Waraka kwa Maaskofu -Wakatoliki

Waraka kwa Maaskofu -Wakatoliki

Sawa!! Huu ni waraka wa waraka wa maaskofu wa katoliki ambao kwa mtazamo wako ulikuwa na chembechembe za uchadema na uchagga!! Umeelezea makosa yao ya miaka 359 iliyopita! Ila umeshindwa kuona kuwa content za waraka wao zinaelezea matukio halisi yaliyotokea ndani ya kipindi cha chini ya miaka mitatu tu iliyopita! Tukio halisi hutazamwa kiuhalisia bila kujali nani anayelitazama! Halihitaji sense of comparability! Kwa mfano chadema waliwahi kusema kuwa ndani ya ccm kuna mafisadi,ccm wakasema hapana! Baadaye ccm wakakiri kuwa kweli kuna ufisadi na wapo tayari kuushughulikia! Hapo main context ni Ufisadi(kitu kibaya) maana kwa hoja yako ya moral authority tukiichukulia serious itatubidi tuwatimue kazi majaji na mahakimu wengi mno kwa kutumia hilo rungu la moral authority!! Bado haujapima moral authority ya maaskofu wa kkkt? Fanya hivyo! Ukimaliza hayo nawewe ujipime moral authority yako juu ya wengine!

Kaka huyu jamaa ana lake tu, nimemsoma kwa umakini sana nimegundua lengo lake ni kutaka kuonesha kwamba TEC inaegemea CHADEMA na kwamba TEC ina ukanda kwa vile kaona maaskofu wengi wanatoka Kilimanjaro ukilinganisha na idadi kutoka mikoa mingine. Sasa kwanza angesema TEC ina maaskofu wangapi kwa jumla yao na je kama maamuzi yanapitishwa kwa kura hao maaskofu wenye asili ya kilimanjaro watashinda kwa kura kweli? . Huyu kada nimempuuza kwasababu ana agenda ya hovyo iliyofichwa kwenye historia ya zamani.
 
Swali hili naamini mtoa mada hawezi kujibu na ndio msingi wa hoja yake ya "ukabila" kanisani. Anazunguka bure na kutoa mifano mingi isiyokuwa na uhusiano na alicho nacho nafsini. Huyu mtu na wengine kama yeye ndio "wakabila" wakubwa na hivyo ni wa kupuuzwa kwani mchango wao hauna tija kwa taifa wala kwa kanisa.

Chanzo cha mtu huyu mwenye moyo wa ukabila uliomzidi na kumpagawisha niwasaidie tu kumwelewa na kuwaelewesha ni uteuzi uliofanywa hivi karibuni wa Fr. Dr. Beatus Urassa (mtawa) kwa Papa Francisco kumteua kuwa askofu mpya wa sumbawanga ambapo mhashamu askofu Damian Kyaruzi anamaliza mda wake (anastaafu).

Kwa vile mtoa mada ni "mkabila" tena aliyeiva kwelikweli yeye angetaka askofu mteule wa sumbawanga awe "mfipa" wa palepale na si kutoka nje. Na kuonesha wazi kuwa huyu mtu si mkabila tu bali pia ana chuki binafsi na baadhi ya makabila ametaja mwenyewe orodha ya mababa maaskofu toka kabila la wachaga na wengine amewateua yeye mwenyewe na kuwapa vyeo wasivyokuwa navyo (mf. kumuita Padri Deogratius Matika askofu), hii ndio tabia ya nongwa ya chuki, haifichiki.

Nimkumbushe mwandishi kuwa amechelewa sana na yuko nyuma ya wakati, haya anayoandika humu yanamdharirisha na kumfunua uchi wake mbele ya walimwengu tena mchana kweupe, au ulitaka uteuliwe wewe kuwa askofu wa sumbawanga, Mwanza, kahama, Kigoma na kwingineko?

