Daudi Shoka
New Member
- May 13, 2018
- 1
- 5
Waraka kwa Maaskofu -Wakatoliki
Wapendwa Maaskofu, miezi michache iliyopita kuliotokea hali ya kutofautiana kati ya viongozi wa kanisa Katoliki na serikali; vile vile kati yenu ninyi viongozi wa kanisa wenyewe kwa wenyewe kutokana na chapisho la Waraka ujulikanao kwa jina la “ujumbe wa Kwaresma” utolewao na kanisa Katoliki nchini Tanzania kila mwaka. Waraka huo wa mwaka huu ulikuwa na ujumbe uliikosoa serikali hasa katika suala ya kuminya demokrasia. Hali kadhalika kwa upande mwingine baadhi ya viongozi wa Kanisa kama Kardinali Pengo alitofautiana na maaskofu wenzake kwa kile alichosema kuwa waraka ulichanganya siasa na dini.
Wapendwa Maaskofu, ni jambo lilodhahiri kuwa ujumbe wenu kupitia waraka ule ulikuwa sehemu ya utume wenu wa kinabii. Kwa mujibu wa utume huo mnapaswa kukemea pale inapobidi na ndivyo ilivyokuwa kwa nyakati mbalimbali. Mifano ipo mingi ambapo viongozi wa Kanisa na baadhi ya waamini wa kawaida wakikemea maovu hata yaliyotendwa na viongozi wa dola ndiyo maana watu kama kina Thomas More waliuawa kule Uingereza katika karne ya 16. Baadaye Thomas More alitangazwa na kanisa kuwa Mtakatifu kwa msimamo wake wa kusimamia ukweli aliouamini na uliokuwa katika misingi ya Injli. Lakini jambo la kukumbuka ni kuwa viongozi wa Kanisa wanaotaka kukemea wengine wanatakiwa wawe na mamlaka ya kimaadili (moral authority), ili waweze kutekeleza jukumu hilo.
Wapendwa Maaskofu, mtakumbuka kuwa katika mitandao ya kijamii, moja ya mambo ambayo serikali ya awamu ya tano inalaumiwa na watu wengi ni pamoja kuwa na upendeleo katika ajira, hasa nafasi nyeti serikalini kwenda kwa watu wa kanda ya Ziwa. Sina uhakika na jambo hili kwa sasa, lakini kama lipo lisiendelee kuwepo na kama halipo lisije likafanyika kabisa. Athari ya ubaguzi na upendeleo litaligawa taifa na kuleta madhara makubwa sana. Ubaguzi unaweza kuanza kwa kuangaliana kwa kanda, baadaye kabila, koo na kadhalika. Ukweli ni kuwa hakuna mwisho mzuri wa jambo kama hilo. Nimesema kama kweli upo upendeleo wa kikanda, kama taifa tunapaswa kulitafutia suluhisho kabla hatujapata madhara. Je, katika hili Kanisa letu/lenu lipo salama?
Wapendwa Maaskofu, ili kupata suluhisho la tatizo la upendeleo na ubaguzi ni jukumu lenu viongozi wa Kanisa kushiriki na ninyi mnao wajibu huo ambao mnapaswa kuutekeleza kwa umakini mkubwa sana. Pamoja na kuwatwisha ninyi viongozi jukumu hilo nina mashaka kama mtalimudu jambo hilo. Mashaka yangu yanatokana na ukweli kuwa viongozi wangu mnanaanza kukosa mamlaka ya kimaadili. Historia ya Kanisa Katoliki inatukumbusha kuwa huko nyuma pamoja na kufanya mambo mazuri lakini kuna nyakati kanisa lilifanya makosa makubwa sana. Mwaka 1663 viongozi wa Kanisa Katoliki walimweka kiti moto mwanasayansi aitwaye Galileo Galilei akanushe nadharia yake kwamba dunia inaizunguka jua. Mwanasayansi huyo alitii maagizo ya viongozi wake akaikana nadharia yake ingawaje wakati anatoka mlangoni alisema kuwa hata hivyo dunia ndiyo inayozunguka jua. Ni baada ya miaka 359, yaani mwaka 1992 kanisa liliomba msamaha na kukiri kuwa lilikosea kwa kungángánia kuwa jua linaizunguka dunia badala ya dunia kuizunguka jua.
