Gangongine
JF-Expert Member
- Dec 31, 2015
- 3,854
- 1,776
Baada ya Viongozi wetu kuacha Sera na Itikadi ya kupinga Ufisadi na kupigania Rasilimali za Umma na badala yake kazi hiyo kufanywa kwa uhodari na Rais JPM, Sisi wapinzani wa kweli tunamuunga mkono Rais wetu na hatutakubali kudanganywa tena na Viongozi wetu ambao kimsingi tumewashtukia.
1. Ajenda yetu kuu ilikuwa kupinga Ufisadi na kutetea Rasilimali za Umma lakini Viongozi wetu wameifuta Ajenda hiyo na wanapigania Wageni wapore Rasilimali zetu! Hapa tumewashtukia!
2. Sasa tunaongozwa na Siasa za misimu za kupinga kila kitu chema cha Serikali ili tu tuonekane tupo. Hapa pia tumewashtukia Viongozi wetu!
3. Wanatetea wanafunzi wenye mimba kurudi shule wakati tukifahamu kwamba Taifa letu linapigania Maadili mema. Hapa tumewashtukia tena!
4. Wanatetea watumishi walioghushi vyeti wakati Sheria zetu zinasema hilo ni kosa la Jinai. Hapa pia tumewashtukia.
5. Wanapigania Bunge Live ili waonekane wakiwakashifu Viongozi wa Serikali na kutafuta Kick kwa nguvu. Hapa pia tumewashtukia!
Sisi Vijana tulioaminishwa kuwa kuna Mabadiliko ya Kweli kwenye upinzani na badala yake tukaletewa watu tuliowatangaza kuwa Mafisadi na kuondoa Orodha ya Mafisadi kwenye Tovuti ya Chama chetu tumeshashtukia kuwa kumbe tulidanganywa.
2020 hatutawapigia tena kura Wapinzani baada ya kuridhishwa kuwa walitutapeli na hawana jipya. Tutaendelea kuiamini CCM chini ya Jemedari JPM.
1. Ajenda yetu kuu ilikuwa kupinga Ufisadi na kutetea Rasilimali za Umma lakini Viongozi wetu wameifuta Ajenda hiyo na wanapigania Wageni wapore Rasilimali zetu! Hapa tumewashtukia!
2. Sasa tunaongozwa na Siasa za misimu za kupinga kila kitu chema cha Serikali ili tu tuonekane tupo. Hapa pia tumewashtukia Viongozi wetu!
3. Wanatetea wanafunzi wenye mimba kurudi shule wakati tukifahamu kwamba Taifa letu linapigania Maadili mema. Hapa tumewashtukia tena!
4. Wanatetea watumishi walioghushi vyeti wakati Sheria zetu zinasema hilo ni kosa la Jinai. Hapa pia tumewashtukia.
5. Wanapigania Bunge Live ili waonekane wakiwakashifu Viongozi wa Serikali na kutafuta Kick kwa nguvu. Hapa pia tumewashtukia!
Sisi Vijana tulioaminishwa kuwa kuna Mabadiliko ya Kweli kwenye upinzani na badala yake tukaletewa watu tuliowatangaza kuwa Mafisadi na kuondoa Orodha ya Mafisadi kwenye Tovuti ya Chama chetu tumeshashtukia kuwa kumbe tulidanganywa.
2020 hatutawapigia tena kura Wapinzani baada ya kuridhishwa kuwa walitutapeli na hawana jipya. Tutaendelea kuiamini CCM chini ya Jemedari JPM.