Kanisa katoliki lilikwisha ondoka zamani huko uliko wewe na unakotaka kwenda, angalia maaskofu wote ktk Baraza na useme wangapi ni wazawa wa majimbo yao, Mimi ni muumini mlei wa jimbo katoliki shinyanga, askofu wetu mhashamu Liberatus Sangu (mfipa) na anatuongoza vzr sana mashallah...nenda DSM, mtwara, songea, bunda, musoma, karagwe, tabora na kwingineko kwingi tu maaskofu wao ni Watanzania sio lazima wa makabila yao bali kanisa moja, takatifu, katoliki, LA mitume. Na hata majimbo yanayoongozwa na wazawa, sio sifa ya uzawa iliyowafanya wateuliwa na Kanisa bali sifa stahiki za cheo hicho.

Kanisa la Tanzania linaadhimisha miaka 150 ya ukatoliki Tanganyika na miaka 155 ukatoliki visiwani Zanzibar mwaka huu 2018, itakuwa ajabu kanisa kongwe namna hii kuchukua mawazo ya kitoto na kishamba kama haya ya huyu mtoa mada hii akijijengea kichaka cha "moral authority" na kufichama ndani yake kumbe kasahau "kufunga zipu"

Namaliza: injili imeonya kuwa "dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu" ndiyo dhambi pekee isiyokuwa na msamaha mbinguni na duniani, kazi za utume ni kazi za Roho Mtakatifu mgawaji wa vipaji na mpangaji wa kazi za wokovu wa waamini (rejea liturujia ya daraja takatifu) kadiri ya imani katoliki. Kujaribu kukosoa, kuhoji au kukataa teuzi za watumishi wa Mungu ktk nafasi yoyote ile ni kuingilia kazi za Mungu Roho Mtakatifu aliye sawa na Mungu Baba na Mwana, ni kukufuru kusiko sameheka.

Kama mleta mada ni "mkatoliki" kweli, nimsihi afanye mambo mawili, ama arudie mafundisho na kuelewa vyema imani yake au atulie anyamae na kuachana na hii biashara yake ya udaku kwani kinyume na hapo aweza ishia kubaya. Mungu mkarimu atusaidie sote, amina.
Nakuunga mkono kwa asilimia kubwa. Naamini mleta mada anatokea Mkoa wa Rukwa na tatizo lake ni kutoona mfipa mwenzake akipewa daraja la Uaskofu. Labda nimuulize; Ni Padri gani Mfipa alistahili kuwa Askofu?
 
Sawa!! Huu ni waraka wa waraka wa maaskofu wa katoliki ambao kwa mtazamo wako ulikuwa na chembechembe za uchadema na uchagga!! Umeelezea makosa yao ya miaka 359 iliyopita! Ila umeshindwa kuona kuwa content za waraka wao zinaelezea matukio halisi yaliyotokea ndani ya kipindi cha chini ya miaka mitatu tu iliyopita! Tukio halisi hutazamwa kiuhalisia bila kujali nani anayelitazama! Halihitaji sense of comparability! Kwa mfano chadema waliwahi kusema kuwa ndani ya ccm kuna mafisadi,ccm wakasema hapana! Baadaye ccm wakakiri kuwa kweli kuna ufisadi na wapo tayari kuushughulikia! Hapo main context ni Ufisadi(kitu kibaya) maana kwa hoja yako ya moral authority tukiichukulia serious itatubidi tuwatimue kazi majaji na mahakimu wengi mno kwa kutumia hilo rungu la moral authority!! Bado haujapima moral authority ya maaskofu wa kkkt? Fanya hivyo! Ukimaliza hayo nawewe ujipime moral authority yako juu ya wengine!
Huwezi kutoa kipande cha mti katika jicho la mwenzako wakati wewe una bonge la banzi
 
Huyu mwandiahi ni zaid ya mchochez hii topic ifutwe.
 