Wapendwa Maaskofu, kuna mambo mengine mengi ndani ya Kanisa yenye ushahidi unaoonesha kuwa pale ambapo viongozi nao wameshiriki katika maovu, ama kwa kukaa kimya au kushirki kimatendo, viongozi wamepata ugumu katika kukemea maovu katika jamii. Kwa kuchukua mifano michache tu ya hivi karibuni, mwaka 1994 wakati yanatokea mauaji ya kimbali kule Rwanda, baadhi ya watu waliuawa wakiwa wamejihifadhi kanisani. Je, viongozi wa Kanisa hawakuwa na mchango katika kufanikisha mauaji? Je, viongozi walikuwa wapi kushindwa kukemea hilo? Kule Nigeria mwaka 2012 aliteuliwa Padre Peter Okpaleke, kuwa Askofu wa Jimbo Katoliki la Ahiara lakini waamini na mapadre wa jimbo hilo walimkataa askofu mteule. Moja ya malalamiko ya waamini wa jimbo hilo ambalo linasemakana kuwa na mapdre zaidi ya 500, ni kuwa anakosekanaje padre mmoja anayefaa kuwa askofu miongoni mwa mapadre 500? Hata hivyo kulikuwa na hisia kuwa kuna upendeleo uliokuwa nyuma ya uteuzi ule, hasa shutuma nyingi zikielekezwa kwa Cardinal Arinze ambako anatoka katika eneo moja na Askofu Peter Okpaleke. Hatimaye huyo askofu alijiuzulu mwaka 2018 baada ya kukataliwa na kutambua mwenyewe kuwa mazingira ya kazi huenda yangekuwa magumu.
Wapendwa Maaskofu, kama shutuma za baadhi ya Watanzania wanaokinyooshea kidole serikali ya awamu tano kwamba inafanya upendeleo na ubaguzi kwa kutoa ajira nyeti kwa watu wa kanda ya ziwa ni kweli, je, maaskofu wetu mna uwezo wa kulitolea waraka jambo hilo? Nina mashaka kama mtaweza kwani wakati waraka wenu ulipoanza kujadiliwa maaskofu mlishutumiwa kuwa mlibeba ajenda ya upinzani hususani Chadema. Na kwa mbali ukitazama shutuma dhidi yenu ilikuwa kwamba ajenda mliyoibeba ilikuwa ya Kanda ya Kaskazini (hasa Kilimanjaro) kwani maaskofu waliotajwa kuwa waandaaji wa waraka wengi wanu mlikuwa na asili ya mkoa Kilimanjaro. Waliotajwa kuandaa waraka ni Askofu Mkuu wa Dodoma – Beatus Kinyaiya (mchaga), Askofu Mkuu wa Mwanza – Thaddeus Ruwaichi (mchaga) na Askofu wa Zanzibar – Augustino Shao (mchaga) na mmoja tu ambaye si mchaga katika kundi hilo la walioandaa waraka ni Askofu Severine Niwemugizi – wa Rulenge Ngara. Kwa kuangalia orodha hiyo utagundua kuwa, wakati wa kupinga ukanda na ukabila ninyi viongozi wetu hamtaweza kutuokoa. Hata ukiangalia orodha yenu katika baraza la maaskofu wa Tanzania utaona kuwa karibu moja ya tatu () ya maaskofu wote Tanzania wana asili ya Kilimanajaro. Tazama orodha ifuatayo yenye Maaskofu Wachaga: (i) Askofu mkuu Thaddeus Ruwaich Mwanza (ii) Askofu mkuu Beatus Kinyaiya –Dodoma (iii) Askofu mkuu Isack Masawe – Arusha (iv) Askofu Augustine Shao - Zanzibar (v) Askofu Ludovick Minde – Kahama (vi) Askofu Rogath Kimario - Same (vii) Askofu Joseph Mlola - Kigoma (viii) Askofu Msaidizi (Arusha) - Prosper Lyimo (ix) Askofu mteule Beatus Urassa – Sumbawanga (x) Msimamizi wa Jimbo Padre Deogratias Matika (Askofu mtarajiwa wa Jimbo la Moshi). Hali kadhalika katika mashirika ya kitawa yanayofanya kazi Tanzania viongozi wao wengi ni watu wenye asili ya Kilimanjaro. Mfano mashrika ya (i) Precious Blood (ii) Holy Ghost, (iii) OSS/ ALCP (iv) Mitume wa Yesu (v) Capuchin (vi) Jesuit nk.
