Wapinzani wamefikia malengo yao

Wapinzani wamefikia malengo yao

Rais kasema Amechoka kuambiwa na watu wenye nia ovu nimeambiwa nimesikia sasa basi kwa Rais.
 
Wewe huwa sikuelewi kama ni mtu au binadamu make katika watu ambao wanaongea ubwabwa wewe wa kwanza.

umeandika nini hapo? Kijana ludi shule hii kazi yakushinda hapo lumumba na hizo elfu 7 itafika mwisho hivi karibuni tu!!!!
 
Tungekuona una busara kama ungeishambulia hoja yake badala ya kumshambulia yeye binafsi!
Kuishambulia hoja iliyoletwa kilaghai ni kuharalisha ulaghai na kuonekanana pia kama ni mmoja wa walaghai.

Lazima kwanza tuushambulie ulaghai wake ili ujenzi wa hoja uwe na mantiki na siyo hii ya kukaa pembeni na kuanza kuwakejeli wanaJf wanaojibu hoja zake bila kufahamu kama mleta hoja ni mlaghai.
 
Una uhakika Mwenezi na unachokisema? Fanya utafiti kwanza Mkuu. Jenga hoja kulinda heshima yako. Mimi sijawahi kuhama chama kama wewe tangu ujana wangu.Karibu Ofisini tuongee vyema
Kwa mtu mwenye ufahamu hawezi kujenga hoja zinazoletwa kilaghai.

Swala la kujenga hoja iliyoletwa kilaghai ni bootless task.

Jitahidi kupata uzoefu kwenye taaluma yako ili upate ofisi ya kudumu kama mwanasheria.

Misingi ya taaluma yako hairuhusu ulaghai.
 
Kuishambulia hoja iliyoletwa kilaghai ni kuharalisha ulaghai na kuonekanana pia kama ni mmoja wa walaghai.

Lazima kwanza tuushambulie ulaghai wake ili ujenzi wa hoja uwe na mantiki na siyo hii ya kukaa pembeni na kuanza kuwakejeli wanaJf wanaojibu hoja zake bila kufahamu kama mleta hoja ni mlaghai.
Mkuu mimi si mlaghai.Tatizo kubwa lililopo ndani ya CCM yetu ni kuwa mkweli huchukiwa na kuonekana mpinzani. MwanaDiwani,wewe ni kiongozi chamani.Ubadilike.Ujenge hoja za haja.Acha kuropoka. Ukinisababisha niasi CCM,nitaanza na wewe. Jadili hoja. Kuwa M-CCM si kuwa mropokaji na muongo.Nyinyi ndio mnatuharibia chama chetu tawala. Njoo Lumumba, ukinikosa rudi hapa.
 
jana JK kamwambia Lissu,"... yatosha, upo sahahi, nakukubali...."

Kimsingi na kwa ujumla wake Kikwete kama Kikwete ni mtu mzuri sana. Binafsi nammaindi. Kikwete kama rais anadanganywa na washauiri wake na hasa wale wanaodhani ikulu ni mali ya CCM. Imagine ingekuwaje kama angewasikiliza washauri wake waliokuwa wanahofia wapinzani kunywa chai na juisi. Lakini akatumia utu akijua ni suala la taifa na tena hana muda mrefu madarakani akaongea na wananchi wenzake. Hongera rais na Kikwete. Wapuuze hao wanaotaka kukutumia kwa manufaa yao ambao miongoni mwao ni mawaziri waandamizi watatu.
 
Sijasoma upuuzi ulioandikwa na mleta mada, ila ningependa nimkumbushe yeye mleta mada na watu wote wa aina yake kuwa muswaada ulisainiwa tangu tar 10 na sasa ni sheria.
 
Sijasoma upuuzi ulioandikwa na mleta mada, ila ningependa nimkumbushe yeye mleta mada na watu wote wa aina yake kuwa muswaada ulisainiwa tangu tar 10 na sasa ni sheria.
Leo utamaliza ID zako zote ndugu yangu. Ukweli ndio huo Mkuu.Tuupokee tu.Asante angalau uliuona uppuzi wangu na kuweka maoni yako. Ubarikiwe sana Mwenezi
 
Tangu kadhia ya kupitishwa 'kimagumashi' na 'kuchomekwa' kwa vifungu katika Muswada wa Mabadiliko ya Sheria ya Katiba Bungeni Dodoma,wapinzani hawakulala.Hawakushindwa. Waliendelea kupigania ustawi wa nchi kupitia Katiba mpya bora nje ya Bunge.Wakaitisha mikutano miwili mikubwa: Jangwani na Kibanda Maiti. Wakaungwa mkono. Wakasikika.

