Wapinzani wamefikia malengo yao

Wapinzani wamefikia malengo yao

Mbowe anaandaa Maandamano ya kumpongeza JK, yanaanzia Arusha, na kuishia Mbeya, ila Moshi hayapiti!

Hivi unajua tafsiri ya neno MSALANI ni chooni? Basi nakupongeza kwa hoja zinazofanana na jina lako.
 
Tangu kadhia ya kupitishwa 'kimagumashi' na 'kuchomekwa' kwa vifungu katika Muswada wa Mabadiliko ya Sheria ya Katiba Bungeni Dodoma,wapinzani hawakulala.Hawakushindwa. Waliendelea kupigania ustawi wa nchi kupitia Katiba mpya bora nje ya Bunge.Wakaitisha mikutano miwili mikubwa: Jangwani na Kibanda Maiti. Wakaungwa mkono. Wakasikika.

Wapinzani walilenga mambo makubwa mawili. Kwanza, kumtaka Rais awe makini katika mchakato huu wa Katiba mpya kwakuwa unabeba mustakabali wa Taifa. Hapa, wakamuomba Rais asisaini Muswada husika.Pia, walitaka kusikilizwa na Rais katika kuwasilisha hoja zao. Walitaka majadiliano na maridhiano ya kitaifa na Rais. Lengo hili limefanikiwa.Mosi, taarifa rasmi za Ikulu zinaonesha kuwa Rais hakusaini Muswada husika. Pili,wapinzani jana wamekutana na Rais Ikulu kusikilizana na kuelewana. Lengo limetimia.

Pia, wapinzani walilenga kurejeshwa Bungeni kwa Muswada huo ili uweze kujadiliwa tena kwa maboresho yalengayo afya ya Taifa.Tayari,Rais 'ameshaamuru' Muswada urejeshwe Bungeni kwa marejesho.Waweza kurejeshwa ukiwa umeshasainiwa au la. Haijalishi. Lengo la pili limetimia pia.

Ingawa wapinzani walibezwa sana hasa na Waandamizi wa CCM yetu, muda si muda mantiki yao itaonekana kwa wengi au wote. Kupigania Katiba bora ni kupigania Taifa bora. Katiba ndiyo msingi wetu wa kwanza. Vingine vyote vinaifuata Katiba. Vingine vyote ndiyo.

Hongereni sana wapinzani: Mbowe,Lipumba na Mbatia na vyama vyenu kwa kufanikiwa hata kwa haya. CCM yetu ijifunze kuendana na wakati na mabadiliko yake.Watanzania si wale jamani,wamebadilika sana.Tusije tukabadilishwa kwa kura!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

Hii kitu Iko wazi kabisa na hii inafaa kua somo kwa wanacm.
Kitendo cha Mh Rais na Hawa viongozi wa vyama kukutana na kuweka mambo sawa ni jambo zuri sana!
Kwa Mtz yeyote Yule Hapa ataona umoja wa kitaifa ulioonyeshwa na Mh Rais na Hawa viongozi!
Na nitumaini langu huo mswaada ukirudishwa bungeni kutakua hakuna vurugu Na kejeli Kama zilizotokea! Ingawa kwa wapinzani wao wametimiza malengo Yao na Ccm wajifunze kua na busara Kama za Rais wetu!
Hongera sana Mh Rais JK kwa busara zako japo najua wafuasi wa Chama chako baadhi hawatapendezwa na haya maamuzi uliyochukua lakini Mimi Kama Mtz wa kawaida nakupongeza sana kwa hili!
Na Pia pongezi sana kwa hawa viongozi wa vyama vya siasa kwa busara na hekima ya kuweza kuchagua njia ya kujadiliana kwanza kwa ajili ya kupata suluhu ya mustakabili wa katiba!
Mungu Ibariki Tanzania
 
Kamalengo la wapinzani lilikuwa ni kupata audience na Rais, basi wametimiza lengo hilo...
ZeMarcopolo mbona macho yako hayaoni kila jambo jema likitokea? Mheshiwa Raisi alijua kuwa mikutano kama ule wa Jangwani na ule wa Kibandamaiti ungeliendelea nchi nzima mwisho wake usingekuwa mzuri kwa umoja wa kitaifa. Akatumia nguvu ya hekima kukutana na wapinnzani na kutafuta nao muafaka! Ametafuta muafaka na wabunge pia kwa kusaini mswada, lakini kuna njia ya kuurekebisha hata kama umesainiwa. Pongezi zimwendee Raisi na Viongozi wa vyama vya upinzani kwa kusilizana na tunaamini mswada utafanyiwa marekebisho sawasawa na makubaliano yao. Lengo la wapinzani limetimia halikadhalika lengo la Raisi limetimia. Malengo ya wale wengine waliobwatuka... ah! tumeshawasamehe! Tusonge mbele!
 