Ni kweli mleta mada ni mkabila, ila suala ambalo hulitambui ni kuwa mtu hatakuwa mkabila kwa sababu anaitwa hivyo. Na mtu hawezi kuitwa kwamba siyo mkabila kwa sababu hataitwa hivyo. Hata madikteta duniani kitu cha kwanza ambacho walikifanya ni kuhakikisha hakuna watu watakaowaita wao kuwa ni madikteta. Kama mleta mada ni mkabila ukweli utajulikana tu, na kama siyo hivyo basi hilo nalo litajulikana pia

Mkuu huyu kaonekana wazi kabisa tena kwa macho ya uchi (nyama) kabisa. kwanza amesema "inasemekana walioandaa waraka ni maaskofu 4 watatu wakiwa na asili ya kilimanjaro na moja ni Niwemugizi ambaye yeye si mchaga" sasa kwanza angetuambia nani anasema. Pili kawataja kwa majina na majimbo yanayoongozwa na Maaskofu Wachaga lakini hajafanya hivyo kwa majimbo mengine wala hajasema kule jimbo la msoma Msonganzila Michael ni kabila gani na ametokea wapi. Hii inaonesha ana agenda ya siri (ukabila) nyuma yake. Mtoa Mada anarudia kile kile ambacho wamefanya kwa maaskofu wa KKKT ambacho hata hivyo haiwezi kuondoa ukweli wa nyaraka zote mbili.
 
Siasa siasani. Ukabila kwa watu wa makabila. Mawazo ya ukabila yanaingizwa madhabahuni kwa nguvu ya nyundo.

Hoja Mufilisi kwa watu mufilisi.

Bazazi
 
MTOA POST ANALALAMIKA MAASKOFU WENGI NI WACHAGGA, KWANZA NAFIKIRI KWA NCHI HII KANDA YA KASKAZINI NDIO INA WAKATOLIKI WENGI ZAIDI AMBAPO PIA NDIO KUNA SHULE NYINGI ZA SEMINARY ZINAZOZALISHA MAPADRI. NAFIKIRI AKIFANYA UCHUNGUZI TENA ATAGUNDUA MAPADRI WENGI NI WACHAGGA SASA SIJUI NA HAPO TENA ATASEMA SHULENI WACHAGA WALIPENDELEWA? NA KAMA MAPADRI WENGI WANATOKEA KASKAZINI NI LAZIMA NA MAASKOFU ITAKUA HIVYO SABABU LAZIMA USOME UPITIE NGAZI YA UPADRI NDIPO UWE ASKOFU.
IKIWA NI KUTAKA KILA MKOA ASKOFU ATOKE MKOA HUSIKA MWISHO WA SIKU WAISLAMU NAO WATALALAMIKA MBONA MASHEKHE WA KILIMAJARO SIO WACHAGGA? HAYA MAMBO YA IMANI NI VIZURI TUKAACHANA NAYO.
 
Binafsi naamini maaskofu wa katoliki walikuja kukubaliana na Galileo miaka zaidi ya 300 baadae kuwa dunia inazunguka jua waliamua makusudi kuwa side na team wasaliti na wapotoshaji wa ukweli dhahiri.

Mpaka leo sio suala la nadharia bali ni ukweli bayana unaothibitika kwa macho na kwa akili, kwamba JUA LINAIZUNGUKA DUNIA NA KAMWE DUNIA HAIZUNGUKI!
Hivyo Maaskofu wa Mwanzo waliomtaka Mpotoshaji Galileo atengue kauli bado ukweli wao unadumu kwa yeyote mwenye macho na akili timamu.

Ila kwa wale ambao ubongo wao umefungwa na Galilee KAMWE MACHO YAO HAYAONI JUA LIKITEMBEA BALI HUONA KINYUME 'KITU AMBACHO HAWAONI NDICHO HUSEMA WANAONA' !!
 
