Pamoja mkuu wazee wa old ngoja tuendelee kufukua machimbo na kufaidi kiuutulivu kabisa.Hahahaa Kideo quality nzuri sana!! Makopokopo yao huwa siyapendi kabisa mimi ni old xulz tu.
Nyimbo inaitwa "tommorow" ya msanii anaitwa Brandy...wimbo ulitoka mwaka 1998 hapo akiwa na umri wa miaka 19..
Ni wimbo wenye hisia Kali Sana na uliomchukua muda mrefu kuurekodi maana alikuwa yupo kwenye maumivi makali ya kuachwa na mpenzi wake ambaye nae alikuwa msanii wa kundi la boys to men akijulikana kwa jina la Wanya Morris
Hivyo alikuwa anaurekodi huku analia hvyo ilimfanya kurudia rudia zaidi ya saa kadhaa..
Mahusiano yao yalidumu kwa miaka miwili,na Brandy ndie aliemshobokea mshkaji hapo akiwa na umri wa miaka 16,kwa kifupi mchizi ndie aliefungua utepe,hvyo ilimpelekea Brandy kuchanganyikiwa na penzi la mtu mzima
Hahaha Usiogope karibu...Nimepotea huku naona wazee wa zamani wanajadili mambo yao
Kwa nn mzeedah!! hii ngoma acha tu
machzi yamenitoka
Muziki ulikuwa zamani aisee,kwasasa ni makopo kopo tu!! Ukija huku unaburudishwa na Shania Twain - You are still the one ,ukienda huku kuna Luther vandros maricah carey - endless luv ,ukienda huku una boy 2 men ,ukirudi huku unapata flavor za wako jako ,ukirudi nyuma unawakuta dru hill - i should be ,ukienda kule unakutana na kina julio glesias ,ukienda mbele kuna ,swv,ukienda kushoto kuna spice girls,ukienda kulia unakutana na britney spears luck,ukija juu unakutana na kci and jojo -tell me its real,ukija kati s club 7- 2 in a millioni ,spice girls-2 became 1...yaani sisi ndio tumeenyoj muziki aiseeeee! Yaani unakuta HDD disk umejaza mp3 zaidi ya elfu 10.
Hahahaa mama wa Enya genre! Nyimbo zake tulivuuuuMpaka sasa sijaona wimbo wa Enya hata mmoja
wakuu nahitaji hii nyimbo everyday we celebrate kwenye mahafali inapigwa sana imeimbwa na mwanadada bado sijamfahamu anaitwa mwenye kuijua anipe link wakuuHaswaaaa yaani umetaja wanamuziki KONKI Next kina RL Too close ,Kina Tevin campbel -can we talk ,acha tu watoto wadogo kwasasa tunawahurumia na makopo kopo yao,kwenye vibanda umiza zamani tunapata mipini ya Nu shooz ,kina black box ,music factory huku tukisubiri ANODI ya JINI au ANODI YA JENI au RAMBO na KINA CHECK NORIS.