watatudharau sana. Matakataka haya ya Dar halafu tunaukataa ukombozi huu. Please Major fungua hiyo/hizo accounts, tuarifu tutachanga. Waambie wahisani wetu, Wajerumani ili watupe muda kidogo tupige harambee tutapata tu hiyo pesa. Nawaomba Watanzania wote wenye mapenzi mema, tuchange. Angalia, Dar ndiyo sebule ya Tanzania.
 
Makonda hamuwezi mstahiki Meya wa Kinondoni hata akileta figisufigisu kwa kutaka kukwamisha juhudi zake za kuwasaidia wakazi wa DSM..Meya aachwe apige kazi awatumikie wananchi wenye uchu wa maendeleo
 
Wazo zuri, ndugu yangu uliyeleta post hii. Mimi siyo mkazi wa Dar/ Kinondoni lakini nipo tayari kuchangia. Tukiukosa mradi huu, wazungu watatudharau sana. Matakataka haya ya Dar halafu tunaukataa ukombozi huu. Please Major fungua hiyo/hizo accounts, tuarifu tutachanga. Waambie wahisani wetu, Wajerumani ili watupe muda kidogo tupige harambee tutapata tu hiyo pesa. Nawaomba Watanzania wote wenye mapenzi mema, tuchange. Angalia, Dar ndiyo sebule ya Tanzania.
Hata mimi ni tayari kuchangia japo nipo mbali na Kinondoni. Nimesoma taarifa ya Meya Jacob, kweli viongozi wa serikali hii wana wivu sawa na genge la wachawi. Yaani wanataka kujenga viwanda wakati huo huo wanahujumu juhudi njema kama hizi!! Meya hadithi yako haitofautiani na yetu Tumeanzisha CBO yetu moja. Tumekuwa na mpango wa kuanzisha maktaba kwa kila shule ya Msingi katika Kata yetu. Tukatafuta marafiki kutoka nje, katika moja ya nchi za Amerika Kaskazini, wakatuma Mzigo umejaa vitabu na vifaa vingine vinavyohusiana na maktaba. Sasa ni karibu miezi miwili tumekwamishwa eti tunakiwa kulipa gharama inayozidi thamani ya mzigo wenyewe. Wazungu wale anashangaa, wakiuliza upeo wa watendaji wa serikali yetu wanaomtaka mtu anayewasaidia wananchi tena mgeni ailipe serikali hiyohiyo inayosaidiwa kodi!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
UMOJA NI NGUVU , MIMI NI MKAZI WA KINONDONI NA NITASHIRIKIANA NA NYIE 100%. WEKENI GROUP TUJADILIANE NA TUONE TUTASHIRIKIANAJE. MILIONI 900 PESA NDOGO SANA HIYO.
 
Mtu anayeleta maendeleo ndio anatapatapa mtaji wenu si mizengwe
Mkuu mimi huwa nasema jamii yetu watanzania ni ya watu wapuuzi kabisa ambao hatukustahili kuwepo duniani. Huwa sielewi kabisa hizi roho mbaya tulizo nazo kwa ajili ya maendeleo yetu wenyewe. Viongozi wetu walio wengi ni tatizo kubwa. Hili sakata lililomkumba Meya wa kinondoni ni sawa na jamaa yangu mmoja anafanya kazi serkalini kapata aliongea na wafadhili kusaidia wanafunzi wanaohitaji interniship baada ya kumaliza masomo vyuoni. Mfadhili alikubali kuchukuwa wahitimu 30 -50 kwa mwaka kwenye NGOs zianazofanya kazi Tanzania. Huyu bwana alipowasilisha hili wazo kwa wakubwa wake wa kazi ambao ndo decision makers, walimuuliza wao watafaidika na kitu gani kwa kuwapeleka hao wahitimu? Hebu fikiria jinsi gani watanzania tulivyo na roho mbaya (roho za kishetani). Kwa sababu tu mtu hana anachopata kwa kumsaidia mtoto wa masikini aligoma katu katu hata kuwasiliana na hao wafadhili ili tu watoto wa masikini wasipate hizo nafasi za kufanya interniship. Jamii ya kitanzania nadhani tumelaaniwa.
 
Back
Top Bottom