Nakuunga mkono kwa asilimia kubwa. Naamini mleta mada anatokea Mkoa wa Rukwa na tatizo lake ni kutoona mfipa mwenzake akipewa daraja la Uaskofu. Labda nimuulize; Ni Padri gani Mfipa alistahili kuwa Askofu?

Sina uhakika kama yupo lakini sina uhakika kama hayupo. Lakini dhana kwamba wanaofaa wanatoka huko unakodhani wanastahili kutokea, basi kuna tatizo lingine linakuja hapo. Hao wa Kilimanjaro wanasomea wapi ambako hao wa Sumbawanga hawakuweza kwenda kusoma, au hawana akili ya kumudu masomo?
 
Daah, hapa ni mababa tu! Vyeo nuksi, tangu enzi za Yesu mwenyewe! Tunasoma, mama wale mitume akataka wanaye tena wawili mmoja akae mkono wa kuume na mwingine mkono wa kushoto! Halafu mnasema mfute Jamii Forum!
 
Ajira: hata enzi za jk mrisho watu walilalama kuwa kuna upendeleo wa kidini katika nafasi nyeti za serikali Leo tena ni hayo yanaendelea.Vip naomba ututhibitishie kwa namna gani au unataka kiligawa taifa?
 
Mtoa mada unasikitisha sana.

Ni wazi kwamba unataka kuaminisha watu kwamba maaskofu Wakatoliki waliotoa barua ya kuonyesha mambo ya hovyo katika nchi hii wamefanya hivyo kwa sababu ni Wachaga. Halafu ukasema ni maaskofu watano tu walioandika huo waraka na wote ni Wachaga isipokuwa mmoja.

Nasema tena, wewe mtoa mada unasikitisha sana, tena sana !.

1. Maaskofu wa Kikatoliki hawateuani wao wenyewe, wanateuliwa na Pope kule Vatican. Kwa hivyo unachotaka kuwaaminisha watu kwamba maaskofu Wakatoliki ni wengi kwa sababu ni Wachaga waliojiteua ni ujinga, tena linaonyesha wewe una ukabila wa hali ya juu.

2. Ukatoliki ulianzia Kilimanjaro ziadi ya miaka 120 iliyopita. Kwa hivyo, lazima utegemee idadi ya mapadri Wakatoliki ambao ndio wanateuliwa kuwa maaskofu ni wengi kuliko sehemu nyingine yoyote Tanzania. Kwa maneno mengine, wingi wa maaskofu Wakatoliki ambao ni Wachaga unatokana na wingi wa mapadri Wachaga.

3. Umesema kwamba ni maaskofu wachache tu walioandika ule waraka. Kama unathubutu kusema jambo kama hilo unajionyesha wazi kwamba hata namna yako ya kufikiri ina kasoro. Unajua wazi kwamba kila askofu aliyetajwa katika ule waraka aliweka sahihi yake kwenye huo waraka. Unataka kutuambia kwamba askofu ambaye ni mtu msomi (wengi wana PhD) atakubali kutia sahihi yake kwenye waraka ambao hakubaliani nao? Unashangaza sana, sana
 
Huyu nadhani haujui ukatoliki anadhani ni kama siasa za bongo ,pole sana. Kwanza tambua mifumo yote ya kiutawala duniania inafuata katoliki,kalenda ya kikatoliki,this church is smart shule nyingi tz za katoliki hospitali pia, roma ina papa ambaye ndio raisi wa pale roma ina system nzuri ya kuteua mkuu haina uchaga
 
Kijana was Lumumba Leo hulipwi maana umeleta mada ya hovyo sana
 
Nachojua Askofu wa Katoliki hachaguliwi na waumini kama makanisa mengine.

Askofu wa Kanisa Katoliki anateuliwa na Papa kule Vatican lkn nashangaa Papa Benedict na Papa Francis ni wakabila sana maana wamewateua Wachaga wengi kuwa Maaskofu Tanzania.

Vv
 
Back
Top Bottom