ZeMarcopolo mbona macho yako hayaoni kila jambo jema likitokea? Mheshiwa Raisi alijua kuwa mikutano kama ule wa Jangwani na ule wa Kibandamaiti ungeliendelea nchi nzima mwisho wake usingekuwa mzuri kwa umoja wa kitaifa. Akatumia nguvu ya hekima kukutana na wapinnzani na kutafuta nao muafaka! Ametafuta muafaka na wabunge pia kwa kusaini mswada, lakini kuna njia ya kuurekebisha hata kama umesainiwa. Pongezi zimwendee Raisi na Viongozi wa vyama vya upinzani kwa kusilizana na tunaamini mswada utafanyiwa marekebisho sawasawa na makubaliano yao. Lengo la wapinzani limetimia halikadhalika lengo la Raisi limetimia. Malengo ya wale wengine waliobwatuka... ah! tumeshawasamehe! Tusonge mbele!

Safi sana Mkuu!
Tusonge mbele Mkuu na bungeni watakua hawana nguvu Maana Hawa wabunge wachache wameonekana kua na hekima!
 
Kwa hiyo unataka niamini kuwa rais amekubali kuwa atapelekewa jina moja tu na kila taasisi aliidhinishe. Sio majina tisa achague moja kama hapo awali.

Taasisi yetu inampendekeza bwana Nassoro Moyo.
 
Lazima tuwapongeze wapinzani hawa, hebu fikiri kama wangenyamaza kimya,mambo mangapi yangepitishwa kiholela?
 
Tangu kadhia ya kupitishwa 'kimagumashi' na 'kuchomekwa' kwa vifungu katika Muswada wa Mabadiliko ya Sheria ya Katiba Bungeni Dodoma,wapinzani hawakulala.Hawakushindwa. Waliendelea kupigania ustawi wa nchi kupitia Katiba mpya bora nje ya Bunge.Wakaitisha mikutano miwili mikubwa: Jangwani na Kibanda Maiti. Wakaungwa mkono. Wakasikika.

Wapinzani walilenga mambo makubwa mawili. Kwanza, kumtaka Rais awe makini katika mchakato huu wa Katiba mpya kwakuwa unabeba mustakabali wa Taifa. Hapa, wakamuomba Rais asisaini Muswada husika.Pia, walitaka kusikilizwa na Rais katika kuwasilisha hoja zao. Walitaka majadiliano na maridhiano ya kitaifa na Rais. Lengo hili limefanikiwa.Mosi, taarifa rasmi za Ikulu zinaonesha kuwa Rais hakusaini Muswada husika. Pili,wapinzani jana wamekutana na Rais Ikulu kusikilizana na kuelewana. Lengo limetimia.

Pia, wapinzani walilenga kurejeshwa Bungeni kwa Muswada huo ili uweze kujadiliwa tena kwa maboresho yalengayo afya ya Taifa.Tayari,Rais 'ameshaamuru' Muswada urejeshwe Bungeni kwa marejesho.Waweza kurejeshwa ukiwa umeshasainiwa au la. Haijalishi. Lengo la pili limetimia pia.

Ingawa wapinzani walibezwa sana hasa na Waandamizi wa CCM yetu, muda si muda mantiki yao itaonekana kwa wengi au wote. Kupigania Katiba bora ni kupigania Taifa bora. Katiba ndiyo msingi wetu wa kwanza. Vingine vyote vinaifuata Katiba. Vingine vyote ndiyo.

Hongereni sana wapinzani: Mbowe,Lipumba na Mbatia na vyama vyenu kwa kufanikiwa hata kwa haya. CCM yetu ijifunze kuendana na wakati na mabadiliko yake.Watanzania si wale jamani,wamebadilika sana.Tusije tukabadilishwa kwa kura!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

Haya kaka uhalisia ni upi kwenye maofisi ya Lumumba ?
 
Lazima tuwapongeze wapinzani hawa, hebu fikiri kama wangenyamaza kimya,mambo mangapi yangepitishwa kiholela?
 
tangu kadhia ya kupitishwa 'kimagumashi' na 'kuchomekwa' kwa vifungu katika muswada wa mabadiliko ya sheria ya katiba bungeni dodoma,wapinzani hawakulala.hawakushindwa. Waliendelea kupigania ustawi wa nchi kupitia katiba mpya bora nje ya bunge.wakaitisha mikutano miwili mikubwa: Jangwani na kibanda maiti. Wakaungwa mkono. Wakasikika.

Wapinzani walilenga mambo makubwa mawili. Kwanza, kumtaka rais awe makini katika mchakato huu wa katiba mpya kwakuwa unabeba mustakabali wa taifa. Hapa, wakamuomba rais asisaini muswada husika.pia, walitaka kusikilizwa na rais katika kuwasilisha hoja zao. Walitaka majadiliano na maridhiano ya kitaifa na rais. Lengo hili limefanikiwa.mosi, taarifa rasmi za ikulu zinaonesha kuwa rais hakusaini muswada husika. Pili,wapinzani jana wamekutana na rais ikulu kusikilizana na kuelewana. Lengo limetimia.