Wapinzani walilenga mambo makubwa mawili. Kwanza, kumtaka Rais awe makini katika mchakato huu wa Katiba mpya kwakuwa unabeba mustakabali wa Taifa. Hapa, wakamuomba Rais asisaini Muswada husika.Pia, walitaka kusikilizwa na Rais katika kuwasilisha hoja zao. Walitaka majadiliano na maridhiano ya kitaifa na Rais. Lengo hili limefanikiwa.Mosi, taarifa rasmi za Ikulu zinaonesha kuwa Rais hakusaini Muswada husika. Pili,wapinzani jana wamekutana na Rais Ikulu kusikilizana na kuelewana. Lengo limetimia.

Pia, wapinzani walilenga kurejeshwa Bungeni kwa Muswada huo ili uweze kujadiliwa tena kwa maboresho yalengayo afya ya Taifa.Tayari,Rais 'ameshaamuru' Muswada urejeshwe Bungeni kwa marejesho.Waweza kurejeshwa ukiwa umeshasainiwa au la. Haijalishi. Lengo la pili limetimia pia.

Ingawa wapinzani walibezwa sana hasa na Waandamizi wa CCM yetu, muda si muda mantiki yao itaonekana kwa wengi au wote. Kupigania Katiba bora ni kupigania Taifa bora. Katiba ndiyo msingi wetu wa kwanza. Vingine vyote vinaifuata Katiba. Vingine vyote ndiyo.

Hongereni sana wapinzani: Mbowe,Lipumba na Mbatia na vyama vyenu kwa kufanikiwa hata kwa haya. CCM yetu ijifunze kuendana na wakati na mabadiliko yake.Watanzania si wale jamani,wamebadilika sana.Tusije tukabadilishwa kwa kura!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

Msosi je
 
Sijasoma upuuzi ulioandikwa na mleta mada, ila ningependa nimkumbushe yeye mleta mada na watu wote wa aina yake kuwa muswaada ulisainiwa tangu tar 10 na sasa ni sheria.

Naona huyu haelewi.
 
Mkuu mimi si mlaghai.Tatizo kubwa lililopo ndani ya CCM yetu ni kuwa mkweli huchukiwa na kuonekana mpinzani. MwanaDiwani,wewe ni kiongozi chamani.Ubadilike.Ujenge hoja za haja.Acha kuropoka. Ukinisababisha niasi CCM,nitaanza na wewe. Jadili hoja. Kuwa M-CCM si kuwa mropokaji na muongo.Nyinyi ndio mnatuharibia chama chetu tawala. Njoo Lumumba, ukinikosa rudi hapa.
Huna lolote endelea na ulaghai wa kuwaokota wenye akili za kibavicha.

Wananchi wengi walishawakataa na ulaghai wenu kama huu wa kujifanya wewe ni kiongozi wa CCM wakati ni CHADEMA.

Unafahamu fika kama ukisema wewe ni CHADEMA hutapata wanaJf watakao kuamini katika hoja zako badala yake unakuja Jf umevaa U-CCM ili kuwahadaa wana JF kwa faida za muda mfupi.

Tutaendelea kuwaeleza ukweli wanaJf ili waendelee kukupuuze katika mabandiko yako.
 
Tangu kadhia ya kupitishwa 'kimagumashi' na 'kuchomekwa' kwa vifungu katika Muswada wa Mabadiliko ya Sheria ya Katiba Bungeni Dodoma,wapinzani hawakulala.Hawakushindwa. Waliendelea kupigania ustawi wa nchi kupitia Katiba mpya bora nje ya Bunge.Wakaitisha mikutano miwili mikubwa: Jangwani na Kibanda Maiti. Wakaungwa mkono. Wakasikika.

Wapinzani walilenga mambo makubwa mawili. Kwanza, kumtaka Rais awe makini katika mchakato huu wa Katiba mpya kwakuwa unabeba mustakabali wa Taifa. Hapa, wakamuomba Rais asisaini Muswada husika.Pia, walitaka kusikilizwa na Rais katika kuwasilisha hoja zao. Walitaka majadiliano na maridhiano ya kitaifa na Rais. Lengo hili limefanikiwa.Mosi, taarifa rasmi za Ikulu zinaonesha kuwa Rais hakusaini Muswada husika. Pili,wapinzani jana wamekutana na Rais Ikulu kusikilizana na kuelewana. Lengo limetimia.