Wapendwa Maaskofu, wengi wenu katika miaka ya 1960 hadi 1970 mlikuwa mnateuliwa katika maeneo yenu kama Sumbawanga, Mbulu, Kigoma, Mwanza, Shinyinga, Tabora nakadhalika. Inakuwaje wakati huo uinjilishaji ukiwa bado siyo wa kina waliweza kupatikana maaskofu katika maeneo yao, lakini leo Askofu anatokea Moshi anaenda Kigoma, Mwanza, Kahama, Sumbawanga? Lakini kinyume chake hakuna anayetoka Kigoma kuelekea Moshi. Hata Yesu alipoanzisha Kanisa aliwateua mitume wake pale Uyahudi siyo Moshi, ndipo baadaye kila mahali Injili ilipofika walipatikana Mitume katika maeneo yao. Ili kuwapotosha na kuwalaghai watu, mtaniambia kuwa karibu majimbo yote Tanzania yana maaskofu wanaotoka maeneo tofauti na maeneo yao ya asili. Umoja wa Kanisa tangu mwanzo ulikuwa katika imani na si katika hili la hadaa na ulaghai wa uteuzi wa maaskofu kutoka Kilimanjaro. Kama mnateua maaskofu kutoka Kilimanjaro kwenda Sumbawanga, kuna sababu gani kwenu ninyi kuwakataa Wahindi na Wazungu wanaofanya kazi za Kimisiaonari hapa Tanzania kuwa maaskofu kama ninyi? Dhambi ya ubaguzi na upendeleo haitawaacha salama. Mkiukataa uweli wangu leo, watakuja watakaogundua hata baada ya miaka 359 kama wenzenu walivyoukubali ukweli kuwa dunia ndiyo inayozunguka jua na siyo kinyume chake. Ni afadhali mkaziba ufa kuliko kujenga ukuta, na majuto ni mjukuu. Mwenye masikio ya kusikia na asikie na mwenye macho ya kuona aone. Mkaiishi Injili kama mlivyoipokea na kuihubiri na siyo vinginevyo.
Wapendwa maaskofu, maangamizo ya umoja wa kitaifa yatakuja kama tutayapuuzia mambo ambayo yanaonekana lakini tunajifanya hatuyaoni. Siku hiyo ya kuangamia kwa taifa kutakuja bila kubagua na ninyi ndio mtakaoulizwa kuwa mlinya nini katika kuzuia hili? Mimi nimenawa mikono kwa sababu nimewaambia. Msishawishike kuwa wajibu wenu unaishia katika kutoa Kipaimara na Upadre. Katika hili tunataka mshiriki kukemea ubaguzi na ukanda mkianzia kwenu wenyewe ili kuliepusha taifa letu kupata madhara yatakayofikia hata walio kondoo wenu na hata wasio kondoo wenu.
Wapendwa maaskofu, bila shaka wengi mtasema maaskofu wa Kanisa katoliki wanapatikana kwa utaratibu maalum na kwamba haya ninawaambia hayawahusu na pia kwamba waraka wangu huu unapandikiza ukabila. Waraka wangu hauleti ukabila bali unawaambia kuwa ukabila mmeupanda na sasa umeota, ila kataeni kuupalilia ili usije ukaiva. Nawaambia kuwa mtaukata ukweli na mtaniambia niukane ukweli wangu, lakini nawaambia ipo siku mtakubaliana na mimi kama ambavyo mlikubaliana na Galileo na mkaukubali ukweli wake baada ya miaka 359. Mimi siyo nabii lakini baada ya miaka kadhaa mtaamini kuwa Wanyarwanda hawakuanza chuki mwaka 1994, bali wapo waliopandikiza chuki, kuipalilia na kuiivisha na wakavuna matunda yake mwaka 1994 huku viongozi wa kanisa wakiwa wameshiriki katika hayo. Vivyo hivyo Kanisa Katoliki lina historia yake nzuri na chafu vile vile, mkubali tu mmefanya makosa na mnaendelea kuyafanya, basi tubuni na mrejee katika misingi ya haki na ukweli; na ukweli utawaweka huru. Kama taifa litafika mahali pabaya isiwe kwa mchango wenu, mnawe mikono yenu kama alivyofanya Pilato wakati wa kuuawa kwa Yesu.
Waraka wenu tuliupokea nanyi muupokee wa kwangu.