Pia, wapinzani walilenga kurejeshwa bungeni kwa muswada huo ili uweze kujadiliwa tena kwa maboresho yalengayo afya ya taifa.tayari,rais 'ameshaamuru' muswada urejeshwe bungeni kwa marejesho.waweza kurejeshwa ukiwa umeshasainiwa au la. Haijalishi. Lengo la pili limetimia pia.

Ingawa wapinzani walibezwa sana hasa na waandamizi wa ccm yetu, muda si muda mantiki yao itaonekana kwa wengi au wote. Kupigania katiba bora ni kupigania taifa bora. Katiba ndiyo msingi wetu wa kwanza. Vingine vyote vinaifuata katiba. Vingine vyote ndiyo.

Hongereni sana wapinzani: Mbowe,lipumba na mbatia na vyama vyenu kwa kufanikiwa hata kwa haya. Ccm yetu ijifunze kuendana na wakati na mabadiliko yake.watanzania si wale jamani,wamebadilika sana.tusije tukabadilishwa kwa kura!

mzee tupatupa wa lumumba,dar es salaam
jambo la vyama pinzani kukutana na rais si kutimiza ama kufanikisha lengo la vyama vya siasa,hasha!katiba si kwa manufaa ya vama vya siasa bali ni kwa ustawi wa umma kwa asiyefahamu juu ya nchi yake na yule mwenye kufahamu na ajitolee kupigania wengine na hilo ndilo linapiganiwa na watanzania wachahce wenye kujitambua.ccm wao wanaona mambo yabaki kama yalivo na wanadhani itaendelea kuwafaa wao tu kama vile nchi hii mali yao na wamepofushwa na ibilisi na wasione watanzania wanaelekea wapi na wachache wanaendelea kudhirihisha kwamba si kila jambo wengi wape na katika hili ccm wameonyesha mgando wa fikra kwa maamuzi waliyoyafanya ndani ya bunge.nadhani kikwete anajitambua na aona huko tuendako hatakuwa na ccm na atabaki kama yeye na hao wanaopwayuka hatakuwa nao asilani.kikwete umefikiri vema katika kusikiliza hoja za kweli na kuutupa unafiki wa watu wanaokuzunguka.na tukifanikisha marekebisho ya katiba yetu si fahari ya mtu binafsi bali itakuwa ni fahari kwa taifa letu kwa malengo ya umma wa watanzania.
 
Ukitaka kujua akili ya mtu mpe nafasi ya kusema au kutenda hapo ndipo utakapo jua nani ni mtu na nani ni juha
 
Walichopata nini zaidi ya kwenda kumsikilza mkuu na kutoka wakikenua meno. Amewaambia rudini bungeni na si kukimbia kama watoto wa mbuzi, wakawa wanatoa meno na kujiona hamnazo, sasa wewe unafurahia nini wakati hata wewe mwenyewe unajua kuwa wanatakiwa wafanye mambo ya sheria bungeni na si barabarani kufurahisha BAVICHA sorry Red Briged na Blue guard. Wanawapotezea muda kwa ulinacha wenu
 
Wewe huna lolote ni mwendelezo wa ulaghai ule ule ambacho CHADEMA inatumia kulaghai watu.

Unajifanya unafanya kazi ofisi ndogo Makao Makuu ya CCM na kuleta vi-propaganda vya kitoto katika jukwaa la siasa kufurahisha wasomaji wenye akili za kibavicha wakati hufahamu hata ofisi zake zimekaa vipi.

Wewe niwa kupuuzwa tu na hizi propaganda zako za kitoto ambazo haziwezi kukufanya kupata Uongozi Pwani kupitia CHADEMA.

Chama chenye mizizi ya kilaghai hakiwezi kusimama kwenye siasa za ukweli. Endelea na ulaghai wako kama kilivyo chama chako CHADEMA.

Kwahiyo unakiri Mmebakia na Support Pwani tu , ambako Elimu ni DUNI.
 
Kama ndivyo,wewe nawe ni CCJ. Watakupuuza nawe.Umefurahi? Haya endelea na sikukuu na majukumu yako mengine.Hofu yangu hapa ni kubomoa chama chetu badala ya kujenga.Tutafute siku tupambane humu kwenye bandiko.Tutaomba ruhusa ya kutajana na kuanikiana kila kitu.Uko tayari Mkuu? Siku njema Mwenezi!

Naunga mkono wazo lako mzee wa Lumumba. Ngoja tumsikize Mwanawadiwani
 
Back
Top Bottom