Pia, wapinzani walilenga kurejeshwa Bungeni kwa Muswada huo ili uweze kujadiliwa tena kwa maboresho yalengayo afya ya Taifa.Tayari,Rais 'ameshaamuru' Muswada urejeshwe Bungeni kwa marejesho.Waweza kurejeshwa ukiwa umeshasainiwa au la. Haijalishi. Lengo la pili limetimia pia.

Ingawa wapinzani walibezwa sana hasa na Waandamizi wa CCM yetu, muda si muda mantiki yao itaonekana kwa wengi au wote. Kupigania Katiba bora ni kupigania Taifa bora. Katiba ndiyo msingi wetu wa kwanza. Vingine vyote vinaifuata Katiba. Vingine vyote ndiyo.

Hongereni sana wapinzani: Mbowe,Lipumba na Mbatia na vyama vyenu kwa kufanikiwa hata kwa haya. CCM yetu ijifunze kuendana na wakati na mabadiliko yake.Watanzania si wale jamani,wamebadilika sana.Tusije tukabadilishwa kwa kura!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Umeeleza vizuri sana shida ni wenzio wa Lumumba buk 7!! watakutusi wakikugundua wanakukolimba, au kukumwangosi/kukuulimboka/kukukibanda wakutupe Mabwepande!! take care!!
 
Huna lolote endelea na ulaghai wa kuwaokota wenye akili za kibavicha.

Wananchi wengi walishawakataa na ulaghai wenu kama huu wa kujifanya wewe ni kiongozi wa CCM wakati ni CHADEMA.

Unafahamu fika kama ukisema wewe ni CHADEMA hutapata wanaJf watakao kuamini katika hoja zako badala yake unakuja Jf umevaa U-CCM ili kuwahadaa wana JF kwa faida za muda mfupi.

Tutaendelea kuwaeleza ukweli wanaJf ili waendelee kukupuuze katika mabandiko yako.
Kama ndivyo,wewe nawe ni CCJ. Watakupuuza nawe.Umefurahi? Haya endelea na sikukuu na majukumu yako mengine.Hofu yangu hapa ni kubomoa chama chetu badala ya kujenga.Tutafute siku tupambane humu kwenye bandiko.Tutaomba ruhusa ya kutajana na kuanikiana kila kitu.Uko tayari Mkuu? Siku njema Mwenezi!
 
Kuishambulia hoja iliyoletwa kilaghai ni kuharalisha ulaghai na kuonekanana pia kama ni mmoja wa walaghai.

Lazima kwanza tuushambulie ulaghai wake ili ujenzi wa hoja uwe na mantiki na siyo hii ya kukaa pembeni na kuanza kuwakejeli wanaJf wanaojibu hoja zake bila kufahamu kama mleta hoja ni mlaghai.
Sasa mbona hukuushambulia huo unaouita ulaghai, badala yake ukamshambulia mtu mwenyewe! ninamashaka na uwezo wako wa kuchambua mambo.
 
Wewe huna lolote ni mwendelezo wa ulaghai ule ule ambacho CHADEMA inatumia kulaghai watu.

Unajifanya unafanya kazi ofisi ndogo Makao Makuu ya CCM na kuleta vi-propaganda vya kitoto katika jukwaa la siasa kufurahisha wasomaji wenye akili za kibavicha wakati hufahamu hata ofisi zake zimekaa vipi.

Wewe niwa kupuuzwa tu na hizi propaganda zako za kitoto ambazo haziwezi kukufanya kupata Uongozi Pwani kupitia CHADEMA.

Chama chenye mizizi ya kilaghai hakiwezi kusimama kwenye siasa za ukweli. Endelea na ulaghai wako kama kilivyo chama chako CHADEMA.

That was completely unnecessary MwanaDiwani, I'm sure you are a much better person than that.

Take care.
 
Last edited by a moderator:
Kiukweli wapinzani malengo yao yametimia , na kwa sasa mbowe,lipumba na hata mbatia binafsi nawaita ni senior citizen, ni wazalendo wa ukweli..
 
Ngumu kumesa hii. Wapinzani wanafanya movement zinazoleta matokeo chanya. Sisi wananchi wakawaida tunawaelewa sana.
 
Back
Top Bottom