MZALENDO,
MPENDA TANZANIA
Wapendwa Maaskofu, miezi michache iliyopita kuliotokea hali ya kutofautiana kati ya viongozi wa kanisa Katoliki na serikali; vile vile kati yenu ninyi viongozi wa kanisa wenyewe kwa wenyewe kutokana na chapisho la Waraka ujulikanao kwa jina la “ujumbe wa Kwaresma” utolewao na kanisa Katoliki nchini Tanzania kila mwaka. Waraka huo wa mwaka huu ulikuwa na ujumbe uliikosoa serikali hasa katika suala ya kuminya demokrasia. Hali kadhalika kwa upande mwingine baadhi ya viongozi wa Kanisa kama Kardinali Pengo alitofautiana na maaskofu wenzake kwa kile alichosema kuwa waraka ulichanganya siasa na dini.
Wapendwa Maaskofu, ni jambo lilodhahiri kuwa ujumbe wenu kupitia waraka ule ulikuwa sehemu ya utume wenu wa kinabii. Kwa mujibu wa utume huo mnapaswa kukemea pale inapobidi na ndivyo ilivyokuwa kwa nyakati mbalimbali. Mifano ipo mingi ambapo viongozi wa Kanisa na baadhi ya waamini wa kawaida wakikemea maovu hata yaliyotendwa na viongozi wa dola ndiyo maana watu kama kina Thomas More waliuawa kule Uingereza katika karne ya 16. Baadaye Thomas More alitangazwa na kanisa kuwa Mtakatifu kwa msimamo wake wa kusimamia ukweli aliouamini na uliokuwa katika misingi ya Injli. Lakini jambo la kukumbuka ni kuwa viongozi wa Kanisa wanaotaka kukemea wengine wanatakiwa wawe na mamlaka ya kimaadili (moral authority), ili waweze kutekeleza jukumu hilo.
Wapendwa Maaskofu, mtakumbuka kuwa katika mitandao ya kijamii, moja ya mambo ambayo serikali ya awamu ya tano inalaumiwa na watu wengi ni pamoja kuwa na upendeleo katika ajira, hasa nafasi nyeti serikalini kwenda kwa watu wa kanda ya Ziwa. Sina uhakika na jambo hili kwa sasa, lakini kama lipo lisiendelee kuwepo na kama halipo lisije likafanyika kabisa. Athari ya ubaguzi na upendeleo litaligawa taifa na kuleta madhara makubwa sana. Ubaguzi unaweza kuanza kwa kuangaliana kwa kanda, baadaye kabila, koo na kadhalika. Ukweli ni kuwa hakuna mwisho mzuri wa jambo kama hilo. Nimesema kama kweli upo upendeleo wa kikanda, kama taifa tunapaswa kulitafutia suluhisho kabla hatujapata madhara. Je, katika hili Kanisa letu/lenu lipo salama?
Wapendwa Maaskofu, ili kupata suluhisho la tatizo la upendeleo na ubaguzi ni jukumu lenu viongozi wa Kanisa kushiriki na ninyi mnao wajibu huo ambao mnapaswa kuutekeleza kwa umakini mkubwa sana. Pamoja na kuwatwisha ninyi viongozi jukumu hilo nina mashaka kama mtalimudu jambo hilo. Mashaka yangu yanatokana na ukweli kuwa viongozi wangu mnanaanza kukosa mamlaka ya kimaadili. Historia ya Kanisa Katoliki inatukumbusha kuwa huko nyuma pamoja na kufanya mambo mazuri lakini kuna nyakati kanisa lilifanya makosa makubwa sana. Mwaka 1663 viongozi wa Kanisa Katoliki walimweka kiti moto mwanasayansi aitwaye Galileo Galilei akanushe nadharia yake kwamba dunia inaizunguka jua. Mwanasayansi huyo alitii maagizo ya viongozi wake akaikana nadharia yake ingawaje wakati anatoka mlangoni alisema kuwa hata hivyo dunia ndiyo inayozunguka jua. Ni baada ya miaka 359, yaani mwaka 1992 kanisa liliomba msamaha na kukiri kuwa lilikosea kwa kungángánia kuwa jua linaizunguka dunia badala ya dunia kuizunguka jua.
Wapendwa Maaskofu, kuna mambo mengine mengi ndani ya Kanisa yenye ushahidi unaoonesha kuwa pale ambapo viongozi nao wameshiriki katika maovu, ama kwa kukaa kimya au kushirki kimatendo, viongozi wamepata ugumu katika kukemea maovu katika jamii. Kwa kuchukua mifano michache tu ya hivi karibuni, mwaka 1994 wakati yanatokea mauaji ya kimbali kule Rwanda, baadhi ya watu waliuawa wakiwa wamejihifadhi kanisani. Je, viongozi wa Kanisa hawakuwa na mchango katika kufanikisha mauaji? Je, viongozi walikuwa wapi kushindwa kukemea hilo? Kule Nigeria mwaka 2012 aliteuliwa Padre Peter Okpaleke, kuwa Askofu wa Jimbo Katoliki la Ahiara lakini waamini na mapadre wa jimbo hilo walimkataa askofu mteule. Moja ya malalamiko ya waamini wa jimbo hilo ambalo linasemakana kuwa na mapdre zaidi ya 500, ni kuwa anakosekanaje padre mmoja anayefaa kuwa askofu miongoni mwa mapadre 500? Hata hivyo kulikuwa na hisia kuwa kuna upendeleo uliokuwa nyuma ya uteuzi ule, hasa shutuma nyingi zikielekezwa kwa Cardinal Arinze ambako anatoka katika eneo moja na Askofu Peter Okpaleke. Hatimaye huyo askofu alijiuzulu mwaka 2018 baada ya kukataliwa na kutambua mwenyewe kuwa mazingira ya kazi huenda yangekuwa magumu.
Wapendwa Maaskofu, kama shutuma za baadhi ya Watanzania wanaokinyooshea kidole serikali ya awamu tano kwamba inafanya upendeleo na ubaguzi kwa kutoa ajira nyeti kwa watu wa kanda ya ziwa ni kweli, je, maaskofu wetu mna uwezo wa kulitolea waraka jambo hilo? Nina mashaka kama mtaweza kwani wakati waraka wenu ulipoanza kujadiliwa maaskofu mlishutumiwa kuwa mlibeba ajenda ya upinzani hususani Chadema. Na kwa mbali ukitazama shutuma dhidi yenu ilikuwa kwamba ajenda mliyoibeba ilikuwa ya Kanda ya Kaskazini (hasa Kilimanjaro) kwani maaskofu waliotajwa kuwa waandaaji wa waraka wengi wanu mlikuwa na asili ya mkoa Kilimanjaro. Waliotajwa kuandaa waraka ni Askofu Mkuu wa Dodoma – Beatus Kinyaiya (mchaga), Askofu Mkuu wa Mwanza – Thaddeus Ruwaichi (mchaga) na Askofu wa Zanzibar – Augustino Shao (mchaga) na mmoja tu ambaye si mchaga katika kundi hilo la walioandaa waraka ni Askofu Severine Niwemugizi – wa Rulenge Ngara. Kwa kuangalia orodha hiyo utagundua kuwa, wakati wa kupinga ukanda na ukabila ninyi viongozi wetu hamtaweza kutuokoa. Hata ukiangalia orodha yenu katika baraza la maaskofu wa Tanzania utaona kuwa karibu moja ya tatu () ya maaskofu wote Tanzania wana asili ya Kilimanajaro. Tazama orodha ifuatayo yenye Maaskofu Wachaga: (i) Askofu mkuu Thaddeus Ruwaich Mwanza (ii) Askofu mkuu Beatus Kinyaiya –Dodoma (iii) Askofu mkuu Isack Masawe – Arusha (iv) Askofu Augustine Shao - Zanzibar (v) Askofu Ludovick Minde – Kahama (vi) Askofu Rogath Kimario - Same (vii) Askofu Joseph Mlola - Kigoma (viii) Askofu Msaidizi (Arusha) - Prosper Lyimo (ix) Askofu mteule Beatus Urassa – Sumbawanga (x) Msimamizi wa Jimbo Padre Deogratias Matika (Askofu mtarajiwa wa Jimbo la Moshi). Hali kadhalika katika mashirika ya kitawa yanayofanya kazi Tanzania viongozi wao wengi ni watu wenye asili ya Kilimanjaro. Mfano mashrika ya (i) Precious Blood (ii) Holy Ghost, (iii) OSS/ ALCP (iv) Mitume wa Yesu (v) Capuchin (vi) Jesuit nk.
Wapendwa Maaskofu, wengi wenu katika miaka ya 1960 hadi 1970 mlikuwa mnateuliwa katika maeneo yenu kama Sumbawanga, Mbulu, Kigoma, Mwanza, Shinyinga, Tabora nakadhalika. Inakuwaje wakati huo uinjilishaji ukiwa bado siyo wa kina waliweza kupatikana maaskofu katika maeneo yao, lakini leo Askofu anatokea Moshi anaenda Kigoma, Mwanza, Kahama, Sumbawanga? Lakini kinyume chake hakuna anayetoka Kigoma kuelekea Moshi. Hata Yesu alipoanzisha Kanisa aliwateua mitume wake pale Uyahudi siyo Moshi, ndipo baadaye kila mahali Injili ilipofika walipatikana Mitume katika maeneo yao. Ili kuwapotosha na kuwalaghai watu, mtaniambia kuwa karibu majimbo yote Tanzania yana maaskofu wanaotoka maeneo tofauti na maeneo yao ya asili. Umoja wa Kanisa tangu mwanzo ulikuwa katika imani na si katika hili la hadaa na ulaghai wa uteuzi wa maaskofu kutoka Kilimanjaro. Kama mnateua maaskofu kutoka Kilimanjaro kwenda Sumbawanga, kuna sababu gani kwenu ninyi kuwakataa Wahindi na Wazungu wanaofanya kazi za Kimisiaonari hapa Tanzania kuwa maaskofu kama ninyi? Dhambi ya ubaguzi na upendeleo haitawaacha salama. Mkiukataa uweli wangu leo, watakuja watakaogundua hata baada ya miaka 359 kama wenzenu walivyoukubali ukweli kuwa dunia ndiyo inayozunguka jua na siyo kinyume chake. Ni afadhali mkaziba ufa kuliko kujenga ukuta, na majuto ni mjukuu. Mwenye masikio ya kusikia na asikie na mwenye macho ya kuona aone. Mkaiishi Injili kama mlivyoipokea na kuihubiri na siyo vinginevyo.
Wapendwa maaskofu, maangamizo ya umoja wa kitaifa yatakuja kama tutayapuuzia mambo ambayo yanaonekana lakini tunajifanya hatuyaoni. Siku hiyo ya kuangamia kwa taifa kutakuja bila kubagua na ninyi ndio mtakaoulizwa kuwa mlinya nini katika kuzuia hili? Mimi nimenawa mikono kwa sababu nimewaambia. Msishawishike kuwa wajibu wenu unaishia katika kutoa Kipaimara na Upadre. Katika hili tunataka mshiriki kukemea ubaguzi na ukanda mkianzia kwenu wenyewe ili kuliepusha taifa letu kupata madhara yatakayofikia hata walio kondoo wenu na hata wasio kondoo wenu.
Wapendwa maaskofu, bila shaka wengi mtasema maaskofu wa Kanisa katoliki wanapatikana kwa utaratibu maalum na kwamba haya ninawaambia hayawahusu na pia kwamba waraka wangu huu unapandikiza ukabila. Waraka wangu hauleti ukabila bali unawaambia kuwa ukabila mmeupanda na sasa umeota, ila kataeni kuupalilia ili usije ukaiva. Nawaambia kuwa mtaukata ukweli na mtaniambia niukane ukweli wangu, lakini nawaambia ipo siku mtakubaliana na mimi kama ambavyo mlikubaliana na Galileo na mkaukubali ukweli wake baada ya miaka 359. Mimi siyo nabii lakini baada ya miaka kadhaa mtaamini kuwa Wanyarwanda hawakuanza chuki mwaka 1994, bali wapo waliopandikiza chuki, kuipalilia na kuiivisha na wakavuna matunda yake mwaka 1994 huku viongozi wa kanisa wakiwa wameshiriki katika hayo. Vivyo hivyo Kanisa Katoliki lina historia yake nzuri na chafu vile vile, mkubali tu mmefanya makosa na mnaendelea kuyafanya, basi tubuni na mrejee katika misingi ya haki na ukweli; na ukweli utawaweka huru. Kama taifa litafika mahali pabaya isiwe kwa mchango wenu, mnawe mikono yenu kama alivyofanya Pilato wakati wa kuuawa kwa Yesu.
Waraka wenu tuliupokea nanyi muupokee wa kwangu.
MZALENDO,
MPENDA TANZANIA